Jumamosi, 6 Desemba 2014

Rapper mwingine wa TZ aliyetunukiwa shahada ya kwanza chuo kikuu

.
.
Rapper kutokea Unity Entertainment Stereo ambaye ameachia wimbo wake uitwao ‘Wako’ aliomshirikisha muimbaji wa Kenya,Victoria Kimani leo Des 6  ameongezewa CV yake ya Elimu baada ya kutunukiwa shahada ya ‘Bachelor of Science in Urban and Regional Planning’  kutoka chuo kikuu cha Ardhi Dar es Salaam.

EPL: Mambo yazidi kuwa magumu kwa Wenger: Matokeo ya Stoke vs Arsenal

IMG_9342.JPG
Wakati akiwa kwenye shinikizo la kutakiwa kutimuliwa, mambo yamezidi kuwa magumu kwa kocha mkongwe zaidi kwenye ligi kuu ya England Arsene Wenger.
Akiiongoza timu kwenda mpaka kwenye dimba la Brittania kucheza dhidi ya Stoke City, na kilichotokea ni majonzi zaidi kwa mashabiki wa Gunners.
Mpaka kufikia mapumziko Arsenal walikuwa nyuma kwa jumla ya magoli 3 kwa nunge.
Magoli ya Peter Crouch, Jonathan Walters na Bojan Kirkic yaliipa Stoke uongozi kwenye mchezo huo.
Kipindi cha pili Bojan aliichambua ngome ya Arsenal na kufunga goli zuri kabla ya mwamuzi wa pembeni kuamua ni offside- na dakika moja baadae Arsenal wakapata penati iliyofungwa na Santi Cazorla.
Dakika baadae Gunners wakafunga goli la pili kupitia Aaron Ramsey.
Wakiwa wanatafuta goli la kusawazisha beki Chambers akapata kadi nyekundu lakini hiyo haikupunguza kasi ya Arsenal kutafuta goli, lakini mpaka mwamuzi anapuliza filimbi ya mwisho matokeo ya Stoke 3-2 Arsenal.