Jumamosi, 4 Oktoba 2014

Wanajeshi 9 wa Umoja wa Mataifa wauawa

 
Mwanajeshi wa Umoja wa Matifa mali 

Ujumbe wa Umoja wa mataifa nchini Mali unasema kuwa watu waliokuwa na silaha ambao walikuwa wakitumia pikipiki wamewaua walinda amani tisa wa Umoja wa Mataifa kaskazini mashariki mwa taifa hilo.
Uvamizi huo ndio mbaya zaidi kuwai kuwakumba wanajeshi hao wa Umoja wa Mataifa
Wanajeshi hao kutoka nchini Niger walikuwa wakisafiri kati ya miji ya Menaka na Ansongo wakati walipovamiwa.
Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa amesikitishwa na kile alichokitaja kuwa vitendo vya kigaidi.
Mwandishi wa BB nchini Mali amesema kuwa kikosi hicho cha umoja wa mataifa kimelalamika kuhusu vifaa duni inavyomiliki.
Walindamani hao walitumwa miaka miwili iliyopita baada ya makundi ya wanamgambo wa kiislamu kuchukua udhibiti wa maeneo ya kaskazini mwa Mali.

Mtoto wa kizazi cha 'msaada' azaliwa

 
Womb Transplant baby 

Mwanamke mmoja nchini Sweden amejifungua mtoto kutokana na kizazi alichowekewa kupitia upasuaji.
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 36 alizaliwa bila kizazi kabla ya kuwekewa kizazi cha mwanamke aliyekuwa katika miaka yake ya sitini.
Jarida la afya la Uingereza ,the Lancet linasema kuwa mtoto huyo alizaliwa kabla ya mda wake kufika mnamo mwezi Septemba akiwa na uziti wa kilo1.8.
Babaake amesema mwanawe ni wa kushangaza.
Matibabu ya ugonjwa wa saratani pamoja na kasoro za mazazi ndio sababu kuu zinazosababisha wanawake kuwa na kizazi kibaya.
Iwapo wanataka kujipatia mtoto basi hulazimika kutumia mwanamke mwengine anayebeba mimba hiyo kwa niaba yake.
Ijapokuwa wazazi wa mtoto huyo hawajatambuliwa ,inaaminika kuwa mwanamke huyo alikuwa na mbegu zilizokuwa zikifanya kazi.
Kulingana na baba ya mtoto huyo ,mwanawe hana tofauti yoyote na watoto wengine.

Je Amisi Tambwe atacheza leo! Simba watoa majibu hapa

IMG_7718.JPG
MSHAMBULIAJI wa Simba SC, Amisi
Tambwe juzi alizua hofu kwa kocha
Patrick Phiri na rais wa klabu hiyo,
Evans Aveva baada ya kuumia
mazoezi Uwanja wa Boko ,
Dar es Salaam.

Tambwe aliumia goti baada ya
kugongana na beki Abdi Banda na
kushindwa kuendelea na mazoezi hadi
akafungwa barafu baada ya kutibiwa
kwa muda na Dk Yassin Gembe.
Kocha Phiri alionekana mwenye
wasiwasi na kufuatilia kwa karibu hali
ya mchezaji huyo wakati akitoka nje. “Hakikisha anakuwa vizuri, ni
mchezaji wangu ninayemtegemea,”alisema Phiri
kumuambia Dk Gembe wakati anatoka
nje na mchezaji huyo.

Lakini sasa yakiwa yamebaki masaa kadhaa kabla ya mchezo wa Simba dhidi ya Stand United, mshambuliaji huyo aliyekuwa mfungaji bora msimu uliopita amethibitishwa kuwa fiti kuivaa timu hiyo ya Stand ambayo imepanda daraja msimu huu.
Tambwe anaweza kuanza leo kwenye safu ya ushambuliaji kwa pamoja na Emannuel Okwi.
Wakati huo huo kiungo Jonas Mkude amerejea kwenye timu baada ya kuandamwa na majeruhi kwa muda kiasi.

Ijumaa, 3 Oktoba 2014

MICROSOFT YAZINDUA WINDOWS 10


Kampuni ya Microsoft imezindua programu mpya ya Windows 10 ambayo imeipiku Windows 9.
Kampuni hiyo pia inatarajia wateja wake watarudi kwani wengi walikuwa wakisitasita kuboresha oparesheni zao tangu Windows 8.
Windows 10 itaingiliana na vifaa vingi hususan kutokana na uwezo wake wa kubadilisha ukubwa wa programu yake.

Usafiri wa treni kuboresha uchumi TZ?

Haba na Haba inaangazia hali ya usafiri wa treni nchini Tanzania. Kwa kuwa mwelekeo uliopo katika sekta ya uchukuzi kwa sasa ni kuhakikisha kuwa mizigo mizito na mingi inayosafirishwa umbali mrefu inatumia usafiri wa reli. Je uboreshwaji wa usafiri wa treni unawezaje kuboresha uchumi na maisha ya mtanzania?

Picha 3 za jinsi Waziri mkuu wa Uganda alivyonyang’anywa ulinzi nyumbani baada ya kutimuliwa kazi.

ug1 
Jana ndio Waziri mkuu mpya wa Uganda Ruhakana Rugunda kaapishwa ila kabla yake alikua ni Amama Mbabazi ambae alifutwa kazi wiki kadhaa zilizopita baada ya kukaa madarakani toka May 2011 akitokea kwenye Uwaziri wa Ulinzi.
September 18 2014 ndio Rais Museveni alimuandikia Spika wa bunge barua kumuarifu kuwa ameamua kumuondoa waziri mkuu huyo na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekua Waziri wa Afya ambae kwa sasa ana umri wa miaka 67.
ug2 
Kwa mujibu wa ripota wa TZA (youngluvega.blogspot.com ) waziri huyu alietimuliwa alikua Waziri mkuu wa nne toka Rais Museveni aanze kuitawala nchi hiyo January 1986 ambapo mpaka sasa amewahi kuwa na Makamu wa Rais wanaofikia wanne.
Picha zote hizi zinaonyesha wakati Serikali ya Uganda ilipomnyang’anya ulinzi wa Wanajeshi waziri huyu mkuu baada ya kufutwa kazi ambapo kwenye hii picha ya chini anaeonekana ni mke wake akilalamika kwa kutoamini kilichotokea kwani mume wake na Rais Museveni wamekua marafiki wakubwa.
Vyombo mbalimbali vya habari vimeripoti kwamba kuna mambo mengi yaliyosababisha kufutwa kazi kwa waziri huyu mkuu lakini mambo hayo hayajawekwa wazi.
ug3
Nyuma hii unayoiona ni nyumba anayoishi na inayomilikiwa na Waziri huyu mkuu aliefutwa kazi.

Kinshasa:Chimbuko la virusi vya HIV

Kinshasa mwaka 1955, janga la HIV lilikuwa linatesa mjini humu na kote nchini DRC hasa mkoa wa Katanga 
Ugonjwa wa ukimwi uligunduliwa miaka ya 1920 mjini Kinshasa, nchini Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo. Wanasayansi wameeleza.
Wanasayansi wa kimataifa wanasema ongezeko la watu,vitendo vya kukutana kimwili na shughuli za usafirishaji kwa njia ya reli zilifanya virusi vya ukimwi kuenea.
Ripoti inasema kuwa biashara ya ngono, ongezeko kubwa la watu na vitu vyenye ncha kali kama sindano kwenye zahanati huenda kulichangia kusambaa kwa ugonjwa huo DRC.
Wakati huo huo reli ilikuwa ina watu takriban milioni moja waliokuwa wakiingia na kutoka kwa wingi jijini Kinshasa kwa mwaka,wakisambaza virusi kwenda kwenye miji mingine.
Takriban watu milioni moja walikua wakitumia reli ya Kinshasa mwishoni mwa mwaka 1940.
Virusi vilisambaa kwa kiasi kikubwa, mpaka nchi jirani ya Congo Brazzaville na katika maeneo ya migodi, katika jimbo la Katanga.
 
Inaarifiwa virusi vya HIV ni sawa na virusi vya Sinium vinavyopatikana katika Sokwe  
Ukimwi ulitambulika kuwa janga kimataifa mwaka 1980 na uliathiri takriban watu milioni 75.
Ugonjwa huu una historia ndefu barani Afrika , lakini ulipotokea ugonjwa huu bado ni mjadala mrefu.
Timu ya wanasayansi kutoka chuo cha Oxford na chuo cha Leuven, nchini ubelgiji walitafiti chanzo cha ugonjwa wa ukimwi wakisema kuwa ulianzia kwa Sokwe.
Virusi vya HIV ni sawa na virusi vinavyopatikana kwa Sokwe ambavyo vinajulilkana kama Simian ambavyo vinadhaniwa vilitoka kwa Sokwe na kuambukizwa binadamu kupitia kwa damu wakati wakitafuta nyama ya wanyamapori.
Virusi hivyo vilikuwa na muundo tofauti na muundo huo ulikuwa unabadilika kila wakati. Virusi vya kwanza viliwaathiri maelfu ya watu nchini Cameroon.
Virusi vilisambaa kwa kiasi kikubwa, mpaka nchi jirani ya Congo Brazzaville na katika maeneo ya migodi, katika jimbo la Katanga.

Vurusi vya HIV 

Idadi kubwa ya wanaume waliokuwa wanafanya kazi mijini na idadi ya wanaume ndio ilikuwa kubwa kuliko wanawake na hivyo biashara ya ngono ikawa kubwa sana.
Mmoja wa watafiti Profesa Pybus anasema kuwa mambo mawili yanesaidia kupunguza maambukizi. Kwanza hamasisho la serikali kuwatibu wagonjwa kwa maradhi tegemezi.
Jambo la pili ingekuwa mfumo wa usafiri ambao uliwawezesha watu kusafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine huku ugonjwa ukienezwa zaidi.
Takriban watu milioni moja walikua wakitumia reli ya Kinshasa mwishoni mwa mwaka 1940.
Virusi vielendelera kuenezwa kwa nchi jirani ya Brazzaville na mkoa wenye madini wa Katanga ambao ulikuwa kitovu cha ugonjwa huo.
Virusi havikukomea tu nchini Congo bali vilianza kuenezwa kote duniani

Picha za palikofanyika birthday party ya Diamond… kabla watu hawajaingia

D 2 
Party ilifanyika Golden Jubilee Towers Dar es salaam ambapo kama hujaona pichaz za kilivyohappen unaweza kuchek post iliyotangulia kabla ya hii kwenye hii siku kubwa ya Diamond aliyotimiza miaka 25 ya kuzaliwa.
D 3
D 4
Screen Shot 2014-10-03 at 12.28.18 PM
Screen Shot 2014-10-03 at 12.28.11 PM
d 5

Mambo 10 aliyoyasema Madee kuhusu ishu yake ya kuwekwa Polisi.

Screen Shot 2014-10-03 at 12.07.41 PM 
Madee alikamatwa na Polisi saa kadhaa zilizopita baada ya tukio la yeye kuibiwa simu akiwa kwenye gari tena likitembea ambapo waliohusika ni watu wawili wakiwa kwenye pikipiki saa tisa usiku akitoka Kigamboni Dar es alaam kufanya show hivyo akawa anavuka bahari ili aelekee nyumbani.
Baada ya kuchoropoa hiyo simu jamaa wa pikipiki walianza kukimbia hivyo na dereva wa Madee akaanza kukimbizana nao na kufanikiwa kuwagonga alafu pikipiki ikaanguka ila jamaa wa nyuma aliechoropoa simu akafanikiwa kukimbia ila yule aliekua anaendesha wakambeba na kwenda nae maskani Tiptop kwa lengo la kumuhoji ili wampate aliekimbia na simu.
Madee 1
Hii ni wakati Madee alipofatwa na kukamatwa na Polisi mtaani kuhusu hii kesi, aliandikwa kwenye page yake ya insta ‘hivi niliua au niliibiwa simu?’ (picha imepigwa na globalpublishers.info)
Kilichomfanya Madee akamatwe na kuwekwa Polisi ni madai yake kwamba kesi hiyo imegeuzwa na sasa yeye ndio anaonekana mwenye makosa kwa kumteka huyu jamaa waliekwenda nae Tiptop Manzese.
Haya ndio mambo 10 anayoyasema Madee.
1. Nilikaa Polisi kwa zaidi ya saa 32, nililala na kuamkia huko.
2. Kule ndani haupo huru ndio maana kuna mateso, unapangiwa muda wa kulala na hautakiwi kuongea kwa sauti kubwa… mle ndani watu wanatolewa njee saa moja usiku tunahesabiwa pale nje alafu mkishaingizwa ndani kimyaaaa.
3. Kwenye room niliyoshikiliwa nilikua na watu kama 30 hivi ila sijui kwenye room nyigine ya pili sijui kulikua na watu wangapi sababu sikuingia.
4. Nilianza kushangiliwa nilipotokeza tu pale kwa juu wakati naingizwa machizi waliponiona mimi wakaanza kuimba ule wimbo wangu wa ‘majuto ni mjukuu‘ niliozungumzia ishu za Polisi.
5. Nilivyofika kule nilikuta kumejaa ila kumbe kuna sehemu tayari nilishawekewa na machizi sehemu poa tu upepo unaingia fresh tu sema ndio hivyo mazoea mazoea tu huwezi kulala….
Hii picha Madee aliipiga na kuiweka instagram muda mfupi baada ya kuachiwa kwa dhamana na kuandika 'Am Freeeeeee' akimaanisha yuko huru
Hii picha Madee aliipiga na kuiweka instagram muda mfupi baada ya kuachiwa kwa dhamana na kuandika ‘Am Freeeeeee’ akimaanisha yuko huru
6. Mle ndani hakuna vitanda zaidi ya sakafu tu nilitamani hata nijaribu kupeleka maombi niwapelekee machizi mikeka kidogo wawe wanalalia.
7. Nilisimamishwa Mahakamani September 25 kwa mara ya kwanza sababu jamaa wamejaribu kutengeneza vitu vingine viwili tofauti na ilivyokua, wanasema mimi nimemteka mtu na pikipiki yake nikaenda kumjeruhi na washkaji zangu ila ukweli ni kwamba huyu jamaa alikua na rafiki yake kwenye pikipiki wakanipora simu yangu wakati nikiwa nimekaa kwenye gari.
8. Baada ya hapo dereva wangu mtundu akakimbia akaiblock pikipiki na kuigonga wakaanguka lakini yule aliekua amechukua simu akakimbia ila aliekua anaendesha tukamkamata tukampakiza kwenye gari na kuondoka nae mpaka maskani ya Tiptop ila nikampigia simu mama yake nikamwambia mwanao yuko hapa njoo uongee nae aturudishie simu yetu.
9. Mama yake alikuja akaondoka na kusema anakwenda kumtafuta aliechukua simu lakini cha kushangaza Mama asubuhi akaja na Polisi wakamchukua jamaa na kumpeleka Magomeni wakati huo mi nilikua nimekwenda Mwanza kwenye show.
10. Niliporudi kutoka Mwanza nikakimbilia Polisi Magomeni kwenda kuulizia napataje haki yangu nikaambiwa hili shauri linahamishiwa Kigamboni, nilipokwenda Kigamboni Polisi nikakuta hiyo kesi kwamba Madee kamteka mtu nikawekwa ndani, hii ni kama mara yangu ya nne au ya tatu nawekwa Polisi…. hizo nyingine zilishatokea zamani ambapo ya mwisho ilikua miaka sita au saba nyuma, hii kesi ya sasa ipo Mahakamani.

USAJILI WA KUDUMU FALCAO MANCHESTER UNITED HABARI KAMILI HII HAPA

1412288001100_wps_42_Manchester_United_4_v_QPRWakati mkataba wake wa mkopo ukiwa umebakisha miezi nane kuisha, usajili Radamel Falcao kwenda Manchester United umechukua nafasi kwenye vyombo vya habari.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Uingereza ni kwamba Man United imekubaliana rasmi mahitaji binafsi na mchezaji huyo kwa ajili ya kukamilisha usajili wa kudumu wa mchezaji huyo wa Colombia.
Taarifa zinaeleza kwamba Man United wanafanya jitihada zote kumaliza suala la usajili wa Falcao ili kuepuka kila kilichotokea miaka mitano iliyopita katika usajili wa Carlos Tevez.
United walimsajili Falcao kwa mkopo kutoka Monaco siku ya mwisho ya usajili wa wakati wa kiangazi.
Wakiwa tayari wameshalipa ada ya mkopo wa £6million kwa klabu ya Ufaransa, United pia walishakubaliana kimsingi na Monaco kuwalipa kiasi cha £43.5m ikiwa wataamua kumchukua Falcao kiujumla mwishoni mwa msimu.
Leo sasa imeripotiwa kwamba mkurugenzi mkuu wa United Ed Woodward tayari amekubaliana na wawakilishi wa Falcao kumlipa mshahara wa £250,000 kwa wiki mchezaji huyo pamoja, bonasi na haki za taswira yake.
Manchester United pia imekanusha taarifa kwamba itakatisha mkataba wa mkopo wa Falcao ikiwa mchezaji huyo ataumia tena goti.

HII NI KUHUSU WANAJESHI KUPIGANA NA POLISI TARIME JUZI, WANGAPI WAMEUMIA? KISA?

Risasi 
Hii ni taarifa kutoka Tarime mkoani Mara ambako watu 12 wamejeruhiwa wakati wa mashambulizi ya kurushiana risasi kati ya askari wa JWTZ kituo cha Nyandoto na polisi wa kituo cha stendi.
Kwa mujibu wa magazeti ya Nipashe na Mwanachi leo, hii ishu ilitokea wakati Wanajeshi hao walipokua wakijaribu kumchukua Mwanajeshi mwenzao aliyekamwatwa na polisi hao kwa kosa la kuendesha pikipiki bila kuvaa kofia (Helmet).
Mashambuliazi hayo ya kurushiana risasi na kupigana ngumi na mateke yalitokea juzi jioni katika kituo hicho cha stendi ambapo Mganga Mfawidhi Hospitali ya Tarime alithibitisha kupokea majeruhi 12 na kati yao wawili ni askari wa JWTZ, Polisi saba na raia watatu.
Kamanda wa Polisi Tarime alisema Mwanajeshi huyo licha ya kukiuka taratibu za barabarani aliwatolea lugha za matusi polisi hao jambo lililowalazimu kumkamata kwa nguvu na wanajeshi wenzake kuingilia kati na kusababisha vurugu.
Alisema Wanajeshi watatu ambao hawakutajwa majina wameshikiliwa na polisi kwa kuvunja utaratibu wa usalama huku Mkuu wa Wilaya hiyo John Henjewele akilaani kitendo hicho cha kurushiana risasi za moto hewani na kusema ni cha utovu wa nidhamu na kilikwamisha shughuli za watu kwa muda sababu ya kuhofia usalama wao.

Jumatano, 1 Oktoba 2014

Tangazo la biashara lazua zogo China

 
Polisi wanachunguza ikiwa kampuni hiyo ilivunja sheria ya matangazo ya biashara 

Kampuni moja nchini China inakabiliwa na tisho la kutozwa kiwango kikubwa cha faini kwa kuwakodi wanawake kuvua nguo zao kwenye treni mjini Shanghai kwa lengo la kutangaza biashara ya kampuni hiyo kwa abiria.
Katika moja ya video iliyowekwa kwenye mtandao wiki jana, wasichana wawili ghafla walianza kuvua nguo zao na kusalia na nguo za ndani pekee katika treni hiyo iliyokuwa imejaa watu.
Abiria walionekana wakirekodi wasichana hao kwa simu zao za viganjani lakini mwanamke mmoja wa makamo aliwakaripia sana.
Mwanamume mmoja kutoka katika kampuni ya huduma za dobi ambayo wasiahana hao walikuwa wakiitangaza, naye alionekana akiokota nguo za wasichana hao walizokua wanavua.
Baada ya filamu ya wasichana hao wakivua nguo kuenea mitandaoni, polisi waliwasiliana na kampuni hiyo kujibu walichokuwa wanakifanya.
Kampuni hiyo inayotoa huduma za dobi ,kwa jina 'Tidy Laundry', ilipoona ikipata sifa mbaya, iliamua kuomba radhi kwa kosa hilo ikisema kuwa ilinuia tu kutangaza huduma zake kwa wabiria waliokuwa ndani ya treni hiyo.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa jarida la Shanghai Daily.
Wamiliki wa kampuni hiyo, wanasema kila aliyehusika kwenye tukio hilo alikuwa muigizaji aliyekuwa amekodiwa.
Hata hivyo huu bila shaka sio mwisho wa masaibu ya kampuni hiyo-polisi wanasema wanachunguza ikiwa ilivunja sheria zinazopiga marufuku matangazo ya kibiasga ambayo yanakera jamii.

AL-SHABAAB WAPATA PIGO SOMALIA

 
Wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab 

Wanajeshi nchini Somali wameidhibiti milima ya Galgala kutoka kwa wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab,kulingana na utawala wa eneo hilo.
Wanamgambo hao walikuwa wakiidhibiti milima hiyo ya Kaskazini mwa taifa hilo kwa miaka kadhaa.
Waziri wa habari wa Puntland amesema kuwa kamanda wa Alshabaab katika eneo hilo alisalimu amri miezi minne iliopita.
Kundi hilo linaloshirikiana na lile la Al-Qaeda lina makao yake makuu kusini na katikati mwa somalia ambapo vikosi vya Umoja wa Afrika vinafanya mashambulizi.
Abdiweli Hirsi Abdille,ambaye ni waziri wa habari wa jimbo la kaskazini mashariki mwa Somalia Puntland amesema kuwa vikosi vya serikali vimeliteka jimbo hilo la Glagala katika mashambulizi yaliotekelezwa alfajiri.
Hatahivyo hakutoa maelezo yoyote kuhusu wafungwa ama waliojeruhiwa.
Lakini kituo cha redio cha Al Furqan,kinachojulikana kwa kuwapendelea wapiganaji wa Al-Shabaab kimeripoti kwamba magari mawili ya kijeshi yaliharibiwa na wanajeshi 16 kuuawa.
Galgala ni eneo la kipekee la Puntland ambalo limekuwa chini ya udhibiti wa Alshabaab.
Kamanda wa Al-Shabaab katika eneo hilo Said Atom alijiunga na vikosi vya serikali mwaka huu na kuwawacha wapiganaji wake katika jimbo la Puntland.
Wapiganaji wa Al-Shabaab wamefurushwa kutoka miji mikuu katika kipindi cha miaka ya hivi karibuni ,lakini bado wanadhibiti miji midogo katika maeneo ya mashambani.

UCL: PSG walivyoivunja rekodi ya Barcelona msimu huu – Beyonce na Jay Z wakishuhudia

IMG_7650.PNG
Mwanasoka wa kibrazil David Luiz jana usiku alikuwa mchezaji wa kwanza kuifunga goli FC Barcelona katika msimu mpya wa soka barani ulaya.
Luiz alifunga goli hilo katika dakika ya 11 ya mchezo wa Champions League kati ya klabu PSG dhidi ya Barca.
Mchezo uliopigwa kwenye dimba la Stade de France na kuhudhuriwa na mastaa kama Rais wa zamani wa nchi hiyo Sarkozy, David Beckham na rapa Jay Z pamoja na mkewe Beyonce.
Matokeo ya mchezo huo ni ushindi wa 3-2 kwa PSG dhidi ya kikosi cha Luis Enrique.
Lionel Messi na Neymar walifunga magoli ya Barca huku Matuidi na Verrati wakihitimisha kipigo hicho cha kwanza cha Barcelona katika
Michuano yote ya msimu huu.

IMG_7651.PNG

UCL: Matokeo ya Man City vs AS Roma na rekodi mpya aliyoiweka Totti

IMG_7652.PNG
Mabingwa wa ligi kuu ya Uingereza klabu ya Manchester City imeendelea kutopata matokeo chanya katika michuano ya ligi ya mabingwa wa ulaya kwa mara ya pili mfululizo msimu huu.

Wakicheza kwenye uwanja wao wa Etihad dhidi ya AS Roma ya Serie A, Sergio Aguero aliipatia timu yake goli katika dakika ya 4 kupitia mkwaju wa penati.
Lakini dakika 19 baadae Francisco Totti ‘Mfalme wa Roma’ akaifungia goli la kusawazisha Roma na kuandika historia ya mchezaji mwenye umri mkubwa zaidi kufunga goli kwenye michuano ya ulaya.
Man City sasa inakuwa imeshindwa kupata matokeo chanya katika mechi 2 za kwanza cha UCL – wiki mbili zilizopita walifungwa na Bayern Munich.
Timu zilipangwa hivi
Manchester City: Hart 7; Zabaleta 6.5, Kompany 6, Demichelis 5.5, Clichy 6; Navas 5 (Milner 46, 6), Toure 5.5, Fernandinho 6, Silva 7; Aguero 6.5 (Jovetic 84), Dzeko 6 (Lampard 57)
Subs (not used): Caballero, Sagna, Kolarov, Mangala
Goals: Aguero (Pen, 4)
Booked: Zabaleta
Roma: Skorupski 6; Maicon 6 (Torosidis, 89), Manolas 6, Yanga-Mbiwa 6.5, Cole 6; Pjanic 7.5, Nainggolan 6.5, Keita 6.5; Florenzi 5.5 (Holebas 83), Totti 7 (Iturbe 72, 6), Gervinho 7.
Subs (not used): Curci, Ljajic, Destro, Paredes
Goals: Totti (23)
Booked: Maicon, Nainggolan
Referee: Bjorn Kuipers (Holland) 7
Star man: Miralem Pjanic
Attendance: 37,509

UCL: Matokeo ya Chelsea vs Sporting Lisbon haya haya

IMG_7653.PNG
Usiku wa jana watu wawili waliowahi kuwa vipenzi vya nchi ya Ureno – Jose Mourinho na Nemanja Matic walirejea nchini humo katika jiji la Lisbon lakini safari hii wakiwa kama wapinzani.
Huku Mourinho akionekana kuchukua ‘attention’ yote ya vyombo vya habari ndani ya jiji Lisbon, Nemanja Matic alikuwa kasahaulika.
Lakini katika dakika ya 34, mchezaji huyo wa zamani wa Benfica aliifungia goli pekee Chelsea katika mchezo huo.
Matic alifunga goli hilo kwa kichwa baada ya kuachwa bila kukabwa vizuri na mabeki wa Sporting Lisbon.
Mchezaji wa zamani wa Manchester United Luis Nani alikuwa akiitumikia Sporting jana na hakuwa kwenye kiwango kizuri katika kipindi cha kwanza – kipindi cha pili alijitahidi lakini akashindwa kubadili matokeo ya mwisho dhidi ya vijana wa Jose Mourinho.
Takwimu na timu zilizopangwa
Sporting (4-3-3): Patricio 7; Cedric 6, Mauricio 5.5 (Oliveira 63, 6), Sarr 5, J.Silva 5; Mario 6, Carvalho 6, A.Silva 6 (Montero 81); Carrillo 6.5 (Capel 81), Slimani 6, Nani 6.
Subs not used: Marcelo, Jefferson, Martins, Rosell.
Bookings: Carvalho, Mario, Cedric, Mauricio
Manager: Marco Silva
Chelsea (4-2-3-1): Courtois 6; Ivanovic 6, Cahill 6, Terry 6, Luis 6.5; Matic 8, Fabregas 7; Schurrle 5 (Willian 57, 6), Oscar 7.5 (Mikel 71, 6), Hazard 7 (Salah 84); Costa 6.
Subs not used: Cech, Zouma, Azpilicueta, Remy.
Bookings: Ivanovic, Hazard, Luis Filipe, Fabregas
Manager: Jose Mourinho.

Amber Rose kaitaja sababu nyingine ya kuachana na Wiz Khalifa, picha ya ushahidi iko hapa pia

Amber1 
Kuvunjika kwa ndoa ya mastaa Amber Rose na Wiz Khalifa kumeendelea kuchukua nafasi kwenye headlines za dunia na hii ni baada ya Amber kutaja chanzo mojawapo cha kuvunjika kwa uhusiano huo.
Kwenye interview ya Radio Amber amesema kingine kilichomkasirisha ni kuona Wiz anawaendekeza warembo flani wawili mapacha ambao inaaminika amekua akijihusisha nao kimapenzi.
Amber amesema alipenda kuiokoa ndoa yake ili waendelee kuwa pamoja lakini anaeonekana kukataa kuendelea kuwa kwenye ndoa ni Wiz mwenyewe, Amber anasema hata taarifa za mwanzoni kwamba walitengana siku nyingi kabla ya kutaka talaka zilikua za uongo…. hakufanya maamuzi yao sababu alitaka kuiokoa ndoa yake.
amber 2
 
Amber amemshutumu Wiz kwa kutoka kimapenzi na hawa mapacha kwenye hii picha hapa chini…
http://i1.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2014/10/amber-3.png