Ijumaa, 17 Machi 2017

Jinsi ya Kuishi na Mwanamke Asikuloge au Kukupa Limbwata..!!!

                          

Nipo tena kwa Mara nyingine katika kubadilishana uzoefu juu ya mambo mbalimbali yanayohusu mahusiano,kuna jambo limekuwa likiniumiza kichwa sana ni swala zima la kulogwa au kupewa limbwata na mwanamke.

Nidhahiri kabisa mambo haya katika jamii yetu yanafanyika kwa baadhi ya wanawake huwa wanawafanyia wanaume,na tatizo hilo limezidi kushamiri zaidi kutokana na ongezeko kubwa la waganga wa kienyeji.

Nimefanya research kwa baadhi ya waganga wameniambia wateja wao wakubwa ni wanawake na shida kubwa wanayokuwa wanahitaji ni kuolewa au kuwadhibiti wanaume zao.

Nami mekuja kugundua wanaume wengi huwa wanafanyiwa madawa ila wakati mwengine mungu huwalinda hawazuriki bila ya wao kujua na wanaume wengi ambao wapo katika hatari hiyo ni wale wenye kipato kidogo ambacho kinarizisha.

Sasa basi nimejaribu kutafuta prevention za ki psychology, ambanzo hazihusiani na mambo ya kishirikina ambazo zinaweza kukusaidia uepukane na janga hilo nimejaribu kutumia experience yangu ni kama zifuatazo:

Kwanza kabisa kama mwanaume unapoanza mahusiano ya kimapenzi na mwanamke unatakiwa umwambie mwanamke vitu ambavyo huvipendi na moja katika ya vitu ambavyo utamwambia hupendi ni mambo ya kishirikina na unatakiwa umsisitizie kwamba endapo kama wewe utagundua yeye anapenda mambo ya kwenda kwa waganga umwambie siku hiyo ndio itakuwa mwisho wa mapenzi yenu.

Jambo la pili ukiwa unaishi na mwanamke ndani usipende kula chakula peke yako hata kama umechelewa kurudi umerudi labda saa sita usiku mwambie mke wako mle wote chakula cause peke yako hujazoea kula au kama mna mtoto wenu ama ndugu wa mwanamke kula nae chakula.

Kwa kufanya hivyo mwanamke atajua hupendi kula peke yako na unampenda yeye na ndugu zake kumbe unalako moyoni unajilinda na limbwata,jambo la tatu pendelea kufanya ibada ukitaka kula na ukitaka kulala na mshirikishe mkeo katika ibada na wakati mwingine msomee maandiko ya vitabu vya mungu ambayo yanakataza ushirikina na adhabu zake watakazo zipata wanaofanya mambo hayo,mengine mnaweza mkaongezea.

Note:Mwanamke anaweza akawa sio mshirikina lakini akashawishiwa na marafiki zake akufanyie hivyo,kwa hiyo kama mwanaume ni bora ukachukua tahadhari mapema.

Kama Huwezi Kuachana Naye Usijaribu Kuchungulia Mawasiliano Yake....!!!


Kuna siku nilijifanya Mjuaji nikadukua mawasiliano ya mchepuko wangu niliyokutana nayo huko sasa ni hatari tupu, sms ya kwanza kuingia jamaa anampongeza kwa shughuli yao ya jana kuja huku whatsaap shughuli nzito nikajikuta naumwa ghafla pressure inanipanda mara nikaona dunia inazunguka mara nataka kuaga dunia ikabidi majirani zangu wafanye mawasiliano na mchepuko wangu maana walikuwa wanaufahamu ile unakuja home. baby jamani unaumwa nn? aiseeeh nikiuangalia homa inanizidia nikifikiria kuucha siwezi.............kilichoendelea.....................ila mpaka sasa nadunda nao course niliona bora tu nijikaze 

Vijana Tuache tabia ya kudukua mawasiliano ya tunaowapenda wakati jeuri za kuwaacha hatunazo, huo ni ushauri tu kama jasiri endelea kupanga mikakati ya kudukua mawasiliano ya mke au mchumba ako soon tu itabaki story

Alikiba Kuweka Muziki Wake Wasafi.com ni Sawa na Safari ya Mwezini..!!


Kwa takribani miaka mitatu sasa mafahari wawili wa muziki wa kizazi kipya yaani Bongo Flava Alikiba na Diamond Platinumz wamekuwa katika bifu zito sana, licha ya wao kujaribu kila siku kuukwepa ukweli huo. Hakuna kati yao ambaye amewahi kujitokeza hadharani na kukiri uhasama kati yao lakini ni wazi kuwa watu hawa hawapikiki chungu kimoja.

Mara kwa mara watu wa karibu wa Diamond wakiwemo watu walio kwenye management yake hususan, mameneja Sallam na Ricardo Momo, wamekuwa wakimtupia vijembe Alikiba. “Wao wakipost tembo, sisi tunapost show” na “waambie dada zao Kariakoo waje Ulaya” ni baadhi tu ya mistari ambayo Diamond amewahi kusikika akiimba ikiwa ni kuelekeza mashambulizi upande wa Alikiba na kambi yake.

Hivi karibuni Diamond akiwa kwenye Interview ya kipindi cha 360 cha Clouds FM, alikaririwa akisema kuwa hana tatizo na Alikiba, ni mtu anayeheshimiana naye na hata uongozi wake uko katika mazungumzo na uongozi wa Alikiba ili Kiba aweze kuuza nyimbo zake kwenye mtandao wa wasafidotcom ambao ni mradi mpya wa Diamond.

Baadaye usiku kupitia akaunti yake ya Instagram Alikiba aliandika caption zenye utata zilizotafsiriwa na mashabiki na wadau mbalimbali kuwa zimelenga kujibu maneno hayo ya Diamond Platnumz.

Wamarekani wana sera zao mbili ambazo wanazitumia sana katika kulifanya taifa lao kuendelea kuwa taifa kubwa duniani. Sera ya kwanza; njia pekee ya kumshinda adui ni kumfanya rafiki, ya pili; wamarekani hawahitaji rafiki dhati wala adui kweli, zaidi ni kutimiza interest zao.

Hivyo watakufanya rafiki ili wapate watakacho na utarudi kuwa adui wakishatimiza azma yao. Lakini Waingereza pia wanasema numbers don’t lie. Nimejaribu kufuatilia rekodi za nyuma za Alikiba katika mtandao wa mkito.com nikagundua kuwa Alikiba ni record breaker. Mwana iliweka rekodi, Chekecha Cheketua iliweka rekodi. Hata nyimbo ya Nisamehe aliyoshirikishwa na Barakah Da Prince pamoja na nyimbo ya Kajiandae aliyoshirikishwa na Ommy Dimpoz zimeingia kwenye Top 5 ya ngoma zilizopakuliwa zaidi kwenye mtandao wa Mkito mwaka 2016.

Kwa rekodu hizi ni dhahiri Diamond anahitaji amani na Alikiba kwasababu za kibiashara zaidi. Anatambua fan base aliyonayo Alikiba itabust zaidi mtandao wake, pesa atakayopata ni kubwa, pia number of visitors itaongezeka kwa kasi kwani kila mtu atataka kuamini ni kweli Ali yumo? Haikushangaza kuona editing kwenye mitandao ikionesha kua profile ya Alikiba ipo kwenye wasafidotcom.

Kwa hali ilivyo sioni na sidhani kama management ya Alikiba itaweza kukubali kuuza nyimbo kwenye mtandao wa Diamond. Kwanza wanajiamini sababu wameshauza kabla na kuweza kuweka baadhi ya rekodi kwenye mtandao wa Mkito. Pili kutoka kwa mfululizo wa mashambulizi ya maneno kutoka kwa Dimond na management yake kwenda kwa Alikiba itakuwa ni fedheha kubwa kwa mashabiki wa Ali kama Ali na uongozi wake utakubaliana na suala hili. Na ndio maana nasema sera za kimarekani za Dimond zimedunda kwa Alikiba

Mwanamitindo afariki dunia kwa kugongwa na treni



Mrembo wa miaka 19 aliyefahamika kwa jina la Fredzania Thompson amegongwa na treni wakati akipiga picha.

Fredzania alikuwa ni mwanafunzi wa chuo cha Blinn na alikuwa na ndoto za kuwa mwanamitindo mkubwa duniani. Mzazi wa mrembo huyo, Akamie Stevenson ameliambia shirika la habari la CNN, “Bila shaka hilo ndio jamba ambalo alilokuwa akilitaka kulifanya katika maisha yake. Ndiyo shughuli aliyoanza kuifanya siku aliyofariki dunia.”

Hata hivyo msemaji wa polisi wa Navasota, Justin Leeth amesema mpaka sasa hawajagundua tatizo lolote juu ya kifo hicho kama kilikuwa cha hila yoyote.

Lissu aachiwa kwa dhamana ya bondi ya Sh10m


Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo (Ijumaa) imemuachia, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema)  kwa dhamana ya bondi ya Sh10 milioni.

Lissu amedhaminiwa na maelezo ya awali yatasomwa Aprili3, mwaka huu.

Leo asubuhi, Lissu alisomewa mashtaka matano na Wakili wa Serikali, Faraja Nchimbi  likiwamo ya kutoa maneno  yenye nia ya kuhimiza hisia za kidini ambayo yangeweza kupelekea uhasama baina ya jamii za Watanzania.

Lissu  ambaye anajiwakilisha yeye mwenyewe mahakamani hapo aliomba maelezo hayo ya awali yasomwe Jumatatu, ili aweze kuhudhuria uchaguzi wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) unaotarajia kufanyika kesho.

Baada ya Video Inayodhaniwa ni ya Mwanae Kusambaa Ikimuonyesha Akifanya Mapenzi na Jibaba,Kajala Afunguka Haya Mapya..!!!1


Muigizaji wa Filamu Tanzania Kajala Masanja amewafungukia wanaomsema kwamba ameshindwa kumlea binti yake ' Paula'  na kusema anatamani awaoneshe watu hao malezi anayompatia binti yake huyo.

Akipiga story na eNewz, Kajala amedai kuwa hawezi kushindwa kumlea mtoto wake na kwamba malezi anayompatia binti yake ni tofauti na yale watu wanayoyazungumzia katika mitandao ya kijamii na kuongeza kuwa binti huyo analelewa katika maadili, yanayotakiwa.

"Sijashindwa kumlea mtoto wangu, natamani wangekuwa wanaona malezi ninayompatia Paula kwani kila wanachokiona na kukisikia kwenye mitandao ni tofauti sana na ninavyomlea". Kajala alisema.

Kajala ameongeza kwamba katika jambo linalomuumiza ni watu kutumia jina la binti yake hyo na kujifanya ni  yeye na wakati mwingine kuweka vitu hasi ambavyo vinamfanya mtoto wake achukuliwe tofauti katika jamii.

Aidha  muigizaji huyo ameongeza kuwa serikali inapaswa kushughulikia matatizo yanayotolewa na watumiaji wa mitandao  kwa umakini wa hali ya juu  ikiwa ni pamoja na kuweka nguvu ya kutosha.

“Ile akaunti siyo ya Paula kwanza, kwani hajawai  kuwa na simu au kumiliki, nimeshawahi  kuwaambia wamiliki wa ukurasa huo wabadilishe jina au waandike ni ‘fanpage’ lakini naona wamegoma , Baba  yake naye amejaribu kuzifunga lakini bado zinaendelea kutumika mpaka sasa nimechoka ila bado hatujajua tuchukue hatua gani". Kajala aliongeza.

Paula ambaye ni mtoto wa muigizaji huyo pamoja na Producer P- Funky Majani aliwahi kukutwa na mkasa wa kufananishwa na binti aliyerekodiwa akiwa mtupu na kusambazwa mitandaoni.

Fahamu Maajabu ya Nanasi Ambayo Yatakuacha Kinywa Wazi..!!!



BAADHI ya watu wamekuwa wakidai tunda la nanasi kuwa siyo salama kwa akina mama wajawazito, ingawa suala hili bado halijathibitishwa kitaalamu, kwani wapo wanaokula na haijawahi kuripotiwa madhara. Linatumika kama tunda ama juisi na lina faida mbalimbali kwa afya ya mwanadamu.

BAADHI YA FAIDA HIZO NI PAMOJA NA:

Lina vitamini A, B na C, madini ya chuma, calcium, copper na phosphorous ambayo yote ni muhimu sana katika afya ya mwanadamu.Tunda hili husaidia kutengeneza damu, kuimarisha mifupa , meno, neva na misuli (muscles).

Hutibu matatizo ya tumbo, bandama na ini, husaidia kusafisha utumbo mwembamba, hutibu homa, vidonda mdomoni, magonjwa ya koo, hutibu tatizo la kupoteza kumbukumbu, hutibu kikohozi, kutetemeka na uoga (Anxiety). Leo nimeandika tiba ya nanasi kwa sababu ni mjadala mkubwa ulioibuka kuwa tunda hili lina madhara, lakini nikuhakikishie msomaji hakuna madhara ya kukufanya

Laurence Masha Ajitoa Kugombea Urais TLS, Amuunga Mkono Tundu Lissu


Mgombea Urais wa Chama cha Wanasheria nchini (TLS) Ndg. Laurence Masha amejitoa kwenye kinyang'anyiro hicho kwa hoja kuwa anaamini uwezo wa Lissu katika kuiongoza TLS.

Amewaomba mawakili wote waliopanga kumpigia kura wampigie Tundu Lissu. 

ARUSHA: Mgombea urais wa TLS, Laurence Masha ametangaza kujitoa kwenye kinyang'anyiro hicho na kudai anamuunga mkono Tundu Lissu 

Ndoto za Mbwana Samatta Kucheza na Mau United Zawekwa Pending


Ndoto za mshambuliaji wa timu ya KRC Genk ya Ubelgiji Mtanzania Mbwana Samatta za kukanyaga katika dimba la Old Trafford la Manchester United zimesubirishwa baada ya matokeo ya droo ya robo fainali kombe la Europa kwenda kinyume na matamanio yake.

Hamu ya Nahodha huyo wa Taifa Stars ilikuwa ni kuona timu yake ya Genk inapangwa kukutana na Man United katika hatua ya robo fainali ya michuano hiyo, ili atimize ndoto yake mojawapo ya kucheza katika uwanja wa huo maarufu na uliotoa mastaa wengi duniani.

Samatta baada ya mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 bora ambao timu yake iliibuka na ushindi wa 5-2 na kutoa nafasi kubwa ya kufuzu robo fainali, alinukuliwa akisema "Moja kati ya ndoto zangu ni kukanyaga katika dimba la Old Trafford, kwahiyo naomba kila siku timu yetu ikivuka, ipangwe na Manchester United"

Hata hivyo, katika droo iliyochezeshwa leo, KRC Genk imepangwa kuanzia nchini Hispania dhidi ya Celta Vigo, na mchezo wa marudiano utapigwa nchini Ubelgiji.

Ili timu hiyo ikutane na Man United msimu huu, inapaswa kwanza kuitoa Celta Vigo, huku ikiomba Man UNited pia ifuzu nusu fainali, halafu droo iwakutanishe.

Kutokana na ukweli kwamba timu ya Man United ndiyo yenye mashabiki wengi zaidi duniani, ingeweza kuwa ni fursa adhimu kwa Samatta kujitangaza zaidi, kwa kuwa watu wengi hawapitwi kutazama mchezo wowote unaoihusu timu hiyo iliyo chii ya kocha Jose Mourinho.

Jumamosi, 11 Machi 2017

NINI CHA KUFANYA BAADA YA KUMALIZA KUFANYA MAPENZI

Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia siha njema na pia kwa kunipa mwangaza wa kuandika hiki ninachokusudia.
Pia niwashukuru wapenzi wasomaji wa safu hii ambao tumekuwa tukiwasiliana na kushauriana hili na lile katika tasnia hii adhimu ya mapenzi. Nawakaribisha sana!
Labda kwa wale wasiofahamu niwaambie tu kwamba dhana ya mapenzi ni dhana yenye wigo mpana sana na ndiyo maana hutasikia hata siku moja tumepumzika kuizungumzia.
Hata hivyo, tunachofanya siku zote ni kukumbushana kwa yale tunayoyafahamu na kushauriana kwa pale tunapohisi wengi hufanya makosa.
Baada ya kusema hayo sasa nigeukie mada yangu ya leo ambayo kwa kiasi kikubwa inawahusu wale walio kwenye ndoa na kikubwa nazungumzia yale ambayo wawili waliotokea kupendana kwa dhati wanatakiwa kuyafanya mara baada ya kumaliza kufanya tendo la ndoa.
Nalazimika kuandika makala haya baada ya kubaini kuwa wengi wamekuwa wakifanya makosa na kujikuta wakishamaliza kufanya tendo hilo takatifu, kila mmoja anageukie kwake kisha kuuchapa usingizi.
Sisemi kwamba ni lazima kuyafanya haya nitakayoyaeleza leo ila 
yakifanywa huwa na manufaa yake na mara nyingi yanaboresha uhusiano.
Kuoga pamoja
Mtakuwa ni watu wa ajabu kama mtamaliza kufanya tendo hilo kisha kila mmoja kulala na majasho yake. Wapo
wasiojali katika hili na kuona kuoga au kutooga ni uamuzi wa mtu. Elewa linapokuja suala la usafi inashauriwa mkimaliza lazima muoge.
Wapo wanawake ambao wakishamaliza hukimbilia kuwaandalia maji wenza wao, wakishaoga ndipo nawo huenda kuoga. Hivi unaona ugumu gani kwenda kuoga na mwenza wako? Unaijua raha ya kuoga na huyo wako wa maisha?
Wanaofanya hivyo wanajua raha yake na wewe ambaye hujawahi, anza leo. Mmemaliza mambo yenu, chukuaneni kimahaba, elekeeni bafuni kisha ogeshaneni kimahaba.
Baada ya hapo rudini chumbani, mkishajifuta maji pandeni kitandani mkiwa wapesi.
Kusifiana
Hakuna muda maalum uliotengwa kwa ajili ya wanandoa kusifiana. Hilo linaweza kufanyika wakati wowote lakini pale mnapomaliza kufanya tendo la ndoa ni lazima utakuwa na jambo zuri la kumuambia mwenza wako.
Msifie kwa utundu na ubunifu wake. Msifie pia kwa mapenzi matamu anayokupa na ikibidi mpe sifa ya uzuri wake kiasi cha kukufanya kila unapokuwa karibu yake ujisikie amani ya kupitiliza.
Wapo ambao hawana kabisa kasumba ya kuwasifia wala kuwashukuru wenza wao kwa mazuri wanayofanyiwa. Yaani wao wanachukulia kila kitu poa tu bila kujali kwamba kusifiana kunanogesha mambo.
Kuelekezana
Kwenye kale kamchezo, wapo ambao wanakosea, kuelekezana na kukosoana kwa wapenzi ni jambo la kawaida. Yawezekana mwenza wako alifanya kitu ambacho hakikukufurahisha wakati mkiendelea na burudani yenu, mnapomaliza mwambie lakini kwa lugha ya kimahaba na ya upole. Naamini kwa kufanya hivyo atakuelewa na kubadilika.
Zungumzieni maisha
Huu ni wakati muafaka wa kujadili changamoto na malengo katika maisha yenu. Hapa akili zinakuwa zimetulia na kila mmoja anakuwa na mawazo chanya kwa mwenza wake. Jadilini mambo yenu, wekeni mikakati ya kuliboresha penzi na maisha yenu kwa ujumla.
Hayo ni baadhi ya mambo ambayo mnashauriwa kuyafanya pale mnapomaliza kufanya tendo la ndoa.
Yapo mnayotakiwa kuyaepuka ili kutotibua furaha iliyopatikana. Hayo nitakuja kuyaeleza katika makala zinazokuja kupitia ukurasa huu.

Wakati Mwingine Wanasiasa Wawe Wakweli, Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa Hakuwa na Ziara Rasmi Tanzania..!!!!

Naona watu wameibeba hii ya Katibu Mkuu wa UN kama "ajenda" tena,huku namuona Mtatiro akirusha makombora,na huku Mbunge Msigwa akirusha kwa upande wa pili.Vijana nao wamebeba mitandaoni kama ajenda ya kumalizia week kimjadala.
Watu wanatakiwa kuelewa tu,mambo mengine sio lazima tuingize siasa saaaanaa.António Guterres hakuwa na ratiba ya ziara ya Tanzania.Ziara yake ilipangwa kufanyika Somalia ili kuonana na Rais mpya kuhusu baa la njaa na ukame unaolikumba eneo hilo.
Sehemu ya pili ikawa Kenya kukutana na Kenyatta,na hii ni kwa sababu,nchini Kenya kuna kambi kubwa sana ya wakimbizi ya Dadaab, inayokaliwa na Wasomali,ambao sera ya Trump ya katazo la Wasomali kuingia US imewaathiri...Umoja wa Mataifa lazima iwahikikishie Kenya ushirikiano ktk kipindi hiki cha mabadiliko ya sera za uhamiaji nchini Marekani.
Maana hivi karibuni,wakimbizi wengi wenye asili ya Somalia ambao walikuwa wafanyiwe "resettlement" na Shirika la Wahamiaji la Kimataifa (IMO),kutoka kambi ya Dadaab kwenda Marekani wamezuiliwa kutokana na sera mpya ya Marekani,hivyo kuwafanya waendelee kusalia Kenya.
Hapa Tanzania alikuwa tu "On Transit",sababu ndege aliyotumia kusafiri ni SwissAir.Schedule ya SwissAir ni Zurich-Nairobi-Dar-Zurich.Na inapotoka Nairobi kuja Dsm kabla ya kwenda Zurich,ndege huwa inakaa Dsm zaidi ya saa moja na nusu.Sasa mtu mkubwa kama Antonio hawezi kukaa muda wote huo ktk ndege wakati anaweza kushuka na kufanya mazungumzo ya kidiplomasia na viongozi wa Tz kama wadau wa Umoja wa Mataifa.
Aina hii ya ugeni ni ya kawaida sana katika viwanja vya ndege ambayo hutumika kama "connection centre".Ukienda Jomo Kenyata International Airport VIP Lounge utakutana na Marais wengi na viongozi wengi maarufu wakipiga soga na Mawaziri wa Mashauriano ya Kigeni wakati wakiwa "on transit".Bole International Airport pale Addis Ababa VIP-Lounge humkuti Waziri Mkuu wa Ethiopia,lakini toka mawio mpaka machweo ya jua,viongozi wa kimataifa huwa "On Transit" kuelekea katika safari zao tarajiwa.
Hata kwa kumtazama tu,wale waliowahi kupanda SwissAir First Class,watakubaliana kuwa alichokuwa amekivaa Guterres ni zile pyjamas (pajama) za abiria wa daraja la kwanza ambao hupatiwa ndani ya ndege kwa ajili ya kupumzikia kwa safari ndefu.Dressing code tu ya pyjamas za SwissAir zinaashiria Katibu Mkuu alikuwa "On Transit".Ratiba na Tanzania haikuwepo.
Sio wa kwanza Guterres kupita tu bila kuonana na Rais,wapo viongozi wengi hupita kama "On transit" hapa Dsm,na husalimiana na viongozi wa chini wa serikali.Mfano King Mswati,yeye "refueling point" yake huwa ni Dsm,katika safari zake za kutoka Mbabane kwenda ama Abu Dhabi shopping au sehemu nyingine,kituo chake cha Cattering na refueling ni Dsm.Toka enzi za JK mpaka sasa,huwezi kumkuta JK anakimbizana kumpokea Mswati,bali utamkuta Membe kwa minajili ya kidiplomasia akimsubiri King Mswati.
Uwanja wetu wa Dsm hutumika kwa ajili ya "On Transit Passengers" na "On Transfer Passengers"."On Transit Passengers" ni wale abiria ambao hupita uwanjani wakiwa ndani ya ndege bila kushuka na kuchukua abiria wengine au kushusha na kuunganisha na ndege hiyohiyo kuelekea "destination" iliyokusudiwa.Mfano wa ndege zenye safari ya aina hii Julius Nyerere Int'nal Airport ni SwissAir (Zurich-Nairobi-Dsm-Zurich),Ethiopia Airways (Addis Ababa-Dsm-Znz au Addis-Dsm-Hahaya Comoro),Oman Air (Muscat-Znz-Dsm-Muscat),Mauritius Air nk.
Siku kadhaa kiongozi wa Mauritius alipita Dsm na Mauritius Air na kuunganisha kuelekea Addis Ababa kwenye mkutano wa viongozi wa Afrika.Toka Sir Seewoosagur Ramgoolam Port Louis kupitia Julius Nyerere International Airport mpaka Addis Ababa.
Walikutana tu na Rais wetu ndani ya ndege,wakapeana mkono na kila mtu akarudi kwenye presidential Suit room yake ya "First class".
Hii ni dalili ya uwanja wetu kukua na kuanza kuwa moja ya "Connection" kubwa ya sehemu mbalimbali za Afrika na dunia.Sasa tunapokea abiria wote wa kutoka Msumbiji kwenda Dubai kupitia Dsm,abiria wa Mayote na Comoro kwenda Dubai.Abiria wa kutoka Mauritius kuja Afrika ya Mashariki na Mashariki ya kati ya Asia.
Tuanze kuzoea,kuwa sio kila abiria ni "mgeni rasmi" wa nchi,wengine wanakuwa wapita njia.Waziri Mkuu wa Ethiopia angekuwa anashinda Airport kama kila kiongozi anayepita Bole Int'nal Airport atamsubiri kumpokea.
Mkuu wa Mkoa wa Dsm angekuwa anajipanga kila siku kupokea viongozi na mawaziri mkoani kwake,maana ofisi zote kubwa zipo kwake.Waziri wa Mambo ya ndani akiwa Simiyu ni "mgeni",ila kwenye viunga vya Dsm ni mpita njia tu.
Hence;haikuwa sehemu ya ratiba,ndio maana ni Balozi Mahiga badala ya Rais JPM

P-Funk: Diamond Anapaswa Kutulia Kidogo, lasivyo Watu Watamchoka


Producer mkongwe wa Bongo Records, P-Funk Majani, amesema kila siku akiendelea kusikia kuhusu Wasafi, itafika muda atawachoka.



Amedai kuwa ili label hiyo iendelee kufanya vizuri kwa muda mrefu, ni lazima ibadilishe sound, kuja na ladha au wasanii wapya. Amedai pia kuwa pamoja na ukubwa wa Diamond, kama asipotengeneza hali ya watu kummiss, watu watamchoka mapema.

Majani amesema hayo kwenye kipindi cha The Playlist cha Times FM kinachoendeshwa na Lil Ommy.

DODOMA: Bashe, Malima na Musukuma Mbaroni Wakidaiwa Kupanga Kuhujumu Vikao Vinavyoendelea

Wabunge wawili Bashe na Musukuma wamekamatwa leo asubuhi kabla ya kikao cha Kamati Kuu kuanza kutokana na kudaiwa kubeba ajenda ya "kwenda kumpinga Mwenyekiti".

Kundi hili la wabunge lililokuwa na mjumbe mwingine, Adam Malima lilipanga Peter Serukamba ndiye awe kinara wa kuanzisha hoja ya kumpinga mwenyekiti.

Hata hivyo, kabla ya kutimiza azma yao walijikuta mikononi mwa Polisi huku Serukamba akidhibitiwa na kukosa kuwasilisha hoja ya kumpinga mwenyekiti, Magufuli.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa amethibisha na kuwataja waliokamatwa kuwa ni Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe na Mbunge wa Geita vijijini ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita, Joseph Kasheku maarufu kama Musukuma na Malima.

“Hao ndio waliokamatwa na bado tunaendelea na mahojiano na wengine bado tunaendelea kuwatafuta,”amesema Mambosasa.

Chanzo chetu kimedokeza kwamba huenda wakaendelea kushikiliwa hadi pale mkutano mkuu utakapomalizika!

Chanzo:Jamii Forums

Rumishael Shoo (Rummy) Ashikiliwa na Polisi Kwa Tuhuma za Dawa ya Kulevya


Kamanda Sirro akiongea na waandishi wa habari amesema Jeshi la Polisi limefanikiwa kuwakamata wahalifu mbalimbali, silaha na magari mawili aina ya Noah yaliyokuwa yakitumika kufanya uhalifu.

Miongoni mwa aliowataja Kamanda Sirro ni pamoja na Vanessa Mdee na Rumishael.

Huyu Rumishael amekuwa akitajwa kwa muda mrefu kujihusisha na biashara hiyo haramu, aliweza kuwaweka polisi mikononi ikiwa pamoja na kuwajengea kituo cha polisi Mwananyamala(Inasemekana).

Huyu huyu mwaka jana TRA ilishikilia magari yake matatu ambayo ni V8 gold plated,Benz gold plated na Benzi metalic blue ambayo yalibainika kuingizwa nchini bila kulipiwa kodi.

Alhamisi, 9 Machi 2017

Ishara Za Kujua Iwapo Umemkuna Mwanamke Wako Vizuri Kunako 6 X 6..!!!

 Leo acha niwape dondoo
kadhaa kuhusu namna ya kujua kama umemkuna ipasavyo mwanamke wakati wa tendo la ndoa.
1.Kufinya shuka kwa nguvu au kitanda kwa nguvu wakati unampa mambo
ni ishara mojawapo ya
kuonyesha kwamba inamkuna vizuri.
2.Kukukumbatia kwa nguvu au kukufinya:
Hii pia ni moja kati ya ishara nyingi anazoonyesha
mwanamke pindi anapo
----- vizuri.
3.Kutokwa na jasho ndani ya
sekunde chache:
Ukiona anatokwa na jasho ndani ya sekunde chache na katika hali isiyo ya kawaida basi jua kua utendaji wako ni mzuri na
unamridhisha.
Acha niishie hapo kwa leo, lakini sina maana kwamba kama mwanamke wako haonyeshi moja kati ya ishara hizo au zote
basi ndio inamaanisha
haumridhishi, hapana. Hizi ni baadhi tu, zipo nyingi tu.

Jamani Nitoke Nnje ya Ndoa..?Nahitaji Ushauri Wenu...!!!

Nimevumilia majaribu ya ndoa yamenishinda, ninaishi na mke wangu lakini hatuna furaha yaani kama tumelazimishwa! 
Hakuna kabisa furaha, tumejaribu kukaa chini na kujadili mara nyingi sana lakini huwa anadai hakuna tatizo! Najiuliza sana hivi kutoka nje ya ndoa kutanosaidia nini? Nitachinwa pesa bure na ndo matatizo yataongezeka lakini pia kiimani hairuhusiwi nami naogopa kukutwa katika dhambi na Mungu wangu!
Nimesali sana lakini kama hakuna badiliko lolote! Nimuache? Yaani kila kitu tabu tupu! Wasichana nawaogopa mno nahisi wataniongeza machungu je, nitamfute mmama wa wastani kama miaka 34 ila awe mzuri? mi nina 25. Kwakweli sijitambui niko njia panda!
Nilikuwa mwajiriwa wa kampuni fulani na nilikuwa nikilipwa laki 5 kwa mwezi sasa nina miezi 2 nkmeacha kazi sababu ya matatizo ya ndoa yangu!
Sijielewi nahisi naelekea kufa ningepata mwanamke wa umri huo na anaishi tofauti na.mji wangu na akanipenda ningeenda kukaa kwake hata kwa miezi 3.
Nahisi maisha yangu yanaharibika sasa,
Nina uchungu sana usiku huu nilikuwa safari nimerudi na zawadi zimepokelewa na kutupwa sitting rum, ninahamu nimemsogelea kitandani kanipiga pepisi jichoni nomeumia sana maana tangu tuoane sijawahi ifurahia ndoa!
Hapa najiuliza nifanyeje napanga nitoke nikalale guest lakini sina hata wakunifariji natoka naenda guest hata nikifika nikaamua kujitoa duniani inatosha.
Kuna wanawake wazuri sana, wapoleee sauti za upole akikukosea kidogo tu utasikia samahani baba yangu, nakupenda haikuwa nia yangu, jaman namimi si nipate mmoja wa hivi?

Kama Umeteseka kwa Muda Mrefu,Hizi Hapa Mbinu za Kuamsha Nguvu za Kiume Kwa Muda Mrefu..!!!!

Suala la nguvu za kiume kwa sasa limeshakuwa ishu kubwa kwa vijana wengi wa sasa,kwa utafiti uliofanywa mwaka 2013 na shirika la Afya duniani unaonesha kuwa zaidi ya asilimia themanini ya wanawake hawatoshelezwi kimapenzi. Moja ya sababu kubwa inayochangia kutotoshelezwa huku kwa hawa wadada ni tatizo la upungufu wa uwezo wa mwanaume kumnyuka mwanamke kisawasawa ili kumkata nyege kabisa kwa kufika kileleni.
Wanaume wengi wa sasa wamekuwa wabovu kabisa katika kusimamisha mashine zao kiasi cha kuwa hata mdada awe mkali na mwenye mvuto namna gani amejitahidi sana kumtandika basi bao tatu kisha kitu inalala kabisaaa,tena kila bao huchukua dakika mbili tayari amekojoaLoo!
Zifuatazo ni njia chache na salama kabisa za kuamsha nguvu za kiume maradufu.
*AINA ZA VYAKULA
 Tusidanganyane chakula ndio kila kitu mwilini,vyakula vya nafaka zisizokobolewa ni vizuri sana kuupa uume nguvu kuliko unavyodhani. Hivyo kama ni ugali basi penda sana kula ugali wa dona na sio sembe kwani sembe huwa haina kiini cha njano chenye protini na wanga ambacho ni silaha sana katika kuutia nguvu uume na mwili kwa ujumla.
Matunda pia kama matango,karoti ni muhimu sana katika kujenga nguvu za kiume.Vyakula vingine ni kama mihogo mibichi,magimbi nk. Lazima uwe na utamaduni wa kutumia aina hii ya vyakula katika maisha yako ya kila siku, sio eti leo una mechi na mdada ndio unajifanya kufakamia mamihogo loo siku hiyo!
*MAZOEZI
Mazoezi ya viungo ni muhimu sana kwani hufanya mwili uwe fit na hivyo huimarisha hata uume na kuufanya usilale kirahisi pale unapokuwa katika show na mrembo. Push up, kukimbia, kurukaruka na mazoezi mengine mengi ni muhimu sana.
*ACHANA NA UNYWAJI WA POMBE ULIOPITA KIASI
Pombe ni hatari sana na inadhoofisha sana nguvu za kiume hivyo chunga sana unywaji wa pombe uliopitiliza kwani ipo siku utajikuta unamwangalia tu mkeo kama dada ako vile wakati yeye nyege zimempanda balaa,matokeo yake itabidi achapwe na njemba zinazojua shughuli huko nje.
*ACHANA NA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME
Hizi dawa ni hatari sana hasahasa zile za hospitali kwani maranyingi zimetengenezwa kwa kemikali ambazo huamsha vichocheo mwili kwa muda flani lakini baada ya muda tatizo litaongezeka maradufu kwani ni tiba kwa muda mfupi tu.
*UWE MAKINI NA UPIGAJI PUNYETO
Hii kitu ni hatari sana hususani kwa wale wanaosugua sana mishipa ya uume hivyo huifanya isiwe ngangari kiasi cha kukusaidia kumshughulikia vizuri mtoto wa kike mwenye nyege zake. Hivyo kama unafanya haka ka mchezo inabidi uwe makini sana usijejutia.

Ukweli Mchungu..Uwepo wa WCB; Bongo Fleva Inachungulia Kaburi...!!!

Hayo yote nayasema kuhusu nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Adul Juma au maarufu zaidi kwa jina la Diamond. Siku za hivi karibuni, Diamond ameanzisha zoezi la kuwachukua wanamuziki na kuwaingiza kwenye kundi lake maarufu sana la Wasafi Classic Baby ‘WCB’ ambalo limetokea kupata jina kubwa katika Muziki wa Kizazi Kipya Bongo.
Lebo hii ya Wasafi kwa sasa inaundwa na watu wanne, Queen Darleen, Rayvanny, Rich Mavoko na Harmonize. Awali, alianza na akina Harmonize, Rayvanny, Rich Mavoko na mwisho ni Queen Darleen. Harmonize na Rayvanny walikuwa hawakutamba sana kabla ya kwenda Wasafi. Mimi kwa hao, naona ni sawa kabisa na wala sina tatizo nao.
ANAINUA VIPAJI
Katika mahojiano yake na vyombo mbalimbali vya habari hapa Bongo, Diamond amekuwa akisema kwamba, anafanya hivyo ili kukuza muziki na kuinua vipaji vya wanamuziki wachanga wa Tanzania. Mimi kwa hilo pia sina tatizo naye. Pia, watu au wadau mbalimbali wa muziki huo wakawa wanampongeza Diamond kwa kuwa, zoezi lake la kuwabeba akina Harmonize linaongeza ushindani mkubwa katika Muziki wa Kizazi Kipya, kwamba kama yeye anawainua hawa, wengine wakainuliwa kule, muziki utapaa. Na kwa hili pia mimi sina tatizo nalo hata kidogo.
NI HOJA ZA MSINGI SANA
Kuna hoja za msingi kwamba, kama si Diamond, hawa akina Rayvanny wasingekuwa hivi walivyo leo. Wasingejulikana kama wanavyojulikana wakiwa kwa Diamond. Hiyo ni hoja ya msingi sana, tena sana. Na kwa hilo mimi sina tatizo na hoja husika.
KUHUSU RICH MAVOKO
Katika zoezi lake la kuendelea kuchukua wasanii, Diamond akamchukua Mbongo Fleva, Rich Mavoko ndani ya kundi lake la Wasafi. Hapa kidogo baadhi ya watu wakahoji uhalali wa usahihi wake. Wengi waliamini kuwa, Diamond kumchukua msanii huyo ambaye alishajenga jina kubwa katika muziki huo ni sawa na kumpoteza njia kwani Rich Mavoko kuwa chini ya Wasafi kunaweza kumfanya afifie kama siyo kufa kabisa kisanii.
NINACHOKIONA
Sasa ninachokiona mimi ni kwamba, nia ya Diamond inaweza kuwa nzuri sana lakini kukatokea makosa madogomadogo kwenye kuchukua aina ya wasanii. Yapo madai ya chini kwa chini kwamba, pia ana mpango wa kumchukua msanii anayevuma sana kwa sasa, Darassa ambaye kibao chake cha Muziki kimeishika nchi kwa kupigwa maeneo mbalimbali. Kama kuna ukweli wa madai haya, naamini kuna siku tutakuja kusikia, hata Ali Kiba, Ommy Dimpoz nani sijui, wote wana mpango wa kujiunga Wasafi. Katika hili, ninatia shaka kwamba, lengo la Diamond kuwakusanya wasanii niliowataja na kumchukua pia Rich Mavoko ni njia moja kwake ya kuelekea kwenye kuudidimiza muziki wa Bongo Fleva.
Wasafi linajiimarisha kuwa kundi kubwa la muziki huo nchini. Sasa je, ikitokea hivyo, upinzani utatoka wapi? Ninavyojua mimi siku zote, palipo na ushindani ndipo panapokuza kitu. Ni sawa na timu za mpira wa miguu wa Tanzani, piga mahesabu kwamba, kuna siku Simba itashuka daraja. Je, Yanga atabaki na mshidani gani? Na kilele cha raha ya mpira wa Tanzania ni kucheza kwa Simba na Yanga.
Ndiyo maana, makocha wa timu hizo bora wafungwe na timu nyingine zote, lakini siyo Simba au Yanga. Hata shule wanazosoma watoto wetu siku hizi, ubora wake inatokana na kuwepo kwa shule bora nyingine. Kama ingekuwa shule moja tu ndiyo bora sifa yake isingekuwa na maana. Sifa  ya mtu mrefu duniani kote inatokana na kuwepo kwa mtu mfupi. Kama watu wote wangekuwa na kimo sawa isingejulikana kama urefu ni bora.
Kuwepo kwa Wasafi kusiwe sababu ya kuwakusanya wanamuziki wengine hawa wenye majina makubwa kwani na wao uwepo wao ndiyo changamoto ya kuwepo kwa Wasafi. Inawezekana nia ya Diamond ikawa nzuri sana lakini mimi naamini anakokwenda, kunaweza kuwa ndiyo kaburi la muziki wenyewe.

Exclusive..Baada ya Kutemwa Yanga,Pluijm Kutua Taifa Stars,Mpango Mzima Uko Hivi..!!!

UNAAMBIWA ukiona cha nini mwenzako anasema nitakipata lini, kwani baada ya Yanga kuamua kumtema kocha wao za zamani, Hans van der Pluijm, nyota ya Mholanzi huyo imezidi kung’aa na sasa ana ofa mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi ambazo zimekuwa zikimiminika kila kukicha.
Pluijm alibadilishwa kutoka kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo na kupewa cheo cha ukurugenzi wa benchi la ufundi muda mfupi baada ya waajiri wake, Yanga, kumwajiri kocha mwingine, George Lwandamina, aliyekuwa akiinoa timu ya Zanaco ya Zambia, lakini hakudumu muda mrefu, baadaye alitimuliwa kabisa kutokana na kile kilichodaiwa na uongozi kuwa ni ukosefu wa fedha.
DIMBA Jumatano limezungumza na Pluijm kuhusu mustakabali wake ambapo amesema anamshukuru Mungu kwa kuendelea kumpigania, kwani kwa sasa amekuwa akipata ofa mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi ambazo zinampa wakati mgumu wa kuamua aende wapi.
Alisema kwa sasa bado yupo Tanzania na wala hajaondoka kwenda kwao Ghana, ambapo amedai kuwa, anafanya mambo yake kimyakimya na yakishakaa sawa atawekakila kitu bayana ili Watanzania na wadau wanaomuunga mkono wafahamu.
“Kama kuna watu wanauliza, kama nipo Tanzania au nimeshakwenda Ghana waambie bado nipo hapa nchini, na kuhusu mustakabali wangu niseme kwamba siwezi kuzungumza mengi kwa sasa ila kwa kifupi nimepata ofa mbalimbali za hapa Tanzania na nje ya nchi.
“Kwa sasa nachukua muda kutafakari na kutuliza akili yangu halafu nitafanya maamuzi sahihi,” alisema kocha huyo, aliyeiletea heshima Yanga kutokana na kuwapa vikombe mbalimbali, huku pia akijenga mashikamano ndani ya timu.
Taarifa zaidi kutoka vyanzo mbalimbali zinadai kuwa, moja ya timu ambazo Pluijm anatajwa kujiunga nazo hapa nchini ni timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ ambayo kwa sasa ipo chini ya Jackson Mayanja.

Unatamani Kumuacha ila Unashindwa? Ngoja Nikwambie Kitu

Kuna watu wana Mikwara sana, ukiachana nae anaanza Maneno ya shombo, wengine hudiriki kukwambia ''you cant live without me utarudi tu'', unajiuliza huyu mtu ana Hisa kwenye mishipa yangu ya moyo au ana mrija wa Oxygen yangu ya kutumia kesho?? Kama nilizaliwa peke yangu kwanini nisiweze kuishi wewe ukiondoka??

Maneno ya mkosaji haya, usiyasikilize kamwe! Unapoamua kufanya Maamuzi magumu usisikilize kingine chochote, Follow your heart. Wengi wamegeuzwa watumwa kwa kuamini they cant live bila watu fulani, kisa wamezoeana, au wamekaa muda mrefu kwenye mahusiano, unahisi kama hutaweza... Hamna kitu kisichowezekana, Mungu ameumba kusahau, utapona maumivu na utasonga! Hakuna destiny rahisi ya Kimapenzi bila kufanya maamuzi magumu, lasivyo Jiandae kuwa mtumwa wa mtu fulani, binadamu fulani ambaye naye amegundua wewe ni dhaifu na anatumia udhaifu wako kukutesa maisha yote...

Amua leo, Uwe mtumwa wa mtu au utengeneze furaha yako kwa Kumove on kupata Lover of you life

Harmo Rappa Azidi Kutembelea Nyota za Wasanii Wakubwa...Amchokoza AY



Msanii Ay mzee wa commercial ameamua kumuachia jina lake Rapa anayekuja kwa kasi kwenye Bongo Fleva HamoRappa.

Jina la Legend alikuwa akitumia mzee wa commercial kwenye mtandao wa Twitter lakini sasa ameliachia rasmi kwa rapa huyo mwenye vituko vingi bongo anayeongoza kwa kufuatiliwa kwenye 411 news.

Baada ya HamoRappa kuitambulisha akaunti yake ya Twitter ikiwa na jina la Legend Harmo, jambo liloshtua ulimwengu vipi kwa Zee Legend aliyokuwa akitumia AY.

Mzee wa commercial ameamua kutumia jina la Masta badala ya Lile la Zee Legend ambalo Harmo amelichukua la Legend!

Ukweli Mchungu Kuhusu Anayejiita Mdogo wa Gwajima...!!!!

Amejitokeza mtu mmoja na kufanya press conference kwa jina anajulikana kama Methusela Gwajima , huyu Bwana ni Mwanasheria na ameajiriwa kwenye law firm ya Francis Stolla ambaye anagombea Urais wa TLS .
Huyu Mwanasheria sio mdogo wake na Gwajima wa kuzaliwa , bali ni ndugu katika Ukoo wao huo, naye ni wa KOLOMIJE .
Historia yake ya Kazi inaonyesha kuwa Aliwahi kuwa Katibu msaidizi wa CCM Wilaya ya Singida na katika Wilaya ya Nzega katika cheo hichohicho kwa nyakati tofauti. Kwa sasa ni miongoni mwa wanasheria wa CCM .
CCM wameamua kumtuma kada wao wakifikiri kuwa anaweza kuaminika au kunyamazisha mjadala wa kudai vyeti halisi vya BASHITE ambaye kwa sasa ana stress nyingi sana na amezidiwa kabisa kabisa , baada ya watanzania kuamua kumuunga mkono Rais Magufuli katika zoezi la kuhakiki Vyeti linaloendelea.
Mjadala wa BASHITE utashika kasi sana kwenye vikao vya CCM na hasa kwenye Halimashauri Kuu ambako tayari yule Mbunge wa kule Geita ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa ameomba kuwasilisha hoja mahususi kwenye kikao cha Halimashauri Kuu kuwa Bashite anakichafua Chama , hivyo anataka waazimie kuwa aondolewe na kama halitafanyika basi hoja itawasilishwa Bungeni ili kumwazimia PM ambaye yuko kwenye Mamlaka yao.