Jumatano, 15 Februari 2017

Naibu Waziri wa Afya kuweka hadharani majina ya mashoga Dar es Salaam

Naibu Waziri Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangalla amesema kuwa atawaweka hadharani wanaume wote wanaojihusisha na mapenzi ya jinsi moja (mashoga) ambao hufanya biashara hiyo kupitia mitandao ya kijamii.

Naibu Waziri aliyasema hao jana usiku kupitia ukurasa wake wa Twitter ambapo alieleza kuwa yupo katika ziara jimboni kwake na mara atakaporejea jijini Dar es Salaam kabla ya kuhamia Dodoma rasmi ataiweka orodha hiyo hadharani.

Aidha, amesema kuwa wale wote wanaodhani kuwa vita dhidi ya wanaume wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja ni mzaha, wataona hali itakavyokuwa kwani vita hiyo ni kubwa sana na wataishinda.

Kigwangalla ambaye pia ni mtaalamu wa afya alisema kuwa suala la mtu kuwa shoga si suala la kibaolojia (asili) bali ni watu tu kujiendekeza na hivyo watakahikikisha wanalikomesha.

Sheria ya ndoa ya Tanzania inapinga watu wa jinsia moja kujihusisha na mahusiano ya kimapenzi, lakini pia ni kitu kilichozuiliwa katika vitabu vitakatifu vya dini.


Dr. Kigwangalla,
Uchunguzi dhidi ya watuhumiwa wa ushoga unaendelea. Watakamatwa kimya kimya! Serikali ina mkono mrefu. Wakipatikana watatusaidia wenza wao!

 Dr. Kigwangalla, 
Kuna watu wanadhani vita dhidi ya ushoga ni ya mzaha, ni vita kubwa na tutaishinda. Mtandao ni mrefu na nitaendesha operation kamata kamata!

 Dr. Kigwangalla, H.
Namalizia ziara jimboni. Nikirudi Dar, kabla ya kuhamia rasmi Dodoma, nitaweka wazi orodha ya watuhumiwa wa ushoga wanaojiuza mitandaoni!

 Dr. Kigwangalla, H.
Kuna nchi marafiki zetu zinafanya jitihada za kupenyeza ushoga Tanzania na kudai ni haki ya binadamu kuchagua ampendaye, sisi tunasema NO!

 Dr. Kigwangalla, H.
Ushoga hauna addiction wala siyo wa kuzaliwa nao, wanaofanya hivyo wanajiendekeza tu! Ushoga siyo biological. Mashoga wote waache mara moja

Hana Hamu ya Kufanya Mapenzi na Mimi..Naomba Ushauri


Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 30, nina mpenzi wangu wa muda mrefu toka 2014 japo mapenzi yetu yamekuwa hayana muendelezo muzuri kutokana na tabia za huyu mwenzangu. Tulianza mahusiano yetu vizuri sana baadae mwenzangu alibadilika ghafla, nikaja kugundua alikuwa na mahusiano na wanaume wengine (zaidi ya mmoja) tukawa tumepotezana kwa mda kidogo coz alikuwa hapokei simu wala kujib text zangu alafu akawa ni mtu wa kusafiri sana kumbe alikuwa anasafiri na hao mabwana zake, siku nimekutana nae nilimuona na dalili za mimba roho iliniuma sana, mwanzoni alidanganya baadae akakubali akawa ametoa hiyo mimba akaomaba nimsamehe kwa sababu nampenda sana tena sana nikawa nmemsamehe.

Tukawa pamoja kwa mda mfupi baadae alianza tabia yake ya kuruka ruka na starehe kwa sana, niliamua kumuacha japo roho ilikuwa inaniuma alafu yeye hata hajali kila kitu kwake poa tu. Baadae alirudi akaanza kunitafuta akaomba msamaha kama kawaida yake, kupenda ni hatari sana jamani nilimsamehe tukaanza kuwa pamoja, alikaa kwangu kwa muda wa week, nikaanza michakato kwenda kutoa posa na mahari kwao.

Sasa alivyorudi nyumbani kwao akaanza tena unaweza mpgia simu anakuambia sipo nyumbani nipo kwa dada angu fulani, au kwa bibi nitarudi kesho, au nipo hospitali bibi anaumwa baadae simu inapotea hewani hata siku mbili akipatika anakuambia huku kijijini simu ilizima charge. Sasa kilichonichosha zaidi sasahivi hana hata hamu ya mapenzi kabisa tofauti na navyomjua mimi, huyu mpenzi wangu hapo awali alikuwa akiniona tu hutumii nguvu nyingi kumuandaa, lakini sasa hivi hata ukifanyeje hawezi kuwa tiyari hadi umpake mafuta kidogo. na unaweza kumuomba hata mwezi nzima anakuambia sijisikii, sina hamu.

Naomba ushauri wadau, nifanje ili aweze thamini hisia zangu, au hata kama nikimuacha nifanyeje coz nampenda sana huyu dada natamani awe mke wangu wa ndoa, kuna vitu huwa vinanifanya nimpende sana ni rafiki, mnataniana na kucheka, mpole ila sasa ndo hayo mambo yake, nilishajaribu kumuacha nashindwa nafuta namba kila kitu ila akinipigia tu au nikumuona tu nabadilisha mawazo.

Ni kweli Diamond Platnumz aliitwa na Polisi leo, sababu na kilichotokea vipo hapa tayari

Kama kuna picha umekutana nazo leo Mitandaoni zikimuonyesha Diamond Platnumz akiwa kituo cha Polisi akihojiwa nina uhakika utakua umejiuliza ni nini kilitokea.
Ni kweli leo Diamond aliitwa na Polisi na kwenye hiyo picha pia anaonekana Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Kamanda Mohamed Mpinga na kilichofanya aitwa Polisi ni ile video fupi iliyosambaa ikimuonyesha Diamond akiendesha gari bila kufunga mkanda na kucheza.
Diamond amethibitisha hilo kupitia Instagram yake kwa kuandika >> ‘picha hizo leo nilireport kituo kikuu cha polisi wa usalama barabarani kutokana na video clip tuliyopost naendesha gari barabarani bila kufunga mkanda na pia kuachia usukani na kucheza
Nikapewa Onyo na kulipa faini kwa mujibu wa sheria… tafadhali watanzania na Vijana wenzangu… tuhakikishe tunafunga mikanda pindi tupandapo na tuendeshapo Magari Maana ni Hatari kwa Maisha yetu na inaweza kukupeleka kunyea debe.

Baada ya Kulianzisha,,Makonda Yupo Hatarini Kuuawa,Vigogo wa Madawa ya Kulevya Wapanga Mikakati ya Kummaliza kwa Gharama Yeyote Ile..!!!!

Wakati vita dhidi ya madawa ya kulevya jijini Dar vikipanuka na kugeuka kuwa suala la kitaifa, kuna kila dalili kuwa usalama wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda upo hatarini, Risasi Mchanganyiko limebaini.
Juzi Jumatatu, Paul Makonda alijitokeza tena hadharani na kutoa ufafanuzi wa mambo kadhaa yanayohusiana na vita alivyovianzisha, huku ikiwa ni mara yake ya tatu kutaja majina ya wanaojihusisha na madawa ya kulevya, safari hii, akitoa orodha ya watu 97.

HATARI YAKE IKOJE?
Biashara ya ‘unga’ ni moja kati ya biashara chache zenye fedha nyingi duniani, ambayo bahati mbaya inapigwa vita na serikali nyingi. Watu wanaojihusisha na shughuli hii, wana fedha nyingi na wako tayari kufanya lolote linalowezekana kuifanya biashara yao kuwa salama.
Kwa Paul Makonda kutangaza vita hadharani, tena akitaja majina ya watu na njia zinazotumika kuuleta, kuusambaza na kuusafirisha, anajiweka katika nafasi mbaya ya kuwa mlengwa wa wafanyabiashara hao, hasa kwa kuwa kukamatwa kwao siyo tu kutaharibu biashara yao hiyo, bali pia wao wenyewe watapotea.
Mfano mmojawapo wa jinsi watu wanaojihusisha na biashara hiyo walivyo na uwezo mkubwa, ni kesi ya bilionea wa unga wa Colombia, Pablo Escobar, aliyeuawa Disemba 2, 1993, baada ya mahakimu zaidi ya 30 waliosimamia shauri hilo kuuawa, licha ya kuendesha kesi hiyo wakiwa mafichoni, tena sauti zao zikiwa zimewekwa mawimbi ya kutofahamika.

MAADUI ZAKE WAMEONGEZEKA
Awali, ilionekana ni wauza madawa ya kulevya pekee ndiyo ambao wanaweza kusemwa kuwa ni maadui zake, lakini baada ya mazungumzo yake na vyombo vya habari Jumatatu iliyopita, watu ambao watafurahia kuona kiongozi huyo kijana anapatwa na matatizo, wameongezeka.
Watu hao ni pamoja na wamiliki wa maduka ya kubadilishia fedha maarufu kama Bureau de Change, wafanyabiashara wa mitungi ya gesi, wamiliki wa mahoteli na klabu za kamari (Casino), achilia mbali watoto wa viongozi wakubwa tokea serikali ya awamu ya tatu, chini ya Benjamin Mkapa.
KWA NINI HAWA?
Licha ya kushangazwa na wingi wa maduka ya kubadilishia fedha (alisema yapo zaidi ya 200 kwa Dar pekee), lakini pia aliyatuhumu kufanya miamala inayozidi kiwango kinachotakiwa kisheria, hivyo kuufanya mzunguko wa fedha zinazopitia hapo kuwa mkubwa.
Alisema wingi huo wa fedha, unatia shaka kuwa huenda unatumiwa na watu wa biashara ya madawa ya kulevya katika kutakatisha fedha. Kwa vyovyote, wenye maduka hawa hawajapendezwa na tuhuma dhidi yao na hivyo nao kuingia vitani kimyakimya.
Biashara ya mitungi ya gesi nayo ilitajwa kuwa ni mojawapo ya njia zinazotumiwa na wafanyabiashara hao kuficha madawa hayo wakati wakisafirisha kutoka au kwenda ughaibuni.
Aidha, alidai kuna hoteli kadhaa kubwa zenye wakazi wa kudumu, ambao wanatambuliwa na wamiliki wake, hivyo atahakikisha anawafanyia kazi, kitu ambacho kinaongeza idadi ya maadui, kama ilivyo kwa wamiliki wa nyumba 200 waliosemwa kuwa wanaruhusu biashara hiyo kufanywa ilhali wakijua ni kosa kisheria.
MBINU ZINAZODAIWA KUANDALIWA
Baadhi ya wanaharakati wanaopinga biashara ya madawa ya kulevya, ambao waliomba hifadhi ya majina yao, wamesema mbinu mbalimbali zinaweza kutumika ili kumdhuru kiongozi huyo, aliyewahi kuwa mkuu wa wilaya ya Kinondoni.
Mbinu hizo ni pamoja na kumwinda na kumuua kwa risasi, kitu ambacho ili kukidhibiti, wameomba kuimarishwa kwa ulinzi wake, nyumbani, kazini na hata awapo barabarani.

VIDOSHO, AJALI ZA KUTENGENEZWA
Eneo lingine alilotahadharishwa kujihadhari nalo ni pamoja na wasichana warembo, kwani wanaweza kutumiwa na maadui ili kumtia matatizoni, ikiwemo kumwekea sumu katika chakula, kinywaji au hata kumdhuru kwa namna nyingine.
Wadau hao wamelitaja eneo lingine la hatari linalopaswa kuangaliwa zaidi, ni kwa maadui zake hao kuweza kumtengenezea ajali ya kumdhuru, ili mradi wafanikiwe kuzima harakati zake za madawa ya kulevya alizoanzisha na kuungwa mkono na watu wengi.

KUHUSU ULINZI, HUYU HAPA SIRRO
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro alizungumza na Risasi Mchanganyiko juu ya ulinzi wa kiongozi huyo. Akionyesha mshangao, alisema suala hilo siyo jambo la kuuliza kwa sababu wao wanaelewa nini kinapaswa kufanyika.
“Tunajua ukubwa wa vita hivi na madhara yake pia tunajua, huyu ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, tunampatia ulinzi imara kabisa na kwa hili wala watu wasiwe na wasiwasi.”

Huu Ndio Msikiti ambao Diamond Anapang Kuujenga..!!!

Diamond amejitolea kujenga msikiti.
Hitmaker huyo wa ‘Marry You’ amesema kwa sasa anajenga msikiti huo lakini upo mkoani Mtwara.
“Mimi nakushukuru sana mama yangu, asante sana. Naamini kabisa nitakuja Mtwara, Mtwara kule sasa hivi kuna msikiti ninaujenga na inshallah nikimaliza nitaenda kuuzindua,” alisema Diamond Jumamosi iliyopita kwenye sherehe ya 40 ya mtoto wake Nillan iliyofanyika nyumbani kwake Madale.
Diamond alisema maneno hayo wakati akimshukuru mama mmoja ambaye alimkabidhi viwanja viwili vya hekta 17 kwa kila kimoja huku kimoja kikiwa ni kitalu cha gypsum.