Ijumaa, 18 Novemba 2016

Model Calisah Afunguka Baada ya Kusambaa Kwa Video yake Akimla ‘Denda’ Wema Sepetu

Weekend hii katika mitandao ya kijamii kumesambaa video inayomuonyesha malkia wa filamu nchini Wema Sepetu akiliwa denda na model Calisah.

Wawili hao ambao walitumia nguvu nyingi kufanya siri mahusiano yao, wameumbuka kupitia video hiyo iliyosambaa katika mitandao ya kijamii.

Akiongea na Bongo5 Jumatatu hii, Calisah amesema hajui ni nani ambaye amesambaza video hiyo mtandaoni kwani walikuwa nayo yeye pamoja na Wema.

“Nilikuwa nachati na Wema kawaida ghafla nikaona notification, kufungua ndio nikakuta hiyo video na mimi ndio nilikuwa mtu wa kwanza kumuuliza Wema kwa sababu video nilikuwa nayo mimi na Wema,” alisema Calisah.

Pia model huyo amedai video hiyo imemsababishia matatizo katika familia yake pamoja na kumpoteza bibi yake kwa presha.

Lady Jay Dee Afunga Ndoa Tena..Apost Picha Akiwa Honey Moon

Msanii nguli na namba moja nchini kwa upande wa kina dada binti machozi, komamdo, anaconda, lady jay dee amefunga ndoa weekend hii kupitia mtandao wa I.G amepost baadhi ya picha akila honey moon uko Zanzibar

Michirizi Inayoonekana Kwenye Miili ya Akina Dada Inaashiria Nini?

Hivi Ile michirizi inayoonekana kwa baadhi ya kinadada nyuma ya goti wakiwa wamevaa sketi fupi huwa ni ishara ya utamu wao kama Mwana FA alivyoimba  "Michirizi ya utamu nyuma ya goti mimi hoi na moyo hai sio toi "  au ugonjwa wa ngozi?

Taarifa Kuhusu Kinachoendelea Kwenye Kesi ya Scorpion Mtoa Macho Mahakamani

Upelelezi wa kesi inayomkabili Salum Njwete maarufu kama Scorpion anayetuhumiwa kumsababishia upofu wa kudumu Saidi Mrisho umekamilika na hatimaye shauri hilo litasomwa Novemba 30 mwaka huu katika mahakama ya manispaa ya Ilala.

Njwete anatarajiwa kusomewa mashtaka yake baada ya yale ya kwanza kufutwa ambapo itakuwa ni mara ya kwanza kusikilizwa baada ya kufunguliwa mashtaka mapya.

Huyu ndiye Scropion, kijana aliyejizolea umaarufu ambapo watu wengi hupenda kumshuhudia kila aingiapo na kutoka mahakamani huku kila mmoja akizungumza lake kwa kesi inayomkabili.

Alipoingia mahakamani leo, aliomba ufafanuzi wa wazi juu ya mashtaka yanayomkabili ambapo upande wa jamhuri kupitia kwa wakili wake Chesensi Gavyole walisema ushahidi umekamilika.

Kutokana na kuombwa ufafanuzi, Hakimu anayesimamia kesi hiyo Flora Haule amesema baada ya upelelezi huo kukamilika kesi hiyo itasomwa Novemba 30 mwaka huu, hivyo mshtakiwa atapata ufafanuzi wa mashtaka yake .

Ikumbukwe kwamba Oktoba 19 mwaka huu, Salum Njwete maarufu kama Scropion alifutiwa kesi na kisha kusomewa upya mashtaka yake kutokana na uamuzi wa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) aliyeomba kufanya hivyo baada ya hati ya awali kuwa na mapungufu ya kisheria

Dalili Muhimu za Mwanamke Aliefika Kileleni Mkiwa Faragha.

Wanaume wengi sana hua tunadanganywa na wenza wetu kua tumewaridhisha vya kutosha lakini ukweli hua hakuna kitu

Hua wanafanya kwa nia njema tu kwani wanaume hua tunajiskia amani sana kuambiwa umemfikisha mtoto wa kike kwani ni jambo la kishujaa kama trumph uchaguzi us

kwa uzoefu wangu,mwanamke aliefika kileleni hua anakua hivi bila hata kuuliza au kusubili kuambiwa

1.MWILI KUISHIWA NGUVU

mwanamke aliefika orgasm hua anaishiwa nguvu mwili baada ya safari ndefu ya mikito,ukiona baada ya sex msichana anauwezo wa kufanya kazi nzito nzito jua umefanya kazi butu sio mpaka uambiwe

2.KUPITIWA NA USINGIZI BAADA YA MECHI

ukiona ka beby kako kamepitiwa na usingiz gafla baada ya sex jua kaz imeenda sawia,ikumbukwe kufika orgasm ni mechanism inzito,

3.MUSCULAR CONTRACTION

mwanamke anaekalibia/ aliefika kileleni misuli hubana na kuachia ,hii ni kwa mwili mzima hadi kwenye vagina,hilitendo pia hufuatiwa na mwili kutoa jasho.
ukiona ivo ujue kazi zimeenda sawia

Wakuu huu ni uzoefu wangu niliopata nikiwa field,

Ukiona mpenz wako hajaonyesha izo dalili muhimu basi jua hakuna kitu

Kama unajua dalili zingine zile kuu na muhimu tiririka

Wazee Pigeni kazi tutokomeze fake orgasm tunazodanganywa na kupewa kiburi ili tutoe chapaa

Udhaifu Huu wa Ali Kiba Unamfanya Diamond Ang'are

Ni ukweli usiopingika wasanii Diamond na Alikiba ni lulu ya taifa kwa sasa hasa unapozungumzia suala la usambazaji wa muziki wa Bongo Fleva kwenda zaidi kimataifa na kuufanya uwe na thamani hata kwa wasanii wengine watakapofikia level zao.

Leo nazungumzia utofauti mkubwa wa wasanii hawa wawili ambao mimi kama #KÄ°JANAMZALENDO nimeuona, Alikiba anaimba vizuri kuliko Diamond lakini kupitia kigezo cha kuimba pekee hakiwezi kumfanya kuwa Msanii mzuri kuliko wengine but kuna mambo mbalimbali ambayo msanii yeyote anapaswa kuyafanya ili awe bora zaidi kuliko wenzake.

1 Alikiba amekuwa akiamini yeye binafsi anaweza kufika international bila kufanya kazi na wasanii wa nje ya nchi Jambo ambalo Si la kweli ili Msanii yeyote uweze kufanikiwa kimataifa lazima ufanye Collabo na wasanii wa level hiyo mfano Wizkid sasa Dunia inamjua kupitia Drake, Davido dunia inamfahamu kupitia Meek Mill,

2 kufanya media tour na Show za kimataifa; Miongoni mwa mambo ambayo Alikiba yanamfanya awe tofauti na Diamond, Alikiba hafanyi media tour za nje anafanya za ndani tu Ndani kila mtu anaufahamu uwezo wake so tunataka aupeleke nje ya Tz pia aanze kufanya matamasha ya kimataifa haiwezekani msanii unataka kwenda kimataifa halafu kwa mwaka Unaperfom Majukwaa matatu tu.

3 Kupunguza Collabo na wasanii wa kawaida; kitu kingine ambacho Kiba anapaswa kukizingatia ni kupunguza Collabo haÅŸa wa wasanii wa kawaida ambao wanataka kupata jina kupitia yeye simaanishi kwamba asikuze vipajj lakini anaweza kuwasaidia kwa kuwasaini kwenye Lebo yake ili bado awe na nguvu ya kuwasapoti.

4 Kuongeza Timu ya washauri: Kingine Kiba anapaswa kuongeza idadi ya watu anaofanya nao kazi ambao ni official lakini hata kuwafanya nao wawe mastaa ili popote wanapofanya interview nado yeye atajwe mfano Alichofanya DÄ°AMOND amembrand DESÄ°GNER, DANCERS ,MAMA, MTOTO, DADA kote huko bado jina lake linatrend

Mwanamke Afa Akiombewa Kwa ‘Nabii’, Akutwa Hana Nywele Kichwani Pamoja na Nyusi za Macho

Mwanamke mkazi wa Unga-Limited jijini hapa, Lightness Kivuyo ameripotiwa kufa wakati akifanyiwa maombi nyumbani kwa mchungaji aliyejulikana kama ‘Nabii Rajabu’ eneo la Kwa-Mrombo pia jijini hapa.

Kwa mujibu wa dada wa marehemu, Juliana Kivuyo, Lightness alikuwa amesindikizwa nyumbani kwa nabii huyo nyakati za usiku na mumewe aliyemtambulisha kama Shafii Mohammed na kwamba wakati akifanyiwa ibada ya maombi, alianguka na kufariki miguuni mwa ‘Mtume,’ huyo.

“Baadaye shemeji alikuja nyumbani akihema, huku anadai kuwa dada alikuwa kwenye hali mbaya kule kwenye maombi,” alisema Juliana na kuongeza kuwa alitoka mbio kwenda Kwa-Mrombo nyumbani kwa Nabii Rajab na kumkuta dada yake amelazwa kwenye kochi, akiwa bila nguo isipokuwa tu khanga alizofunikwa nazo.

Nabii huyo pia anadaiwa kumnyoa nywele zote pamoja na nyusi za macho wakati akimfanyia ‘huduma,’ hiyo.

Polisi jijini hapa wamethibitisha tukio hilo wakiongeza kuwa tayari watu wawili wamekamatwa kutokana na kifo hicho cha ‘maombi tatanishi.’

Aidha, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Charles Mkumbo ameongeza kuwa atatoa taarifa kamili mara baada ya kikao chake na Mkuu wa Mkoa.

Mganga Mkuu katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, Jacqueline Uriwo amekiri kupokea mwili wa marehemu, lakini akasema, “Kwanza walijaribu kutudanganya kuwa huyo mama alikuwa hai na kwamba aliletwa kwa ajili ya matibabu, lakini tukagundua kuwa walichokileta ni mwili mfu, hivyo tukampeleka kwenye chumba cha kuhifadhi maiti!.”

Mkurugenzi wa Huduma ya Mazishi katika hospitali hiyo ya mkoa, Dk Francis Coster alisema mwili ulipelekwa hapo na mume wa marehemu ambaye alisisitiza kuwa mkewe hajafa, bali kazimia tu na kwamba mara nyingi huzimia kwa saa nyingi.

Dk Coster aliongeza kuwa ilibidi na wao wasiweke mwili kwenye jokofu na kuulaza kwenye machela kwa saa sita na ndipo wakaamua kuuweka kwenye droo za maiti, kwani ilikuwa wazi sasa kwamba asingeamka tena asilani.

Waganga hospitalini hapo wamekiri kuwa mwili wa marehemu uliletwa hospitalini hapo ukiwa umenyolewa upara, lakini ukiwa na mikwaruzo pamoja na uvimbe hususan maeneo ya mikono na kifua.

Baba mkubwa wa marehemu, Ally Kivuyo ambaye ndiye mlezi wa Lightness, alisema mume wa marehemu alimtaarifu juu ya kifo hicho na kuongeza; “Lakini baadaye nikaletewa taarifa nyingine kuwa Lightness kumbe alikufa wakati akifanyiwa maombi au vitu vingine, nyumbani kwa mtu anayeitwa ‘Nabii Rajabu,’ hapo basi ikabidi niwataarifu polisi ambao walikuja kumkamata mumewe pamoja na huyo anayejiita nabii au mtabiri.

Source: Habari Leo

Je, Paul Makonda Anajua Mantiki ya Alichosema Kuhusu Waliotaka Kumuhonga Mil 50 Kisheria?

Kwanza nianze kwa kusema kuna mambo mengi ninakubaliana na utendaji wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda lakini kuna mambo machache ambayo yananipa ukakasi unaonifanya nitimize wajibu wangu kama raia katika kumkosoa, kumuelimisha na kumjenga zaidi katika utendaji wake kama Mkuu wa Mkoa.

Jambo moja ambalo linapelekea msingi wa mada yangu ni kuhusu hii kauli yake aliyonukuliwa akisema,
"Kuna kikundi cha watu kumi ambao hao walikuja kwangu na mimi niliamua kuwatambua kama maajenti wa shetani, walikuja kwangu wanapata faida kati ya milioni 35 mpaka 45 kwa mwezi, wao walio kumi wakakubali kupanga mkakati eti wa kunishawishi nikubali niwe napokea milioni tano tano kwa mwezi kwa watu kumi maana yake milioni 50. Nikae kimya nisipige kelele juu ya shisha ili wao waendelee kupata faida".

Hii kauli ukiichambua katika msingi wa lateral thinking huwezi kugundua impact iliyobeba hasa ikichukuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama.

Mkuu wa Mkoa kama mwakilishi wa Rais wa Tanzania ambaye pia Rais ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama lazima aelewe kuwa sheria ya kupambana na rushwa katika kifungu cha 39(1-2) inamtaka aijulishe TAKUKURU kama anadhani kuna matendo ya rushwa.

Kifungu cha 39(1) kinasema;
39.-(1) Every person who is or becomes aware of the commission of or the intention by another person to commit an offence under this Act shall be required to give information to the Bureau.

Kama hiyo haitoshi, Makonda lazima aelewe kuwa soliciting bribes ni kosa la jinai ambalo limefafanuliwa katika kifungu cha 15(1a-b) ya sheria ya The Prevention and Combating of Corruption Act 2007.

Moja ya vifungu vya Sheria inasema;
15.-(1) Any person who corruptly by himself or in conjunction with any other person-
(a) solicits, accepts or obtains, or attempts to obtain, from any person for himself or any other person, any advantage as an inducement to, or reward for, or otherwise on account of, any agent, whether or not such agent is the same person as such first mentioned person and whether the agent has or has no authority to do, or forbearing to do, or having done or forborne to do, anything in relation to his principal’s affairs or business; or

(b) gives, promises or offers any advantage to any person, whether for the benefit of that person or of another person, as an inducement to, or reward for, or otherwise on account of, any agent whether or not such agent is the person to whom such advantage is given, promised or offered and whether the agent has or has no authority to do, doing, or forbearing to do, or having done or forborne to do, anything in relation to his principal’s affairs or business, commits an offence of corruption.

(2) A person who is convicted of an offence under this section, shall be liable to a fine of not less than five hundred thousand shillings but not more than one million shillings or to imprisonment for a term of not less than three years but not more than five years or to both.

Hoja ya msingi hapa ni kutaka kufahamu kama Mkuu wa Mkoa, Makonda ametoa taarifa hii TAKUKURU? Kama alitoa taarifa, kwa nini hakuweka mtego wa kuwakamatisha kwa TAKUKURU.

Kama hajatoa taarifa rasmi, kwa nini hajatoa wakati sheria inamtaka afanye hivyo achilia mbali yuko ndani ya serikali ambayo imelifanya tatizo la rushwa kama ni kipaumbele cha kwanza katika kuwatumikia Watanzania?

Makonda hafahamu kuwa kukaa kimya bila kutoa taarifa kwenye vyombo husika kunamfanya avunje sheria kama ilivyoainishwa kwenye Penal Code CAP 16 Chapter V na pia sheria ya kupambana na rushwa ambayo imeaninishwa katika kifungu cha 30 kinachosema;
30. Any person who aids or abets another person in commission of an offence under this Act commits an offence and shall be liable on conviction to a fine not exceeding two million shillings or to imprisonment for a term not exceeding two years or to both.

Makonda hafamu kuwa sheria hazina siasa pamoja na kwamba siasa wakati mwingine hazina sheria?

Makonda kama Mkuu wa Mkoa anatakiwa awe mfano kwa wananchi wake katika kuwafichua wavunja sheria lakini anachokifanya kwa sasa ni kuwaficha wavunja sheria huku akicheza mchezo wa kisiasa.

Makonda timiza wajibu wako wa kuwafichua wahalifu kama Raia na Mkuu wa Mkoa lakini pia unatakiwa ufahamu ukubwa na umuhimu wa madaraka uliyopewa katika kuwatumikia wananchi.

Makonda naomba uwataje waliotaka kukupa rushwa ya milioni 50 ili watanzania wawafahamu kwa sababu wana haki kikatiba kuwafahamu.

Mama Diamond Afunguka Kuhusu Nyumba ya Madale..Adai ni yake Kama ni Kuhama Ahame Diamond na Zari

Nasemaje bim'danga Mama Chibu Ndo kishasema Mjengo wa Madale anaumiliki yeye, na wale waliokua wakimsimanga kuwa awapishe Kina chibu Na Zari kwenye Mjengo washindweeee, bi Maza anasema wataondoka wao Na wajukuu ila yeye wa hapahapa haondoki ng'ooooooo, Hiyo imekuja baada ya kukumbusha kauli ya Diamond kabla hajatoka ya kuwa nyumba ya kwanza kujenga itakuwa zawadi kwa mama..... 

Haya Hapa Matokeo ya Forbes Person of the Year Aliyokuwa Anawania Rais Magufuli

Aliyekuwa Mwendesha Mashtaka wa Serikali na Wakili nchini Afrika Kusini Thuli Madonsela leo ametangazwa kuwa ndiye mshindi  wa Tuzo ya Mtu Mashuhuri Afrika ya Forbes (Person of the Year #POY2016).

Tuzo huyo hupewa mtu aliyetoa mchango mkubwa katika kuiinua jamii kwenye njanja mbalimbali za maisha kama vile uchumi, siasa, utamaduni.

Katika kinyang’anyiro cha tuzo hiyo, Thuli Madonsela alikuwa akichuana na Michiel Le Roux kutoka Afrika Kusini, Rais wa Mauritania, Ameenah Gurib, Jamii ya watu wa Rwanda na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli.

Mwaka 2015 tuzo hii ilikwenda kwa Mkurugenzi Mtendaji wa makampuni ya MeTL, Mohammed Dewji.

Mimba ya Nisha Bebee Yazua Balaa..Adai Baba Kijacho Wake Hawezi Hata Kujinunulia Sabuni ya Kufulia Boxer

Ujauzito wa Mwigizaji Nisha Bebee umezidi kuzua sinto fahamu kutokana na vichambo anavyopost mtandaoni kwenda kwa Muhusika wa Ujauzito huo..leo tena amepost akimtolea uvivu kama ifuatavyo:
"Watu wanasema nimepewa mimba na kutelekezwa, guyz kuna tofauti kati ya kutelekezwa na kutotaka mtoto wako amjue baba ake.
Since nimeamua kuwa wazi wananipigia kama machizi.. NASEMA HIVI SUBIRINI DNA ZA MACHO naanzaje kumtambulisha mwanangu kwa baba namnunulia hadi sabuni ya kufulia boxer mwanaume mzima unaolewa na demu.. star ushuzi star jina pesa hana mfukoni tena koma kutuma marafiki zangu.. tena moods zangu za sasa hivi sizo nichokonoe nikupost unazopiga vizinga hela za maandalizi ya show xiiew.. I'M DONE" Nisha

Kinara wa Matusi Instagram Akamatwa na Polisi Baada ya Kutoa Matusi Makubwa Kuhusu Perfume Mpya ya Diamond

Kijana mmoja ambaye anatumia jina la Shilolekiuno_official Huko Instagram  hatimae amekamatwa na jeshi la polisi kwa kutukana na kukashifu watu mbali mbali mtandaoni, kijana huyo amekuwa akiandika matusi mazito na kukashifu watu mbalimbali akiwemo Mwanamuziki Diamond,

 Jana Baada ya Diamond Kutangaza Kuleta Perfume mpya zenye jina lake sokoni, mtu huyo anayetumua jina la @shilolekiuno_officail aliingia mtandaoni na kuandika matusi makubwa ambayo siwezi kuyaweka hapa kuhusu Perfume hiyo ya Diamond

Meneja wa Diamond Ameandika Haya:


Lemutuz Naye Ameandika Haya: