Jumapili, 30 Novemba 2014

FIFA:Madai mapya ya ufisadi yazuka

 
Rais wa FIFA Sepp Blatter akimkabidhi rais wa Urusi Vladmir Putin Haki za kuandaa dimba la dunia la mwaka 2018 


Madai zaidi yameibuka kuhusu ufisadi uliofanyika wakati wa shughuli ya kuwatafuta waandalizi wa kombe la dunia la mwaka 2018 na 2022.
Nafasi hizo zilichukuliwa na Urusi pamoja na Qatar. Gazeti la Sunday Times nchini Uingereza limesema kuwa rais wa Urusi Vladimir Putin alihusika pakubwa wakati nchi yake ilipokuwa ikitafuta nafasi hiyo na hata alimuomba rais wa FIFA Sepp Blattter kuisaidia kupata kura.
   
Rais wa FIFA Sepp Blatter akiikabidhi Qatar mkataba wa kuandaa kombe la dunia la mwaka 2022

Pia kuna madai kuwa nchi ya Qatar ilitumia ushawishi wake katika sekta ya gesi kupata kura kupitia kandarasi za kibiashara.
Urusi na Qatar zimekana kuhusika kwenye vitendo hivyo na ziliondolewa lawama na shirikisho la soka duniani FIFA hivi majuzi.

Man U na Arsenal zawika,Chelsea yazuiwa

           Mchezaji wa chelsea Wiilian akikabiliana na mwenzake wa Sunderland 

Mkufunzi Gus Poyet aliihangaisha timu ya Chelsea na kuwajaribu viongozi hao wa Ligi kupitia mchezo mzuru wa timu yake Sunderland.
Chelsea ilishindwa kuliona lango la Sunderland kupitia ngome mahsusi ya Sunderland iliowazuia washambuliaji wake.
Shambulizi kali ambalo nusra liiweke Chelsea kifua Mbele ni lile lakKiungo wa kati Willian ambalo liligonga chuma cha goli na kutoka nje.
Hatahivyo Mshambuliaji wa Sunderland pia naye alipiga mkwaju mkali uliogonga chuma cha goli la Chelsea huku Sunderland ikidhibiti safu ya kati na kuimarisha mashambulizi yake katika ngome ya Chelsea.
 
Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger afurahi baada ya timu yake kuichapa West Brom 1-0 
Mchezo huo ulikamilika na sare ya bila kwa bila na kuifanya Sunderland kuwa timu ya kwanza kuwazuia viongozi hao wa Ligi kufunga tangu msimu huu uanze.
Katika matokeo mengine Arsenal ilizuia kupoteza kwa mara ya tatu mafululizo pale walipoishinda West Brom ugenini.
The Gunners kama wanavyojulikana walianza mechi hiyo wakiwa na alama za chini zaidi baada ya kucheza mechi 12 katika kipindi cha miaka 32,lakini cichwa kizito cha mshambuliaji Danny Welbeck, kilihakikisha vijana wa Arsene Wenger wanatia kibindoni alama tatu.
        Wayne Rooney afurahia baada ya kufunga bao la pili dhidi ya timu ya Hull City 
Katika uwanja wa Old Trafford,bao la Robbin Van Persie Robin liliimarisha ushindi wa Manchester United dhidi ya Hull City na kuzima midomo ya wale waliokuwa wakijiuliza maswali mengi kuhusu hali ya mchezaji huyo msimu huu.
Miongoni mwa wakaosoaji wake ni kocha Louis Van Gaal ambaye aliyemuorodhesha mshambuliaji huyo katika mechi hiyo licha ya kudai kwamba alikuwa na mchezo m'baya wakati wa mechi kati ya Arsenal na Manchester wikendi iliopita.
Manchester United ilipata ushindi wa mabao 3-0 kupitia wachezaji wake Chris Smalling na nahodha Wayne Rooney.
katika matokeo mengine
Burnley 1 - 1 Aston Villa
Liverpool 1 - 0 Stoke
QPR 3 - 2 Leicester
Swansea 1 - 1 Crystal Palace
West Ham 1 - 0 Newcastle

ESCROW:Spika adaiwa kuwalinda washukiwa

 
                     Spika wa bunge la Tanzania Anne Makinda 
Speaker wa Tanzania Anne Makinda ameshtumiwa kwa kujaribu kuwatetea wale wanaodaiwa kuhusika katika kashfa ya ufisadi ya Escrow.
Kulingana na wachambuzi,wasomi na wataalam wa sheria hatua yake ya kujenga mazingira ya kuwapendelea washukiwa huenda ikasaidia kuwalinda watu hao.
Wakili maarufu mjini Daresalaam Sylvanus Sylivand ameliambia gazeti la the Citizen kwamba spika makinda alitarajiwa kufuata mfano mzuri uliowekwa na wenzake katika kashfa za awali ambapo bunge lina uwezo wa kuwashinikiza mawaziri na waziri mkuu kujiuzulu.
Ni wazi kwamba bunge linaweza kuishauri serikali kuwachukulia hatua viongozi wanaoshukiwa lakini si lazima kwamba rais afuate agizo hilo.
Kulingana na Sylivand,ni wazi kwamba kuna kitu kinachofichwa ili kuendesha ajenda tofauti ambayo itasadia aibu iliopata serikali.
  
                                           Bunge la Tanzania 


Muhadhiri wa chuo kikuu cha Dodoma Paul Loisulie amesema kuwa bunge sharti lichukue hatua kama taasisi.
''Kile ambacho kimetokea bungeni kuna uwezekano mkubwa kitaligawanya bunge na wananchi.''.
Inaonekana kwamba baadhi ya wabunge wa CCM wanajaribu wawezalo kuwatetea viongozi wanaoshukiwa bila kujali maslahi ya raia walio masikini.
Julius Mtatiro wa Chama cha Civic Front amesema kuwa CCM inataka kuwalinda viongozi wake wakuu ili raia wasielewe kuhusu kilichotokea baada ya Spika Makinda kuwataka baadhi ya washukiwa hao kupendekeza hatua ambazo zingefaa kuchukuliwa dhidi yao.
Kulingana na Profesa Kitila wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam Wabunge wana uwezo wa kuwaweka katika mizani watu watatu pekee ,rais,waziri mkuu na Spika na kile kilichokuwa kikendelea bungeni ni fursa ya wananchi kufikiria sana kabla ya kuipitisha katiba mpya.

Walichokisema Wabunge Kafulila, Peter Msigwa, Aeshi Hilary na Maige kuhusu maamuzi ya Bunge jana

news0
Kikao cha Bunge la Tanzania kilichoahirishwa siku ya jana Novemba 29 ni moja ya vikao ambavyo vilivuta hisia za watu wengi na kutengeneza historia nyingine mpya kutokana na mjadala wa ishu ya Escrow, baada ya kikao hicho kuahirishwa Wabunge Ezekiel Maige, Aeshi Hilary, David Kafulila na Mchungaji Peter Msigwa walizungumzia kuhusu maamuzi ya Bunge hilo.
…Tumekuwa na Bunge la kipekee sana katika muda wangu wa kuwa Mbunge karibu miaka nane sasa, hii ni experience yangu ya kwanza kuwa na kipindi kigumu kama hiki. Bunge limekuwa kwenye mtihani wa ama kuamua kulinda viwango vyake vya utendaji wa miaka yote au kuamua kuwa na viwango tofauti…” —Ezekiel Maige.
… Niwaombe Watanzania wawe wavumilivu kila kitu kina wakati wake na muda wake… Nilipongeze Bunge, nipongeze kamati ya usuluhishi vilevile nimpongeze Waziri Mkuu kwa kukubaliana na haya, ninaamini Serikali itachukua hatua zake…”– Aeshi Hilary.
…Niliamini siku zote kwamba kuna makosa yamefanyika katika utoaji wa fedha zile na chunguzi za CAG, PCCB, na hatimaye kamati ya PAC zimeonyesha hivyo na hatimaye Bunge limeweza kuchukua hatua hii. Kuna changamoto nyingi katika kupambana na mambo kama haya, kuna vitisho, kudhalilishwa mimi niliitwa ‘tumbili’ na kuna watu walitishia kuniua, lakini yote kwa ujumla wake ni changamoto katika kupambania yale ninayoamini…” –David Kafulila.
… Tumetimiza wajibu wetu kuishauri Serikali, tumeona watu wengine hawakutimiza wajibu wao… Upande wetu wa upinzani tuling’ang’ania kwamba watu wawajibike, niwasihi wananchi tuendelee kushirikiana kwa sababu mwisho wa siku hii ni nyumba ya kwetu sote mtu yeyote asiyetimiza wajibu wake lazima abebe mzigo wake …”—Mchungaji Peter Msigwa.

Maneno 6 ya Davido baada ya ushindi wa Diamond Platnumz Channel O 2014.

Davido 12 
Ushindi wa tuzo tatu za Channel O 2014 alizochukua Mtanzania Diamond Platnumz umekua mkubwa sio tu kwa Tanzania bali Afrika na kona zake ambapo miongoni mwa walioandika baada ya Diamond kushinda ni Davido.
Msanii huyu wa Nigeria ambae alifanya remix ya number one ya Diamond aliandika kwenye page yake ya instagram >>> TANZANIA STAND UP! HE DID IT na kisha akammention Diamond Platnumz.
Kwenye post hii ya Davido ambae hakupata tuzo yoyote ya Channel O japo alikua anawania, imepata likes zaidi ya elfu kumi na nne kutoka kwa followers wake ambao ni zaidi ya laki nne huku comments zikiwa ni zaidi ya mia saba.
Davido on Diamond
Davido 13