Jumanne, 9 Septemba 2014

NYAMA YA KIBOKO YAWALETEA MAAFA.


Watu kumi walikanyagwa na gari lililokuwa linakwenda kwa mwendo wa kasi walipokuwa wanajaribu kujipatia angalau kipande cha nyama ya Kiboko mwishoni mwa wiki.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa mtandao wa Daily Nation.
Kiboko huyo alikuwa amegongwa na gari na kufariki Jumamosi jioni katika mkoa wa Limpopo wakati ambapo wanakijiji walikimbia katika sehemu hiyo angalau kujipatia kipande cha nyama.
Msemaji wa polisi aliambia shirika la habari la AFP kwamba mnyama huyo aligongwa na wanakijiji wakaona fursa ya nyama ya bure ambapo walikimbia kuinyakua na kuanza kuikatakata, ''
''Hapo ndipo gari lililokuwa linakwenda kwa kasi liliwagonga watu 8 walipokuwa wanakata nyama hiyo na kuwaua,'' aliongeza kusema msemaji huyo wa polisi.
Watu wengine wawili walifariki kutokana na majereha yao mabaya wakiwa wanapokea matibabu hospitalini.
Polisi wanasema kuwa watu wengine saba akiwemo dereva wa gari hilo wanapokea matibabu hospitalini.

EBOLA INAENEA KWA KASI NCHINI LIBERIA.


Ugonjwa wa Ebola unaenea kwa kasi nchini Liberia huku maelfu ya watu wakiambukizwa upya na idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka katika muda wa wiki tatu zijazo.
Hii ni kwa mujibu wa shirika la afya duniani WHO.
Shirika hilo linasema kuwa njia zinazotumika kukabiliana na janga la Ebola hazijafanikisha vita dhidi ya Ebola.
Takriban watu 2,100 wamefariki kutokana na ugonjwa huo katika kanda ya Afrika Magharibi hasa katika mataifa ya Guinea, Liberia, Sierra Leone na Nigeria mwaka huu.
Kwa mujibu wa shirika hilo wahudumu 79 wa afya pia wamefariki kutokana na ugonjwa huo.
Kadhalika shirika hilo limesema kuwa, mashirika yanayopambana na mlipuko wa ugonjwa huo, yanahitajika kuongeza juhudi.
Wakati huohuo , shirika la madaktari wasio na mipaka la Medecins Sans Frontieres linasema kuwa limelemewa kabisa na idadi inayozidi kuongezeka ya wagonjwa wa Ebola nchini Liberia.
Shirika hilo linasema kuwa kituo chake cha kutoa matibabu mjini Monrovia huwarudisha nyumbani watu wanaohitaji matibabu kila siku .
Msemaji wa shirika hilo Sophie Jane Madden aliambia BBC kuwa hali hiyo sasa ni ya vurugu na isiyodhibitika ambapo ametoa wito wa msaada wa kimataifa.
Mapema shirika la afya duniani WHO lilionya kuwa Liberia huenda ikashuhudia maelfu ya visa vya maambukizi mapya ya ugonjwa wa Ebola majuma yanayokuja.
Watu 1000 tayari wameaga dunia kutokana na ugonjwa huo kwenye taifa hilo la Afrika Magharibi.

EURO 2015:ENGLAND YAIFUNGA USWISI


England imeanza kusaka tiketi ya kucheza fainali za kombe la Ulaya kwa kuifunga Uswisi.
England imeanza harakati hizo za kucheza fainali hizo zitakazofanyika huko Ufaransa baada ya kuishindilia Uswisi mabao 2-0 usiku wa kuamkia leo.
Mshambuliaji mpya wa Arsenal, Danny Welbeck, aliibuka nyota wa kocha Roy Hodgson kwa kazi nzuri ya kutumbukiza kimiani mabao yote mawili, huku akifunga bao la pili dakika ya mwisho ya mchezo huo uliopigwa mjini Basel Uswisi.

WACHUNGUZI WASEMA MH17 ILIDUNGULIWA.


Wachunguzi wa Kijerumani dhidi ya ndege ya abiria ya Malaysia ambayo ilipata ajali huko Ukraine mwezi July na kuripuka angani wanaeleza kua ndege hiyo baada ya kukumbwa na kitu chenye ncha na kugongwa mara kadhaa na vifaa vyenye mionzi mikali ndio chanzo cha ajali.
Mwandishi wa youngluvega.blogspot.com amesema kwamba ushahidi huo ni wawazi na kwamba ndege hiyo ilishambuliwa kwa kombora..katika ripoti yao ya kwanza ya kiuchunguzi ,maafisi wa kijerumani katika masuala ya usalama wa anga wameeleza kua hakukuwa na tatizo la kiufundi lililosababisha ndege hiyo ipate ajali, ama makosa ya rubani yalosababisha ndege aina ya MH17 kuripuka.
Wataalam hao wameendelea kueleza kwamba kisanduku cha kurikodia mwenendo wa ndege hiyo hakikuonesha kwamba kulikua na dharura.
Abiria wote miambili na tisini na nane walipoteza uhai pindi ilipo anza safari kutoka uwanja wa ndege wa Amsterdam kueleke Kuala Lumpur.kutokana na ajali hiyo kuna shaka kwamba vikundi vya waasi wa Urusi viliiidungua ndege hiyo.Lakini mpaka sasa Urusi imepinga kuhusika kwa namna yoyote na ajali hiyo.
Inaarifiwa kwamba ripoti kamili juu ya ndege hiyo MH17 inaweza kupatikana pindi mwakani.

Wasanii waliporudi tena kutoa misaada kwa majeruhi wa ajali ya Musoma baada ya Fiesta.

1msm 
September 05 zaidi ya watu 35 walipoteza maisha yao kutokana na ajali ya mabus mawili kugongana uso kwa uso eneo la Saba saba ambalo liko nje kidogo na mji wa Musoma,wasanii waliahidi kwenda kutoa misaada kwa watu waliokutwa na matatizo ya ajali hiyo.
Asubuhi ya leo September 08 kabla wasanii kuanza safari ya kurudi Dar walitiza ahadi yao kwa ndugu na jamaa pamoja ma majuruhi wa ajali kwa kuwatembelea katika hospitali ya mkoa wa mara walipolazwa majuruhi hao na kugawana nao kidogo walichokipata kupitia show yao ya Serengeti Fiesta 2014 iliyofanyika jana.
14msm
Hii ilikua ni mara ya tatu kwa timu ya Serengeti Fiesta kutoa misaada na fedha kwa Waliojeruhiwa.
13msm
12msm
11msm
10msm
9msm
3msm
5msm
6msm
7msm
8msm
2msm
4msm