Jumanne, 30 Septemba 2014

Raila Odinga atandikwa kiboko

 
Raila Odinga alichapwa mara mbili kwa kiboko katika tukio ambalo limewashangaza wengi 
Hali ya taharuki iliibuka katika mkutano wa hadhara katika jimbo la Kwale nchini Kenya, baada ya mwanamume mmoja kwenda ukumbini na kuanza kutandika bakora kiongozi wa upinzani Raila Odinga pamoja na wanasiasa wengine.
Raila alikuwa amejiunga na kikundi cha wanawake waliokuwa wanacheza densi ya kitamaduni kuwatumbuiza wageni, pamoja na gavana wa jimbo la Kwale Pwani ya Kenya Salim Mvuruya katika mkutanmo wa kisiasa.
Walikuwa wameambatana na viongozi wengine, wakiwemo, Seneta Juma Boy, Hassan Omar, Agnes Zani, James Orengo, Johnstone Muthama na wengineo.

 
Kiongozi wa upinzani Raila Odinga 

Mwanamume huyo alimshambulia Odinga ambaye ni waziri mkuu wa zamani na kumchapa mara mbili kabla ya kumgeukia gavana wa jimbo hilo na pia kumchapa mara mbili. Hata hivyo mwanamume huyo alishindwa nguvu na walinzi wa Raila Odinga.
Polisi walithibitisha kuwa walimkamata mwanamume huyo na kumwachilia baada ya kugundua kuwa alikuwa na matatizo ya kiakili.
Haijulikani kwa nini mwanammume huyo alimshambulia Raila ila baadhi wabnasema ni kwa sababu alighadhabishwa pale waziri mkuu alipocheza densi na mwanamke aliyesemekana kuwa mke wake ambaye alikuwa katika kikundi cha wanawake waliokuwa wanawatumbuiza wageni waheshimiwa.
Viongozi waliofika walilazimika kusitisha densi hiyo kabla ya mwanamume huyo kushindwa nguvu.

Eti umoja wa Ma-Girlfriend wamekuja na hii baada ya Diamond kutoa zawadi ya Gari kwa Wema…

zawadi 
September 26 ilikua ni siku ambayo mrembo kutoka Tanzania Wema Sepetu alisherehekea siku yake ya kuzaliwa ambapo ndani ya siku yake hii ukitoa party aliyoifanya kulikuwa na vitu mbalimbali vya kuvutia.
Siku hiyo Diamond platnumz aliamua kumzawadia zawadi ya gari mpenzi wake Wema Sepetu gari aina ya Nissan Murano ambapo alipost instagram na kuandika maneno yafuatayo yaliyoambatana na picha ya zawadi hiyo.
zawadi
msg 
Mbali na zawadi aliyoitoa Diamond Platnumz ya gari hilo pia Meneja wake Martin Kadinda nae alimpatia Wema Sepetu zawadi ya Gari aina ya BMW mpya kabisa ikiwa na namba mpya za sasa.
bmw
Sasa baada ya zawadi hizo kuonekana eti umoja wa Ma-Girlfriend Tanzania nao wameamua kutoa Ya moyoni kwa Ma-Boyfriend wao kuhusu birthday zao inapofika muda wa kusherehekea,hiki ndicho walichokiandika.
www

Maneno ya Rais wa Simba baada ya hizi droo zao ligi kuu

soccer 
Rais Simba Evans Aveva kwa mara ya kwanza amefungua mdomo wake na kulizungumzia suala la sare mbili katika mechi zao za Ligi kuu bara ambapo Rais huyu amewataka mashabiki na wanachama wa Simba kuungana na kuwa pamoja katika kipindi ambacho alikiita hawajapoteza wala kufanya vizuri.
Baada ya hayo akasema anamuamini Kocha Patrick Phiri hivyo wampe muda kidogo kwa kuwa wanapita kwenye kipindi cha mpito >>>  “Hatujafanya vibaya wala kufanya vizuri, sare mbili na hakuna mchezo tuliopoteza, ni suala la kujipanga ili kuangalia tutafanya nini katika mechi zinazofuatia, uongozi una changamoto nyingi utaona tulifanya kila linalowezekana kwenye uchaguzi baadaye kwenye usajili lakini sasa bado mambo hayajakaa vizuri, ni suala la kupambana tu

Ulisikia ile show ya Jose Chameleone ambayo kiingilio ni milioni moja? amezitaja sababu 3 hapa

stage 1 
Kwa hapa Tanzania tumezoea show kubwa kama Fiesta tunaona mastaa wakubwa kama Rick Ross, Ludacris na wengine kwa kiingilio kisichozidi elfu 20 ambapo mwaka huu anashuka T.I October 18 lakini tukirudi kwenye show binafsi za Wasanii, kumbukumbu zangu zinaniambia Diamond na Mwana FA ni miongoni mwa waliowahi kufanya show zao wao wenyewe lakini viiingilio havikufika shilingi laki moja.
Nimekuandikia hiyo sentensi hapo juu nikiweka kumbukumbu vizuri wakati huu ambapo imebaki miezi miwili kufanyika kwa show ya Jose Chameleone wa Uganda ambae amepanga kuifanya show yake mwenyewe nchini kwao December hii huku kiingilio kikiwa ni zaidi ya laki sita za Tanzania ambazo ni shilingi milioni moja za Uganda.
j chameleone 1
 
Kwenye Exclusive interview na youngluvega.com Jose Chameleone amesema >>> ‘nachekelea watu ambao wanasema Milioni? nani atampa hiyo milioni? watu wengi wanauliza mbona milioni moja? msanii mmoja? kuna watu ambao hawajapata bahati ya kumuona Chameleone akiwa anafanya mazuri yake, kuna matajiri flani wanataka kuja kwenye show yangu lakini wanaogopa wakija kuna cameraman wengi wanawasumbua na vitu kama hivyo’
  1. ‘Sio eti nimetaka kujipandisha bei lakini nataka kuwajali pia wale ambao hawawezi kunitembelea kwenye show za kawaida, najua watu wanashangaa na kuuliza mbona milioni?? …….sio sababu wewe au mimi hatuna milioni ndio wote hatuna milioni, kuna watu ambao milioni ni kama elfu moja, elfu kumi au laki moja’
  2. ‘Usiulize wanaotengeneza Benz mbona wanauza bei kubwa zaidi ya Toyota, kama huna hela ya Benz nunua Toyota, sio kwa ubaya lakini nataka nijali watu wote.. hii ni kwa wale wasioweza kuja kwenye show za elfu 10 na elfu 20, na wao wapate wakati wao…. hii hela ni kwa ajili ya kuwasaidia watu wa Karamoja wanaoishi kwenye maisha duni’

Jumatatu, 29 Septemba 2014

Omar Gonzalez White House

Mlango huo unavyoonekana 
Taarifa kutoka mjini Washngton zinaeleza kua mwanamume mmoja aliyekua ameshikilia kisu mikononi mwake aliruka uzio wa makao ya Rais wa Marekani Brack Obama na kukimbia kuelekea kwenye makazi hayo mwezi huu .
Maafisa wa Ikulu hiyo wamemtambua mtu huyo kua ni Omar Gonzalez,askari wa zamani aliyepigana Iraq, alikua pamoja na kisu,alikuwa akikimbilia katika mlango mkuu wa makazi ya Rais Obama kabla hajakatwa na maofisa wa Ikulu hiyo maarufu kama White House .
Taarifa zinaeleza kuwa kiboksi chenye kengele ya tahadhari kilikuwa kimezimwa .Mkuu wa shughuliza siri za ikulu hiyo Julia Pearson anatarajiwa kuhojiwa kufuatia tukio hilo na jopo la wanasheria.
Wakati hayo yakitukia Rais Obama na familia yake hawakuwa katika Ikulu hiyo.

NI KIVUMBI LIGI YA MABINGWA ULAYA

 
Katika michuano ya Klabu Bingwa barani Ulaya leo kuna kivumbi kingine ambapo CSKA Moscow itakuwa na kibarua kigumu pale watakapowakaribisha Bayern Munich.
Wakati huo huo Man City waliopigwa bao moja na Bayern Munich watakutana na AC Roma iliyowapiga CSKA Moscow mabao matano katika mechi iliyopita.
Paris St G ya Ufaransa wao wanakutana uso kwa uso na Barcelona
Ukumbumbuke katika mechi ya wikendi iliyopita Paris St G walitoka sare na Ajax bao moja kwa moja.
Ajax inakutana leo na Apoel Nic ambayo ilipigwa na Barcelona bao moja katika mechi ya awali.
Sporting Lisbon ya Ureno leo wanapepetena na Chelsea ya England. Meneja Jose Mourinyo amesema kutokana na umuhimu wa mechi hii atajitoa muhanga kwa kumchezesha mshambuliaji machachari Diego Costa.
Schalke waliotoka moja moja na Chelsea wanacheza na NK Maribor ambayo wiki iliyopita ilitoana jasho na Sporting Lisbon kiasi cha kutoka na bao moja kwa moja.
BATE Bor itakipiga na Ath Bilbao
Shakt Donsk inashuka dimbani dhidi ya FC Porto iliyowachapa mabao sita BATE Bor
Mechi kamili za leo hizi hapa
  • CSKA v Bayern Munich
  • City v Roma
  • Paris St G v Barcelona
  • Sporting v Chelsea
  • Apoel Nic v Ajax
  • Schalke v NK Maribor
  • BATE Bor v Ath Bilbao
  • Shakt Donsk v FC Porto

Taarifa kuhusu kifo cha msanii wa bongofleva Side Boy Mnyamwezi.

rip
Ingawa Nafasi yake katika muziki wa Bongo Fleva ilikuwa ikipanda taratibu kulingana na aina ya muziki aliokuwa akiumba,single iliyomtambulisha zaidi kwenye muziki wa Bongo Fleva inaitwa Kua uone ambayo alimshirikisha Ally Kiba.
sideeee
Mchana wa jana imetoka taarifa kuwa amefariki dunia ambapo kwa zaidi ya mwezi mmoja alikua amelazwa kwenye hospitali ya Nyangao iliyopo Mkoani Lindi ambako ndiko nyumbani kwao.
ss
Mipango ya mazishi imepangwa ambapo atazikwa kesho huko huko Lindi,Rest In Peace Side Boy,moja ya post zake kwenye mtandao wa Facebook aliandika ‘habari za usiku huu wapendwa!dua zenu zinahitajika coz hali yangu c poa kabisa’
Hii ni moja ya post za mwisho za Side boy kwenye page yake ya facebook
Hii ni moja ya post za mwisho za Side boy kwenye page yake ya facebook
Hii ni post nyingine kati ya post zake za mwishomwisho, mtoto Nasra ni yule aliekua amefichwa kwenye box kwa miaka minne
Hii ni post nyingine kati ya post zake za mwishomwisho, mtoto Nasra ni yule aliekua amefichwa kwenye box kwa miaka minne
Side Boy Alitoa single kadhaa ikiwemo Hujafa hujaumbika,Jifungue salama,Usimdharau Usiyemjua na Kua Uone,Hii ni moja ya single zake ambayo ili hit miaka 6 iliyopita inaitwa Kua uone.

Ijumaa, 26 Septemba 2014

Waaga mchuano baada ya kuagizwa kuvua hijab

Timu ya wanawake ya Qatar ya mchezo wa mpira wa kikapu imejiondoa kutoka mashindo ya bara Asia.
Timu ya wanawake ya Qatar ya mchezo wa mpira wa vikapu imejiondoa kutoka mashindo ya bara Asia yanayofanyika huko Korea Kusini baada ya kuagizwa kuvua hijab kabla ya mechi yao dhidi ya timu ya Mongolia .
Wanawake hao walikataa kata kata kuvua vazi hilo na wakajiondoa mashindanoni wakidai inakiuka maagizo ya dina ya Kiislamu inayomtaka mwanamke kujistiri nywele zake haswa akiwa faraghani.
Sheria za shirika la mchezo huo duniani haziruhusu kuvaliwaj kwa vitambaa vya kichwani wakati wa mechi lakini sasa wamekuwa wakijadili iwapo sheria hiyo itaondolewe.
Hata hivyo ilipowadia wakati wa mechi yao dhidi ya Nepal sheria hiyo haikuwa imebadilishwa na hivyo iliwabidi kuyaaga mashindano.
Fani nyengine za michezo katika mashindano hayo ya Bara Asia zinaruhusu uvaliwaji wa hijab.
Timu ya taifa ya unyanyuaji uzani ya Iran imekuwa ikishiriki mashindano hayo huku wakiwa wamevalia hijab.
Baraza la mashindano ya Olimpiki ya Bara asia OCA imesema kuwa haki za wachezaji ni zinapaswa kupewa kipaombele .
Sheria za shirikisho la mpira wa vikapu haziruhusu mavazi kichwani 
Baada ya kuyaaga mashindano hayo mchezaji wa Qatar Amal Mohamed A Mohamed alisema kuwa walikuwa wamehakikishiwa kuwa wataruhusiwa kushiriki mashindano hayo wakiwa wamevalia hijab na hivyo hawaelewi kwanini sheria hiyo haijabadailishwa.
''nina hakika kuwa hatutashiriki mashindano yeyote ya Bara Asia hadi sheria hiyo ibadilishwe''
Mashindano hayo hufanyika kila baada ya miaka 4 na huwaleta pamoja washiriki 9000 kutoka mataifa 45 yakishindana katika fani 36 ya michezo.
Mashindano hayo yatamalizika tarehe 4 Oktoba.

Van Gaal:tuna mlinzi wa kati mmoja tu

 
Kocha wa Manchester United Louis Van Gaal.
Kocha wa machester United, Louis van Gaal amesema Manchester united ina mlinzi wa kati mmoja tu mwenye uzoefu wakati huu kikosi hicho kinapotarajia kukipiga na west ham katika michuano ya ligi kuu ya England.
Marcos Rojo yuko fiti, lakini timu hiyo ina majeruhi kama Chris Smalling ana jeraha la mguu, Phil Jones ana jeraha kwenye, Jonny Evans ana jeraha la kifundo cha mguu na Tyler Blackett hatacheza mchezo huo.
Van Gaal analazimika sasa kuchukua wachezaji kwenye kikosi cha vijana ili kuziba mapengo yaliyopo kwenye timu yake.miongoni mwao ni vijana Tom Thorpe na Paddy MacNair ambao wataungana na kikosi cha kwanza cha Manchester United kwa mara ya kwanza.

'VIPIMO VYA SKETI KIGEZO CHA SARATANI'

 
Baadhi ya watafiti wana sahuku ikiwa vipimo vya sketi vitamtahadharisha mwanamke kuhusu tisho la Saratani.
Utafiti unaonyesha kuwa wanawake wanaonenepa maishani bila ya kuwa waangalifu wanajiweka katika hatari ya kupata Saratani.
Watafiti kutoka chuo Kikuu cha London wanasema kwamba wanawake walio kati ya umri wa miaka 24-28 ambao huendelea kunenepa kila baada ya miaka 10, wako katika hatari zaidi ya kupata Saratani ya Matiti baada ya kupitisha umri wa kuzaa.
Sasa je ni nini ishara ya mwanamke kunenepa? Watafiti wanasema vipimo vya sketi yake vinaweza kukusaidia kujua ikiwa uko katika hatari ya kpatwa Saratni ya Matiti au la.
Kila unapogundua kuwa sketi yako inaendelea kuwa ndogo kiunoni, basi inakubidi ujue kuwa mwili wako unaongekeza kwa unene. Na pia ni rahisi kwa wanawake kukumbuka kipimo cha sketi kuliko kitu kingine chochote.
Kwa hilo watafaiti wanasema mwanampe anapaswa kutahadhari kila sketi yake inapoendelea kuwa ndogo kwake maana kwamba amenenepa zaidi. Ikiwa ukubwa wake unazidi kwa kipimo cha sketi mbili katika kipindi kimoja basi mwanamke anakuwa katika hatari ya kupatwa na Saratani hata zaidi.
'Mfumo wa maisha'
 
Tisho hili linawakabili zaidi wanawake waliopitisha umri wa kupata watoto 

Akizungumzia utafiti huo, Simon Vincet kutoka shirika la kupambana na saratani ya Matiti la Breakthrough Breast Cancer, alisema kuwa saratani ya Matiti miongoni mwa wanwake inaweza kupunguka ikiwa watu watabadilisha mfumo wa maisha kwa kujiuzia kunenepa kupita kiasi na kufanya mazoezi sana.
Utafiti huu unaangazia njia rahisi sana kwa wanawake kuwa waangalifu kuhusu unene wa miili yao.
Kuangalia kipimo cha sketi kati ya wanawake walio kati ya miaka 24 na 28 wenye miaki katikati ya 20 na zaidi wanaweza kuwa na njia rahisi ya kufuatilia uzito wa miili ya Unene wa kupita kiasi unajulikana kwa sababu ni hatari kubwa inayochangia katika ugonjwa wa saratani , hususan mafuta ya yaliyoko tumboni.
Prof Usha Menon wa shirika lakupambana na satratani ya matiti, ndiye aliyeongoza utafiti huo na kuambia BBC kuwa "Kama kipimo cha sketi kinaweza kuthibitishwa na wengine kama kigezo cha wanawake watu wazima kuapa Saratani, basi hii itakuw anjia nzuri na rahisi ya mtu kuwa mwangalifu ili asinenepe kupita kiasi.
'Changamoto'
 Unene kupita kiasi ni moja ya mambo yanayohatarisha afya ya wanawake waliopitisha umri wa kuzaa.

Watafiti hao walisema utafiti wao ulikuwa na changamoto kadhaa kwamba uliangazia zaidi wanawake kukumbuka vipimo vya sketi zao tangu tangu wawe na umri wa miaka 20
Lakini ikiwa matokeo ya utafiti huo yatathibitishwa, itakuwa njia rahisi kwa wanawake kuelewa hatari zinazowakabili hasa wanapoendelea kunenepa.
Tom Stansfeld kutoka shirika la utafiti wa Saratani nchini Uingereza,anasema utafiti huo unaweza kuaminika lakini unazingatia zaidi wanawake kukumbuka vipimo vya sketi walizovalia miaka ya zamani.
Utafiti unasema kuwa baadhi ya mambo muhimu ambayo mwanamke anaweza kufanya kupunguza tisho la kuugua Saratani ya Matiti , hasa baada ya kupitisha miaka yake ya kuzaa ni pamoja na kufanya mazoezi , kula vizuri na kupunguza ulevi.
Kupunguza unene ni njia moja wapo ya kupunguza tisho la kupata Saratani baada ya kupitisha miaka ya kuzaa na kuangalia vipimo vya sketi za wanawake kuwahamasisha wanawake.

KILICHOWAKUTA CHADEMA WALIOANDAMANA MWANZA Sept.25

news 1 
Kutoka 88.1 Mwanza ambapo Polisi wamekamata viongozi sita na wafuasi kadhaa wa (CHADEMA) waliokuwa wakijiandaa kuandamana baada ya kukaidi amri ya polisi kusitisha maandamano.
Ni September 25 saa 5.40 asubuhi muda mfupi baada ya wafuasi hao kujipanga kwa maandamano yaliyokuwa yaanzie viwanja vya Sahara mpaka ofisi za mkuu wa wilaya ya Nyamagana na kufanya mkutano mfupi wa hadhara kufikisha ujumbe.
Purukushani ilidumu kwa zaidi ya dakika 120 ikiambatana na wafuasi hao kupigwa virungu huku taarifa zisizo rasmi zikisema Polisi wamewatia mbaroni watu 14 wanaodaiwa kuandamana bila kibali.
Kwa mujibu wa ripota wa nguvu Paul Luvega, licha ya kuthibitisha kutokea kwa tukio hilo Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza bado halijatoa taarifa kamili ambapo John Nzwalile katibu wa CHADEMA Mwanza amesema >>> ‘naweza kusema kwa ujumla tumefanikiwa, Polisi ndio wameandamana kwa wingi kuliko hata sisi, tokea asubuhi ukienda chooni au kunywa chai Askari kanzu wanakufatili, ukinywa chai na wao wanajifanya wanakunywa chai
 ‘Niseme maandamano yetu yamefanikiwa kwa sababu yalikua yamepangwa kwa akili kubwa sana, tuliandamana kuanzia kichwani… hatukuandamana ovyoovyo, hawakujua tunaanzia wapi tunaishia wapi…. tumeshangaa Polisi wamekuja na vifaa utadhani unaangalia movie ya vita’
‘Mpaka sasa taarifa nilizonazo mwenyekiti wangu wa Nyamagana amekamatwa, Katibu mwenezi Nyamagana, Mwenyekiti kata ya Bugogwa, Katibu wilaya ya Ilemela wamekamatwa…. watu ambao kosa lao ni kuwaambia Watanzania kuna pesa inaliwa na Wabunge kwenye batili la katiba’
‘Kwa kauli moja ya chama niseme tu kwamba maandamano na migomo isiyokua na kikomo itaendelea…. tunazidi kujipanga vizuri kuangalia namna bora zaidi ya kuandamana, tunataka watu wetu watoke Wanasheria wetu wanajipanga…. kuhakikisha wanatoka bila masharti’

Hukumu ya muuguzi aliesababisha kifo cha mjamzito mwaka 2009.

hosp 1 
Kwenye moja kati ya taarifa kubwa za Kenya September 25 2014 ni pamoja na hii ya Muuguzi mmoja ambae kesi yake ilianza kusikilizwa toka mwaka 2009 nchini humo kwenye kaunti ya Kyambuu.
Kituo cha Radio Jambo kimeripoti kwamba muuguzi huyu Jackson Tali mwenye umri wa miaka 41 amehukumiwa kifo baada ya kupatikana na hatia ya kusababisha kifo cha msichana aliyetafuta huduma za ujauzito wake kwa muuguzi huyu.
Jackson anadaiwa kutenda kosa hilo July 27 2009 huko Kyambuu.

Alhamisi, 25 Septemba 2014

Mchongo mpya alioupata Diamond Platnumz,huu unahusu application ya simu.

Diamond Platinumz
Ingawa hajaweka wazi namna dili hii itakavyokuwa lakini kupitia ukurasa wake wa Instagram,Diamond Platnumz amepost picha ambayo imebeba maandishi yasemayo ‘Ningependa kukutaarifu shabiki wangu pendwa kuwa kijana wako sasa ni balozi wa application mpya iitwayo Mziiki’.
Hii ni application ambayo itatumiwa na watu wenye simu za androad kusikiliza muziki huu ndiyo muonekano wake utakapokuwa ume instal kwenye simu yako.
mond3
Maandishi ya Diamond pamoja na alichokipost ni hiki.
mond
mond 2

ILICHOSEMA CLUB YA SIMBA JUU YA IVO MAPUNDA KUVUNJIKA

Mapunda 
Zikiwa zimebakia wiki mbili kabla ya kukutana na mahasimu wao wa jadi, Simba imepata pigo kubwa katika timu kwa sababu kipa namba moja wa timu hiyo Ivo Mapunda amevunjika kidole mazoezini Zanzibar jana asubuhi na anatakiwa kuwa nje ya uwanja kwa wiki nane.
Hatoweza kusimama golini wakati tiu yake ikicheza na Yanga October 12 2014 ambapo daktari wa Simba SC Yassin Gembe amesema Ivo aliumia wakati anachupia mpira katika mazoezi ya asubuhi na kwa bahati mbaya mpira ukamgonga kwenye kidole kidogo cha mwisho mkono wa kulia.
Gembe amesema Ivo alitoka mazoezini baada ya tukio hilo na baadaye akapelekwa hospitali ya Mnazi Mmoja kisiwani humo ambako baada ya vipimo ikagundulika amevunjika sana.
Si kuvunjika kwa mzaha, amevunjika sana na anatakiwa kupumzika kwa wiki nane, baada ya hapo aanze taratibu… ina maana makadirio ya kurudi tena uwanjani ni hadi baada ya miezi mitatu‘ – Gembe.
Kuumia kwa Ivo kunatoa nafasi kwa makipa chipukizi Hussein Sharrif  ‘Cassilas’ na Peter Manyika kujibidiisha ili kuziba pengo lake ambapo sasa Ivo anafanya idadi ya wachezaji majeruhi ambao ni tegemeo Simba kufikia wanne baada ya Paul Kiongera anayetakiwa kuwa nje wiki sita, Haroun Chanongo na Issa Rashid ‘Baba Ubaya’.

Jumanne, 23 Septemba 2014

Msikiti uliozua utata wafungwa A.Kusini

Bwana Taj Hargey anasema msikiti huo unawalenga watu wenye mawazo chanya 

Msikiti ambao unasemekana kuunga mkono watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja, na ambao pia wanawake wataruhusiwa kuswali ndani,umefungwa.
Afisaa mmoja mjini Cape Town, anasema kuwa msikiti huo umevunja sheria za baraza la jiji kwa kukosa nafasi za kuegesha magari ya waumini.
Msikiti huo, ulifunguliwa rasmi siku ya Ijumaa wiki jana licha ya kukosolewa na waumini wa kiisilamu katika eneo uliko.
Mwanzilishi wa msikiti huo, Taj Hargey, alisema kuwa msikiti huo utasaidia katika kupambana na kuenezwa kwa itikadi kali za kidini.
''Tunafungua msikiti huu kwa watu walio na muonekano chanya kwa baadhi ya mambo wala sio wenye muonekano finyu,'' alisema bwana Hergey kabla ya ufunguzi wa masikiti huo.
Kadhalika bwana Hargey alikana kwenda kinyume na mafunzo ya dini ya kiisilamu.
Maafisa wa baraza la jiji wamekanusha madai kuwa kufungwa kwa msikiti huo ni kwa nia mbaya.
 Msikiti huu umefungwa kutokana na kukosa nafasi za kuegeshea magari
"swala hili linazua sana hisia, baadhi ya maafisa wa baraza la jiji, ambao ni waisilamu wangeteka kuunga mkono kufungwa kwa msikiti huo, lakini wasio waisilamu wangependa kuuona ukiwa wazi, lakini cha muhimu hapa ni kwamba, tungetaka kuona sheria ikifuatwa, '' alisema afisa mmoja wa baraza la jiji.
Inaarifiwa kuwa bwana Hargey hakuomba idhini ya kuruhusu jengo lililokuwa likitumiwa kama sehemu ya kuweka vitu kubadilishwa na kuwa msikiti.
Kuambatana na masharti ya baraza la jiji, kila sehemu ya maombi inapaswa kuwa na sehemu ya kuegeshea magari ya waumini lakini msikiti huo hauna sehemu hiyo.
Shughuli ya kuwasilisha maombo ya kuwezesha kuwepo sehemu ya kuegeshea magari huenda ikachukua hadi miezi sita.
Bwana Hargey aliambia BBC kwamba anaamini kuwa kila kitu kiko shwari.
Wanawake wataruhusiwa kuswali pamoja na wanaume na hata kuongoza maombi.

Ebola:Watu kusalia nyumbani S:Leone

Serikali iansema ikiwa juhudi z akupambana na Ebola zitashuka, madhara yatakuwa makubwa zaidi 

Rais wa Sierra Leone amesema kuwa serikali inatafakari kutangaza awamu ya pili ya amri ya kutotoka nje kote nchini ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa hatari wa Ebola.
Rais Ernest Bai Koroma, amesema kuwa kwa sasa ameridhika na mafanikio yaliyotokana na kuwazuia watu kutoka nje kwa saa 72 .
Awamu ya kwanza ya amri hiyo ilimalizika Jumapili.
Alisema kuwa maafisa wakuu walizuru zaidi ya nyumba milioni moja na kuwapata watu wengi ambao walikuwa wameathiriwa na ugonjwa huo.
Pia walipata mili ya watu waliokuwa wamefariki kutokana na ugonjwa huo.
Shirika la afya duniani limesema kuwa hadi pale hatua zaidi zitakapochukuliwa kukabiliana na janga la Ebola, visa vya maambukizi huenda vikaongezeka.

Visa vya mapenzi haviishi…. huyu wa Dodoma kamuua mke kwa rungu, chanzo?

Screen Shot 2014-09-23 at 8.05.41 AM 
Siku hizi mapenzi yamekua kama karata hivyo kila mmoja anacheza ajuavyo au awezavyo kwenye huu uwanja mpana ambao kwa kiasi kikubwa miaka inavyosogea ndio vifo vingi hutokea kutokana tu na visa vya mapenzi.
Taarifa kutoka Dodoma na kuthibitishwa na Polisi, zinahusu Wananchi kupatwa na hasira na kumuua Mwanaume aliyemuua mke wake kwa kumpiga na rungu tumboni kwenye kijiji cha Mzogole.
Mwanamke aliyeuwawa ana umri wa miaka 48 Mwajuma Chomola na mume wake ambae ndio mtuhumiwa ana umri wa miaka 55 anaitwa Richard Kodi ambapo kwa mujibu wa gazeti la HabariLEO, Mwanaume huyu alifariki dunia wakati akihudumiwa hospitali ya wilaya ya Mpwapwa.
Wakati uchunguzi ukiendelea, matokeo ya awali yanaonyesha chanzo cha yeye kumuua mke wake waliekua wakiishi pamoja ni wivu wa kimapenzi na kwamba ishu ilianzia pale Mwanamke alipochelewa kurudi nyumbani akitokea kwenye sherehe iliyofanyika kwenye kijiji hichohicho wanachoishi lakini mume alidhani mke kaenda kwengine.
Yaani sio kwamba alimfumania bali alihisi tu mke wake kaenda kwengine ndio sababu iliyomfanya akachukua haya maamuzi, mara nyingi kwenye mapenzi kumekua na kesi nyingi zinazosababisha Wanawake kupigwa au kuuwawa kwa sababu tu Mwanaume anahisi vitu kama hivi bila kuwa na ushahidi.

Safari za Treni Tanzania kuongezeka.

Screen Shot 2014-09-23 at 9.43.10 AM 
Dr. Harryson Mwakyembe ni miongoni mwa Mawaziri ambao wanazungumziwa sana na vijana pamoja na Watanzania wengine kwenye marika mbalimbali kutokana na jinsi anavyochapa mzigo ndio maana sio ajabu hata kumsikia akitajwa kwenye nyimbo za Wakali wa bongofleva.
Kwenye Exclusive na millardayo.com Waziri Mwakyembe amethibitisha kwamba itafikia time Tanzania usafiri wa Treni utakua bora na wengi watakimbilia huko kutokana na mabadiliko yanayofanyika.
Anasema ‘Usafiri wa Treni umeanza kuimarika na baada ya muda sio mrefu tutaanza kufanya safari nne au tano kwenda Kigoma na Mwanza, watu watapanda Treni

Huyu ndio msanii staa wa kimataifa anaekuja Fiesta Dar 2014.


Screen Shot 2014-09-23 at 3.40.20 PM 
Wakati Tour ya Fiesta ikiwa inazunguka kwenye mikoa mbalimbali Tanzania ambapo weekend hii ni Mbeya na Songea, ametangazwa msanii wa kimataifa ambae ni rasmi atapanda kwenye stage ya Fiesta Dar es salaam October 2014 Leaders Club Kinondoni.
Rapper T.I ndio msanii wa kimataifa kwenye stage ya Fiesta October 18 2014 akiwa ni mkali ambae kwa sasa anamiliki chati za muziki kwa single yake ya No Mediocre

Jumatatu, 22 Septemba 2014

WATU 115 WAFARIKI KANISANI NIGERIA

 
Muhubiri T.B Joshua amewashangaza wengi kwa kusema aliona ndege ikizunguka jengo hilo kabla ya kuporomoka

Serikali ya Afrika Kusini inasema kuwa watu miamoja na kumi na tano wengi wao wakiwa raia wa Afrika Kusini, walifariki baada ya kanisa kuporomoka nchini Nigeria.
Idadi kamili ya raia wa Afrika Kusini waliofariki ilikuwa 84.
Ndege iliyowabeba manusura wa mkasa huo, kumi na sita kati yao wakiwa wamejeruhiwa vibaya, imewasili mjini Pretoria.
Zaidi ya watu 300 kutoka Afrika Kusini walikuwa wametembelea kanisa hilo la 'All Nations' mjini Lagos, ambalo linaongozwa na mhubiri T.B. Joshua.
Inaarifiwa jengo hilo liliporomoka kutokana na ujenzi mbovu.
Mhubiri TB Joshua, amezua wasiwasi baada ya kuzungumzia kuona ndege iliyokuwa inazunguka juu ya kanisa hilo kabla ya jengo lenyewe kuporomoka.

MANUEL"CHELSEA NI TIMU NDOGO"

Pellegrini ameikejeli Chelsea kwa kucheza kama timu ndogo 
Kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini ameikejeli Chelsea kwa kucheza kama timu ndogo timu hizo zilipoambulia sare ya Moja kwa moja uwanjani Etihad.
Andre Schurrle ndiye aliyeiweka Chelsea mbele kabla ya mchezaji wa akiba Frank Lampard kuisawazishia man City ambayo ilikuwa na wachezaji . Pellegrini, 61,alisema "nafikiri tulicheza dhidi ya timu ndogo iliyokuwa inalinda ngome yake wala haitaki kucheza mbele.
Sio jambo la kufurahisha kamwe .
Wachezaji wangu 10 walilinda ngome yao na kupata bao la kusawazisha hadi tamati ya mechi.''
Pellegrini alifananisha mchezo wa Chelsea na ule wa Stoke ambayo iliilaza City 1-0 mwezi uliopita nyumbani kwao.
''Nafkiri tulicheza dhidi ya timu sawa na ile ya Stoke .Ilikuwa vigumu sana kwetu kufunga bao kwa sababu walikuwa wanalinga ngome yao badala ya kucheza mchezo wa hadhi inayostahili''
Sina haja ya kuwatathmini hata kidogo hilo nawachia timu zingine ''
City ilitoka nyuma na kusawazisha hata baada ya mlinzi wa kutegemewa Pablo Zabaleta kuoneshwa kadi ya pili ya njano baada ya kumchezea visivyo mshambulizi mpya wa Chelsea Diego Costa.
Kwa upande wake kocha wa Chelsea Jose Mourinho alikataa kata kata kujibu madai hayo ya Pellegrini akisema ''mbona yeye husema kuwa hazungumzi kuhusi mimi na timu yangu ilihali anaendelea kupiga domo ?
Usiniulize chochote kumhusu Manuel"

MASHABIKI WAMTUKANA BALOTELLI

Ujumbe wa Balotelli ulioibua hisia za ubaguzi wa rangi kwenye mtandao wa twitter 
Polisi nchini Uingereza wameanzisha uchunguzi kuhusu tukio ambalo mshambulizi wa Liverpool kutoka Italia Mario Balotelli alitukanwa kutokana na rangi ya ngozi yake kupitia kwa mtandao wa kijamii wa Twitter.
Polisi katika mji wa Merseyside wameanzisha uchunguzi kufuatia matusi hayo yaliyotokea baada ya mshambulizi huyo wa Liverpool kutuma ujumbe akiicheka kichapo cha Manchester United mikononi mwa timu ndogo ya Leicester siku ya jumapili.
Baloteli aliandika ''Man Utd...LOL'' na ujumbe wake ukasambazwa zaidi ya mara 150,000 na mashabiki wake.
Hata hivyo miongoni mwa mwa wale waliouona ujumbe huo walimfokea kwa kuicheka United na wakamtusi kwa misingi ya rangi yake.
Japo ni raiya wa Italia Balotelli mwenye umri wa miaka 24 ana asili ya kiafrika.Polisi wanafanya Uchunguzi kujua ni nani waliomtukana Balotelli. 

Polisi tayari wamefunga kurasa kadha zilizotuma jumbe hizo huku wakianza uchunguzi waliozimiliki ni kina nani na wanaishi wapi iliwakamatwe na kujibu mashataka ya ubaguzi wa rangi.
Kundi linalopigania kumaliza ubaguzi wa rangi katika michezo Kick It Out lilisema kuwa baada ya kuarifiwa kuwepo kwa matusi yenye kumdhalilisha Balotelli, kundi hilo lilianzisha uchunguzi kwa ushirikiano na polisi wa mitandao ya kijamii.
Sio mara ya kwanza kwa Mshambulizi huyo kudhulumiwa kwa misingi ya rangi yake .
Balotelli ambaye alikuwa uwanjani Liverpool ilipolazwa 3-1 na West Ham jumamosi amewahi kudhulumiwa kwa misingi ya rangi yake timu ya Italia ilipokuwa ikijifua kwa kombe la dunia mwezi mei mwaka huu .
Awali pia aliwahi kutukanwa akiwa Inter Milan na pia akihudumu AC milan.

EPL: Matokeo ya Man City vs Chelsea haya hapa


Home » General News » EPL: Matokeo ya Man City vs Chelsea haya hapa

EPL: Matokeo ya Man City vs Chelsea haya hapa

IMG_7407.JPG
Baada ya Man United kupokea kipigo kutoka kwa Leicester City, miamba mingine ya ligi kuu ya Uingereza Chelsea ilijitupa uwanjani kucheza na Manchester City.
Mchezo huo uliopigwa kwenye uwanja wa Etihad umeisha kwa matokeo ya sare 1-1.
Dakika chache baada ya Pablo Zabaleta kutolewa kwa kadi nyekundu Chelsea walipata goli la kwanza kupitia mchezaji aliyetokea benchi Andry Schurrle.
Akitokea benchi mchezaji wa zamani wa Chelsea Frank Lampard aliunganisha krosi ya James Milner na kuisawazishia Man City.
Mpaka mpira unamalizika Man City 1-1 Chelsea.

PICHA HIZI ZINAONESHA SHANGWE YA SERENGETI FIESTA 2014 MKOANI MOROGORO NI SHEEEEEDAH


.
.
Show ya Serengeti Fiesta 2014 iliyofanyika Jumapili,Sept 21 kwenye uwanja wa Jamhuri Stadium imefana baada ya wakazi wa (88.5) Morogoro kupokea kwa shangwe burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali
Tazama picha za wasanii wakiwa jukwaani
.
.
.
.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.