Jumamosi, 4 Oktoba 2014

Wanajeshi 9 wa Umoja wa Mataifa wauawa

 
Mwanajeshi wa Umoja wa Matifa mali 

Ujumbe wa Umoja wa mataifa nchini Mali unasema kuwa watu waliokuwa na silaha ambao walikuwa wakitumia pikipiki wamewaua walinda amani tisa wa Umoja wa Mataifa kaskazini mashariki mwa taifa hilo.
Uvamizi huo ndio mbaya zaidi kuwai kuwakumba wanajeshi hao wa Umoja wa Mataifa
Wanajeshi hao kutoka nchini Niger walikuwa wakisafiri kati ya miji ya Menaka na Ansongo wakati walipovamiwa.
Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa amesikitishwa na kile alichokitaja kuwa vitendo vya kigaidi.
Mwandishi wa BB nchini Mali amesema kuwa kikosi hicho cha umoja wa mataifa kimelalamika kuhusu vifaa duni inavyomiliki.
Walindamani hao walitumwa miaka miwili iliyopita baada ya makundi ya wanamgambo wa kiislamu kuchukua udhibiti wa maeneo ya kaskazini mwa Mali.

Mtoto wa kizazi cha 'msaada' azaliwa

 
Womb Transplant baby 

Mwanamke mmoja nchini Sweden amejifungua mtoto kutokana na kizazi alichowekewa kupitia upasuaji.
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 36 alizaliwa bila kizazi kabla ya kuwekewa kizazi cha mwanamke aliyekuwa katika miaka yake ya sitini.
Jarida la afya la Uingereza ,the Lancet linasema kuwa mtoto huyo alizaliwa kabla ya mda wake kufika mnamo mwezi Septemba akiwa na uziti wa kilo1.8.
Babaake amesema mwanawe ni wa kushangaza.
Matibabu ya ugonjwa wa saratani pamoja na kasoro za mazazi ndio sababu kuu zinazosababisha wanawake kuwa na kizazi kibaya.
Iwapo wanataka kujipatia mtoto basi hulazimika kutumia mwanamke mwengine anayebeba mimba hiyo kwa niaba yake.
Ijapokuwa wazazi wa mtoto huyo hawajatambuliwa ,inaaminika kuwa mwanamke huyo alikuwa na mbegu zilizokuwa zikifanya kazi.
Kulingana na baba ya mtoto huyo ,mwanawe hana tofauti yoyote na watoto wengine.

Je Amisi Tambwe atacheza leo! Simba watoa majibu hapa

IMG_7718.JPG
MSHAMBULIAJI wa Simba SC, Amisi
Tambwe juzi alizua hofu kwa kocha
Patrick Phiri na rais wa klabu hiyo,
Evans Aveva baada ya kuumia
mazoezi Uwanja wa Boko ,
Dar es Salaam.

Tambwe aliumia goti baada ya
kugongana na beki Abdi Banda na
kushindwa kuendelea na mazoezi hadi
akafungwa barafu baada ya kutibiwa
kwa muda na Dk Yassin Gembe.
Kocha Phiri alionekana mwenye
wasiwasi na kufuatilia kwa karibu hali
ya mchezaji huyo wakati akitoka nje. “Hakikisha anakuwa vizuri, ni
mchezaji wangu ninayemtegemea,”alisema Phiri
kumuambia Dk Gembe wakati anatoka
nje na mchezaji huyo.

Lakini sasa yakiwa yamebaki masaa kadhaa kabla ya mchezo wa Simba dhidi ya Stand United, mshambuliaji huyo aliyekuwa mfungaji bora msimu uliopita amethibitishwa kuwa fiti kuivaa timu hiyo ya Stand ambayo imepanda daraja msimu huu.
Tambwe anaweza kuanza leo kwenye safu ya ushambuliaji kwa pamoja na Emannuel Okwi.
Wakati huo huo kiungo Jonas Mkude amerejea kwenye timu baada ya kuandamwa na majeruhi kwa muda kiasi.