Jumapili, 30 Novemba 2014

FIFA:Madai mapya ya ufisadi yazuka

 
Rais wa FIFA Sepp Blatter akimkabidhi rais wa Urusi Vladmir Putin Haki za kuandaa dimba la dunia la mwaka 2018 


Madai zaidi yameibuka kuhusu ufisadi uliofanyika wakati wa shughuli ya kuwatafuta waandalizi wa kombe la dunia la mwaka 2018 na 2022.
Nafasi hizo zilichukuliwa na Urusi pamoja na Qatar. Gazeti la Sunday Times nchini Uingereza limesema kuwa rais wa Urusi Vladimir Putin alihusika pakubwa wakati nchi yake ilipokuwa ikitafuta nafasi hiyo na hata alimuomba rais wa FIFA Sepp Blattter kuisaidia kupata kura.
   
Rais wa FIFA Sepp Blatter akiikabidhi Qatar mkataba wa kuandaa kombe la dunia la mwaka 2022

Pia kuna madai kuwa nchi ya Qatar ilitumia ushawishi wake katika sekta ya gesi kupata kura kupitia kandarasi za kibiashara.
Urusi na Qatar zimekana kuhusika kwenye vitendo hivyo na ziliondolewa lawama na shirikisho la soka duniani FIFA hivi majuzi.

Man U na Arsenal zawika,Chelsea yazuiwa

           Mchezaji wa chelsea Wiilian akikabiliana na mwenzake wa Sunderland 

Mkufunzi Gus Poyet aliihangaisha timu ya Chelsea na kuwajaribu viongozi hao wa Ligi kupitia mchezo mzuru wa timu yake Sunderland.
Chelsea ilishindwa kuliona lango la Sunderland kupitia ngome mahsusi ya Sunderland iliowazuia washambuliaji wake.
Shambulizi kali ambalo nusra liiweke Chelsea kifua Mbele ni lile lakKiungo wa kati Willian ambalo liligonga chuma cha goli na kutoka nje.
Hatahivyo Mshambuliaji wa Sunderland pia naye alipiga mkwaju mkali uliogonga chuma cha goli la Chelsea huku Sunderland ikidhibiti safu ya kati na kuimarisha mashambulizi yake katika ngome ya Chelsea.
 
Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger afurahi baada ya timu yake kuichapa West Brom 1-0 
Mchezo huo ulikamilika na sare ya bila kwa bila na kuifanya Sunderland kuwa timu ya kwanza kuwazuia viongozi hao wa Ligi kufunga tangu msimu huu uanze.
Katika matokeo mengine Arsenal ilizuia kupoteza kwa mara ya tatu mafululizo pale walipoishinda West Brom ugenini.
The Gunners kama wanavyojulikana walianza mechi hiyo wakiwa na alama za chini zaidi baada ya kucheza mechi 12 katika kipindi cha miaka 32,lakini cichwa kizito cha mshambuliaji Danny Welbeck, kilihakikisha vijana wa Arsene Wenger wanatia kibindoni alama tatu.
        Wayne Rooney afurahia baada ya kufunga bao la pili dhidi ya timu ya Hull City 
Katika uwanja wa Old Trafford,bao la Robbin Van Persie Robin liliimarisha ushindi wa Manchester United dhidi ya Hull City na kuzima midomo ya wale waliokuwa wakijiuliza maswali mengi kuhusu hali ya mchezaji huyo msimu huu.
Miongoni mwa wakaosoaji wake ni kocha Louis Van Gaal ambaye aliyemuorodhesha mshambuliaji huyo katika mechi hiyo licha ya kudai kwamba alikuwa na mchezo m'baya wakati wa mechi kati ya Arsenal na Manchester wikendi iliopita.
Manchester United ilipata ushindi wa mabao 3-0 kupitia wachezaji wake Chris Smalling na nahodha Wayne Rooney.
katika matokeo mengine
Burnley 1 - 1 Aston Villa
Liverpool 1 - 0 Stoke
QPR 3 - 2 Leicester
Swansea 1 - 1 Crystal Palace
West Ham 1 - 0 Newcastle

ESCROW:Spika adaiwa kuwalinda washukiwa

 
                     Spika wa bunge la Tanzania Anne Makinda 
Speaker wa Tanzania Anne Makinda ameshtumiwa kwa kujaribu kuwatetea wale wanaodaiwa kuhusika katika kashfa ya ufisadi ya Escrow.
Kulingana na wachambuzi,wasomi na wataalam wa sheria hatua yake ya kujenga mazingira ya kuwapendelea washukiwa huenda ikasaidia kuwalinda watu hao.
Wakili maarufu mjini Daresalaam Sylvanus Sylivand ameliambia gazeti la the Citizen kwamba spika makinda alitarajiwa kufuata mfano mzuri uliowekwa na wenzake katika kashfa za awali ambapo bunge lina uwezo wa kuwashinikiza mawaziri na waziri mkuu kujiuzulu.
Ni wazi kwamba bunge linaweza kuishauri serikali kuwachukulia hatua viongozi wanaoshukiwa lakini si lazima kwamba rais afuate agizo hilo.
Kulingana na Sylivand,ni wazi kwamba kuna kitu kinachofichwa ili kuendesha ajenda tofauti ambayo itasadia aibu iliopata serikali.
  
                                           Bunge la Tanzania 


Muhadhiri wa chuo kikuu cha Dodoma Paul Loisulie amesema kuwa bunge sharti lichukue hatua kama taasisi.
''Kile ambacho kimetokea bungeni kuna uwezekano mkubwa kitaligawanya bunge na wananchi.''.
Inaonekana kwamba baadhi ya wabunge wa CCM wanajaribu wawezalo kuwatetea viongozi wanaoshukiwa bila kujali maslahi ya raia walio masikini.
Julius Mtatiro wa Chama cha Civic Front amesema kuwa CCM inataka kuwalinda viongozi wake wakuu ili raia wasielewe kuhusu kilichotokea baada ya Spika Makinda kuwataka baadhi ya washukiwa hao kupendekeza hatua ambazo zingefaa kuchukuliwa dhidi yao.
Kulingana na Profesa Kitila wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam Wabunge wana uwezo wa kuwaweka katika mizani watu watatu pekee ,rais,waziri mkuu na Spika na kile kilichokuwa kikendelea bungeni ni fursa ya wananchi kufikiria sana kabla ya kuipitisha katiba mpya.

Walichokisema Wabunge Kafulila, Peter Msigwa, Aeshi Hilary na Maige kuhusu maamuzi ya Bunge jana

news0
Kikao cha Bunge la Tanzania kilichoahirishwa siku ya jana Novemba 29 ni moja ya vikao ambavyo vilivuta hisia za watu wengi na kutengeneza historia nyingine mpya kutokana na mjadala wa ishu ya Escrow, baada ya kikao hicho kuahirishwa Wabunge Ezekiel Maige, Aeshi Hilary, David Kafulila na Mchungaji Peter Msigwa walizungumzia kuhusu maamuzi ya Bunge hilo.
…Tumekuwa na Bunge la kipekee sana katika muda wangu wa kuwa Mbunge karibu miaka nane sasa, hii ni experience yangu ya kwanza kuwa na kipindi kigumu kama hiki. Bunge limekuwa kwenye mtihani wa ama kuamua kulinda viwango vyake vya utendaji wa miaka yote au kuamua kuwa na viwango tofauti…” —Ezekiel Maige.
… Niwaombe Watanzania wawe wavumilivu kila kitu kina wakati wake na muda wake… Nilipongeze Bunge, nipongeze kamati ya usuluhishi vilevile nimpongeze Waziri Mkuu kwa kukubaliana na haya, ninaamini Serikali itachukua hatua zake…”– Aeshi Hilary.
…Niliamini siku zote kwamba kuna makosa yamefanyika katika utoaji wa fedha zile na chunguzi za CAG, PCCB, na hatimaye kamati ya PAC zimeonyesha hivyo na hatimaye Bunge limeweza kuchukua hatua hii. Kuna changamoto nyingi katika kupambana na mambo kama haya, kuna vitisho, kudhalilishwa mimi niliitwa ‘tumbili’ na kuna watu walitishia kuniua, lakini yote kwa ujumla wake ni changamoto katika kupambania yale ninayoamini…” –David Kafulila.
… Tumetimiza wajibu wetu kuishauri Serikali, tumeona watu wengine hawakutimiza wajibu wao… Upande wetu wa upinzani tuling’ang’ania kwamba watu wawajibike, niwasihi wananchi tuendelee kushirikiana kwa sababu mwisho wa siku hii ni nyumba ya kwetu sote mtu yeyote asiyetimiza wajibu wake lazima abebe mzigo wake …”—Mchungaji Peter Msigwa.

Maneno 6 ya Davido baada ya ushindi wa Diamond Platnumz Channel O 2014.

Davido 12 
Ushindi wa tuzo tatu za Channel O 2014 alizochukua Mtanzania Diamond Platnumz umekua mkubwa sio tu kwa Tanzania bali Afrika na kona zake ambapo miongoni mwa walioandika baada ya Diamond kushinda ni Davido.
Msanii huyu wa Nigeria ambae alifanya remix ya number one ya Diamond aliandika kwenye page yake ya instagram >>> TANZANIA STAND UP! HE DID IT na kisha akammention Diamond Platnumz.
Kwenye post hii ya Davido ambae hakupata tuzo yoyote ya Channel O japo alikua anawania, imepata likes zaidi ya elfu kumi na nne kutoka kwa followers wake ambao ni zaidi ya laki nne huku comments zikiwa ni zaidi ya mia saba.
Davido on Diamond
Davido 13

Jumamosi, 29 Novemba 2014

DIAMOND PLATNUMZ ANYAKUA TUZO 3 ZA CH0AMA14

 
Tar 29 Noember ni siku ambayo imewekwa historia kwenye tasnia ya muziki wa bongo fleva baada ya Diamond Platnumz kuchukua tuzo tatu za chanel O, pia ni historia kwa Afrika nzima.
Diamond alikua ametajwa kwenye vipengele vinne. Vipengele hiyo ni pamoja na Most Gifted East Video, Most Gifted Afro Pop video na Most Gifted Newcomer.
Kwenye tuzo hizo Diamond amefanikiwa kuwapiku wasanii nguli wa Afrika  wakiwemo Iyanya, Daido, Flavor, Mafikizolo na Sauti Sol.

 "TANZANIA STAND UP! HE DID IT! @ diamondplatnumz", amepost Davido



Ifahamu idadi ya majeraha kwa Manchester United.

2397624900000578-2854114-image-12_1417275965806
Unapozungumzia suala la majeraha ya wachezaji bila shaka mashabiki wa Manchester United wanapata homa ya ghafla .
Hii ni kwa sababu timu hii imekuwa na orodha isiyoisha ya wachezaji wenye majeraha .
Mbaya zaidi ni kwamba kila orodha hii inapoonyesha dalila za kungua mchezaji mwingine anaemia na inazidi kuwa ndefu .
239764A900000578-0-image-5_1417275401405
Orodha hii iliongezeka kwenye mchezo dhidi ya Hull City wakati ambapo kiungo mshambuliaji Angel Di Maria alipoumia misuli ya nyonga kwenye dakika ya 14 ya mchezo na kulazimika kutoka.
Bado haijafahamika Di Maria atakaa nje ya uwanja kwa muda gani lakini kwa kawaida jeraha kama hili huhitaji kati ya siku 7 mpaka 10 ili kupona na wakati mwingine kuendana na ukubwa wake linaweza kuhitaji muda mrefu zaidi .
2397647A00000578-2854114-image-11_1417275874223
Kwa jumla Jeraha la Di Maria ni jeraha la 41 kwa mchezaji wa Manchester United kwa msimu huu tangu kuanza kazi kwa kocha Mholanzi Louis Van Gaal .
Idadi hii ndio idadi kubwa ya majeraha kwa wachezaji kwa timu yoyote ya ligi kuu ya England msimu huu hali inayowafanya United waamini kuwa huenda timu yao ina mkosi wa aina Fulani.
239745C000000578-2854114-image-21_1417276088569     

Haya hapa majina yaliyoteuliwa na PAC kuandika maazimio ya kuwawajibisha watuhumiwa wa Escrow

PAC 
Baada ya Spika wa Bunge kuahirisha Bunge mara mbili siku ya leo Novemba 29 ili kuipa nafasi kamati ya PAC iweze kufanya marekebisho ya maneno yaliyoandikwa kwenye maazimio yaliyowasilishwa na Kamati ya PAC, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Zitto Kabwe ametaja majina ya walioteuliwa na Kamati hiyo kuandika maazimio ya kuwajibisha watuhumiwa wa Tegeta Escrow.
Kupitia ukurasa wake wa Facebook (@Zitto Kabwe) ameandika majina ya wajumbe hao.
Zitto Leo

Kilichosemwa na Kamanda Kova na Waziri Lazaro Nyalandu kuhusu ajali ya Helikopta

Name:  jf2.jpg
Views: 0
Size:  163.2 KB

Taarifa ambayo imeripotiwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari ni kuhusu watu wanne kufariki kutokana na ajali ya Helikopta inayomilikiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii, yenye namba 5HTWA kuanguka katika eneo la Kipunguni B, Ukonga Dar es salaam.
Akizungumza na kituo cha ITV Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Suleiman Kova amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuahidi kutoa taarifa kamili juu ya tukio hilo muda mfupi ujao.
 Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Waziri wa Maliasili na Utalii  ameandika hivi; “Naelekea Dar kutokea Dodoma kwenda kwenye eneo la tukio la ajali ili kuwapa pole wafiwa. Nitazidi kuwafahamisha.”
Name:  jf.jpg
Views: 0
Size:  178.8 KB                      Muonekano wa Helikopta eneo la tukio

Hiki ndicho alichokiongea yule Msichana aliyempiga Mtoto Uganda.

baby021
Baada ya story ya yule msichana kwa anayefanya kazi za ndani Uganda kuchukua headlines katika vyombo mbalimbali vya Kimataifa Duniani, leo kipo ambacho amekizungumza kwa mara ya kwanza tangu afanye kosa hilo.
Msichana huyo Jolly Tumuhiirwe ambaye kwa sasa amekamatwa na Polisi amesema sababu iliyomfanya amtese mtoto Arnella Kamanzi, ni kutokana na kuchanganyikiwa baada ya waajiri wake kutompatia pesa ili amtumie baba yake ambaye alikuwa anaumwa.
Amesema anajiona mwenye hatia kwa alichokifanya japo anadhani alifanya hivyo kama njia ya kumkanya mtoto huyo kwa kuwa alikuwa akimuona mama wa mtoto huyo akimpiga kama njia ya kumkanya.
Jolly amelalamika kuwa anajisikia vibaya pale ambapo wafungwa wenzake wamekuwa wakimtenga sana na kutaka kumpiga.

Alhamisi, 27 Novemba 2014

Mnigeria mwingine kwenye hatia ya kusafirisha dawa za kulevya

Man-looks-out-of-prison-w-010 
Idadi ya raia wa Nigeria wanaokamatwa na dawa za kulevya inazidi kupanda siku hadi siku, ambapo taarifa iliyopo ni kwamba mtu mmoja mwenye umri wa miaka 35 amehukumiwa kunyongwa baada ya kukutwa na hatia ya kusafirisha dawa za kulevya.
Jamaa huyo Abuchi Ngwoke alikamatwa mwaka 2012 uwanja wa ndege wa Malaysia baada ya kukamatwa na dawa hizo zenye uzito wa gramu 251.66 aina ya Methamphetamine  ambazo alikuwa akisafirisha kutoka Nigeria kwenda Malaysia.
Ni mara nyingi tumekuwa tukisikia kuhusu watu wanaokamatwa kwa kusafirisha dawa hizo huku wengi wao wakitajwa kuwa ni Wanigeria.
Abuchi-Ngwoke

Baada ya ishu ya Escrow, haya ni majibu mawili ya Waziri Mkuu Pinda ikiwemo kujiuzulu

question_mark_20166
Kikao cha Bunge leo Novemba 27 kimeanza kwa maswali mawili kuulizwa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Freeman Mbowe kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

…Chini ya uongozi wako kama Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ukiwa kiongozi wa shughuli za Kiserikali Bungen, tumeiona Serikali ikikumbana na matatizo na vikwazo vingi ikiwemo ‘Operesheni Tokomeza’ ambayo ilipelekea wananchi wengi kupoteza maisha na wengine kupata vilema…“– Mbowe.
Tumeona mauaji ya raia yakiendelea Kiteto, kashfa kubwa ambayo iko current sasa hivi ikiwa ni pamoja na kauli zako ulizowahi kuzisema kwamba fedha zilizopotea za akaunti ya Escrow hazikuwa fedha za umma bali zilikuwa fedha za watu binafsi…“– Mbowe.
Baada ya Ripoti ya CAG kutolewa hadharani kuhusiana na fedha za Escrow na baada ya Ripoti ya PCCB kutolewa na hatimaye jana hapa Bungeni kusomwa taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, nini msimamo wako kuhusu kauli yako ya awali kwamba fedha zile zilikuwa ni za watu binafsi na sio fedha za umma?Mbowe.
Kwa uzito huo ukichanganya na matukio mengine mbalimbali ambayo yamepelekea fedheha kubwa kwa taifa letu, huoni kama ingekuwa muafaka kwako binafsi na taifa kupumzika kidogo ili kupisha nafasi kwa watu wengine kuweza kumalizia ngwe hii ya utawala wenu?”– Mbowe.
Akijibu maswali hayo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema; “…Inawezekana Mheshimiwa Mbowe una shauku ya kutaka litokee hilo lakini mambo haya yanategemea kama ndivyo Mungu kapanga au hapana…
Ningeweza nikajaribu kukujibu lakini sina sababu ya kufanya hivyo, sina sababu ya kufanya hivyo kwa sababu suala lenyewe ndiyo subject ya mjadala hapa Bungeni ambao unaanza leo.. Tusubiri mjadala utakavyokwenda naamini na mimi nitapata nafasi ya kusema mawili matatu, kwa hiyo nadhani mwisho wa yote Bunge litakuwa limefikia mahali ambapo tunaweza tukasema kwa uhakika ni hatua stahiki namna gani inaweza kuchukuliwa…” Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Baada ya majibu hayo, Mbowe alipata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwa Waziri Mkuu; “…Pamoja na kwamba jambo hili litajitokeza baadaye katika mijadala ya leo, bado haiondoi ukweli kwamba una wajibu wa kulijibu swali langu. Naomba kwa heshima sana nikuulize tena kwa mara nyingine, taifa limepata fedheha kubwa sana kutokana na sakata hili, nchi nzima inasikiliza tatizo hili…“– Mbowe.
…Una heshima kama kiongozi wa Serikali lakini heshima ambayo itakuwa imethibitishwa zaidi kama utaamua kujiwajibisha mwenyewe ili kuweka heshima yako na heshima ya Serikali, je kwa mara nyingine huoni ingekuwa vema kama basi utujibu kama unafikiri bado zile fedha ni za umma kama hutaki ku-declare kujiuzulu katika hatua ya sasa?”– Mbowe.
Akijibu swali hilo, Waziri Mkuu amesema; “…Naomba nirudie nilichosema, suala la kujiuzulu si jipya lakini maadam jambo hili liko hapa Bungeni, unatanguliza hili jambo kwanini? Tungoje tujadili tufikie mwisho halafu tutaamua…”– Mizengo Pinda.
Nimekurekodia sauti ya wakati maswali hayo yakiulizwa na kujibiwa Bungeni leo Dodoma, unaweza kusikiliza kwa kubonyeza play.

Picha ya kwanza ya mbrazil mpya wa Yanga mazoezini, je atafuzu majaribio

kelvingoalWiki iliyopita nilikuletea taarifa juu ya ujio wa mchezaji mpya wa kimataifa wa klabu ya Yanga Emerson de Oliveira Neves Roque  – mbrazil ambaye ameletwa nchini kuja kufanya majaribio na endapo ikifuzu basi ndio itachukua nafasi ya mbrazil aliyeondoka Jaja.
Jana jioni mchezaji huyo huyo aliwasili na leo hii mchezaji huyo ameanza mazoezi mepesi asubuhi katika Uwanja wa shule ya Sekondari Loyola kufuatia kusaifri kwa zaidi ya masaa 11 kutoka jijini Rio de Janeiro.
emrsn
Kiungo mbarazil Emerson de Oliveira a(wa pili kutoka kulia) akiwa mazoezini leo asubuhi katika uwnaja wa shule ya sekondari Loyola, wengine ni Kizza, Javu na Coutinho
Emerson ameungana na wachezaji wengine wa Young Africans katika mazoezi ya leo asubuhi ikiwa ni siku yake ya kwanza katika ardhi ya Tanzania na kufanya mazoezi mepesi mepesi chini ya kocha msaidizi Leonardo Neiva kuijiweka fit na kutoa uchovu safari.
Kiungo huyo mwenye umbo lililonyumbulika ambae alikuwa akichezea timu ya Bonsucesso FC iliyopo lii daraja la pili nchini Brazi katika jiji la Rio de Janeiro pia msimu uliopita alikua akicheza soka la kulipwa katika nchi ya Poland latika klabu ya Piotrkow Trybunalski FC.
Kocha mkuu wa Young Africans Marcio Maximo amesema mchezaji huyo leo alikua na programu ya mazoezi mepesi tu kutokana na uchovu wa safari na kesho anatarajiwa kuendelea na mazoezi na wenzake kulingana na ratiba iliyopo.
Endapo Emerson atafanikiwa kulishawishi benchi la Ufundi kumsajili  basi moja kwa moja ataingia makubaliano na klabu ya Young Africans kwa ajili ya kuitumikia kwenye michuano ya kimataifa na Ligi Kuu ya Vodacom Tanznaia bara.

Picha: Diamond Platnumz na Fally Ipupa kwa mara nyingine tena kwenye Mjengo wa BBA

.
Hii ni mara ya pili kwa msanii Diamond Platnumz kualikwa ndani ya jumba la BBA akiwa na mwanamuziki kutoka Congo, Fally Ipupa ambapo wameshiriki chakula cha mchana pamoja na washiriki waliobaki kwenye Jumba hilo, safari hii wasanii hao wameingia kwa ajili ya kuhamasisha ONE Campain ambayo inahusu kilimo, moja ya Project zilizowahi kufanywa na Kampeni hiyo ni ile nyimbo ya Cocoa na Chocolate ambayo wameshiriki pia mastaa wengine kibao kutoka Afrika.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

NI MWINGINE TOKA KIGOMA,DIAMOND NA KIBA MJIPANGE KIJANA AMEKUJA NA SPIDI KALI

Ni msanii mwingine hatari ambae anachipukia kwenye game Mkasulu Junior huku akisindikizwa ngoma yake kali inayokwenda kwa jina la tulichart ambayo amefanya kwa producer makini MARO.Hofu yangu mi kuwapoteza hawa wakongwe ambao ametoka nao mkoa mmoja,mkoa ambao unatamba katika game ya muziki Tanzania si mwingine nazungumzia Kigoma.Tumpokee kwa mikono miwili wapenzi wa bongo fleva ili alete ushindani ndani ya sanaa ya muziki Tanzania.
Download ngoma yake hapo chini au kwenye link Mkasulu - tulichart ili upate kuisikiliza.
http://www.hulkshare.com/youngluvega/unknown-artist-unknown-album-01-01-track-01-01

Jumapili, 23 Novemba 2014

Rekodi aliyoivunja Diamond Platnumz na kuiacha ya P Square

.
.
Tumeshazoea kuona baadhi ya mastaa wa Afrika wanapoweka video zao kwenye youtube wanapata views nyingi ndani ya siku chache lakini Good news time hii imeangukia kwa mkali wa Tanzania.
Mmiliki wa hit single ya ‘Mdogo Mdogo’ Diamond Platnumz ameipiku video ya wakali wa Nigeria P Square baada ya kupata views nyingi ndani ya siku nne.
Video ya P Square  ‘Shekini’  iliyowekwa youtube Nov 17 ina views 286,165 huku Diamond ambaye  video yake ‘Nitampata Wapi’ iliyoweka Nov 20 ina views 354,910.

Ijumaa, 21 Novemba 2014

Kipa wa Chelsea yuko sokoni.

Chelsea+v+Southampton+Premier+League+aQgqk_Wv1pBx
Klabu za Arsenal , Liverpool na Real Madrid ziko kwenye vita kali ya kuwania kumsajili kipa wa Chelsea Petr Cech .
Chelsea inaalzimika kumuuza kipa huyo kwa kuwa hana nafasi ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza baada ya kurudi kwa kipa Mbelgiji Thibaut Courtois .
Hadi sasa Chelsea haijapoteza mchezo wowote msimu huu huku Thibaut akicheza kwenye mechi karibu zote hali inayomfanya Cech kulazimika kutafuta mahali kwingine ambako atakuwa chaguo la kwanza .
Cech ameidakika Chelsea kwa mafanikio makubwa kwa muda wa miaka 11 tangu aliposajiliwa kwa mara ya kwanza akitokea Rennes ya Ufaransa .
Cech analazimika kuondoka baada ya kupokonywa nafasi kwneye kikosi cha kwanza.
Cech analazimika kuondoka baada ya kupokonywa nafasi kwneye kikosi cha kwanza.
Katika kipindi hicho Cech amefanikiwa kutwaa mataji kadhaa yakiwemo matatu ya ligi kuu ya England , UEFA Champions league na UEFA Europa League bila kusahau kombe la Fa na kombe la Carling ambalo siku hizi hufahamika kama Capitol One Cup.
Akijibu maswali ya waandishi wa habari kocha wa Chelsea Jose Mourinho alikanusha taarifa kuhusu Cech kuwa mbioni kuhama ambapo alisema kuwa hajawahi kupata taarifa yoyote kama hiyo .
Thibaut Courtois ndio kipa namba moja kwenye ikosi cha Chelsea.
Thibaut Courtois ndio kipa namba moja kwenye ikosi cha Chelsea.
Kwa upande mwingine wakala wa Cech Viktor Kolar ameendelea kushikilia msimamo ulioripotiwa na vyombo vya habari kuwa kuna klabu zisizopungua tano ambazo zimeonyesha nia ya kumsajili kipa huyo .
Hadi sasa inafahamika kuwa Arsenal ndio iko kwenye nafasi ya juu kumsajili Cech kwa thamani ya puandi milioni 7 lakini kumekuwa na ishara toka kwa klabu za Ac Milan , As Roma , Real Madrid na Liverpool za kutaka kumsajili Cech .

Ni Diamond Platnumz kwenye XXL leo Novemba 21, isikilize hapa full interview…

e0a8228fb8L 
Kupitia youngluvega.blogspot.com siku ya juzi ulipata taarifa kuhusu msanii wa Bongo Fleva Diamond Platnumz kuachia nyimbo yake mpya ambapo kwa mara ya kwanza ilionyeshwa kupitia kituo cha MTV, na jana ikawa siku rasmi ambayo Diamond aliachia nyimbo hiyo.
Leo Novemba 21, Diamond amesikika kwenye show ya XXL ambapo amezungumzia mambo mengi, baadhi ya yale aliyoyazungumzia ni pamoja na story zilizoenea mitandaoni kwamba mahusiano ya msanii huyo na Wema yameisha pamoja na story ambayo imetokana na kuenea kwa picha mitandaoni za msanii huyo na Zari the Boss Lady kutoka Uganda.
Hii ni sehemu ya mahojiano aliyofanya Diamond kwenye XXL:
Adam Mchomvu :”…Nataka kujua ile vibe ya Fiesta that day, story zilikuja ooh Diamond kazomewa.. kazomewa kazomewa..na vitu kama vile, sijapata chance ya kukusikia wewe una kipi cha kuzungumzia kuhusiana na that situation..?
Diamond :- “… Siku zile kwangu ilikuwa kama mchezo, unajua muziki ushakuwa kama sio fani tena, ushakuwa kama siasa.. So, lazima uichukulie hivyo wewe mwenyewe kama msanii ujue una control vipi kwa sababu sio mara ya kwanza vitu kama hivyo vishatokea Maisha.. Maisha yalitupwa mpaka na mayai viza kabisa.. Ni vitu ambavyo vikitokea naonaga kama ni kawaida…
B 12  :-“…Kwa hiyo ukweli uko wapi kati yako wewe na Wema Sepetu?...”
Diamond  :- “…Kuna vitu vitu fulani nadhani kuvizungumza sio vizuri… Lakini ikifikia kuvizungumzia vinazungumziwa… Uzuri wa mahusiano yetu ni kwamba kila mtu anafahamu… Haijafikia kuweka wazi ndio maana ninapoulizwa inakuwa ni swali gumu kulijibu..
B 12 :- “.. Ni gumu kwa upande wako lakini yeye yuko tayari kuzungumza kwamba it’s over kati yangu mi’ na Diamond…
Diamond  :- “… Sijui…
B 12  :- “...Hii ngoma kama umemzungumzia yeye direct hivi… watu wamekuza akili zao zikaenda mbali zaidi kimawazo lakini, kwamba inawezekana ile singo umemwimbia yeye hivi kwamba bado unamzimia japokuwa bado kama kakutosa hivi…
Diamond  : “.. Waswahili wanasema ‘A’ na ‘B’ yote majibu, halafu ukisikiliza ile nyimbo kama kweli mtu mwenye ufahamu wako, kweli kabisa hauwezi kuwa na maswali mengi …
Kuhusiana na mahusiano yake na Zari the Boss Lady, Diamond amejibu hivi:
Diamond  :- “.. Zari ni rafiki yangu tu, alipokuja hapa mimi ndio nilikuwa mwenyeji wake Tanzania na kama mimi ndiyo mwenyeji sikutaka kuleta roho za kibaguzi, unajua hata alipokuja Davido pia ilibidi awe na mimi karibu ili hata kesho na kesho kutwa  mimi nikiwa Nigeria basi Davido anipokee hivyo hivyo…
Iko hapa full Interview ya Diamond kwenye XXL, unaweza kuisikiliza kwa kubonyeza play.

Alhamisi, 20 Novemba 2014

Louis van Gaal kayatoa ya moyoni…. anataka nani ashinde Ballon d’Or 2014? Ronaldo na Messi ?

Screen Shot 2014-11-20 at 3.53.45 AM 
Wanaowania tuzo ya Ballon d’Or 2014 walishatangazwa ambapo list hiyo pia inawahusisha mastaa wa soka kama Cristiano Ronaldo na Lionel Messi, huku list hiyo ikiwa pia na wachezaji wa Ujerumani iliyoshinda kombe la dunia mwaka 2014 nchini Brazil.
Baada ya ushindi wa Ronaldo na Messi kuchukua headlines sana kocha wa Manchester United Louis van Gaal (63) ameamua kuyatoa ya moyoni na kusema mwaka huu Ronaldo na Messi hawatakiwi kuchukua hiyo tuzo bali ni halali ikachukuliwa na mchezaji wa Ujerumani.
Wajerumani wanaowania tuzo hiyo ni Mario Gotze, Toni Kroos, Philipp Lahm, Thomas Muller, Manuel Neuer na Bastian Schweinsteiger.
Screen Shot 2014-11-20 at 4.04.25 AM 
Anasema ‘Naamini Ujerumani inafaa kuchukua hii tuzo, mara nyingi imekua tu ni wachezaji maarufu/wanaofahamika ndio wanashinda hii tuzo, kitu kikubwa kushinda ni kombe la dunia ndio maana naamini itachukuliwa na mchezaji wa Ujerumani sababu kiukweli wanastahili
Screen Shot 2014-11-20 at 3.50.45 AM 
Umeonaje mawazo ya Van Gaal? ungependa nani ashinde Ballon d’Or ya 2014 mtu wangu? naomba niachie maoni yako kwenye comment hapa chini.

Baada ya kuandikwa amemuomba Diamond collabo, Jose Chameleone ametoa haya majibu

Screen Shot 2014-11-20 at 4.14.24 AM 
Ni stori nyingi tunakutana nazo kwenye vyombo vya habari kila tunapoamka na mara nyingi tunaamka nazo kwenye mitandao ya kijamii moja wapo ikiwa hii ya mwimbaji wa Uganda Jose Chameleone kudaiwa kumuomba Diamond wafanye collabo.
Kwenye interview na Mambo Mseto ya Radio Citizen November 19 2014 Chameleone amekanusha hizo taarifa kwa kusema ‘kitu ambacho nitakwambia kabla ya kusema chochote, mimi naheshimu wasanii wote mashariki na duniani na nataka niwakumbushe kitu kingine, nimekaa kwenye muziki kwa miaka kumi na nne… mimi sio msanii mchanga’
Diamond 2 
‘Ilikua ni uongo sijui umetokea wapi eti mimi nimemuomba collabo, Yes…. tunaweza kufanya collabo lakini mimi sijamuomba collabo, wamesema mimi nimezungumza na Diamond kwenye whatsapp… yes tumezungumza lakini ilikua ni kirafiki wala hatujaongea maneno ya kimuziki’ – Jose
‘Mimi ni msanii mkubwa, sio msanii mchanga… naheshimu kila msanii kuanzia mchanga mpaka mkubwa na vilevile mimi pia ni msanii mkubwa na siwezi kuomba collabo kama hivyo, nimeshangazwa sana’

Kauli ya Raisi wa Simba kuhusu usajili wa Mnigeria Emeh Izechukwu

IMG_8912.JPG
Siku chache baada ya dirisha la usajili kufunguliwa kumekuwepo na tetesi za usajili kumhusu mshambuliaji wa kinigeria Emeh Izuchukwu kurudi Msimbazi.
Lakini Rais wa Simba SC, Evans Elieza Aveva amesema kwamba hawana nafasi ya kusajili ya mshambuliaji wa kigeni na kwamba Emmanuel Okwi, Amisi Tambwe na Paul Kiongera wanawatosha.
Kauli hiyo ya Aveva inakuja wakati tayari vyombo vya habari vimekuwa vikiwahusisha washambuliaji Mnigeria, Emeh Izuchukwu na Mganda Danny
Sserunkuma kusajiliwa na Simba.
Aveva amesema kwamba Izuchukwu ambaye ni mchezaji wao wa zamani, ameomba mwenyewe kurejea kuchezea klabu hiyo, lakini anasikitika hawana nafasi ya mchezaji
wa kigeni.
“Hao wachezaji wengine hao, ni magazeti tu yamekuwa yakiandika, lakini ukweli ni kwamba hatujazungumza nao,”amesema Aveva

Kwa wale watumiaji wa mboga za majani Dar, hii imetokea jana kwenye habari

dothao-12190000
Huenda wewe ni mmoja kati ya walaji wa mbogamboga za majani lakini hujui mboga hizi zinalimwa katika mazingira gani… sasa baraza la mazingira Tanzania NEMC limebaini kuwa wakulima wa mboga za majani Dar wamekuwa wakitumia majitaka kumwagilia hizi mboga.
Afisa wa NEMC amezungumza na ITV na kusema; “… Kama Serikali hatuwezi kuruhusu kitu kama hicho.. hatutaruhusu tena kumwagilia kinyesi kwenye mchicha, haturuhusu hicho kitu, hakuna serikali hiyo ambayo itaruhusu vitu hivi…
Kama unataka kuisikiliza taarifa hiyo bonyeza play hapa.