Jumatano, 1 Oktoba 2014

Tangazo la biashara lazua zogo China

 
Polisi wanachunguza ikiwa kampuni hiyo ilivunja sheria ya matangazo ya biashara 

Kampuni moja nchini China inakabiliwa na tisho la kutozwa kiwango kikubwa cha faini kwa kuwakodi wanawake kuvua nguo zao kwenye treni mjini Shanghai kwa lengo la kutangaza biashara ya kampuni hiyo kwa abiria.
Katika moja ya video iliyowekwa kwenye mtandao wiki jana, wasichana wawili ghafla walianza kuvua nguo zao na kusalia na nguo za ndani pekee katika treni hiyo iliyokuwa imejaa watu.
Abiria walionekana wakirekodi wasichana hao kwa simu zao za viganjani lakini mwanamke mmoja wa makamo aliwakaripia sana.
Mwanamume mmoja kutoka katika kampuni ya huduma za dobi ambayo wasiahana hao walikuwa wakiitangaza, naye alionekana akiokota nguo za wasichana hao walizokua wanavua.
Baada ya filamu ya wasichana hao wakivua nguo kuenea mitandaoni, polisi waliwasiliana na kampuni hiyo kujibu walichokuwa wanakifanya.
Kampuni hiyo inayotoa huduma za dobi ,kwa jina 'Tidy Laundry', ilipoona ikipata sifa mbaya, iliamua kuomba radhi kwa kosa hilo ikisema kuwa ilinuia tu kutangaza huduma zake kwa wabiria waliokuwa ndani ya treni hiyo.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa jarida la Shanghai Daily.
Wamiliki wa kampuni hiyo, wanasema kila aliyehusika kwenye tukio hilo alikuwa muigizaji aliyekuwa amekodiwa.
Hata hivyo huu bila shaka sio mwisho wa masaibu ya kampuni hiyo-polisi wanasema wanachunguza ikiwa ilivunja sheria zinazopiga marufuku matangazo ya kibiasga ambayo yanakera jamii.

AL-SHABAAB WAPATA PIGO SOMALIA

 
Wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab 

Wanajeshi nchini Somali wameidhibiti milima ya Galgala kutoka kwa wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab,kulingana na utawala wa eneo hilo.
Wanamgambo hao walikuwa wakiidhibiti milima hiyo ya Kaskazini mwa taifa hilo kwa miaka kadhaa.
Waziri wa habari wa Puntland amesema kuwa kamanda wa Alshabaab katika eneo hilo alisalimu amri miezi minne iliopita.
Kundi hilo linaloshirikiana na lile la Al-Qaeda lina makao yake makuu kusini na katikati mwa somalia ambapo vikosi vya Umoja wa Afrika vinafanya mashambulizi.
Abdiweli Hirsi Abdille,ambaye ni waziri wa habari wa jimbo la kaskazini mashariki mwa Somalia Puntland amesema kuwa vikosi vya serikali vimeliteka jimbo hilo la Glagala katika mashambulizi yaliotekelezwa alfajiri.
Hatahivyo hakutoa maelezo yoyote kuhusu wafungwa ama waliojeruhiwa.
Lakini kituo cha redio cha Al Furqan,kinachojulikana kwa kuwapendelea wapiganaji wa Al-Shabaab kimeripoti kwamba magari mawili ya kijeshi yaliharibiwa na wanajeshi 16 kuuawa.
Galgala ni eneo la kipekee la Puntland ambalo limekuwa chini ya udhibiti wa Alshabaab.
Kamanda wa Al-Shabaab katika eneo hilo Said Atom alijiunga na vikosi vya serikali mwaka huu na kuwawacha wapiganaji wake katika jimbo la Puntland.
Wapiganaji wa Al-Shabaab wamefurushwa kutoka miji mikuu katika kipindi cha miaka ya hivi karibuni ,lakini bado wanadhibiti miji midogo katika maeneo ya mashambani.

UCL: PSG walivyoivunja rekodi ya Barcelona msimu huu – Beyonce na Jay Z wakishuhudia

IMG_7650.PNG
Mwanasoka wa kibrazil David Luiz jana usiku alikuwa mchezaji wa kwanza kuifunga goli FC Barcelona katika msimu mpya wa soka barani ulaya.
Luiz alifunga goli hilo katika dakika ya 11 ya mchezo wa Champions League kati ya klabu PSG dhidi ya Barca.
Mchezo uliopigwa kwenye dimba la Stade de France na kuhudhuriwa na mastaa kama Rais wa zamani wa nchi hiyo Sarkozy, David Beckham na rapa Jay Z pamoja na mkewe Beyonce.
Matokeo ya mchezo huo ni ushindi wa 3-2 kwa PSG dhidi ya kikosi cha Luis Enrique.
Lionel Messi na Neymar walifunga magoli ya Barca huku Matuidi na Verrati wakihitimisha kipigo hicho cha kwanza cha Barcelona katika
Michuano yote ya msimu huu.

IMG_7651.PNG

UCL: Matokeo ya Man City vs AS Roma na rekodi mpya aliyoiweka Totti

IMG_7652.PNG
Mabingwa wa ligi kuu ya Uingereza klabu ya Manchester City imeendelea kutopata matokeo chanya katika michuano ya ligi ya mabingwa wa ulaya kwa mara ya pili mfululizo msimu huu.

Wakicheza kwenye uwanja wao wa Etihad dhidi ya AS Roma ya Serie A, Sergio Aguero aliipatia timu yake goli katika dakika ya 4 kupitia mkwaju wa penati.
Lakini dakika 19 baadae Francisco Totti ‘Mfalme wa Roma’ akaifungia goli la kusawazisha Roma na kuandika historia ya mchezaji mwenye umri mkubwa zaidi kufunga goli kwenye michuano ya ulaya.
Man City sasa inakuwa imeshindwa kupata matokeo chanya katika mechi 2 za kwanza cha UCL – wiki mbili zilizopita walifungwa na Bayern Munich.
Timu zilipangwa hivi
Manchester City: Hart 7; Zabaleta 6.5, Kompany 6, Demichelis 5.5, Clichy 6; Navas 5 (Milner 46, 6), Toure 5.5, Fernandinho 6, Silva 7; Aguero 6.5 (Jovetic 84), Dzeko 6 (Lampard 57)
Subs (not used): Caballero, Sagna, Kolarov, Mangala
Goals: Aguero (Pen, 4)
Booked: Zabaleta
Roma: Skorupski 6; Maicon 6 (Torosidis, 89), Manolas 6, Yanga-Mbiwa 6.5, Cole 6; Pjanic 7.5, Nainggolan 6.5, Keita 6.5; Florenzi 5.5 (Holebas 83), Totti 7 (Iturbe 72, 6), Gervinho 7.
Subs (not used): Curci, Ljajic, Destro, Paredes
Goals: Totti (23)
Booked: Maicon, Nainggolan
Referee: Bjorn Kuipers (Holland) 7
Star man: Miralem Pjanic
Attendance: 37,509

UCL: Matokeo ya Chelsea vs Sporting Lisbon haya haya

IMG_7653.PNG
Usiku wa jana watu wawili waliowahi kuwa vipenzi vya nchi ya Ureno – Jose Mourinho na Nemanja Matic walirejea nchini humo katika jiji la Lisbon lakini safari hii wakiwa kama wapinzani.
Huku Mourinho akionekana kuchukua ‘attention’ yote ya vyombo vya habari ndani ya jiji Lisbon, Nemanja Matic alikuwa kasahaulika.
Lakini katika dakika ya 34, mchezaji huyo wa zamani wa Benfica aliifungia goli pekee Chelsea katika mchezo huo.
Matic alifunga goli hilo kwa kichwa baada ya kuachwa bila kukabwa vizuri na mabeki wa Sporting Lisbon.
Mchezaji wa zamani wa Manchester United Luis Nani alikuwa akiitumikia Sporting jana na hakuwa kwenye kiwango kizuri katika kipindi cha kwanza – kipindi cha pili alijitahidi lakini akashindwa kubadili matokeo ya mwisho dhidi ya vijana wa Jose Mourinho.
Takwimu na timu zilizopangwa
Sporting (4-3-3): Patricio 7; Cedric 6, Mauricio 5.5 (Oliveira 63, 6), Sarr 5, J.Silva 5; Mario 6, Carvalho 6, A.Silva 6 (Montero 81); Carrillo 6.5 (Capel 81), Slimani 6, Nani 6.
Subs not used: Marcelo, Jefferson, Martins, Rosell.
Bookings: Carvalho, Mario, Cedric, Mauricio
Manager: Marco Silva
Chelsea (4-2-3-1): Courtois 6; Ivanovic 6, Cahill 6, Terry 6, Luis 6.5; Matic 8, Fabregas 7; Schurrle 5 (Willian 57, 6), Oscar 7.5 (Mikel 71, 6), Hazard 7 (Salah 84); Costa 6.
Subs not used: Cech, Zouma, Azpilicueta, Remy.
Bookings: Ivanovic, Hazard, Luis Filipe, Fabregas
Manager: Jose Mourinho.

Amber Rose kaitaja sababu nyingine ya kuachana na Wiz Khalifa, picha ya ushahidi iko hapa pia

Amber1 
Kuvunjika kwa ndoa ya mastaa Amber Rose na Wiz Khalifa kumeendelea kuchukua nafasi kwenye headlines za dunia na hii ni baada ya Amber kutaja chanzo mojawapo cha kuvunjika kwa uhusiano huo.
Kwenye interview ya Radio Amber amesema kingine kilichomkasirisha ni kuona Wiz anawaendekeza warembo flani wawili mapacha ambao inaaminika amekua akijihusisha nao kimapenzi.
Amber amesema alipenda kuiokoa ndoa yake ili waendelee kuwa pamoja lakini anaeonekana kukataa kuendelea kuwa kwenye ndoa ni Wiz mwenyewe, Amber anasema hata taarifa za mwanzoni kwamba walitengana siku nyingi kabla ya kutaka talaka zilikua za uongo…. hakufanya maamuzi yao sababu alitaka kuiokoa ndoa yake.
amber 2
 
Amber amemshutumu Wiz kwa kutoka kimapenzi na hawa mapacha kwenye hii picha hapa chini…
http://i1.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2014/10/amber-3.png