Jumanne, 3 Machi 2015

Waziri MEMBE amesema huu ni mchango wa Marehemu Kapteni KOMBA kwenye mgogoro wa Ziwa Nyasa

IMG_0231 
Leo ni siku ambayo mwili wa Marehemu Kapteni John Damian Komba umepumzishwa katika makaburi ya Kijijini kwao Lituhi, Mbinga mkoa wa Ruvuma.
Leo kwenye kipindi cha Power Breakfast Clouds FM, alisikika Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akizungumzia mchango wa Marehemu Komba kwenye suala la mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa kati ya Tanzania na Malawi.
Kwenye mgogoro wetu wa Malawi tulimchukua Kapteni Komba kwenda kutoa ushuhuda unaoonyesha kwamba Ziwa Nyasa kwa kweli mpaka ni katikati, ndio alikwenda kutoa ushuhuda.. Kapteni Komba alieleza kwamba toka enzi za mababu zake na mabibi zake makaburi ya wazee wake yako ndani ya maji, ukifika pale Lituhi na huwa wanachukua mitumbwi wanakwenda kunyunyizia na kutoa baraka zao makaburi yale yako ndani ya maji na bado yapo misalaba iko kule kwa hiyo akawa anauliza na yale makaburi sasa yawe mali ya Malawi?
Maji ya Ziwa Nyasa yanakuja kwenye ardhi miaka yote na huchukua Shule, huchukua Mahakama na makaburi ya wazee mbalimbali, huu ni ushuhuda alioutoa Kapteni Komba tulipokwenda Malawi na ushuhuda uliochukuliwa na wasuluhishi kuonyesha kwamba Ziwa lile linakula ardhi ya Tanzania.
Komba lilimleta hilo na alizungumza vizuri sana kwa hiyo katika diplomasia ya mgogoro wa Ziwa Nyasa kati yetu na Malawi huyu alikuwa miongoni mwa watu waliozungumza kwa niaba ya watu wanaokaa kwenye mwambao wa Ziwa Nyasa kwamba mpaka kwa kweli upo pale katikati
Aliwahi kualikwa kwenda kusaidia kampeni kwa nyimbo zake, kwa hamasa zake na wengine waliogopa wakimuona ameingia kwenye nchi, wanatuletea barua kutuambia bwana muondoeni haraka sana.. akikupigia kampeni kushindwa haiwezekani.. tumepoteza mtu, tumepoteza shujaa, tumepoteza mkereketwa, tumepoteza kiongozi aliyekuwa mstari wa mbele kukiletea chama cha mapinduzi ushindi miaka nenda rudi“– Waziri Bernard Membe.