Jumanne, 5 Agosti 2014

Umeipata hii ya Weusi kusemekana wamecopy wimbo?

we
Kupitia You heard ya August 04,Weusi wamesemekana kucopy wimbo na kuurudia kuanzia namna wanavyorap mpaka beat iliyotumika kwenye wimbo huo,Joh Makini kaongea na kapatikana pia producer wa wimbo huo NahReel nae kazungumza.
88.0 Clouds Fm inasikika ukiwa Tabora.
Bonyeza play kusikiliza.

Sina muda kujadili upuuzi huu kuhusu Ridhiwani – Rais Jakaya Kikwete

kikwere
Taarifa kutoka ofisi ya Rais kuhusu maneno yanayosemekana kwamba Rais Jakaya Kikwete kushiriki kusaidia kumwokoa mwanae ambaye ni mbunge wa jimbo la Chalinze Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete baada ya kukwamatwa na dawa za kulevya nchini China.
Hii ni taarifa kutoka ofisi ya Rais yenye maneno ya Rais Jakaya Kikwete.
k1
k2

Magazine yamuomba msamaha 2 Face Idibia baada ya kesi ya Naila milioni 100.

idibiaIcon Weekly magazine walitoa habari kwamba 2 Face Idibia ametoka nje ya ndoa yake na kuanzisha uhusiano na mfanyakazi wa benki. Magazine hiyo haikuishia hapo iliendelea kusema kwamba 2 face amempa ujauzito mwanamke huyo.
Habari hiyo ilimchafua 2 face kwasababu yupo ndani ya ndoa na ndio ilikuwa habari kubwa ya magazine kwa kuwekwa mbele ya cover. Baada ya magazine kutoka 2 face alifungua mashtaka dhidi ya magazine hiyo kwa kudai fidia ya Naila millioni 100.
Baada ya magazine kushindwa kuthibitisha habari hiyo wametumia page moja nzima ya tolea jipya kumuomba msamaha 2 face. Japokuwa Idibia hajajibu hadharani kuhusu msamaha huo, taarifa zinasema kwamba amekubali maombi yao.
e

Yaliyoikuta Yanga Kagame Cup baada ya kupeleka kikosi cha Pili

DSC_0082-1Baada ya jana usiku katibu mkuu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) Nicholas Musonye kutoa onyo kwa Yanga kuwasilisha majina mapya ya wachezaji wa kikosi cha kwanza kwa ajili ya Kagame Cup, leo hii CECAFA wametoa uamuzi mpya dhidi ya Yanga.
Yanga SC sasa rasmi imeondolewa kwenye michuano ya Kagame kutokana na Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati kupinga kupeleka timu ya vijana.
Yanga ilitaka kupeleka timu yenye vijana wengi iliyochanganyika na wakongwe wachache.
Lakini Katibu Mkuu wa Cecafa, Nicholas Musonye akasema hizo ni dharau. Wanasema ni timu ina wachezaji wa timu ya kwanza, vipi Maximo abaki Dar es Salaam.
“Halafu timu isafiri kwenda kwenye mashindano makubwa kama ya Kagame. Huu ni utani, ndiyo maana sasa tumeipa nafasi Azam,”alisema jana.
Mabingwa wa Tanzania Bara, Azam FC, watapambana Kundi A lenye timu za Rayon Sport ya Rwanda, Coffee ya Ethiopia, Atlabara ya Sudan Kusini na KMKM ya Zanzibar.
Kundi B lina timu za APR ya Rwanda, KCC ya Uganda, Flambeau de L’Est ya Burundi, Gor Mahia ya Kenya na Telecom ya Djibouti wakati Kundi C linaongozwa na mabingwa watetezi, Vital’O ya Burundi, El Merreikh ya Sudan, Polisi ya Rwanda na Benadir ya Somalia.
Rais Paul Kagame wa Rwanda ndiye mlezi wa mashindano haya ambaye hutoa dola za Kimarekani 60,000 kila mwaka kwa ajili ya zawadi.
Kwa kuwa Azam imechukua nafasi ya Yanga, sasa itacheza mechi ya ufunguzi dhidi ya wenyeji Rayon Sport Uwanja wa Amahoro Agosti 8, mwaka huu.
Mechi ya saa 8 mchana itakuwa ni kati ya KMKM ya Zanzibar  dhidi ya  Atlabara ya Sudan Kusini. 
Mechi ya pili ya Azam FC itakuwa  Agosti 10 dhidi ya KMKM, kabla ya kuivaa Atlabara Agosti 12, halafu itamaliza makundi dhidi ya Coffee ya Ethiopia Agosti 16.