Jumamosi, 11 Machi 2017

NINI CHA KUFANYA BAADA YA KUMALIZA KUFANYA MAPENZI

Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia siha njema na pia kwa kunipa mwangaza wa kuandika hiki ninachokusudia.
Pia niwashukuru wapenzi wasomaji wa safu hii ambao tumekuwa tukiwasiliana na kushauriana hili na lile katika tasnia hii adhimu ya mapenzi. Nawakaribisha sana!
Labda kwa wale wasiofahamu niwaambie tu kwamba dhana ya mapenzi ni dhana yenye wigo mpana sana na ndiyo maana hutasikia hata siku moja tumepumzika kuizungumzia.
Hata hivyo, tunachofanya siku zote ni kukumbushana kwa yale tunayoyafahamu na kushauriana kwa pale tunapohisi wengi hufanya makosa.
Baada ya kusema hayo sasa nigeukie mada yangu ya leo ambayo kwa kiasi kikubwa inawahusu wale walio kwenye ndoa na kikubwa nazungumzia yale ambayo wawili waliotokea kupendana kwa dhati wanatakiwa kuyafanya mara baada ya kumaliza kufanya tendo la ndoa.
Nalazimika kuandika makala haya baada ya kubaini kuwa wengi wamekuwa wakifanya makosa na kujikuta wakishamaliza kufanya tendo hilo takatifu, kila mmoja anageukie kwake kisha kuuchapa usingizi.
Sisemi kwamba ni lazima kuyafanya haya nitakayoyaeleza leo ila 
yakifanywa huwa na manufaa yake na mara nyingi yanaboresha uhusiano.
Kuoga pamoja
Mtakuwa ni watu wa ajabu kama mtamaliza kufanya tendo hilo kisha kila mmoja kulala na majasho yake. Wapo
wasiojali katika hili na kuona kuoga au kutooga ni uamuzi wa mtu. Elewa linapokuja suala la usafi inashauriwa mkimaliza lazima muoge.
Wapo wanawake ambao wakishamaliza hukimbilia kuwaandalia maji wenza wao, wakishaoga ndipo nawo huenda kuoga. Hivi unaona ugumu gani kwenda kuoga na mwenza wako? Unaijua raha ya kuoga na huyo wako wa maisha?
Wanaofanya hivyo wanajua raha yake na wewe ambaye hujawahi, anza leo. Mmemaliza mambo yenu, chukuaneni kimahaba, elekeeni bafuni kisha ogeshaneni kimahaba.
Baada ya hapo rudini chumbani, mkishajifuta maji pandeni kitandani mkiwa wapesi.
Kusifiana
Hakuna muda maalum uliotengwa kwa ajili ya wanandoa kusifiana. Hilo linaweza kufanyika wakati wowote lakini pale mnapomaliza kufanya tendo la ndoa ni lazima utakuwa na jambo zuri la kumuambia mwenza wako.
Msifie kwa utundu na ubunifu wake. Msifie pia kwa mapenzi matamu anayokupa na ikibidi mpe sifa ya uzuri wake kiasi cha kukufanya kila unapokuwa karibu yake ujisikie amani ya kupitiliza.
Wapo ambao hawana kabisa kasumba ya kuwasifia wala kuwashukuru wenza wao kwa mazuri wanayofanyiwa. Yaani wao wanachukulia kila kitu poa tu bila kujali kwamba kusifiana kunanogesha mambo.
Kuelekezana
Kwenye kale kamchezo, wapo ambao wanakosea, kuelekezana na kukosoana kwa wapenzi ni jambo la kawaida. Yawezekana mwenza wako alifanya kitu ambacho hakikukufurahisha wakati mkiendelea na burudani yenu, mnapomaliza mwambie lakini kwa lugha ya kimahaba na ya upole. Naamini kwa kufanya hivyo atakuelewa na kubadilika.
Zungumzieni maisha
Huu ni wakati muafaka wa kujadili changamoto na malengo katika maisha yenu. Hapa akili zinakuwa zimetulia na kila mmoja anakuwa na mawazo chanya kwa mwenza wake. Jadilini mambo yenu, wekeni mikakati ya kuliboresha penzi na maisha yenu kwa ujumla.
Hayo ni baadhi ya mambo ambayo mnashauriwa kuyafanya pale mnapomaliza kufanya tendo la ndoa.
Yapo mnayotakiwa kuyaepuka ili kutotibua furaha iliyopatikana. Hayo nitakuja kuyaeleza katika makala zinazokuja kupitia ukurasa huu.

Wakati Mwingine Wanasiasa Wawe Wakweli, Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa Hakuwa na Ziara Rasmi Tanzania..!!!!

Naona watu wameibeba hii ya Katibu Mkuu wa UN kama "ajenda" tena,huku namuona Mtatiro akirusha makombora,na huku Mbunge Msigwa akirusha kwa upande wa pili.Vijana nao wamebeba mitandaoni kama ajenda ya kumalizia week kimjadala.
Watu wanatakiwa kuelewa tu,mambo mengine sio lazima tuingize siasa saaaanaa.António Guterres hakuwa na ratiba ya ziara ya Tanzania.Ziara yake ilipangwa kufanyika Somalia ili kuonana na Rais mpya kuhusu baa la njaa na ukame unaolikumba eneo hilo.
Sehemu ya pili ikawa Kenya kukutana na Kenyatta,na hii ni kwa sababu,nchini Kenya kuna kambi kubwa sana ya wakimbizi ya Dadaab, inayokaliwa na Wasomali,ambao sera ya Trump ya katazo la Wasomali kuingia US imewaathiri...Umoja wa Mataifa lazima iwahikikishie Kenya ushirikiano ktk kipindi hiki cha mabadiliko ya sera za uhamiaji nchini Marekani.
Maana hivi karibuni,wakimbizi wengi wenye asili ya Somalia ambao walikuwa wafanyiwe "resettlement" na Shirika la Wahamiaji la Kimataifa (IMO),kutoka kambi ya Dadaab kwenda Marekani wamezuiliwa kutokana na sera mpya ya Marekani,hivyo kuwafanya waendelee kusalia Kenya.
Hapa Tanzania alikuwa tu "On Transit",sababu ndege aliyotumia kusafiri ni SwissAir.Schedule ya SwissAir ni Zurich-Nairobi-Dar-Zurich.Na inapotoka Nairobi kuja Dsm kabla ya kwenda Zurich,ndege huwa inakaa Dsm zaidi ya saa moja na nusu.Sasa mtu mkubwa kama Antonio hawezi kukaa muda wote huo ktk ndege wakati anaweza kushuka na kufanya mazungumzo ya kidiplomasia na viongozi wa Tz kama wadau wa Umoja wa Mataifa.
Aina hii ya ugeni ni ya kawaida sana katika viwanja vya ndege ambayo hutumika kama "connection centre".Ukienda Jomo Kenyata International Airport VIP Lounge utakutana na Marais wengi na viongozi wengi maarufu wakipiga soga na Mawaziri wa Mashauriano ya Kigeni wakati wakiwa "on transit".Bole International Airport pale Addis Ababa VIP-Lounge humkuti Waziri Mkuu wa Ethiopia,lakini toka mawio mpaka machweo ya jua,viongozi wa kimataifa huwa "On Transit" kuelekea katika safari zao tarajiwa.
Hata kwa kumtazama tu,wale waliowahi kupanda SwissAir First Class,watakubaliana kuwa alichokuwa amekivaa Guterres ni zile pyjamas (pajama) za abiria wa daraja la kwanza ambao hupatiwa ndani ya ndege kwa ajili ya kupumzikia kwa safari ndefu.Dressing code tu ya pyjamas za SwissAir zinaashiria Katibu Mkuu alikuwa "On Transit".Ratiba na Tanzania haikuwepo.
Sio wa kwanza Guterres kupita tu bila kuonana na Rais,wapo viongozi wengi hupita kama "On transit" hapa Dsm,na husalimiana na viongozi wa chini wa serikali.Mfano King Mswati,yeye "refueling point" yake huwa ni Dsm,katika safari zake za kutoka Mbabane kwenda ama Abu Dhabi shopping au sehemu nyingine,kituo chake cha Cattering na refueling ni Dsm.Toka enzi za JK mpaka sasa,huwezi kumkuta JK anakimbizana kumpokea Mswati,bali utamkuta Membe kwa minajili ya kidiplomasia akimsubiri King Mswati.
Uwanja wetu wa Dsm hutumika kwa ajili ya "On Transit Passengers" na "On Transfer Passengers"."On Transit Passengers" ni wale abiria ambao hupita uwanjani wakiwa ndani ya ndege bila kushuka na kuchukua abiria wengine au kushusha na kuunganisha na ndege hiyohiyo kuelekea "destination" iliyokusudiwa.Mfano wa ndege zenye safari ya aina hii Julius Nyerere Int'nal Airport ni SwissAir (Zurich-Nairobi-Dsm-Zurich),Ethiopia Airways (Addis Ababa-Dsm-Znz au Addis-Dsm-Hahaya Comoro),Oman Air (Muscat-Znz-Dsm-Muscat),Mauritius Air nk.
Siku kadhaa kiongozi wa Mauritius alipita Dsm na Mauritius Air na kuunganisha kuelekea Addis Ababa kwenye mkutano wa viongozi wa Afrika.Toka Sir Seewoosagur Ramgoolam Port Louis kupitia Julius Nyerere International Airport mpaka Addis Ababa.
Walikutana tu na Rais wetu ndani ya ndege,wakapeana mkono na kila mtu akarudi kwenye presidential Suit room yake ya "First class".
Hii ni dalili ya uwanja wetu kukua na kuanza kuwa moja ya "Connection" kubwa ya sehemu mbalimbali za Afrika na dunia.Sasa tunapokea abiria wote wa kutoka Msumbiji kwenda Dubai kupitia Dsm,abiria wa Mayote na Comoro kwenda Dubai.Abiria wa kutoka Mauritius kuja Afrika ya Mashariki na Mashariki ya kati ya Asia.
Tuanze kuzoea,kuwa sio kila abiria ni "mgeni rasmi" wa nchi,wengine wanakuwa wapita njia.Waziri Mkuu wa Ethiopia angekuwa anashinda Airport kama kila kiongozi anayepita Bole Int'nal Airport atamsubiri kumpokea.
Mkuu wa Mkoa wa Dsm angekuwa anajipanga kila siku kupokea viongozi na mawaziri mkoani kwake,maana ofisi zote kubwa zipo kwake.Waziri wa Mambo ya ndani akiwa Simiyu ni "mgeni",ila kwenye viunga vya Dsm ni mpita njia tu.
Hence;haikuwa sehemu ya ratiba,ndio maana ni Balozi Mahiga badala ya Rais JPM

P-Funk: Diamond Anapaswa Kutulia Kidogo, lasivyo Watu Watamchoka


Producer mkongwe wa Bongo Records, P-Funk Majani, amesema kila siku akiendelea kusikia kuhusu Wasafi, itafika muda atawachoka.



Amedai kuwa ili label hiyo iendelee kufanya vizuri kwa muda mrefu, ni lazima ibadilishe sound, kuja na ladha au wasanii wapya. Amedai pia kuwa pamoja na ukubwa wa Diamond, kama asipotengeneza hali ya watu kummiss, watu watamchoka mapema.

Majani amesema hayo kwenye kipindi cha The Playlist cha Times FM kinachoendeshwa na Lil Ommy.

DODOMA: Bashe, Malima na Musukuma Mbaroni Wakidaiwa Kupanga Kuhujumu Vikao Vinavyoendelea

Wabunge wawili Bashe na Musukuma wamekamatwa leo asubuhi kabla ya kikao cha Kamati Kuu kuanza kutokana na kudaiwa kubeba ajenda ya "kwenda kumpinga Mwenyekiti".

Kundi hili la wabunge lililokuwa na mjumbe mwingine, Adam Malima lilipanga Peter Serukamba ndiye awe kinara wa kuanzisha hoja ya kumpinga mwenyekiti.

Hata hivyo, kabla ya kutimiza azma yao walijikuta mikononi mwa Polisi huku Serukamba akidhibitiwa na kukosa kuwasilisha hoja ya kumpinga mwenyekiti, Magufuli.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa amethibisha na kuwataja waliokamatwa kuwa ni Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe na Mbunge wa Geita vijijini ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita, Joseph Kasheku maarufu kama Musukuma na Malima.

“Hao ndio waliokamatwa na bado tunaendelea na mahojiano na wengine bado tunaendelea kuwatafuta,”amesema Mambosasa.

Chanzo chetu kimedokeza kwamba huenda wakaendelea kushikiliwa hadi pale mkutano mkuu utakapomalizika!

Chanzo:Jamii Forums

Rumishael Shoo (Rummy) Ashikiliwa na Polisi Kwa Tuhuma za Dawa ya Kulevya


Kamanda Sirro akiongea na waandishi wa habari amesema Jeshi la Polisi limefanikiwa kuwakamata wahalifu mbalimbali, silaha na magari mawili aina ya Noah yaliyokuwa yakitumika kufanya uhalifu.

Miongoni mwa aliowataja Kamanda Sirro ni pamoja na Vanessa Mdee na Rumishael.

Huyu Rumishael amekuwa akitajwa kwa muda mrefu kujihusisha na biashara hiyo haramu, aliweza kuwaweka polisi mikononi ikiwa pamoja na kuwajengea kituo cha polisi Mwananyamala(Inasemekana).

Huyu huyu mwaka jana TRA ilishikilia magari yake matatu ambayo ni V8 gold plated,Benz gold plated na Benzi metalic blue ambayo yalibainika kuingizwa nchini bila kulipiwa kodi.