Jumanne, 14 Novemba 2017

Idriss Atuma Salamu za Pole kwa Mama Lulu "Mama Ndio Tunahitaji Kukuangalia Zaidi"

Idriss Atuma Salamu za Pole kwa Mama Lulu "Mama Ndio Tunahitaji Kukuangalia Zaidi"MCHEKESHAJI na mshindi wa Big Brother Africa, Idris Sultan, ametoa pole kwa mama wa mwigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’, Lucresia Kalugira, kwa kipindi kigumu alichokianza jana baada ya bintiye kuhukumiwa kifungo cha miaka miwili jela kutokana na kumuua bila kukusudia msanii mwenzake, Steven Kanumba.

Sultan amesema jamii impe faraja na kumtia moyo wakati akiwa katika huzuni ya kuwa mbali na binti yake.  Pia Sultan amemuelezea Lulu kuwa alikuwa ni rafiki yake wa karibu na ni mwanamke shupavu ambaye huzuni yake ikiwa jela itachukua muda mfupi kabla ya kupata marafiki na kujipa moyo wa kuhimili maisha hayo mapya ya miaka miwili.
Hayo ni maneno aliyoyatuma kwenye akaunti yake ya Instagram kama yafuatavyo:
My last piece on this, Mama Lulu tunakuombea kwa Allah upate nguvu ya kukubaliana na hii hali ambayo ni chungu kwetu sote. Tunalazimika kukubali kwasababu Mungu tu ndiye anajua kubaki na jambo kama hili moyoni kwa mda mrefu hivi linaondoaje amani. Binafsi nampenda sana Lulu na anajua, kwa mda wa miaka michache niliyojuana na Liz najua wewe mama ndio tunahitaji kukuangalia zaidi maana Lulu najua atalia wiki ya kwanza na ya pili, ya tatu atapata kazi jikoni, ya nne anajisomea, ya tano kashapata marafiki kote because your daughter is the strongest woman I have ever met maishani mwangu yani ningekua mwanamke ningekua yeye. Baby is good to go na nitajaribu kuwa positive na kusema kua ntammiss sana ila mara mbili tatu sitoacha kumtembelea na tunasubiri siku anatoka na ku-take over her throne. Hakuna aliyependa haya yatokee ila ndio yametokea we only have God and each other now. Be blessed
                              

Related Posts:

  • NI KIVUMBI LIGI YA MABINGWA ULAYA   Katika michuano ya Klabu Bingwa barani Ulaya leo kuna kivumbi kingine ambapo CSKA Moscow itakuwa na kibarua kigumu pale watakapowakaribisha Bayern Munich. Wakati huo huo Man City waliopigwa bao moja na Bayer… Read More
  • Omar Gonzalez White HouseMlango huo unavyoonekana  Taarifa kutoka mjini Washngton zinaeleza kua mwanamume mmoja aliyekua ameshikilia kisu mikononi mwake aliruka uzio wa makao ya Rais wa Marekani Brack Obama na kukimbia kuelekea kwenye makazi… Read More
  • Taarifa kuhusu kifo cha msanii wa bongofleva Side Boy Mnyamwezi. Ingawa Nafasi yake katika muziki wa Bongo Fleva ilikuwa ikipanda taratibu kulingana na aina ya muziki aliokuwa akiumba,single iliyomtambulisha zaidi kwenye muziki wa Bongo Fleva inaitwa Kua uone ambayo alimshirikisha A… Read More
  • Waaga mchuano baada ya kuagizwa kuvua hijab Timu ya wanawake ya Qatar ya mchezo wa mpira wa kikapu imejiondoa kutoka mashindo ya bara Asia. Timu ya wanawake ya Qatar ya mchezo wa mpira wa vikapu imejiondoa kutoka mashindo ya bara Asia yanayofanyika huko Korea Kus… Read More
  • Van Gaal:tuna mlinzi wa kati mmoja tu  Kocha wa Manchester United Louis Van Gaal. Kocha wa machester United, Louis van Gaal amesema Manchester united ina mlinzi wa kati mmoja tu mwenye uzoefu wakati huu kikosi hicho kinapotarajia kukipiga na west ham kat… Read More

0 comments:

Chapisha Maoni