Jumamosi, 7 Mei 2016

Serikali yakamata Tani 4,900 za Sukari iliyofichwa Mbagala na Tabata jijini Dar

Baada ya muda mfupi wa rais kusema kuwa kuna wafanyabiashara wameficha Sukari, muda huu imeripotiwa kuwa huko Mbagala kuna Sukari ya zaidi ya tani 4,900 kwenye ghala la mfanyabiashara mmoja na imeelezwa zitachukuliwa hatua stahiki.
Chanzo: TBC, habari mpasuko

Shetta Akanusha Taarifa Kuwa Diamond Amewahi Kutoka Kimapenzi na Mkewe

Shetta amekanusha taarifa zilizozagaa mitandaoni kuwa Diamond amewahi kutoka kimapenzi na mama Qayllah.
Wiki kadhaa zilizopita Shetta alifuta picha zote kwenye akaunti yake ya instagram huku akiwaacha mashabiki wake wakijiuliza maswali mengi kutokana na kitendo hicho.
Akiongea kwenye kipindi cha Leo Tena, kinachoruka kupitia Clouds FM, Shetta amesema, “kuhusu suala la mama Qayllah kutoka na Diamond hakuna ukweli wowote.”
“Kuhusu suala la kufuta picha ni management yangu mpya ilinishauri hivyo ndiyo maana unaona nilifuta picha zote hizo. Team team tu wameanzisha na kuzisambaza mitandaoni lakini hakuna ukweli wowote namuamini sana mke wangu. Mimi na Diamond tuko vizuri ila hizo,” aliongeza.


Kajala Ahusishwa Undani wa Wimbo wa ‘Haya Yote ni Maisha’ ya P Funk

Msanii Madee amefunguka undani wa wimbo wa ‘Haya Yote Maisha’ wa Producer P Funk Majani ambao ameimba yeye, wimbo ambao ulishika chati na kugusa hisia za watu wengi.
Akiongea kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Madee amesema wimbo huo ni historia ya kweli ya P Funk na mwanamke ambaye ndiye mama wa mtoto wake wa kwanza, Kajala Masanja.
Madee aliendelea kusema baada ya mazungumzo P Funk alikubali kumpa beat na kwenda kuifanyia kazi, baada ya kukumbuka Madee mtindo alioutumia kwenye nyimbo zake.

“Haya yote maisha imetokea kipindi ambacho bado nipo na P Funk, alafu P Funk ana matatizo na mama mtoto wake Kajala, kwa hiyo wakati mi naenda pale kurekodi cheza kidogo, kabla sijamalizana na ile nakutana na beat ya yote maisha inaplay, alafu inaplay na chorus lakini hakuna verse, lakini the way ile beat inavyoplay majani anavyoiimba anaimba kwa feelings kinoma, nikamwambia bwana hii nyimbo mbona kali nigaie niimbe akasema hii na chana mwenyewe babu,” alisema Madee.
“Sema wewe ulivyochana kwenye kazi yake mola kuna ryhmes fulani naona unapita pita, unaongea kimajonzi hebu chukua hii beat kaandike, kwa hiyo nikapewa ile beat, aliniambia kwamba hii nyimbo ina feeling zangu, nataka uandike kitu hiki na hiki, kwa hiyo idea iliyotoka mule ni idea ya P Funk,” alisema Madee akimuongelea P Funk Majani.


Idadi ya Ajali zilizojitokeza wakati wa Majaribio Mabasi yaendayo Haraka

Wakala wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) umesema kutozingatia sheria za barabara za mradi wa mabasi hayo, kwa vyombo vingine vya moto vimesabisha ajali 14 wakati madereva wa mabasi hayo wakiendelea na mazoezi kwa ajili ya kuelekea kipindi cha mpito cha mradi kinachotarajia kuanza hivi karibuni.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala huo, Mhandisi Ronald Rwakatale amesema kuwa ajali hizo zimejitokeza wakati madereva wa mabasi ya mradi wakifanya mazoezi na kisha vyombo vingine vya moto viingilia barabara zake na kusabisha ajiali hizo.
Amesema ajali hizi ni matokea ya vyombo vingine vya usafiri kama magari madogo, daladala, bodaboda na waenda kwa miguu wamekuwa wakiingilia barabara za mabasi hayo na kusabisha ajali kutokana na kwamba barabara hizo haziruhusu mabasi hayo kupisha na vyombo vingine.
Mhandisi Rwakatale amesisitiza kuwa barabara za mabasi hayo ambazo ni za zege zimejengwa mahususi kwa ajili ya mabasi hayo hivyo madereva wa vyombo vingine wanahitajika kuheshimu sheria zinazoongoza mradi huo na kupita katika barabara walizotengewa na watakaokiuka sheria itachukua mkondo wake.
Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka unatarajiwa kuanza kipindi cha mpito mwezi huu wa Mei kutoa huduma ya usafiri kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam


IMEBAINIKA Rihanna na Drake Wamekuwa Kwenye Mahusiano ya Siri Kwa zaidi ya Mwezi sasa

Jarida la PEOPLE limefumua bonge moja la siri kuwa staa Rihanna na rapa Drake wamekuwa na mahusiano ya siri kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa.
Rihanna na Drake wamefanya collabo kama “Take Care” .“What’s My Name?” na “Work” ila pia wamekuwa wapenzi kwa muda sasa bila kutaka dunia ijue.
Rihanna ndio sababu ya Drake na Chris Brown kutoelewana ila kwa sasa inasemekana Kwa Rihanna pale Drake beki hazikabi

Young Dee Aporomoshewa Matusi Baada ya Kupost Picha Akivuta Bang

Usiku wa kuamkia May 6 2016 Paka Rapa Young Dee alipost picha akiwa anavuta kitu ambacho mashabiki wake kwenye mtandao wa instagram walitafsiri ni bangi na kuanza kumporomosshea comments kuwa anaelekea kuwa kama Chidi Benz,
Je Young hapa alikuwa anavuta bangi ? na kama ni bangi ni sawa kwa msanii kufanya hivi bongo kama tunavyoona nje kwa kina Wiz Khalifa.


Shilole Akanwa Laivu Mchana Kweupe...Nedy Adai Hawana Mahusiano ya Kimapenzi

Bongo fleva super staa Nedy Music ambaye hivi karibuni amejiunga na lebel ya Ommy Dimopz ya Pozi Kwa Poz amekanusha uvumi kuwa Shilole ni Mpenzi wake...Akihojiwa Clouds FM amesema hana uhisiano wa Kimapenzi na Shilole
Awali Nedy alitajwa akuwa mpenzi wa Shilole baada ya staa huyu kuachana na Nuh Mziwanda.


TAZAMA HAPA WIMBO MPYA WA SHETTA

Tazama Hapa Chini Video Mpya ya Mwanamuziki Shetta ya Wimbo Unaoitwa Namjua, Video Imefanywa South Africa...


Jason Rweikiza Achaguliwa Kuwa Katibu wa Wabunge wa CCM

WABUNGE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamemchagua Mbunge wa Bukoba Vijijini, Jason Rweikiza kuwa Katibu wao.
Rweikiza anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Mbunge wa Peramiho, Jenista Mhagama, ambaye safari hii hakuwania nafasi hiyo.
Katika uchaguzi huo uliofanyika juzi usiku katika ukumbi wa Msekwa uliopo ndani ya viwanja vya Bunge, Katibu huyo mpya wa Wabunge wa CCM alikuwa akipambana na Mary Chatanda, Mariam Kisangi na Abdalah Ulega.
Wabunge wote wa CCM pia walipiga kura kuwachagua wabunge 10 kati ya 21 walioomba ujumbe wa NEC.
Waliochaguliwa ni Livingstone Lusinde, Dk Hamis Kigwangalla, Stanslaus Nyongo, Steven Ngonyani, Peter Serukamba, Faida Bakari, Agness Marwa, Munde Tambwe, Angella Kairuki na Jamal Kassim Ali.
Wabunge ambao kura hazikutosha ni Mbaraka Dau, Alex Gashaza, Hawa Ghasia, Ibrahim Raza, Profesa Norman Sigalla ‘King’, Almas Maige, Angelina Malembeka, Yahya Massare, Mattar Ali Salum na Hafidh Ali Tahir


Snura Atoboa Siri Alipojifunzia Mauno

Msanii Snura ambaye jana video ya wimbo wake wa ‘Chura’ ulifungiwa na serikali kutokana na kutokuwa na maadili na kukiuka utamaduni wa kitanzania amefunguka na kusema kuwa yeye kukata viuno amejifunzia kwenye ngoma za asili.
Snura ameyasema hayo leo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari ambapo alikuwa akitoa ufafanuzi na kuomba radhi kwa watanzania kutokana na video yake hiyo kutokuwa na maadili na kuwadhalilisha wanawake.
“Mimi ni mwanamke na niliwachukua wanawake wenzangu kucheza lakini haina maana kuwa niliwachukua ili niwadhalilishe hapana, ila nakiri kuwa nilichokosea ni kuwaingiza kwenye maji ndiyo maana ilionekana kama ni udhalilishaji kwao. Lakini kucheza hakumdhalilishi mtu na ndiyo maana kuwa bendi wachezaji show wake wanakatika hata kwenye ngoma zetu za asili tunakatika, mimi nimejifunza kukatika kwenye ngoma za asili kwani ndiyo kipaji changu cha kwanza na huko ndiyo nimejifunzia kiuno” alisema Snura