Jumatatu, 1 Desemba 2014

Man city wazidi kupanda

 
              Wachezaji wa Klabu ya Man city 
Kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini amesema ushindi wa timu yake dhidi ya Southampton unadhihirisha kikosi chake ni imara kuweza kukabiliana na Chelsea katika mbio za kuusaka ubingwa wa ligi ya England.
Kwa ushidi wa mabao 3-0 dhidi Southampton siku ya jumapili, Machester city imepanda hadi nafasi ya pili wakiwa na pointi sita nyuma ya vinara Chelsea.
Pellegrin amewamwagia sifa kem kem wachezaji wake kwa kuwa na moyo wa kujituma wakiwa uwanjani hali iliyozaa matunda hayo.

Obama na vurugu za Marekani

                                                             Barack Obama

Rais Barack Obama wa Marekani na baraza lake leo anatarajiwa kuwa na majadiliano kuhusiana na machafuko yanayoendelea katika miji ya Ferguson na Missouri kutokana na kuuawa kwa kijana mweusi na polisi wa kizungu.
Mkutano huo utalenga namna ya kuleta hali ya kuaminiana kati ya polisi na jamii na pia kuangalia vyombo vya kupitia mipango ya serikali kuendeleza hali ya amani.
Meya wa jimbo la Ferguson ametangaza siku ya jumapili polisi Darren Wilson alitangaza kujiuzuru hatalipwa mafao yake kama sehemu ya adhabu kwa kitendo alichokifanya cha mauaji.
Hatua iliyofikiwa ya kupitisha kutomfungulia mamshtaka ndiko kulikoshuka ghasia katika jimbo la Ferguson na katika maeneo mengine ndani ya Marekani.