THE game is over! Sasa ni wazi kuwa familia ya staa mkubwa wa muziki wa
kizazi kipya Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Plutnamz’ imemtema rasmi mzazi
mwenzake Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kwa kile wanachodai ….
“Tumechoshwa na uzungu wake”, Risasi Mchanganyiko linaweza kuandika.
Chanzo kilicho karibu na familia hiyo kililiambia gazeti hili kuwa kina
taarifa kuwa mama Latiffa ‘Tiffah’ hatarejea tena nchini kutokana na
kushindwana na wanafamilia, kwani wanaendekeza uswahili, kitu ambacho
yeye hakiwezi.
“Familia ya Diamond ndiyo imemchoka, unajua yule hajazoea mambo ya
kiswahili swahili, ametofautiana nao sana na ndiyo maana hata wao
wamesema hawamtaki tena, wanahitaji mswahili mwenzao,” kilisema chanzo
hicho.
FAMILIA YA DIAMOND HII HAPA
Ili kujua ukweli wa maelezo hayo, mwandishi wetu alimtafuta mama mzazi
wa Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’ kupitia simu yake ya mkononi, na
alipoulizwa, alihamaki na kuanza kufoka, akidai hataki kuingiliwa mambo
yake ya ndani na kwamba kama kuna mtu anataka kujua zaidi amfuate Zari
huko kwao (South Afrika).
“Hata kama ni kweli, mimi na huyo sijui Zari wenu tumegombana wewe
yanakuhusu nini? sipendi kuingiliwa kwenye mambo ya familia yangu,
ninachojua ni kwamba hayupo hapa na maisha yanaendelea,” alisema Mama
Diamond na kukaa kimya huku simu ikiwa hewani.
Wakati simu ikiwa hewani, ghafla sauti ya kiume ilisikika na
kujitambulisha kwa jina la Anko Salum, aliyemtaka mwandishi kuachana na
habari hizo, kwani ni za ndani na zitamalizwa na wenyewe kama familia.
Wakati mwandishi wetu akiendelea kuzungumza na Anko Salum, ghafla tena
sauti nyembamba na kali masikioni ilisikika na mwanahabari wetu
akaibaini kuwa ni ya Esma, ambaye ni dada wa Diamond.
“Mbona mnatufuatilia sana jamani? Nani anafuatilia mambo yenu? Nafasi ya
Zari imefika mwisho, tunamkaribisha mwingine yeyote, kama kuna msichana
mrembo unamjua, tuletee nyumba yetu ni kubwa sana, na sisi tunaruhusiwa
kuoa hata wanawake wanne, Zari ameishia hapo, tena hatujagombana naye,
lakini tumechoshwa na uzungu wake, awamu hii tunahitaji mswahili
mwenzetu.
“Zari ameenda kwao, kulea watoto wake na kuangalia ustaarabu mwingine,
tunamtakia kila la kheri, lakini hatuna ugomvi naye kabisa,” alisema
Esma.Jitihada za kumpata Diamond hazikuzaa matunda kutokana na namba
yake ya mkononi kutokuwa hewani kila alipopigiwa, hata hivyo jitihada
zaidi zinaendelea kumtafuta.
Source:Global Publishers
Pages - Menu
▼
Pages - Menu
▼
SAMPLE
▼
Alhamisi, 22 Oktoba 2015
Picha 16 Za MAFURIKO Ya Lowassa Huko Tanga- Jana Oktoba 21
CHADEMA Wafichua Mbinu Zilizopangwa Kuvuruga Uchaguzi wa Jumapili hi
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chadema, Reginald Munisi (kulia) akifafanua
jambo. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Prof. Abdallah
Safari
**
ZIKIWA zimebaki siku tatu kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimefichua mikakati iliyopangwa kuvuruga uchaguzi huo.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chadema, Reginald Munisi amebainisha mipango ‘ovu’ inayoratibiwa ili kuvuruga uchaguzi mkuu huku mipango hii ikishirikisha baadhi ya makampuni ya simu za mkononi, Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na wakurugenzi wa uchaguzi katika majimbo mbalimbali.
Munisi ametaja baadhi ya mipango hiyo kama ifuatavyo, huku akitahadharisha watakaoshiriki mipango hiyo kuwa wataliingiza taifa katika machafuko bila sababu ya msingi.
Mpango wa kukata mawasiliano ya simu na data; upo mpango wa kuzuia mawasiliano ya simu za mkononi kwa kusitisha huduma ya kupiga na kupokea simu, kuzuia ujumbe mfupi wa maneno (sms), kuzuiwa kwa intaneti (data) na hivyo mawasiliano kuwa magumu, hasa wakati wa matokeo kubandikwa vituoni.
Mpango huu unatajwa kuwa na lengo la kukwamisha watu kuwasiliana na kupeana matokeo yatakayokuwa yakibandikwa vituoni ili kujumlisha na kupata matokeo ya jumla ya nafasi za udiwani, ubunge na urais. Utekelezaji wa mpango huu utashirikisha baadhi ya makampuni ya simu ambayo hakutaka kuyataja.
“Tunaziomba kampuni za simu zenye mpango huo, kuacha mara moja kwani zitajiongeza katika orodha ya watuhumiwa watakaoenda ‘The Hague’ mara baada ya uchaguzi kumalizika,” alieleza Munisi bila kuyataja makampuni hayo kwa kuwa bado chama hicho kinakusanya vielelezo.
Mpango wa kukata umeme maeneo yenye nguvu kubwa ya upinzani; maeneo ambayo vyama vya upinzani vina nguvu kubwa umeme utakatwa baada ya giza kuingia ili kuhakikisha mchakato wa kuhesabu na kujumlisha matokeo unaingia dosari na hata vurugu kutokea ili katika taharuki hiyo wizi wa kura uweze kufanyika.
Baadhi ya wakurugenzi wa uchaguzi kutoruhusu mawakala wa akiba wa upinzani kuapishwa; wakati uapishaji wa mawakala ukiendelea katika maeneo mbalimbali nchini, baadhi ya maeneo vyama vya upinzani vinazuiwa kuapisha mawakala wa akiba na wakurugenzi kutaka mawakala waape idadi sawa na idadi ya vituo vya kupigia kura.
Mkakati huu unalenga kuvifanya vyama vya upinzani vikose mawakala wa akiba iwapo itatokea dharura miongoni mwa wale walioapishwa, dharura zinazoweza kujitokeza ni kuumwa, kusafiri nje ya vituo, au kutekwa kabla ya kufika katika vituo vyao.
Iwapo mawakala hao watakosekana kwa dharura, baadhi ya vituo watabaki mawakala wa CCM pekee kwani hakutakuwa na mawakala wa akiba wa kuziba nafasi zao kwa kuwa ni lazima mawakala wawe wamekula viapo vya kisheria ili kupata uhalali wa kufanya kazi hiyo.
Reginald Munisi ameleza kuwa Chadema na Ukawa kiujumla wamejipanga vyema kuzikabili mbinu hizo chafu huku akiwaonya wale watakaoshiriki mipango hiyo kuachana nayo mara moja kwani tayari imefahamika na wanaweza kukumbana na nguvu ya Umma.
**
ZIKIWA zimebaki siku tatu kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimefichua mikakati iliyopangwa kuvuruga uchaguzi huo.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chadema, Reginald Munisi amebainisha mipango ‘ovu’ inayoratibiwa ili kuvuruga uchaguzi mkuu huku mipango hii ikishirikisha baadhi ya makampuni ya simu za mkononi, Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na wakurugenzi wa uchaguzi katika majimbo mbalimbali.
Munisi ametaja baadhi ya mipango hiyo kama ifuatavyo, huku akitahadharisha watakaoshiriki mipango hiyo kuwa wataliingiza taifa katika machafuko bila sababu ya msingi.
Mpango wa kukata mawasiliano ya simu na data; upo mpango wa kuzuia mawasiliano ya simu za mkononi kwa kusitisha huduma ya kupiga na kupokea simu, kuzuia ujumbe mfupi wa maneno (sms), kuzuiwa kwa intaneti (data) na hivyo mawasiliano kuwa magumu, hasa wakati wa matokeo kubandikwa vituoni.
Mpango huu unatajwa kuwa na lengo la kukwamisha watu kuwasiliana na kupeana matokeo yatakayokuwa yakibandikwa vituoni ili kujumlisha na kupata matokeo ya jumla ya nafasi za udiwani, ubunge na urais. Utekelezaji wa mpango huu utashirikisha baadhi ya makampuni ya simu ambayo hakutaka kuyataja.
“Tunaziomba kampuni za simu zenye mpango huo, kuacha mara moja kwani zitajiongeza katika orodha ya watuhumiwa watakaoenda ‘The Hague’ mara baada ya uchaguzi kumalizika,” alieleza Munisi bila kuyataja makampuni hayo kwa kuwa bado chama hicho kinakusanya vielelezo.
Mpango wa kukata umeme maeneo yenye nguvu kubwa ya upinzani; maeneo ambayo vyama vya upinzani vina nguvu kubwa umeme utakatwa baada ya giza kuingia ili kuhakikisha mchakato wa kuhesabu na kujumlisha matokeo unaingia dosari na hata vurugu kutokea ili katika taharuki hiyo wizi wa kura uweze kufanyika.
Baadhi ya wakurugenzi wa uchaguzi kutoruhusu mawakala wa akiba wa upinzani kuapishwa; wakati uapishaji wa mawakala ukiendelea katika maeneo mbalimbali nchini, baadhi ya maeneo vyama vya upinzani vinazuiwa kuapisha mawakala wa akiba na wakurugenzi kutaka mawakala waape idadi sawa na idadi ya vituo vya kupigia kura.
Mkakati huu unalenga kuvifanya vyama vya upinzani vikose mawakala wa akiba iwapo itatokea dharura miongoni mwa wale walioapishwa, dharura zinazoweza kujitokeza ni kuumwa, kusafiri nje ya vituo, au kutekwa kabla ya kufika katika vituo vyao.
Iwapo mawakala hao watakosekana kwa dharura, baadhi ya vituo watabaki mawakala wa CCM pekee kwani hakutakuwa na mawakala wa akiba wa kuziba nafasi zao kwa kuwa ni lazima mawakala wawe wamekula viapo vya kisheria ili kupata uhalali wa kufanya kazi hiyo.
Reginald Munisi ameleza kuwa Chadema na Ukawa kiujumla wamejipanga vyema kuzikabili mbinu hizo chafu huku akiwaonya wale watakaoshiriki mipango hiyo kuachana nayo mara moja kwani tayari imefahamika na wanaweza kukumbana na nguvu ya Umma.
Madai ya Kumuua Mwigizaji Kanumba LULU MICHAEL Mahakani Tena...
Stori: Na Brighton Masalu
MAMBO yameiva!
Nyota wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’ (20) yu
mbioni kupanda tena Kizimba cha Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es
Salaam kwa ishu yake ile ya madai ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa
msanii wa filamu nchini, marehemu , Amani lina ripoti mkononi.
Nyota wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’.
Kwa mujibu wa
chanzo chetu kutoka ndani ya mahakama hiyo jijini Dar, kesi hiyo
ilisimama kwa muda wa mwaka mmoja na zaidi kutokana na matatizo yaliyo
nje ya uwezo wa mahakama, lakini sasa matatizo hayo yameisha hivyo kesi
hiyo itaanza kurindima siku yoyote kuanzia sasa.
NI BAADA YA MWAKA MMOJA NA MIEZI NANE
Tangu kusimama
kwa kesi hiyo, mwaka 2013, ilitarajiwa kuanza tena kusikilizwa Februari
17, 2014 lakini ikakwama kutokana na matatizo mbalimbali ya kimahakama.
ITAANZA UPYA
Kwa mujibu wa
mtoa habari wetu, mwendesha mashtaka wa serikali atamsomea mashtaka upya
Lulu lakini neno la msingi kwenye mashtaka hayo ni; mnamo Aprili 7,
2012 anadaiwa kumuua bila kukusudia, Steven Kanumba.
“Baada ya
kuulizwa, Lulu akiwa kama Elizabeth Michael atajibu anachotaka kutoka
moyoni kulingana na ukweli anaoujua kisha jaji atampangia tarehe ya
kurudi tena,” alisema mtoa habari huyo.
MAHAKAMA ITATUMIA MWONGOZO WA JAJI MKUU
Tofauti na
madai ya awali kwamba, kesi hiyo ingeendeshwa kwa siku 730, habari za
uhakika zinasema kuwa, kesi itakapoanza safari hii haitasimamishwa mpaka
siku ya hukumu. Kwa hiyo itategemea na kasi ya hakimu husika.
“Lakini pia,
kauli ya Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman anayoitoa kila
Siku ya Sheria Duniani (Februari 3) kwamba kesi zote za jinai
zisipitishe miaka miwili, itazingatiwa,” kilisema chanzo.
Kikaongeza:
“Lakini nadhani ikianza safari mwaka huu, naamini mpaka mwaka 2017
itakuwa imemalizika kama sheria ya miaka miwili itazingatiwa.”
Marehemu Steven Charles Kanumba ‘The Great’ enzi za uhai wake.
CHENI BADO MDHAMINI
Chanzo hicho
kilisema kuwa, bado mcheza sinema maarufu Bongo, Mahsein Awadh ‘Dk.
Cheni’ anaendelea kutambulika na mahakama kama mdhamini wa Lulu. Kwa
hiyo, anatakiwa kuendelea na jukumu la kumlinda Lulu ili asiruke dhamana
(asitoroke, asikiuke masharti ya dhamana).
MASHAHIDI WAJIPANGE
Chanzo kilisema baadhi ya mashahidi muhimu nao watapewa taarifa ya kimaandishi ili tarahe ya kesi wafike mahakamani.
Mashahidi hao
ni Dokta Kidume ambaye alikuwa akimtibu Kanumba pia ndiye alikuwa mtu wa
pili kufika kwenye chumba cha marehemu mara baada ya kuanguka na
kupoteza maisha.
Seth Bosco
naye anatakiwa kujiandaa kupokea wito huo kwani yeye siku ya tukio
alikuwa nyumba moja na marehemu (vyumba tofauti). Yeye alimshuhudia
Kanumba akiwa katika hali mbaya baada ya kutoelewana na Lulu na kukimbia
kwenda kumwita Dokta Kidume.
WAKILI WA LULU AZUNGUMZA
Peter Kibatala ni wakili maarufu jijini Dar. Yeye ndiye mwanasheria katika kesi ya Lulu. Amani lilimtafuta ili kujua hatima ya kesi hiyo na madai kwamba iko njiani kuanza upya. Alisema:
“Aaa! Sijajua.
Lakini kwa kawaida mahakama itakapoona mambo yameanza, kesi inatakiwa
kuanza kusikilizwa itatakiwa kutoa taarifa siku sita kabla.”
AMZUNGUMZIA LULU
Wakili
Kibatala alikwenda mbele zaidi kwa kusema kuwa, mteja wake (Lulu)
amekuwa akimpigia simu mara kwa mara akitaka kujua tarehe ya kesi yake
kuanza tena.
“Hata Lulu
mwenyewe amekuwa akinipigia simu kuulizia ni tarehe ngapi kesi yake
itaanza tena. Nitapewa taarifa siku sita kabla,” alisema mwanasheria
huyo.
LULU PRESHA INAPANDA
Naye rafiki wa karibu wa Lulu, akizungumza na gazeti hili huku akiomba hifadhi ya jina lake, alisema:
“Ninyi
mnaandika Lulu siku hizi anakunywa sana pombe. Mnajua hayuko sawasawa.
Ile kesi yake ya kumuua (bila kukusudia) Kanumba inamtesa sana kichwani.
“Ukimya wa
kesi unamfanya ashindwe kujua hatima yake. Kila akikumbuka anampigia
simu wakili wake. Mbaya zaidi kuna watu wanamwambia kesi inaweza kukaa
kimya kwa muda mrefu halafu siku moja ikalipuka na kuwa nzito. Kwa hiyo
wakati mwingine mjue hilo.”
WASOMAJI WETU
Baadhi ya
wasomaji wa Magazeti Pendwa ya Global Publishers wamekuwa wakipiga simu
chumba cha habari na kuulizia kama kesi ile ilifutwa kinyemela au
kihalali.
“Jamani
Global, mimi shida yangu ni kuulizia kuhusu ile kesi ya Lulu na Kanumba.
Hivi bado ipo au ilishafutwa kinyemela. Maana si mnajua watu maarufu
tena huenda kuna kubebana,” aliwahi kuuliza msomaji mmoja.
LULU ASAKWA
Jumatatu
na Jumanne iliyopita, simu ya Lulu ilipopigwa iliita muda mrefu bila
kupokelewa. Hata hivyo, baadhi ya watu wake wa karibu walisema Lulu huwa
hapokei simu ambayo jina halipo kwenye simu yake.
Source:GPL
Hatimaye Mama Maria Nyerere Ampigia Kampeni Magufuli
CCM tayari wameshatengeneza video ya mama Maria Nyerere akiwaomba akina
mama wotewampigie kura Magufuli. Video hii iko inasambaa Whatsup.
Kaongea mengi kuwa ni mchapa kazi na Mwadilifu. Swali langu kwa bibi angu mama Maria, ikiwa CCM itashindwa, heshima yote tunayokupa sisi wananchi itakuwaje? Maana yake wote watakaoongoza rohoni mwao watakuwa wanajua kabisa hukuwapenda ila basi.
Ni bora mama ungebaki neutral. Na ungejikita kutuombea tuchaguane kwa Amani ili uendeleee kuwa Mama wa Taifa.
Ila tutasamehe tukiamini imekulazimu, maana hakuna jinsi
Kaongea mengi kuwa ni mchapa kazi na Mwadilifu. Swali langu kwa bibi angu mama Maria, ikiwa CCM itashindwa, heshima yote tunayokupa sisi wananchi itakuwaje? Maana yake wote watakaoongoza rohoni mwao watakuwa wanajua kabisa hukuwapenda ila basi.
Ni bora mama ungebaki neutral. Na ungejikita kutuombea tuchaguane kwa Amani ili uendeleee kuwa Mama wa Taifa.
Ila tutasamehe tukiamini imekulazimu, maana hakuna jinsi
UKAWA Watishia Kutoshiriki Uchaguzi Mkuu wa Jumapili
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinachoungwa mkono na Umoja
wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kimetishia kutoshiriki katika Uchaguzi
Mkuu utakaofanyika Oktoba 25, mwaka huu.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chadema, Reginald Munisi amesema wanadhamilia kutoshiriki katika uchaguzi huo kutokana Tume yaTaifa ya Uchaguzi (NEC) kutokuwa na msimamo katika kazi zake.
Anasema zikiwa zimebaki siku tatu wananchi kuelekea kwenye uchaguzi mkuu lakini NEC hadi sasa haina msimamo na kuonekana kuyapuuza madai mengi yenye hoja yanayotolewa na Ukawa.
Akiyataja baadhi ya madai ambayo NEC imeyapuuza ni kutotoa ushirikiano wa kufafanua juu ya upigaji kura kwa watu ambao hawakuona majina yao kwenye daftari la kupiga kura na kutotoa sababu ya utofauti wa namba za kupigia kura kutoka kwenye daftari na kwenye kitambulisho.
Munisi ameongeza kuwa, NEC wamepuuza kutoa ufafanuzi juu ya picha ambazo haziitajiki katika upigaji kura, kutoa ufafanuzi juu ya listi mpya ya wapiga kura iliyosemwa na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva, kwamba kutakuwa na watu wa ziada ambao hawapo kwenye daftari, Je, wanatoka wapi na wapo wangapi? Amehoji.
“Kwa mtindo huu ambao NEC inaenda nao wa kukubali watu wasiokuwa kwenye daftari wapige kura na hata wasiokuwepo kwenye orodha wapige kura mbona hawakutushirikisha sisi wadau wa uchaguzi? Inaweza kupelekea uvunjifu wa amani. Hilo ndio bao la mkono ambalo lilisemwa na hatutaki litokee,” anasema Munisi.
Munisi amesema sababu nyingine kubwa ambayo inaweza kupelekea wasishiriki kwenye uchaguzi ni kuhusu madudu yaliyopo ndani ya daftari la wapiga kura, ambapo hadi sasa NEC haijatoa jibu linaloeleweka juu ya makosa ambayo yalionekana kwenye daftari.
Sababu nyingine ya kutaka kutoshiriki amesema, “Hatuna imani na ujumlishaji wa matokeo ya kura kwa njia ya mashine zao za kujumlisha kwani zinamapungufu mengi. Tuliomba tume itumie njia ya kawaida kwa njia ya kalukuleta ili kila mtu alidhike lakini walidai tunawaingilia kazi zake. Sisi hatutakubali,” amesema Munisi.
Kwa mujibu wa Munisi amesema, hadi sasa bado wanaendelea na uchunguzi kwenye madaftari ya wapiga kura ambapo amesema wameshakagua katika mikoa tisa na kubaini matatizo mengi zaidi yakiwemo ya picha hewa, picha za watu wawili na majina ya kiume kwenye picha za kike.
“Hapo hatujafanya katika majimbo yote tulifanya baadhi. Bado tunaendelea na uchunguzi hadi kesho, tukiona makosa yanazidi kiwango cha kufanya uchaguzi usiende vizuri basi tunaiomba NEC ipeleke uchaguzi mbele,” amesema Munisi.
Aidha, ameitaka NEC kutoa orodha maalumu ya vituo vya kupigia kura kwani hadi sasa Ukawa bado hawajajua idadi kamili ya vituo hivyo wanashindwa kuwaapisha mawakala kwa idadi ya vituo kubadilishwa kila siku.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chadema, Reginald Munisi amesema wanadhamilia kutoshiriki katika uchaguzi huo kutokana Tume yaTaifa ya Uchaguzi (NEC) kutokuwa na msimamo katika kazi zake.
Anasema zikiwa zimebaki siku tatu wananchi kuelekea kwenye uchaguzi mkuu lakini NEC hadi sasa haina msimamo na kuonekana kuyapuuza madai mengi yenye hoja yanayotolewa na Ukawa.
Akiyataja baadhi ya madai ambayo NEC imeyapuuza ni kutotoa ushirikiano wa kufafanua juu ya upigaji kura kwa watu ambao hawakuona majina yao kwenye daftari la kupiga kura na kutotoa sababu ya utofauti wa namba za kupigia kura kutoka kwenye daftari na kwenye kitambulisho.
Munisi ameongeza kuwa, NEC wamepuuza kutoa ufafanuzi juu ya picha ambazo haziitajiki katika upigaji kura, kutoa ufafanuzi juu ya listi mpya ya wapiga kura iliyosemwa na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva, kwamba kutakuwa na watu wa ziada ambao hawapo kwenye daftari, Je, wanatoka wapi na wapo wangapi? Amehoji.
“Kwa mtindo huu ambao NEC inaenda nao wa kukubali watu wasiokuwa kwenye daftari wapige kura na hata wasiokuwepo kwenye orodha wapige kura mbona hawakutushirikisha sisi wadau wa uchaguzi? Inaweza kupelekea uvunjifu wa amani. Hilo ndio bao la mkono ambalo lilisemwa na hatutaki litokee,” anasema Munisi.
Munisi amesema sababu nyingine kubwa ambayo inaweza kupelekea wasishiriki kwenye uchaguzi ni kuhusu madudu yaliyopo ndani ya daftari la wapiga kura, ambapo hadi sasa NEC haijatoa jibu linaloeleweka juu ya makosa ambayo yalionekana kwenye daftari.
Sababu nyingine ya kutaka kutoshiriki amesema, “Hatuna imani na ujumlishaji wa matokeo ya kura kwa njia ya mashine zao za kujumlisha kwani zinamapungufu mengi. Tuliomba tume itumie njia ya kawaida kwa njia ya kalukuleta ili kila mtu alidhike lakini walidai tunawaingilia kazi zake. Sisi hatutakubali,” amesema Munisi.
Kwa mujibu wa Munisi amesema, hadi sasa bado wanaendelea na uchunguzi kwenye madaftari ya wapiga kura ambapo amesema wameshakagua katika mikoa tisa na kubaini matatizo mengi zaidi yakiwemo ya picha hewa, picha za watu wawili na majina ya kiume kwenye picha za kike.
“Hapo hatujafanya katika majimbo yote tulifanya baadhi. Bado tunaendelea na uchunguzi hadi kesho, tukiona makosa yanazidi kiwango cha kufanya uchaguzi usiende vizuri basi tunaiomba NEC ipeleke uchaguzi mbele,” amesema Munisi.
Aidha, ameitaka NEC kutoa orodha maalumu ya vituo vya kupigia kura kwani hadi sasa Ukawa bado hawajajua idadi kamili ya vituo hivyo wanashindwa kuwaapisha mawakala kwa idadi ya vituo kubadilishwa kila siku.
Katibu Mwenezi wa CCM Nape Nnauye Apata Ajali Mbaya ya Gari
KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye
amepata ajali mbaya jana usiku akiwa njiani kuelekea Lindi akitokea
jijini Dar es Salaam.
Nape ambaye pia ni mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtama, Lindi alipata ajali hiyo baada ya tairi la mbele la gari aliyokuwa akiendesha aina ya Toyota Land Cruiser kupasuka na kupinduka mara kadhaa katika eneo la Nyangao mkoani Lindi.
Katika gari hilo, Nape alikuwa peke yake na ndiye alikuwa akiendesha gari hilo ambapo amepata majeraha madogo ila anaendelea vizuri.
Akizungumza na mtandao huu, Nape amesema: “Namshukuru Mungu nimetoka salama na nawaomba wananchi wasiwe na hofu japo ajali ilikuwa mbaya maana gari lilipinduka mara kadhaa, nimepata majeraha madogomadogo na michubuko ila ni mzima.
Gari limeharibika vibaya ila ninachoshukuru nilikuwa nimefunga mkanda na ‘air bag’ nazo zimenisaidia.”
Kabla ya ajali hiyo, Nape alikuwa jijini Dar es Salaam ambapo aliungana na mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Pombe Magufuli aliyekuwa na mikutano kadhaa ya kampeni katika jiji la Dar na baada ya shughuli hiyo alikuwa akirejea Lindi kuendelea na kampeni kwenye jimbo lake la Mtama.
Source:GPL
Nape ambaye pia ni mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtama, Lindi alipata ajali hiyo baada ya tairi la mbele la gari aliyokuwa akiendesha aina ya Toyota Land Cruiser kupasuka na kupinduka mara kadhaa katika eneo la Nyangao mkoani Lindi.
Katika gari hilo, Nape alikuwa peke yake na ndiye alikuwa akiendesha gari hilo ambapo amepata majeraha madogo ila anaendelea vizuri.
Akizungumza na mtandao huu, Nape amesema: “Namshukuru Mungu nimetoka salama na nawaomba wananchi wasiwe na hofu japo ajali ilikuwa mbaya maana gari lilipinduka mara kadhaa, nimepata majeraha madogomadogo na michubuko ila ni mzima.
Gari limeharibika vibaya ila ninachoshukuru nilikuwa nimefunga mkanda na ‘air bag’ nazo zimenisaidia.”
Kabla ya ajali hiyo, Nape alikuwa jijini Dar es Salaam ambapo aliungana na mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Pombe Magufuli aliyekuwa na mikutano kadhaa ya kampeni katika jiji la Dar na baada ya shughuli hiyo alikuwa akirejea Lindi kuendelea na kampeni kwenye jimbo lake la Mtama.
Source:GPL
Muonekano wa Gari ya Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye, Toyota Land Cruiser Baada ya Kupata Ajali Mbaya Jana Usiku
Muonekano wa gari ya Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye,
Toyota Land Cruiser baada ya kupata ajali mbaya jana usiku akiwa njiani
kuelekea Lindi akitokea jijini Dar es Salaam.
Magufuli Asimamisha Jiji La Dar.......Asema Tanzania Inahitaji Rais Mkali. CHADEMA Wampokea Kwa Ishara Ya Vidole Viwili Juu
Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, amesema
nchi inahitaji rais mkali ili mambo yaende huku akishangazwa na mmoja wa
vigogo kufungua kesi kupinga mradi wa maji.
Amesema watu wa aina hiyo watakiona na anamuomba Mungu kwa siki tatu zilizobaki apewe urais kwa vile hao ndiyo ataanza kushughulika nao.
Kauli hiyo aliitoa Dar es Salaam jana kwa nyakati tofauti katika mikutano ya kampeni iliyofanyika Kigamboni, Mbagala, Temeke, Ubungo na Kinondoni.
Alisema hayuko tayari kuona watu wanaendelea kupoteza maisha kwa kipindupindi huku kigogo huyo akikimbilia mahakamani.
Kitendo cha kigogo huyo kufunga njia ya maji kwa kujenga bomba la majitaka kimesababisha wananchi wa Dar es Salaam kupoteza maisha kwa kuugua kipindupindu, alisema.
“Ninajua hapa Temeke kuna mtu amekimbilia mahakamani na kukwamisha mradi wa maji lakini mahakama haitoi haki kwa wakati.
“Zimebaki siku nne ninichague kuwa rais, mtu anachelewesha mradi wa maji kwa kwenda mahakamani ngoja nipate urais. Amejenga juu ya njia ya maji watu wanakufa kwa kipindupindu haki ya Mungu ngoja nipate urais.
“…tunahitaji rais mkali mambo yaende kesi ni lazima iamuriwe kama Serikali tumeshindwa tukate rufaa. Tena huyo mtu aliyefungua kesi ana udugu na mmoja wa wagombea wa Ukawa,” alisema Dk. Magufuli.
Mgombea huyo wa urais alisema atakapochaguliwa Jumapili atakwenda kuanza na hilo.
“Haiwezekani, haiwezekani, haiwezekani mradi wa maji una manufaa wao wanakunywa maji ya Kilimanjaro wananchi wanateseka. Lakini watu wachache kwa tamaa zao na madaraka yao wanakwamisha.
“Wanasema mimi ni mkali, hapana nina hofu ya Mungu, tunaomba kesi hii iamuriwe kama tumeshindwa tukate rufaa,” alisema Dk. Magufuli
Mgombea huyo wa urais alisema yeye ni mtu wa uamuzi makini anayekuja kuijenga Tanzania mpya na yenye matumaini kwa watanzania wote.
Alisema anashangazwa na watu wanaohangaika na uamuzi mgumu kwani wanaofanya hivyo ni majambazi, wezi na mafisadi pekee.
Dk. Magufuli, alisema ataongoza taifa kwa umakini kwa kuleta maendeleo ya kweli.
Alisema anashangazwa na watu wanaopita na kujinasibu kwa kuleta uamuzi mgumu wakati ndiyo walioleta matatizo katika nchi na hata kusababisha kero ya umeme kila kukicha.
“Watakuja wapinzani wetu na kusema eti wanakuja na uamuzi mgumu, jamani uamuzi mgumu hufanywa na majambazi, wezi na wauaji wa watu wenye albino. Inashangaza sana hawa watu msiwakubalie hata kidogo.
“… hivi jana itokee upate mume au mke anayetamba kwa kuwa na uamuzi mgumu si atakunyonga kitandani. Eti atafanya uamuzi mgumu mbona hujinyongi kwa kamba? Mimi kwangu Magufuli kazi tu,” alisema Dk. Magufuli.
Akizungumzia ujenzi wa daraja la Kigamboni, Dk. Magufuli alisema litakamilika mwezi ujao na wananchi wa eneo hilo watavuka bure ila watu wenye magari ndiyo watakaolipa ada.
Alisema yeye ni mtu anayesimamia sheria hivyo katu hawezi kuzivunja kwa kutoa ahadi za uongo kwa lengo la kutafuta kura za watanzania.
“Daraja la Kigamboni litakamilika mapema mwezi ujao na litakapokamilika wakazi wa Kigamboni watapita bure ila wenye magari watalipia kama ilivyokuwa kwenye kivuko cha pantoni.
“Kigamboni ya sasa imekuwa na maendeleo na kwa sababu mbunge wenu, Dk. Ndugulile (Faustine) ni mfuatiliaji nami nawaomba mumchague ninamuhitaji.
“Alipambana kwa ajili ya yenu na sasa ninasema hapa Rais Jakaya Kikwete amenisaidia sana kwa kuiteua Kigamboni kuwa wilaya nami kazi yangu itakuwa ni kuleta maendeleo ya kweli,” alisema.
Mgombea huyo wa urais alisema kwa mujibu wa sheria, ardhi ni mali hivyo kwa Kigamboni kujengwa mji mpya ni hatua kubwa ya maendeleo.
Dk. Magufuli aliwataka wakazi hao kuhakikisha wanasimamia haki zao ikiwamo kumiliki ardhi yao na hata kushirikiana na wawekezaji.
“Ardhi ni mali na hapa Kigamboni sasa mji mpya wakija wawekezaji kwanza wawape noti na hata mshirikiane pamoja kutokana na ardhi yenu,” alisema.
Chadema wampokea Ubungo huku wakimshangilia Lowassa
Mgombea huyo wa urais wa CCM alipofika katika Kituo cha Mabasi Ubungo, alisimamishwa na wafuasi wa Ukawa ambao walimnyoonshea vidole viwili juu huku wakimshangilia Mgombea wao kwa kuimba Lowassa!!! Lowassa!!
Baada ya hali hiyo,Magufuli aliwasalimia wafuasi hao wa Ukawa kwa ishara ya salamu zao na kuwaambia kuwa maendeleo hayana chama.
“Maendeleo hayana chama iwe Chadema, CCM, CUF na hata Ukawa mimi kwangu ni kazi tu,” alisema.....Tazama Video Hii https://youtu.be/NI_JKb9KJSc
Amesema watu wa aina hiyo watakiona na anamuomba Mungu kwa siki tatu zilizobaki apewe urais kwa vile hao ndiyo ataanza kushughulika nao.
Kauli hiyo aliitoa Dar es Salaam jana kwa nyakati tofauti katika mikutano ya kampeni iliyofanyika Kigamboni, Mbagala, Temeke, Ubungo na Kinondoni.
Alisema hayuko tayari kuona watu wanaendelea kupoteza maisha kwa kipindupindi huku kigogo huyo akikimbilia mahakamani.
Kitendo cha kigogo huyo kufunga njia ya maji kwa kujenga bomba la majitaka kimesababisha wananchi wa Dar es Salaam kupoteza maisha kwa kuugua kipindupindu, alisema.
“Ninajua hapa Temeke kuna mtu amekimbilia mahakamani na kukwamisha mradi wa maji lakini mahakama haitoi haki kwa wakati.
“Zimebaki siku nne ninichague kuwa rais, mtu anachelewesha mradi wa maji kwa kwenda mahakamani ngoja nipate urais. Amejenga juu ya njia ya maji watu wanakufa kwa kipindupindu haki ya Mungu ngoja nipate urais.
“…tunahitaji rais mkali mambo yaende kesi ni lazima iamuriwe kama Serikali tumeshindwa tukate rufaa. Tena huyo mtu aliyefungua kesi ana udugu na mmoja wa wagombea wa Ukawa,” alisema Dk. Magufuli.
Mgombea huyo wa urais alisema atakapochaguliwa Jumapili atakwenda kuanza na hilo.
“Haiwezekani, haiwezekani, haiwezekani mradi wa maji una manufaa wao wanakunywa maji ya Kilimanjaro wananchi wanateseka. Lakini watu wachache kwa tamaa zao na madaraka yao wanakwamisha.
“Wanasema mimi ni mkali, hapana nina hofu ya Mungu, tunaomba kesi hii iamuriwe kama tumeshindwa tukate rufaa,” alisema Dk. Magufuli
Mgombea huyo wa urais alisema yeye ni mtu wa uamuzi makini anayekuja kuijenga Tanzania mpya na yenye matumaini kwa watanzania wote.
Alisema anashangazwa na watu wanaohangaika na uamuzi mgumu kwani wanaofanya hivyo ni majambazi, wezi na mafisadi pekee.
Dk. Magufuli, alisema ataongoza taifa kwa umakini kwa kuleta maendeleo ya kweli.
Alisema anashangazwa na watu wanaopita na kujinasibu kwa kuleta uamuzi mgumu wakati ndiyo walioleta matatizo katika nchi na hata kusababisha kero ya umeme kila kukicha.
“Watakuja wapinzani wetu na kusema eti wanakuja na uamuzi mgumu, jamani uamuzi mgumu hufanywa na majambazi, wezi na wauaji wa watu wenye albino. Inashangaza sana hawa watu msiwakubalie hata kidogo.
“… hivi jana itokee upate mume au mke anayetamba kwa kuwa na uamuzi mgumu si atakunyonga kitandani. Eti atafanya uamuzi mgumu mbona hujinyongi kwa kamba? Mimi kwangu Magufuli kazi tu,” alisema Dk. Magufuli.
Akizungumzia ujenzi wa daraja la Kigamboni, Dk. Magufuli alisema litakamilika mwezi ujao na wananchi wa eneo hilo watavuka bure ila watu wenye magari ndiyo watakaolipa ada.
Alisema yeye ni mtu anayesimamia sheria hivyo katu hawezi kuzivunja kwa kutoa ahadi za uongo kwa lengo la kutafuta kura za watanzania.
“Daraja la Kigamboni litakamilika mapema mwezi ujao na litakapokamilika wakazi wa Kigamboni watapita bure ila wenye magari watalipia kama ilivyokuwa kwenye kivuko cha pantoni.
“Kigamboni ya sasa imekuwa na maendeleo na kwa sababu mbunge wenu, Dk. Ndugulile (Faustine) ni mfuatiliaji nami nawaomba mumchague ninamuhitaji.
“Alipambana kwa ajili ya yenu na sasa ninasema hapa Rais Jakaya Kikwete amenisaidia sana kwa kuiteua Kigamboni kuwa wilaya nami kazi yangu itakuwa ni kuleta maendeleo ya kweli,” alisema.
Mgombea huyo wa urais alisema kwa mujibu wa sheria, ardhi ni mali hivyo kwa Kigamboni kujengwa mji mpya ni hatua kubwa ya maendeleo.
Dk. Magufuli aliwataka wakazi hao kuhakikisha wanasimamia haki zao ikiwamo kumiliki ardhi yao na hata kushirikiana na wawekezaji.
“Ardhi ni mali na hapa Kigamboni sasa mji mpya wakija wawekezaji kwanza wawape noti na hata mshirikiane pamoja kutokana na ardhi yenu,” alisema.
Chadema wampokea Ubungo huku wakimshangilia Lowassa
Mgombea huyo wa urais wa CCM alipofika katika Kituo cha Mabasi Ubungo, alisimamishwa na wafuasi wa Ukawa ambao walimnyoonshea vidole viwili juu huku wakimshangilia Mgombea wao kwa kuimba Lowassa!!! Lowassa!!
Baada ya hali hiyo,Magufuli aliwasalimia wafuasi hao wa Ukawa kwa ishara ya salamu zao na kuwaambia kuwa maendeleo hayana chama.
“Maendeleo hayana chama iwe Chadema, CCM, CUF na hata Ukawa mimi kwangu ni kazi tu,” alisema.....Tazama Video Hii https://youtu.be/NI_JKb9KJSc
Jumamosi, 17 Oktoba 2015
P-square na Fally Ipupa Walitamani Kuwachukua Dancers wa Diamond
Dancers wa P-Square pamoja na msanii mkubwa wa nchini Congo, Fally Ipupa
walijaribu kumshawishi Diamond ili wafanye kazi ya pamoja na dancers
wake.
Akizungumza na Bongo5 jana mmoja wa dancers hao, Imma Platnumz, alisema hali hiyo ya kufuatwa na dancers wa P-Square inaonyesha kazi wanayoifanya inakubalika.
“Tulikuwa tupo Nigeria tunafanya show, dancers wa P-Square wakataka kufanya kazi na sisi,” amesema. “Wakamfuta Diamond lakini Diamond akakataa kwa sababu walikuwa wanataka tujoin halafu tufanye show pamoja kitu ambacho hakiwezekani,” ameongeza.
“Pia tulikutana na Fally Ipupa, aliomba kufanya show na sisi lakini management imeshindwa kutuachia kwa sababu tuna kazi zetu binafsi.”
Akizungumza na Bongo5 jana mmoja wa dancers hao, Imma Platnumz, alisema hali hiyo ya kufuatwa na dancers wa P-Square inaonyesha kazi wanayoifanya inakubalika.
“Tulikuwa tupo Nigeria tunafanya show, dancers wa P-Square wakataka kufanya kazi na sisi,” amesema. “Wakamfuta Diamond lakini Diamond akakataa kwa sababu walikuwa wanataka tujoin halafu tufanye show pamoja kitu ambacho hakiwezekani,” ameongeza.
“Pia tulikutana na Fally Ipupa, aliomba kufanya show na sisi lakini management imeshindwa kutuachia kwa sababu tuna kazi zetu binafsi.”
PICHA ZA MABAKI YA HELIKOPTA ILIYOPOTEZA UHAI WA MBUNGE DEO FILIKUNJOMBE
Mwili wa Deo Filikunjombe ukitolewa Eneo la tukio baada ya kuteketea kwa Moto kufuatia ajali ya helkopta.
Waliofariki
mbali ya Filikunjombe wengine ni Mwenyekiti wa TLP Mkoa wa Iringa Blanka
Francis Haule ,Egdi Francis Nkwela na rubani wa helkopta hiyo Wiliam
Slaa.
Miili yote imepelekwa jijini Dar esalaa kutoka katikati ya mbuga ya Selou kitalu R3 .
Mwili wa Filikunjombe utaagwa leo jumamosi jijini Dar na kusafirishwa kwenda Ludewa kwa mazishi yatakayofanyika jumapili .
Mkuu wa Majeshi Jenaral Davis Mwamunyange Arejea Nchini Mzima wa Afya..Baada ya Tetesi za Kulishwa Sumu
Ijumaa, 16 Oktoba 2015
BAADA YA KUJITOA CCM BAKOZI JUMA MWAPACHU ATOA MPYA..ADAI HATA NYERERE ANGEKUWEPO ANGEJITOA CCM
Siku moja baada ya kutangaza kujitoa CCM, kada mkongwe wa chama hicho,
Balozi Juma Mwapachu amesema uamuzi alioufanya ni sahihi ambao hata Baba
wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere angekuwa hai angeufanya kwa sasa.
Balozi Mwapachu alieleza hayo jana katika mahojiano maalumu na kuongeza kuwa chama chake cha zamani kimepoteza mwelekeo kwa kuwa kinara wa kuvunja katiba na taratibu kitendo ambacho Nyerere alikichukia katika maisha yake.
Alisema anafahamu fika kuna watu watakosoa uamuzi wake huo lakini hatababaishwa na maneno yao na atasimamia msimamo wake huo huku akieleza kuwa anajisikia amani kujitoa katika siku ya kumbukumbu ya miaka 16 ya kifo cha Nyerere.
Mwapachu alitangaza kujitoa CCM juzi akisema kilivunja taratibu wakati wa mchakato wa uteuzi wa mgombea wa urais uliofanyika Julai ambao Dk John Magufuli alichaguliwa.
“Nimefanya makusudi kujitoa wakati huu kwa sababu hata Nyerere mwenye angekuwapo hai leo hii angefanya uamuzi kama niliofanya. Hata yeye alikuwa ameshachoshwa na chama chake kwa uvunjaji wa kanuni, taratibu na katiba na alikwishaona kuwa kinaanza kupitwa na wakati.”
Alisema mengine yanayojitokeza kwa sasa ndani ya CCM yanaonyesha bayana kuwa chama hicho hakiendi na wakati na kilijisahau na kuendesha mambo kama kipo kwenye mfumo wa chama kimoja wakati ni wa vyama vingi.
Alisema CCM ya sasa siyo ile aliyojiunga nayo akiwa chuo kikuu, ndiyo maana amejitoa kutokana na kutekwa na watu wachache ambao humpiga vita mtu ambaye si mwenzao.
Balozi Mwapachu alieleza hayo jana katika mahojiano maalumu na kuongeza kuwa chama chake cha zamani kimepoteza mwelekeo kwa kuwa kinara wa kuvunja katiba na taratibu kitendo ambacho Nyerere alikichukia katika maisha yake.
Alisema anafahamu fika kuna watu watakosoa uamuzi wake huo lakini hatababaishwa na maneno yao na atasimamia msimamo wake huo huku akieleza kuwa anajisikia amani kujitoa katika siku ya kumbukumbu ya miaka 16 ya kifo cha Nyerere.
Mwapachu alitangaza kujitoa CCM juzi akisema kilivunja taratibu wakati wa mchakato wa uteuzi wa mgombea wa urais uliofanyika Julai ambao Dk John Magufuli alichaguliwa.
“Nimefanya makusudi kujitoa wakati huu kwa sababu hata Nyerere mwenye angekuwapo hai leo hii angefanya uamuzi kama niliofanya. Hata yeye alikuwa ameshachoshwa na chama chake kwa uvunjaji wa kanuni, taratibu na katiba na alikwishaona kuwa kinaanza kupitwa na wakati.”
Alisema mengine yanayojitokeza kwa sasa ndani ya CCM yanaonyesha bayana kuwa chama hicho hakiendi na wakati na kilijisahau na kuendesha mambo kama kipo kwenye mfumo wa chama kimoja wakati ni wa vyama vingi.
Alisema CCM ya sasa siyo ile aliyojiunga nayo akiwa chuo kikuu, ndiyo maana amejitoa kutokana na kutekwa na watu wachache ambao humpiga vita mtu ambaye si mwenzao.
LULU, WEMA WAFIKA PABAYA..KISA UHUSIANO NA DAIMOND ..
Pamoja na wenyewe kudai hawajui kilichotokea, mastaa wawili wenye
sura za mauzo kunako sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Wema
Isaac Sepetu, kwa sasa wanadaiwa kufikia pabaya kufuatia bifu zito
linalofukuta kati yao.
Habari za mjini zinadai kwamba, Wema amekuwa akishtushwa na kuchukizwa na kitendo cha Lulu kuwa upande wa aliyewahi kuwa mwandani wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kiasi cha kwenda nyumbani kwake, Madale-Tegeta jijini Dar, usiku wa manane na kujiachia na jamaa huyo anavyotaka.
“Kama mtakumbuka, kabla ya kifo cha Kanumba (Steven), Wema na Lulu walikuwa ni mashosti kama ilivyokuwa kwa Wema na Snura (Mushi) au Wema na Kajala (Masanja) au Wema na Aunt (Ezekiel).
“Lakini baada ya jamaa (Kanumba) kuondoka na kisa kizima cha Lulu ndipo Wema akavunja urafiki na Lulu kwa sababu Kanumba aliwahi kuwa ‘mtu’ wa Wema kama ilivyo kwa Diamond.
“Ulipita ukimya wa muda mrefu bila Wema na Lulu kuwa mashosti zaidi ya salamu.
“Lakini mambo yalianza tena kuwa mabaya baada ya Lulu kumponda Wema alipokuwa akigombea Ubunge wa Viti Maalum kupitia CCM (Chama Cha Mapinduzi).
“Sasa hivi ishu ni kitendo cha Lulu kujiachia na Diamond kwenye birthday ya Rome Jones (binamu na DJ wa Diamond) kisha ile pati ya birthday Diamond kuifanyia nyumbani kwake huku (Lulu) akitupia picha za mafumbo yaliyoelekezwa kwa Wema.
“Hicho ndicho kinachoendelea na unaambiwa hali ni tete mno,” kilisema chanzo hicho ambacho ni mtu wa karibu wa mastaa hao.
Baada ya kupata ‘ubuyu’ kamili, Amani lilimtafuta Wema na kummwagia data ambapo alionesha kushtushwa na kudai kwamba hata yeye anashangaa ni nini kimetokea.
Kwa upande wake Lulu hakupatikana hewani lakini kwa mujibu wa mahojiano aliyofanya hivi karibuni juu ya uhusiano wake na Wema, mwanadada huyo alikiri kuwa rafiki wa Wema kitambo hicho lakini akasema hajui ni nini kilichotokea zaidi ya kwamba huwa wanasalimiana tu wanapokutana.
Kabla ya mambo kwenda mrama, Lulu na Wema walikuwa mashosti wakubwa ambapo gazeti hili liliwahi kuwashuhudia wakiwa lokeshi na kulala pamoja chumba kimoja kama mtu na dada au mtu na mdogo wake.
Chanzo: GPL
Habari za mjini zinadai kwamba, Wema amekuwa akishtushwa na kuchukizwa na kitendo cha Lulu kuwa upande wa aliyewahi kuwa mwandani wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kiasi cha kwenda nyumbani kwake, Madale-Tegeta jijini Dar, usiku wa manane na kujiachia na jamaa huyo anavyotaka.
“Kama mtakumbuka, kabla ya kifo cha Kanumba (Steven), Wema na Lulu walikuwa ni mashosti kama ilivyokuwa kwa Wema na Snura (Mushi) au Wema na Kajala (Masanja) au Wema na Aunt (Ezekiel).
“Lakini baada ya jamaa (Kanumba) kuondoka na kisa kizima cha Lulu ndipo Wema akavunja urafiki na Lulu kwa sababu Kanumba aliwahi kuwa ‘mtu’ wa Wema kama ilivyo kwa Diamond.
“Ulipita ukimya wa muda mrefu bila Wema na Lulu kuwa mashosti zaidi ya salamu.
“Lakini mambo yalianza tena kuwa mabaya baada ya Lulu kumponda Wema alipokuwa akigombea Ubunge wa Viti Maalum kupitia CCM (Chama Cha Mapinduzi).
“Sasa hivi ishu ni kitendo cha Lulu kujiachia na Diamond kwenye birthday ya Rome Jones (binamu na DJ wa Diamond) kisha ile pati ya birthday Diamond kuifanyia nyumbani kwake huku (Lulu) akitupia picha za mafumbo yaliyoelekezwa kwa Wema.
“Hicho ndicho kinachoendelea na unaambiwa hali ni tete mno,” kilisema chanzo hicho ambacho ni mtu wa karibu wa mastaa hao.
Baada ya kupata ‘ubuyu’ kamili, Amani lilimtafuta Wema na kummwagia data ambapo alionesha kushtushwa na kudai kwamba hata yeye anashangaa ni nini kimetokea.
Kwa upande wake Lulu hakupatikana hewani lakini kwa mujibu wa mahojiano aliyofanya hivi karibuni juu ya uhusiano wake na Wema, mwanadada huyo alikiri kuwa rafiki wa Wema kitambo hicho lakini akasema hajui ni nini kilichotokea zaidi ya kwamba huwa wanasalimiana tu wanapokutana.
Kabla ya mambo kwenda mrama, Lulu na Wema walikuwa mashosti wakubwa ambapo gazeti hili liliwahi kuwashuhudia wakiwa lokeshi na kulala pamoja chumba kimoja kama mtu na dada au mtu na mdogo wake.
Chanzo: GPL
HABARI KUHUSU HELIKOPTA YA CCM ILIYOANGUKA MBUGANI IKIWA NA MBUNGE DEO FILIKUNJOMBE
Usiku wa kuamkia leo October 16 2015 majukwaa ya siasa Tanzania
yametawaliwa na ajali ya Helikopta ambayo imeanguka na kulipuka kwenye
mbuga ya Wanyama ya Selous ambapo Waziri wa maliasili na utalii Lazaro
Nyalandu alithibitisha kwamba mmoja wa waliokuwemo ndani ni Mbunge wa
Ludewa Deo Filikunjombe (CCM).
Kupitia ukurasa wake wa Twitter,Nyalandu aliandika;
"Tumetuma vikosi vya maafisa na maaskari katika eneo la Selous kulikotokea ajali ya helikopta katika harakati za uokozi, ajali ya helikopta imetokea katika kitalu R3 ndani ya mbuga ya Selous na mashuhuda wanasema ilianguka na kulipuka ng’ambo ya mto Ruaha
"Mashuhuda wa ajali ya helikopta iliyotokea Selous walikuwa kitalu R2 na walishuhudia ikianguka na kulipuka ng’ambo ya mto Ruaha Kitalu R3, Maafisa na Maaskari wanaelekea eneo la tukio kutokea Msolwa na Matambwe na tumeagiza vikosi vilivyo kwenye doria Selous kushiriki uokoaji
"Mashuhuda wa ajali ya helikopta Selous walikuwa Kitalu R2 wanasema ilianguka baada ya majira ya saa 12 jioni na kulipuka, serikali kupitia wizara ya maliasili na utalii inachukua hatua zote kuwafikia wahanga na majeruhi wa ajali ya helikopta Selous usiku huu
"Nimeagiza section 2 zenye askari 16 kutoka Matambwe na Msolwa (Selous) kwenda eneo la tukio, RPC Morogoro na mkuu kanda ya Msolwa (Selous) wanashirikiana, hatujui kitakachokuwa kimewapata wasafiri ndani ya helikopta iliyoanguka akiwepo Mh, Filikunjombe, tuungane kuwaombea kwa Mungu"
Katika taarifa nyingine kutoka upande wa CCM iliyotolewa na naibu waziri wa mawasiliano sayansi na teknolojia January Makamba mida ya saa sita usiku ilisema: "Tumesikia habari za chopa kuanguka huko Selous. Mungu aepushe kusiwe na majeruhi. Chopa zote zinazotumiwa na CCM kwenye kampeni ziko salama"
Baadae aliandika :"Kwakuwa ilisemekana kuwa chopa ya kampeni ya CCM imeanguka, tulifuatilia/kubaini/kuripoti kuwa tulizokodi kama Chama hakuna iliyoanguka". Hiyo ndio ilikua tweet ya mwisho kuandikwa na January Makamba usiku lakini badae aliretweet kilichoandikwa na Waziri Nyalandu na Zitto Kabwe.
Zitto aliandika: "Naomba utulivu.(1) ajali ya helkopta imethibitishwa (2) kuwaka hakujathibitishwa (3) ndugu yangu Deo alikuwamo (4) hakuna uthibitisho wa madhara, naomba utulivu mpaka tupate taarifa rasmi zilizothibitishwa na mamlaka husika, naomba sana hilo ili kuepuka sintofahamu"
Kupitia ukurasa wake wa Twitter,Nyalandu aliandika;
"Tumetuma vikosi vya maafisa na maaskari katika eneo la Selous kulikotokea ajali ya helikopta katika harakati za uokozi, ajali ya helikopta imetokea katika kitalu R3 ndani ya mbuga ya Selous na mashuhuda wanasema ilianguka na kulipuka ng’ambo ya mto Ruaha
"Mashuhuda wa ajali ya helikopta iliyotokea Selous walikuwa kitalu R2 na walishuhudia ikianguka na kulipuka ng’ambo ya mto Ruaha Kitalu R3, Maafisa na Maaskari wanaelekea eneo la tukio kutokea Msolwa na Matambwe na tumeagiza vikosi vilivyo kwenye doria Selous kushiriki uokoaji
"Mashuhuda wa ajali ya helikopta Selous walikuwa Kitalu R2 wanasema ilianguka baada ya majira ya saa 12 jioni na kulipuka, serikali kupitia wizara ya maliasili na utalii inachukua hatua zote kuwafikia wahanga na majeruhi wa ajali ya helikopta Selous usiku huu
"Nimeagiza section 2 zenye askari 16 kutoka Matambwe na Msolwa (Selous) kwenda eneo la tukio, RPC Morogoro na mkuu kanda ya Msolwa (Selous) wanashirikiana, hatujui kitakachokuwa kimewapata wasafiri ndani ya helikopta iliyoanguka akiwepo Mh, Filikunjombe, tuungane kuwaombea kwa Mungu"
Katika taarifa nyingine kutoka upande wa CCM iliyotolewa na naibu waziri wa mawasiliano sayansi na teknolojia January Makamba mida ya saa sita usiku ilisema: "Tumesikia habari za chopa kuanguka huko Selous. Mungu aepushe kusiwe na majeruhi. Chopa zote zinazotumiwa na CCM kwenye kampeni ziko salama"
Baadae aliandika :"Kwakuwa ilisemekana kuwa chopa ya kampeni ya CCM imeanguka, tulifuatilia/kubaini/kuripoti kuwa tulizokodi kama Chama hakuna iliyoanguka". Hiyo ndio ilikua tweet ya mwisho kuandikwa na January Makamba usiku lakini badae aliretweet kilichoandikwa na Waziri Nyalandu na Zitto Kabwe.
Zitto aliandika: "Naomba utulivu.(1) ajali ya helkopta imethibitishwa (2) kuwaka hakujathibitishwa (3) ndugu yangu Deo alikuwamo (4) hakuna uthibitisho wa madhara, naomba utulivu mpaka tupate taarifa rasmi zilizothibitishwa na mamlaka husika, naomba sana hilo ili kuepuka sintofahamu"