Jumatatu, 8 Desemba 2014

DADA WA KAZI ALIYEMTESA MTOTO UGANDA AOMBA MSAMAHA

Jolly Tumuhirwe
Mfanyakazi wa nyumbani aliyenaswa kwenye kanda ya video akimchapa na kumkanyaga mtoto nchini Uganda, amefikishwa mahakamani leo.
Mfanyakazi huyo Jolly Tumuhirwe aliambia mahakama kuwa anajulia kile alichokifanya na hata kuomba msamaha. Ameshitakiwa kwa kosa la kumtesa mtoto Arnella.
Licha ya taarifa ya polisi kusema Jolly atashitakiwa kwa kosa la jaribio la ,mauaji, kiogozi wa mashitaka alimshitaki Jolly kwa kosa la kumtesa mtoto mdogo.
 Jolly Tumuhirwe ameomba mahakama kumsamehe kwa kumtesa mtoto 

Bi Tumuhirwe alikiri makosa yake na kuomba msamaha. Hakuna wakili yeyote aliyemwakilisha Jolly mahakamani licha ya mmoja wa mawakili mashuhuri kusema angemwakilisha Jolly bila malipo.
Kesi hio imeakhirishwa hadi Jumatano, wakati ambapo hakimu anatarajiwa kutoa hukumu yake dhidi ya Jolly.
Huenda akafungwa jela miaka 15 au kutozwa faini ya dola mianne au adhabu zote mbili.

Nguvu ya Mapenzi itamrudisha Chris Brown kwa Karrueche? Soma alichokiandika @Instagram

chris-brown-and-karrueche
Weekend iliyopita imeisha kwa habari za kuisha kwa penzi la Chris Brown na Karrueche, halafu story kuibwa ya pili ikawa yale madongo ambayo kila mmoja akimtuhumu mwenzake kwamba  ndiye sababu ya mapenzi yao kuisha.
Imekuwa ni kama mchezo wa kuigiza kwa wawili hao kuachana na kurudiana, lakini kupitia ukurasa wake wa Instagram Chris ameandika ujumbe wa kumuomba radhi Karrueche huku akisema hajali watu wanamchukuliaje.
Ujumbe huo unasomeka hivi;Being young and dumb is one of my strong suits and emotional at best. I love hard and react impulsively when I’m hurt at times. I don’t think social media is a place to air out or hash out personal problems and a nigga feel hella WACK for doing it. So I AM APOLOGIZING I live in a glass house and the same sh*t that makes me great also is my curse. Everybody know I love that girl. I don’t care how my image my look to the public because I’m still gonna be the best at what I do. I just want baby girl to know I apologize!
Ujumbe huo umewekwa na picha hii
Karu & cHRIS

TAKWIMU MBAYA KWA ARSENAL.

wenger
Hali ndani ya klabu ya Arsenal imezidi kuwa mbaya baada ya mashabikiw a klabu hiyo kuendelea kushinikiza kuondoka kwa kocha wao Arsene Wenger . Shinikizo hilo liliongezeka mwishoni wa wiki iliyopita wakati Arsenal ilipofungwa na Stoke City kwa matokeo ya 3-2 kwenye uwanja wa Brittania .
Mashabiki wa Arsenal baada ya mchezo huo walichapana Makonde baada ya kutokea mabishano makubwa baina ya makundi mawili ambayo mojawapo lilikuwa linaunga mkono Wenger Kuondoka huku lingine likimtaka kocha huyo aendelee kubaki madarakani.
Wachezaji wa Arsenal wakionesha masikitiko baada ya kufungwa moja kati ya mabao matatu waliyofungwa na Stoke City.
Wachezaji wa Arsenal wakionesha masikitiko baada ya kufungwa moja kati ya mabao matatu waliyofungwa na Stoke City.

Takwimu zinazidi kuwapa sauti wale wanaotaka Wenger aondoke ambapo imefahamika kuwa Arsenal imekuwa ikifungwa baada ya wapinzani wake kupiga shuti la kwanza lililolenga shabaha ya lango katika michezo takribani saba kati ya 15 ambayo Arsenal imecheza. Hadi sasa Arsenal ambayo iko kwenye nafasi ya tano ambaimekusanya pointi 23 baada ya michezo 15 huku ikiwa imeshinda michezo 6 pekee , ikitoka sare kwenye michezo mitano na kupoteza michezo sita .
Arsenal imefungwa mabao saba yaliyotokana na shuti la kwanza katika michezo saba kati ya 15 ya ligi ya England.
Arsenal imefungwa mabao saba yaliyotokana na shuti la kwanza katika michezo saba kati ya 15 ya ligi ya England.
Mabingwa hawa wa kombe la FA wataingia uwanjani hapo kesho kutafuta tiketi ya kufuzu hatua ya 16 kama washindi wa kundi lake watakapokuwa wanacheza na Galatasaray ya Uturuki.