Jumapili, 1 Mei 2016

TANZANIA YA VIWANDA KUANZIA MOROGORO

SERIKALI ya Awamu ya Tano imeanza kutekeleza kwa vitendo azma yake ya kujenga uchumi unaotegemea viwanda baada ya kuzindua ujenzi wa mradi maalumu wa uwekezaji wa viwanda mkoani Morogoro ili kukuza uchumi na kuongeza ajira nyingi kwa vijana nchini.
Utekelezaji huo ni kutokana na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage juzi kuzindua eneo maalumu la ujenzi wa miradi ya uwekezaji la Star City katika Manispaa ya Morogoro.
Eneo hilo la miradi ya uwekezaji lina ukubwa wa ekari 10,661 na lilikuwa ni shamba la mkonge Tungi Sisal Estate ambalo kwa sasa likijulikana kwa jina la Dominio Plantation Limited (DPL).
Waziri Mwijage kabla ya kuzindua eneo hilo maalumu la uwekezaji, alisema Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli imeanza utekelezaji wa Tanzania kuwa nchi ya viwanda kwa kuanza na Mkoa wa Morogoro.
“Morogoro haijapendelewa isipokuwa ina historia tangu wakati wa Serikali ya Awamu ya Kwanza ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ambapo Waziri Jamal (Amir) aliwezesha kujengwa kwa viwanda hivi hapa Morogoro,” alieleza Mwijage na kuongeza: “Morogoro ina bahati ya kuwa na sifa ya kujenga viwanda kutokana na mazingira na jiografia yake naweza kusema ina bahati ya kuzaliwa ilivyoumbwa na Mungu kuvutia uwekezaji.”


75000 WAFANYA MTIHANI KIDATO CHA 6 LEO

WATAHINIWA 74,920 leo wanaanza kufanya mtihani wa kuhitimu Kidato cha Sita katika shule mbalimbali nchini huku watahiniwa 11,597 wakifanya mtihani wa Ualimu.
Ofisa Habari wa Baraza la Mitihani (NECTA), John Nchimbi amesema kuwa mtihani wa kidato cha sita unaanza leo hadi Mei 19, mwaka huu. Nchimbi alisema kati ya watahiniwa hao waliosajiliwa, watahiniwa 65,610 ni watahiniwa wa Shule huku watahiniwa wa Kujitegemea wakiwa 9,310.
“Kati ya watahiniwa wa shule 65, 610, watahiniwa wasichana ni 24,549 na wavulana ni 41,061 huku watahiniwa wa kujitegemea wasichana wakiwa ni 3,176 na wavulana ni 6,134,” alisema Nchimbi.
Kwa upande wa mtihani wa ualimu, Nchimbi alisema kati ya watahiniwa 11,597 watakaofanya, watahiniwa 10,942 wanafanya Ualimu Daraja A na watahiniwa 654 wanafanya mtihani wa Stashahada ya Sekondari na mmoja anafanya Stashahada ya Ufundi.


SERIKALI KULIPA MADENI YA WALIMU YALIYOHAKIKIWA TU


WAZIRI wa Fedha na Mipango Dokta Philip Mpango, ameliambia Bunge mjini DODOMA, kuwa serikali inaendelea kuhakiki madeni ya walimu yaliyowasilishwa kwa ajili ya malipo baada ya kubaini kuwepo kwa udanganyifu kwenye baadhi ya madai hayo.

Waziri Mpango amesema kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2015/2016, serikali ilipokea madai yenye jumla ya shilingi Bilioni 29 na Milioni 800 na imelipa shilingi Bilioni 20.125, huku madai mengine yakizuiwa baada ya kubainika hayakuwa halali.
Alitolea mfano wa mtumishi mmoja aliyewasilisha madai ya shilingi Milioni 600 badala ya shilingi laki 6, huku madai mengine yaliyolipwa miaka ya nyuma yakiwasilishwa kama madeni mapya.
Dokta Mpango amesema kuwa serikali inathamini mchango wa walimu katika maendeleo ya sekta ya elimu nchini na kwamba itaendelea kulipa madai yaona watumishi wengine wa umma baada ya kuyachambua, kuyahakiki na kujiridhisha kuwa ni halali.



Prof. Lipumba Apongeza Mipango ya Rais Magufuli

Mwanasiasa mkongwe ambaye pia ni mtaalamu wa masuala ya uchumi nchini Profesa Ibrahimu Lipumba amesema anaunga mkono mpango wa serikali wa miaka mitano huku akisema ni vema serikali ihakikishe inawekeza zaidi katika nishati ya umeme ili kufikia lengo la kuwa nchi ya viwanda.
Wakati tayari mpango wa serikali ukiwa umekwishawasilishwa kwa miaka mitano ijayo, ambapo umeanisha namna utakavyofanikisha asilimia 40 ya ajira ifikapo mwaka 2020 zikitokana na viwanda, huku miongoni mwa miradi mikubwa uinayotarajiwa kutekelezwa ya viwanda ni ujenzi wa kiwanda cha chuma.
Aidha Mchumi huyo pia amesema adhima ya serikali ya kujenga nchi ya viwanda itafanikia ikiwa itawekeza katika nishati ya umeme wa uhakika, licha ya miradi mikubwa kama ya Power Afrika na MCC kusitishwa huku akiishauri serikali kufanyia kazi maazimio ya bunge kuhusu sakata la Tegeta esrow.
Mahojiano hayo maalum yamefanyika Dar es Salaam, muda mfupi baada ya Prof Lipumba kupokea ujumbe maalum wa wawafuasi wa chama cha CUF kutoka mjini bagamoyo waliokuwa lengo la msihi kurejea kwenye nafasi yake ya uenyekiti wa chama cha CUF.


Haya Hapa Matokeo ya Simba na Azam Yaliyofanya Mashabiki wa Yanga Waendelee Kuchekelea Kileleni...

Ligi Kuu soka Tanzania bara imeendelea leo Mei 1 2016 kwa mchezo kati ya Simba dhidi ya Azam FC kuchezwa katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam, huu ni mchezo wa 26 kwa vilabu vyote na ulikuwa mchezo muhimu kwa kila klabu hili kujiweka pazuri katika nafasi ya kuwania ubingwa.
Azam FC kabla ya mchezo dhidi ya Simba kumalizika kwa sare ya 0-0 walikuwa na point 58 wakiwa nafasi ya pili ya Ligi, wakati Simba walikuwa nafasi ya tatu wakiwa na point 57 wakiongozwa na Yanga ambao wapo kileleni wakiwa na point 65 na michezo 26. Sare ya mchezo huu ilikuwa ni furaha kwa Yanga ambao wameongeza tofauti ya point kwa Azam FC na Simba.
Kwa idadi ya mechi Simba na Azam FC huu ulikuwa ni mchezo muhimu kwao kuhakikisha wanapata point tatu ili kuweza kupunguza tofauti yao ya point na Yanga wanaoongoza Ligi wakiwa na tofauti ya point sita na Azam FC anayefuatia, umuhimu wa mchezo kwa pande zote mbili ndio ulifanya mchezo kuwa na tension kubwa kitu ambacho kilifanya wachezaji wa pande zote kukosa magoli ya wazi wakati mwingine.


Wanawake Muwe Makini… Huyu Amefariki Guest House kwa Kulishwa Sumu, Mwanaume Kakimbia

Tukio limetokea Guest House Kimara Dar es salaam usiku wa May 1 2016 ambapo Mwanaume mmoja aliyeingia kwenye nyumba hiyo ya Wageni akiwa na Mwanamke, alikimbia kwa kusingizia kwenda dukani kununua vocha wakati Mwanamke huyo akikaribia kukata roho na hakurudi tena.
Wakati tunasubiri uchunguzi wa Polisi, mashuhuda kwenye eneo la tukio wamesema inavyoonekana Mwanamke huyo atakua kawekewa sumu kwenye chips alizokua anakula ndani ya chumba cha nyumba hiyo ya Wageni chips ambazo inadaiwa walitokanazo kwenye safari yao na kuja nazo Guest House.


Diamond Azipangua Shutuma za Kutoka na Mrembo Lyyn..Adai Wanajaribu Lakini Zari

Diamond Ameamua Kuwakata watu vidomo wanaosema kuwa yeye na Zari kwa sasa hakuna mawasiliano mazuri kisa mrembo aliyecheza kwenye video mpya ya Rayvan...kwa kumpost Zari kwenye page yake ya Instagram...Tetesi za Diamond kutoka na msichana huyo zimekuwa gumzo kubwa instagram ....
Roho ya SIMBA!!!.... wanajaribu ila hawatokaa Waweze... Nakupenda Mpaka Naugua! @Zarithebosslady 😙 #Mmechelewa

Gigy Money Afunguka Kuhusu Mapicha yake ya Nusu Utupu Mtandaoni..Adai Ndio zinampatia Pesa.....

Video queen aliyetokelezea kwenye video kibao za bongo Gigy Money ameamua kufunguka juu ya masinema yake.
Giggy ambaye haishi vituko na kuibua mapya kila siku mitandaoni aliiambia eNewz kuwa yeye wala hajali maneno ya watu na anapenda sana yale mapicha picha yake ya utupu.
“Mimi sipo kwa ajili ya kiki mimi napenda kile ninachokifanya na ndio ninachokifanya mimi nipo kwa ajili ya kutengeneza pesa tu na kipo kiwango ambacho nakitaka nifikie na sasa natarajia kufikia,” alisema Gigy.


Mama Wema Sepetu Aonyesha Alivyoumbika Adai Mtoto wake Amechukua Kwake..Awashangaa Wanaosema Wema Ametumia Dawa Kukuza Makalio

Mama Wema Sepetu Ameongea na Kusema kuwa anawashangaa wale wote wanaosema mtoto wake ameongeza makalio kwa dawa wakati wanaona kabisa kuwa amerisi makalio hayo kutoka kwa mama yake...Mama huyo amekwenda mbali zaidi na kuweka video yake hapa akionyesha jinsi alivyo mashalaaa......
Tazama Video Hapa:


HASARA ZA KUTOFANYA MAPENZI KWA MUDA MREFU

Ukidumu bila tendo la ndoa muda mrefu, baadhi ya madhara madogo madogo yanaweza kujitokeza kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa kiafya karibu twende sawa katika darasa la leo Mwalimu ndio nshakuandalia vitu vitamu jisomee ili ufaulu somo Mapenzi.
Zifautazo ni athari hasi za kutofanya tendo la ndoa kwa muda mrefu;
1.Hasira za mara kwa mara katika mambo madogo Mara kwa mara huwa anakasirishwa na vitu vidogo hata visivyokuwa na maana yeye huvitilia maanani .
2.Kutokwa damu nyingi wakati wa hedhi (Mwanamke), Tafiti zinaonesha kuwa mwanamke anapokuwa kwenye mzunguko wake wa siku 28 kama hatoshiriki tendo la ndoa kwa kipindi kirefu basi hupoteza damu nyingi wakati wa hedhi.
3.Kupenda kurukiarukia mambo ya watu wengine (tabia ya kufuatilia mambo yasiyokuhusu) hii pia ni tabia inayoibuka kisaikolojia kutokana na kile watoto wa mtaani wanachoita mizuka inampanda kwa yasiyo muhusu.
4.Kuumwa na kichwa, Wataalamu wametaja maumivu ya kichwa mara kwa mara wakati mwingine husababishwa na kutofanya mapenzi kwa muda mrefu.
5.Kukakamaa mgongo (wanaume), Inasemekana kuwa mwanaume akikaa bila kufanya mapenzi kwa muda mrefu husumbuliwa na maumivu ya mgongo ya mara kwa mara.
6.Kuingiliwa kirahisi na jini mahaba, Hii imeelezwa ni kutokana na ndoto zile utakazoota kifikra kwamba unafanya tendo la ndoa ndio hupelekea kumkaribisha jini mahaba katika mwili wako.
7.Kupoteza umakini katika kazi, Wataalamu wa mambo wanasema kwamba pindi unapokaa muda mrefu bila kushiriki tendo la ndoa unapoteza uwezo wa kufanya kazi kwa umakini unaotakiwa.
8.Siku ukikutana kimwili na mwenye virusi bila kinga utaambukizwa kirahisi mno, Inasemekana utakuwa umekamia mechi hivyo utauanza mchezo bila maandalizi yanayotakiwa hivyo msuguano utakuwa mkali na kuleta madhara.


JPM AAGIZA ASKARI ALIYETUKANWA NA MKE WA WAZIRI APANDISHWE CHEO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli amemuagiza Kamishna wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Ernesti Mangu kumpandisha cheo mara moja askari wa Usalama Barabarani ambaye alitukanwa na Mke wa Waziri wakati akitekeleza majukumu yake ya kazi.
Rais ameyasema hayo wakati akifungua Kikao cha Makamanda wa Polisi wa Mikoa na kusema tayari amekwishamuonya Waziri huyo ambaye mke wake alimtusi Askari wa Usalama Barabarani.
Wakati akitoa agizo hilo, Rais Magufuli amesema hakuna kiongozi au familia ya kiongozi iliyo juu ya sheria.
Chanzo: TBC1


IDADI YA WANAOSUBIRI KUNYONGWA TANZANIA YAONGEZEKA

Januari 29, 2009 Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda alimwaga machozi Bungeni na kufikia hatua ya kutoa kauli kali juu ya wanaofanya vitendo vya kikatili vya mauaji dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi kwamba “wanaoua albino nao wauawe”
Hadi sasa idadi ya Watanzania wanaosubiri kunyongwa imekuwa ikiongezeka siku hadi siku na kufikia 465 kutokana na hukumu ya kifo kutotekelezwa nchini tangu mwaka 1994.
Ripoti ya Mpango wa Kujitathmini Kuhusu Hali ya Utekelezaji wa Haki za Binadamu (UPR), unaotekelezwa kwa mara ya pili nchini Tanzania, umeonesha ongezeko la mahabusu 465 wanaosubiri adhabu ya kifo, kati yao wanaume ni 445 huku wanawake wakiwa 20 baada ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, kubainisha hakuna hukumu yoyote ya kifo iliyosainiwa na Rais Dk. Magufuli ili kutekelezwa tangu Oktoba mwaka jana alipoingia madarakani.
Hata hivyo Ofisa Uchunguzi Mkuu wa Tume hiyo Philemon Mponezya, amesema Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, inaitaka Serikali kufuta adhabu ya kifo kwa kuwa haitekelezeki ingawa kumekuwa na mvutano mkali kati yao na baadhi ya asasi hasa zinazohusika na haki za walemavu wa ngozi zikipinga vikali kufutwa kwa adhabu hiyo.
“Watetezi wengi wa haki za binadamu nchini Tanzania wanataka adhabu hiyo ifutwe kwa kuwa ni kinyume cha haki za binadamu na kwa Tanzania, imekuwa mbaya zaidi kwa baadhi ya wahukumiwa waliosubiri zaidi miaka 20 bila hukumu dhidi yao kutekelezwa, jambo hili linawaathiri kisaikolojia”. Amesema Mponezya.
Jiunge nasi
Insta@ubuyuhotz , fb@ubuyuhotz .


DALILI ZA MWANAMKE ANAYEKUPENDA KUTOKA MOYONI

Wahenga walinena kuwa “penzi ni kikohozi kulificha hauwezi” hakika wazee wetu hawakukosea Mapenzi ni hisia ambazo huwezi kuzizuia kwa namna yeyote ile kwani huanza kwa siri baina ya wawili lakini baadaye huwa sio siri tena, vivyo hivyo kwa mwanamke anayekupenda kwa dhati huwa na tabia hizi;
1. Utaona mabadiliko katika muonekano wake. Ukitaka kumfahamu msichana ambaye yupo katika mapenzi kama alikuwa hajipendi kwa maana kuwa rafu hata akiwa katika mazingira ya nyumbani basi katika kipindi hiki atakuwa msafi kuanzia mwili mavazi na hata nywele ataweka kila staili itakayompendeza ili kukuvutia.
2. Anajali kama mwanamke anakupenda atakujali hatopenda kuwa mbali na wewe kama atagundua upo katika tatizo, atakufanya ufahamu yupo kwa ajili yako pale utakapomhitaji.
3. Anajitoa kwa ajili yako. Atachukua muda wake mwingi kuwa na wewe atafanya vitu ambavyo unavipenda na kuviacha vya kwake pale inapobidi
4. Huwa muwazi kwa kila anachokifanya nini anapanga kufanya na nani anakutana naye kwa wakati gani.
5. Wewe ni mvulana pekee anayetazamia uje kuwa mume wake anazungumzia mambo mengi kuhusu maisha ya baadaye kama vile ndoa watoto wangapi atatamani kuzaa pamoja na familia yenu iwe vipi.
6. Anapenda kuwa na wewe muda mwingi. Msichana mwenye mapenzi hufanya haraka kumaliza shughuli zake ili asipoteze muda mwingi akashindwa kukuona tena kwa siku hiyo. Anaweza kuacha hata shughuli zake ili aje kukaa na wewe hata kama mkutano wenu hauna maana na faida kwake.
7. Anakushika kwa hisia, msichana aliyezama katika mapenzi huwa na hisia ndio maana hupenda kukushika kila sehemu yako ya mwili kwa hisia za kweli akihitaji na wewe uhisi anachohisi kupitia mguso wake.
8. Atakutambulisha kwa ndugu jamaa na rafiki zake
, hupenda kila mtu wake wa karibu akufahamu hivyo hupenda kukutambulisha kwa kila mtu haoni aibu kufanya hivyo kwa kuwa anatarajia utakuwa wake wa kudumu.