Ijumaa, 5 Februari 2016

Mke wa Dr Slaa Josephine Mushumbusi Ajibu Kuhusu Tuhuma za Kuomba Mkopo Bank Kwa Kutumia Nyumba ya Slaa

Mke wa Dr Slaa Amejibishana na Wadau Katika page yake ya Facebook na kujikuta akijibu tuhuma zilizozagaa jana kwenye magazeti kuwa aliomba mkopo wa sh mil 300 kwa kutumia nyumba ya Dr Slaa...

Soma Majibisha yao hapa;

Bryton Myrium Chadema 
"Mama ni kweli ulitumia nyumba ya dr slaa kumuombea mkopo jamaa mwingine sory kama nimekosea kuulliza"


Josephine Mushumbusi
"Sandra Bahati mbaya sana huwa siamini taarifa za magazeti,hivyo huwa hazipotezi mda Wangu sana. Pili hiyo ni taarifa hakuna mahala wamewasiliana na mimi.
Tusubiri,maana najua wapi pa kuwauliza taarifa hizo walizitoa wapi.
Ufupi bado mtu WA kuniumiza hajazaliwa"

Aggrey Charles
"Mama Josephine Mushumbusi kwa nafasi yako nadhani ugeiga hata zuri moja la Lowassa la UKIMYA. Kwani ni lazima ujibu kila kitu mama? Na ukijibu utajibu mangapi? Ushauri wangu kwako tulia kimya ujisomee tu huku mitandaoni siku zisogee. Mimi ni moja ya wafuasi wazuri wa Mh Dr W. SLAA ila si mama (yaani wewe) lakini heshima yenu ipo kwangu siku zote. UKIMYA wako utakuongezea kitu kuliko huku kuja kulumbana na vijana wenye njaa ya kuona kuna kitu kipya kinazaliwa katika nchi. Watu wenye njaa na kiu ya mabadiliko halisi hugombana na yeyote wanayemwona kama kikwazo. Ni Ushauri tu mama".

Josephine Mushumbusi
"Sometimes it is too much.
Nimekuawa kimya sana.
Na nafikiri ni Leo tu nimeonekana hapa.
Lowasa Hana ukimya naomba tusifananishwe"

Njia Kumi na Moja za Kumfanya Mpenzi Wako Asitoke nje na Michepuko


1. TAMBUA THAMANI YAKE

Unapokuwa Umeapa Kuwa Utampenda Mwenzako Hadi Kifo Kitakapowatenganisha, Uwe
Umefanya Hivyo Kwenye Nyumba Ya Ibada Au Kwingine, Lazima Ufahamu Jinsi Ya Kutambua
Juhudi Za Mpenzi Au Mwenzi Wako, Ili Kuepukana Na Uwezekano Wa Mwenzi Wako Kukuona
Kama Vile Unamchukulia Kawaida Na Hujali Jitihada Zake. Mtu Anapodhani Mwenzake
Hajali Jitihada Zake Ni Rahisi Kushawishika Kutoka Na Kwenda Kwa Mtu Atakayeitambua
Thamani Yake.

Ili Kuondoa Uwezekano Wa Mwenzako Kudhani Humjali Wala Kuthamini Juhudi Zake, Mara
Kwa Mara Jiulize Unaweza Kumfanyia Nini Ili Kumwonesha Kuwa Unamtambua. Jambo
Lenyewe La Kumfanyia Linaweza Kuwa Rahisi Tu, Mathalani Kumtumia Ujumbe Mfupi Kwa
Ajili Tu Ya Kumwambia Kuwa Yuko Mawazoni Mwako. Iwapo Utajenga Mazingira Ya
Kuitambua Thamani Ya Mwenzako Mara Kwa Mara Haitakuwa Rahisi Kwa Mwenzako Huyo
Kufikiria Kuchepuka.

2. JENGA UKARIBU NAYE

Mara Nyingi Jamii Huwachukulia Wanaume Kama Watumwa Wa Ashiki Zao, Lakini Matukio
Mengi Ya Kukosekana Kwa Uaminifu Hutokana Zaidi Na Mahusiano Ya Kikaribu Baina Ya
Mwanamke Na Mwanamume Na Si Tamaa Ya Mwili Ya Mwanamume. Iwapo Wanawake Wote
Wataufahamu Ukweli Huu, Watajua Jinsi Ya Kujenga Ukaribu Na Wanaume Zao Ili
Kuwaondolea Uwezekano Wa Kutekwa Na Wanawake Wengine.

Ni Kweli Kuwa Wapo Wanaume Wasioweza Kujenga Mshikamano Wa Kihisia Katika Suala La
Mapenzi, Lakini Huku Bado Wakiendelea Kuvutika Kimwili. Jambo Kubwa Ambalo Mwanamke
Anaweza Kulifanya Na Kumwepusha Mwanamume Kutoka Ni Kuhakikisha Ndiye Mtu Wake Wa
Karibu, Huku Mara Kwa Mara Akiwa Ndiye Mwanzilishi Wa Wazo La Kufanya Mapenzi.

3. MSIKILIZE VEMA MWENZAKO

Wanawake/Wasichana Huwa Na Mazoea Ya Kusemezana Na Marafiki Zao Mambo Mengi Ikiwa Ni
Pamoja Na Siri. Hata Hivyo, Wanaume Huogopa Kuwashirikisha Wenzao Mambo Binafsi Ya
Ndani. Ili Uweze Kuishi Vema Na Mwanamume, Lazima Ujue Jinsi Ya Kumhakikishia
Mwanamume Kuendelea Kuwa Mwanamume Hata Unapomweleza Mambo Yaamshayo Mihemko.

Kwako Wewe Mwanamke, Iwapo Utahisi Kuwa Mwanamume Wako Anataka Kuwa Wazi Katika
Mambo Fulani Binafsi Lakini Anahisi Tu Kuwa Atapoteza Uanaume Wake Kwa Kueleza Mambo
Yake, Mwekee Mazingira Ya Kumhakikishia Kuwa Ataendelea Kuwa Mwanamume. Msikilize Na
Usimlaumu, Muulize Maswali Yanayohitaji Majibu Chanya. Utashangaa Jinsi
Utakavyoboresha Ukaribu Wako Na Mwanamume Huyu Hivyo Kupunguza Uwezekano Wa
Kukusaliti.

4. MWACHE AWE NA MARAFIKI

Jambo Jingine Ambalo Linaweza Kumpunguzia Mwanamume Uwezekano Wa Kufanya Mapenzi Nje
Ya Uhusiano Ni Kumhakikishia Urafiki Na Wanaume Wenzake. Kwa Vyovyote Vile, Lazima
Mwanamume Wako Utakuwa Ulimkuta Na Marafiki. Usimzuie Kuendelea Kuwa Nao.

Unapomuunga Mkono Mwanamume Katika Kampani Yake Na Wanaume Wenzake Utakuwa
Umemwongezea Mwanamume Huyu Fursa Ya Kuendeleza Ukaribu Na Watu Wake, Hivyo
Kupunguza Fursa Ya Kujipenyeza Kwa Wanawake Wengine Katika Maisha Yake. Ukimbanabana
Halafu Na Wewe Ukashindwa Kuwa Rafiki Kwake, Akimpata Mwanamke Aliye Tayari
Atashikamana Naye.

5. TEKELEZA MALENGO NAYE

Hata Kama Uhusiano Wako Na Mpenzi Wako Umedumu Tangu Mlipokuwa Vijana Wadogo Chuoni,
Bado Haitoshi Kujihakikishia Kuwa Mmeshakua Pamoja. Ili Kuweza Kuepukana Na
Uwezekano Wa Mwenzako Kukusaliti, Lazima Nyote Msaidiane Katika Kutekeleza Mambo
Muhimu. Huku Ndiko Kukua Pamoja.

Njia Rahisi Zaidi Ya Kukua Pamoja Na Mpenzi Wako Au Mwenzi Wako Wa Maisha Ni Kuweka
Malengo Na Kuyatekeleza Kwa Pamoja. Mfano, Kama Mmeishi Katika Nyumba Ile Ile Kwa
Miaka Kadhaa Na Mazingira Yamewachosha (Pengine Nyumba Yenyewe Ni Ya Kupanga),
Pendekeza Kuhamia Sehemu Nyingine — Unaweza Kukuta Hata Mwenzako Kumbe Ana Hisia
Kama Hizo. Iwapo Utazigusa Hisia Zake Kwa Pendekezo Lako, Mpenzi Wako Atajihisi
Kuonekana Wa Tofauti Machoni Pako. Na Kwa Kuwa Baadhi Ya Watu Wanaotoka Nje Ya Ndoa
Huenda Kutafuta Utofauti, Utakuwa Umemzuia.

6. JITAHIDI KUMWELEWA

Mojawapo Ya Vishawishi Vikuu Vya Mwanamume Kujiingiza Katika Mapenzi Ni Kumpata Mtu
Ambaye Atamwelewa. Kama Huna Sifa Hii, Ni Rahisi Kwa Mwanamume Wako Kutoka Kwa Ajili
Ya Kuitafuta Kwingine.

Ili Kumzuia Mwanamume Kutoka, Onesha Jitihada Za Kutaka Kumwelewa Na Kufahamu
Matakwa Yake Ili Uweze Kuyatimiza. Katika Hili Usiogope Kumuuliza Maswali Magumu,
Mathalani Waweza Kumuuliza “Unajisikiaje Kuhusiana Na Uhusiano Wetu?” Au “Ni Kitu
Gani Ulichokuwa Unakitaka Katika Uhusiano/Ndoa Ambacho Hujakipata Mpaka Sasa?” Namna
Hii Utakuwa Umeonesha Jitihada Za Kutaka Kumfahamu Na Kumridhisha.

7. SISITIZA ZAIDI MATENDO

Wanawake Wana Utamaduni Wa Kupenda Kuyazungumza Mambo Yao, Ikiwa Ni Pamoja Na
Matatizo. Hili Ni Jambo Jema, Isipokuwa Tu Kinachotakiwa Ni Kuweka Uwiano Kati Ya
Maneno Na Matendo.

Mwanamke Hapaswi Kujiondoa Katika Hulka Yake Asilia Ya Kupenda Kusema Ili Aweze
Kudumisha Uhusiano Wake Na Mwanamume, Lakini Mara Kwa Mara Ni Vema Badala Ya Kusema
Tu Ukafanya Shughuli Kama Mbadala Wa Kusema. Badala Ya Kusema Sana, Unaweza
Kumshirikisha Mwanamume Katika Shughuli Fulani Ambayo Nyote Mnaipenda, Jambo Ambalo
Litaonesha Umoja Wenu, Huku Kila Mmoja Akipata Jibu Kwa Nini Alichagua Kuishi Na
Mwenzake.

Mathalani, Badala Ya Kuzungumzia Jinsi Usivyojisikia Vema Kwa Namna Msivyopata Muda
Mwingi Wa Kuwa Pamoja Na Kuzungumza, Tumia Fursa Hiyo Kuzungumza Kile Ambacho
Umekuwa Ukitaka Kuzungumza Na Mpenzi Wako, Maana Sasa Yupo. Badala Ya Kuzungumzia
Jinsi Unavyopenda Kujifunza Mapishi Fulani, Chukua Hatua Ya Kwenda Kujifunza, Na
Ikibidi Uende Na Mwenzako. Namna Hii Utaonekana Zaidi Kama Mtu Ambaye Unatenda
Maneno Yako, Si Kuzungumza Tu. Kwa Jinsi Hii Mpenzi Wako Atavutika Kwako Zaidi.

8. USIMWONDOLEE UJINSIA WAKE

Watu Wengi Katika Makuzi Yao Huwa Na Dhana Kuhusiana Na Jinsi Mwanamume Au Mwanamke
Anavyopaswa Kuwa. Kwa Mwanamume, Wengi Huamini Kuwa Atakuwa Mtendaji Kuliko Msemaji,
Asiyetawaliwa Na Mihemko, Mtawala, Jasiri, Hodari Na Kadhalika. Lakini Katika
Kipindi Cha Takriban Miongo Mitano Iliyopita, Hadhi Na Hulka Za Wanaume Na Wanawake
Zimebadilika. Isipokuwa, Bado Wanaume Halisi Wameendelea Kuwa Wanaume, Kama Ambavyo
Wanawake Halisi Wameendelea Kuwa Wanawake.

Iwapo Utakuwa Na Mazoea Ya Kumlazimisha Mwanamume Wako Kufanya Mambo Ambayo Si Ya
Kianaume, Au Ambayo Hayadhanii Kuwa Ya Kianaume, Mwanamume Huyu Anaweza Kulazimika
Kwenda Kumtafuta Mwanamke Ambaye Anampa Fursa Ya Kuendelea Kuwa Mwanamume.

Ili Kuondoa Uwezekano Wa Mwanamume Kutafuta Mahala Ambapo Uanaume Wake Utatambuliwa,
Jaribu Kufikiria Mambo Ambayo Humfanya Mwanamume Kujihisi Kuwa Mwanamume Kweli.
Namna Hiyo Utaongeza Mapenzi Yake Kwako.

9. PUNGUZA TAHADHARI

Mojawapo Ya Mambo Ambayo Huzuia Mahusiano Kufikia Ukamilifu Wake Ni Watu Kuishi Kwa
Tahadhari Wakiogopa Kuingia Katika Maeneo Ambayo Yanaweza Kuondoa Furaha Yao,
Pengine Kwa Mmoja Wa Wenza Hao Kukwazika. Ni Kweli Kuna Umuhimu Wa Kuepuka Kumkwaza
Mwenzako, Lakini Mnapoishi Kwa Tahadhari Kubwa Ni Vigumu Kufikia Ukamilifu Wa
Uhusiano Wenu Na Ni Rahisi Kwa Mwenza Kutoka Kwa Ajili Ya Kupata Uhuru Na Amani
Zaidi.

Ili Kuepusha Balaa, Jiulize Ni Wapi Wewe Na Mwenzako Hamkubaliani. Ukishayapata
Mambo Ambayo Hamkubaliani, Jaribu Kuweka Uwiano Na Kumpa Uhuru Mwenzako Katika
Kuyafanya Hayo. Namna Hii Utaongeza Ukamilifu Katika Uhusiano Wenu Na Hisia Za
Kubanwa Zitaondoka.

10. JISHUGHULISHE AKUKOSE

Wanawake Hupenda Zaidi Vitu Ambavyo Ni Haba Au Hupatikana Kwa Nadra. Katika Uhusiano
Wa Kimapenzi Mwanamke Hatakwambia Kuwa Anataka Uondoke Ili Aweze Kupata Fursa Ya
Kukumisi Na Kutamani Kukuona, Lakini Ukweli Ni Kwamba Ukipatikana Kwa Nadra
Utaongeza Mvuto Wako Kwake, Ilimradi Tu Uwe Na Sababu Ya Kupatikana Kwa Nadra.

Lazima Ujue Jinsi Ya Kumfanya Mpenzi Wako Akuhitaji. Jishughulishe Na Uchakarike,
Kwani Kwa Kufanya Hivyo Utaongeza Kipato Chako Na Kumwongezea Usalama Na Uhakika
Mpenzi Wako, Lakini Pia Utampa Mpenzi Wako Fursa Ya Kukumisi Na Kupunguza Uwezekano
Wa Kukusaliti.

11. MWEKE HURU AWE NA MUDA WAKE

Mwache awe na muda wake binafsi. Huwezi Kumzuia Mpenzi Wako Kutoka Na Wanaume/Wanawake Wengine Kwa Kuwa Na Wivu Na Kumfuatiliafuatilia. Lakini Kwa Kuzingatia Mambo Haya Yaliyobainishwa Hapa, Utakuwa
Umeondoa Sababu Nyingi Za Mpenzi Wako Kufikiria Kuwa Na Uhusiano Na Mtu Wa Nje.

Imebainika Mashine ya CT Scan Iliyofungwa Muhimbili Hospital ni ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)

WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto imekiri kwamba mashine ya CT Scan iliyofungwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ilikuwa ni ya kituo cha kisasa cha kutolea huduma za afya cha Benjamin Mkapa kilichopo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Akijibu swali la nyongeza bungeni mjini Dodoma, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Khamis Kigwangalla alisema mashine hiyo iliingia nchini kwa lengo la kupelekwa katika kituo hicho lakini ikapelekwa Muhimbili kutokana na kutokamilika kwa majengo ya kufungwa mashine hiyo katika kituo hicho.

Alisema, uamuzi huo waliuchukua pia kwa sababu hela ya kununua mashine nyingine ambayo itapelekwa kufungwa katika kituo hicho ilikuwepo na kwa sasa mchakato wa ununuzi unaendelea.

Dk Kigwangalla alikuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Chemba, Juma Nkamia (CCM) aliyetaka jibu la Serikali kama ni kweli ilichukua mashine ya kituo hicho na kufunga katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ama ilinunua.

Awali katika swali la msingi msingi, Nkamia alitaka kujua mpango wa Serikali wa kununua mashine mpya ya CT -Scan kwa ajili ya Hospitali ya Taifa Muhimbili.

 Kuhusu hilo, Dk Kigwangalla alisema, Desemba mwaka jana Serikali ilipeleka mashine ya CT-Scan katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambayo inatumia teknolojia ya kisasa yenye X-ray tube mbili na uwezo wa kupiga picha ya 128 slice mara mbili.

Bomoa Bomoa Zaikumba Sinza...Baa za Uwanjani Legho Zavunjwa

BAADHI ya baa zilizopo katika viwanja vya Legho, Ubungo jijini Dar, leo zimevunjwa kufuatia agizo la mahakama kwa kile kilichodaiwa wamiliki walivamia eneo ambalo siyo lao.
Akizungumza na mwandishi wetu, dalali wa mahakama kutoka katika kampuni ya Mem Auctioneers and General Brokers Ltd, Elieza Mbwambo, alisema mmiliki halali  wa eneo hilo ni Dar Cool Makers Limited ambaye baada ya  kuvamiwa eneo lake alifungua kesi mahakamani mwaka 1993 ambapo iliendelea mpaka ilipofikia leo.

Wavamizi wa eneo hilo ambao ni John Ondoro Chacha, Jumuiya ya Wazazi CCM na mtu mwingine mmoja baada ya kuona mmiliki halali amepeleka kesi mahakamani nao wakaenda kuweka zuio ambapo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliamuru eneo hilo lirudi kwa mmliki halali ambapo wavamizi walitakiwa wabomoe vibanda walivyokuwa wamejenga walikokuwa wakifanya biashara ya baa.

“Januari 25 mwaka huu tulipewa oda na mahakama tuje kuwatoa hawa wavamizi, tuliweka tangazo kama wiki moja iliyopita lakini hawakujali hivyo leo ikawa ndiyo siku rasmi ya kuwaondoa na kama unavyoona ndiyo tunabomoa hivi.

“Mwenye kesi ya msingi ambaye ni John Ondoro Chacha alitakiwa kuwaambia wapangaji wake kwamba ameshindwa kesi lakini hakuwaambia ndiyo maana hata tangazo lilipowekwa hawakushtuka, kwa mujibu wa mahakama huyu Chacha ambaye kwa sasa ni marehemu na watoto wake ndiyo walikuwa wakipokea kodi ya kila mwezi kwa wafanyabiashara waliowapangia  wakati eneo hili siyo lao,” alisema Mbwambo.

Watu mbalimbali walionekana wakiwa wamesimama huku wakishangaa eneo hilo huku wengine wakilalamika kwamba watakuwa wanajiachia  wapi wakati walikuwa wamezoea viwanja hivyo.

Source-Global Publishers

Siri Imefichuka..Kumbe Rwanda ilitoa Mafunzo ya Kijeshi kwa Wakimbizi wa Burundi Wamwondoe Nkurunziza Madarakani

Ripoti ya siri ya Umoja wa Mataifa(UN): Rwanda ilitoa mafunzo ya kijeshi kwa wakimbizi wa Burundi wamwondoe Nkurunziza madarakani.

Burundi imekabiliwa na machafuko tangu mwezi Aprili 2015, wakati Rais Pierre Nkurunziza alipotangaza kwamba atawania muhula wa tatu wa urais, ambao alishinda.

Akijibu madai hayo, waziri wa maswala ya kigeni nchini Rwanda Louise Mushikiwabo amesema kuwa mgogoro huo wa Burundi ni mzito na wa kujitakia miongoni mwa viongozi wa Taifa hilo na kwamba jamii ya kimataifa inafaa kuuangazia na kuwacha kutafuta sababu za kuuepuka. ''Ni Muhimu kuelewa kwamba usimamizi wa wakimbizi wa taifa jirani ni suala gumu, hivyo basi Serikali ya Rwanda imelazimika kuweka sheria kali dhidi ya wakimbizi wa Burundi''. Mushikiwabo amesema kuwa madai hayo yanatokana na hatua ya Rwanda kuwahifadhi wakimbizi wa Burundi ambao wanadaiwa kuwa wapinzani wa Serikali.

Waziri huyo ameongezea: Hatuwezi kuwarudisha wakimbizi hao hadi pale kutakapokuwa na mfumo ambao utalinda maisha yao nchini Burundi

______________________
A United Nations report has accused Rwanda of recruiting and training refugees from Burundi to oust President Pierre Nkurunziza, according to a Reuters news agency report.

Rebel fighters told the UN panel of experts who monitored sanctions on the Democratic Republic of Congo, that the training was done in a forest camp in Rwanda.

“They told the group that they had been recruited in the Mahama Refugee Camp in eastern Rwanda in May and June 2015 and were given two months of military training by instructors, who included Rwanda military personnel,” according to Reuters.

18 Burundian combatants including six children in South Kivu province, in eastern Congo told the experts they were trained in military tactics, use of assault rifles, rocket propelled grenades among others.

Rwanda Ambassador to the UN Eugene Gasana dismissed the claims.

“This further undermines the credibility of the Group of Experts, which seems to have extended its own mandate, but apparently investigating Burundi,” Ambassador Gasana told Reuters.

In December, Burundi had accused Rwanda of supporting a rebel group that was recruiting Burundi refugees in Rwanda but President Paul Kagame dismissed the claims describing it as “childish”.

Rais Magufuli Afunguka na Kusema Yeye si Kichaa wala Dikteta ila Inafika Wakati Lazima Afanye Hivyo!!

RAIS Dk. John Magufuli amesema anapochukua hatua yeye si kichaa, si dikteta, si shetani wala si mnyama, ila ni mpole, lakini amefika mahali lazima afanye hivyo kwani ndani ya Serikali yanafanyika mambo ya ajabu.

Kauli hiyo aliitoa jana jijini Dar es Salaam katika kilele cha Siku ya Sheria nchini, alipokuwa mgeni rasmi kwa mara ya kwanza katika uzinduzi wa Mwaka wa Mahakama tangu alipoapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Alisifu kazi kubwa inayofanywa na Idara ya Mahakama, huku akitangaza uamuzi wa gharama za kurusha matangazo ya moja kwa moja ya Bunge zaidi ya Sh bilioni nne ni bora zikawasaidia wananchi.


“Ninapochukua hatua mimi si mnyama, si dikteta, si shetani, ni mpole kweli, lakini inafika mahali lazima nifanye, yanayofanyika serikalini ni mambo ya ajabu sana, nataka kutoa sadaka yangu, inawezekana hata nikifa naweza kuwa rais wa malaika,” alisema.

Alipongeza kazi kubwa inayofanywa na mahakama huku akibaki kujiuliza kwanini katika maadhimisho ya siku yao hawarushi matangazo yao moja kwa moja kupitia luninga.


“Mnafanya kazi kubwa, nilipofika niliuliza kwanini hii siku yenu hamrushi ‘live’, nikajibiwa fedha za kurusha ‘live’ zinapelekwa kuwahudumia wananchi.


“Kipindi kimoja kurusha ‘live’ kwa wiki mbili inatumika zaidi ya Sh bilioni nne, ni vizuri kuzikata hizo fedha zinazopelekwa kurusha ‘live’ zikapelekwa katika kesi za ubunge zinazohitaji shilingi bilioni tatu kusikilizwa hadi kumalizika kwake,” alisema.

Alisema mahakama ilikuwa inapewa bajeti ya Sh bilioni 41, lakini mwaka 2015/2016 ilishuka wakatakiwa kupewa Sh bilioni 12 ambazo hadi sasa hawajapewa.

“Kiongozi lazima ufikirie wapi pa kupeleka fedha na wapi pa kunyima, watu wa mahakama mnafanya kazi ya Mungu, nawaahidi ndani ya siku tano nitakuwa nimewapa Sh bilioni 12 zote.


“Sina tatizo la masilahi ya wafanyakazi wa mahakama, katika bajeti ya mwaka huu nitawapa fedha nyingi kuliko bajeti zote zilizopita, fedha zipo,” alisema.

Mahakimu Kutumbuliwa
Rais Magufuli alisema anamwagiza Jaji Mkuu kuwachukulia hatua mahakimu 502 ambao hawakufikia malengo ya kumaliza kesi 250-260 kwa mwaka. Walimaliza kesi chini ya 100.


“Mahakimu ambao hawajafikia kumaliza kesi 260 hayo ndiyo majipu yako Jaji Mkuu, unatakiwa kuyatumbua, wewe uliniapisha hata mimi, leo unapitisha agizo mwingine anapinga.


“Unatoa siku saba sasa sijui ndiyo watamaliza kutoa hizo hukumu, nakuagiza wachukulie hatua, tusipochukua hatua hakuna kitakachofanyika.


“Walioshindwa kufikia lengo unawabakiza wa nini, wasomi wako wengi, hata ukitangaza leo watajitokeza, niruhusu mimi nitangaze, sitaki kuingilia mahakama,” alisema.

Mabilioni ya NIDA
Akizungumzia hatua yake kwa watendaji wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), alisema ilipewa Sh bilioni 176.6, lakini vitambulisho vilivyotengenezwa havifiki hata milioni mbili na havina sahihi wakati vitambulisho vya kupigia kura fedha iliyotolewa haizidi Sh bilioni 70, lakini vina sahihi za wapigakura wote wa Tanzania ambao ni milioni 23,253,982.


“Utaona ugumu wa kuongoza, nchi inatawaliwa na madudu ya kila aina, wapo watu wanacheza na fedha wanavyotaka wakati wapo watu masikini sana, wengine wanataka bodi zao wakakae Ulaya.

“Hapo ndipo tulipofikia, wengine wanalipwa mshahara kwa mwezi Sh milioni 35, naomba mniombee kabla ya kunihukumu, toeni hukumu kwa haki kwa hawa wanaotaka kuifikisha nchi pabaya, toeni hukumu zao haraka,” alisema.

Kesi za Wakwepa kodi
Rais Magufuli alisema kuna kesi 442 za kukwepa kodi ambazo zingeamuliwa Serikali ingepata Sh trilioni moja, ambayo ingeweza kununua ndege zaidi ya sita.

Alimuomba Jaji Mkuu kuzimaliza kesi 442 na kama zikimalizika fedha hizo Sh trilioni moja ataipa Idara ya Mahakama Sh bilioni 259 na Sh bilioni 750 zilizobakia zitanunuliwa ndege sita na wafanyafakazi 250 ATCL waliopo sasa wataondolewa.

Akizungumzia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, alisema kuna kesi 26 za watu waliokutwa na nyara za Serikali, ambazo zipo zaidi ya miaka mitano hazijaamuliwa kwa sababu upelelezi bado.


“Polisi wapo, DPP yupo, upelelezi unaendelea kila siku, hapo unaona tatizo lilipo, DPP upo unapeleleza nini au unatafuta rushwa?” alisema.

Alisema suala la kuanzishwa kwa mahakama ya mafisadi ya wahujumu uchumi halihitaji kwenda bungeni kufanya mabadiliko, lifanywe haraka, mahakama ianze kwani nchi inachezewa.

Pamoja na hali hiyo Rais Magufuli alikubali kupokea maombi yote yaliyotolewa na mahakama na kuyazingatia kwani lazima ayaunge mkono ikiwamo kukubali watumishi wa Idara ya Mahakama wasome na kupatiwa mikopo na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB).


“Nimeamua nchi iende na itaenda, anayefikiria ataikwamisha atakwama yeye, nategemea zaidi mahakama katika kufanikisha hilo,” alisema.

Alhamisi, 4 Februari 2016

Mbunge Godbless Lema Awachana CCM Laivu....Hawawezi Kukaa Madarakani Kwa Maisha yote

Mbunge wa arusha mjini Godbless lema amesema leo bungeni swala la Zanzibar si la kichama,Ni swala la nchi na lisipotafutiwa ufumbuzi lina athari kwa kila mtu,

Lema ameenda mbali zaidi na kuwaambia Wabunge Wa CCM hii nchi ikiharibika hata watoto wao wataharibikiwa na hawawezi kukaa madarakani kwa maisha yao yote.

Lema amemtolea mafano mbunge Marry nagu na kumwambia akumbuke serakali iliyopita alikuwa waziri,Lakini leo naye anauliza maswali ya nyongeza.

Lema alienda mbali zaidi na kumwambia Mwenyekiti wa bunge Chenge asijione ni mdogo wake mungu kwa kukalia kiti cha spika.