Jumamosi, 5 Desemba 2015

Diamond Platnumz na Mama yake Wakaa Kikao Kizito..Kisa Zari

Supastaa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na mama’ke mzazi, Sanura Kassim ‘Sandra’ wamelazimika kukaa kikao kizito ili kupata muafaka wa mzazi mwenzake na staa huyo, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kurejea Bongo na kuishi katika nyumba moja na mkwewe huyo ambaye walipishana kauli hivi karibuni.

Hivi karibuni, Zari aliyekuwa akiishi na mama Diamond nyumbani kwake, Tegeta-Madale jijini Dar, walipishana kauli na mzazi huyo sambamba na ndugu zake hadi kufikia hatua mrembo huyo aliyezaa mtoto mmoja na Diamond (Tiffah) kurejea nyumbani kwake Afrika Kusini kupisha kile alichokiita ni ‘uswahili’.

Chanzo makini kimeeleza kuwa, baada ya kuona Diamond anampenda Zari na mapenzi yao ni motomoto, familia haikuwa na jinsi zaidi ya kukaa kikao kulijadili kwa kirefu suala hilo na kupata muafaka ambapo habari njema ni kwamba, mama Tiffah anatarajia kutua Bongo siku chache zijazo.
“Diamond si unajua ndiyo kichwa katika familia. Amewaita ndugu akawaeleza dhamira na mikakati yake na Zari hivyo wamekubaliana arejee Bongo,” kilisema chanzo hicho.
Alipoulizwa Diamond kuhusiana na suala hilo, hakutaka kufunguka kwa undani akidai ni mambo ya kifamilia.

“Kila kitu kipo sawa. Zari ataibuka na maisha yataendelea kama kawaida, haya mambo ya kifamilia bwana,” alisema Diamond.

Kabla ya kufikia muafaka huo, Zari aliripotiwa kuwa anakuja nchini Desemba 8, mwaka huu wakati mama Diamond akionekana kupinga lakini hatimaye muafaka umepatikana.

GPL

Watorosha Makontena Bandarini Bila Kulipia Ushuru Hawa Hapa...Majina Yatajwa

Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) imetaja majina ya kampuni 43 na wamiliki wa makontena 329 ambayo yalipitishwa bandarini bila kulipiwa na kufichuliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wiki iliyopita.
Aidha, TRA imesema imesimamisha kazi watumishi wake 35 wanaofanya kazi katika ngazi mbalimbali, wakiwemo 27 waliokamatwa wiki hii katika Geti Namba Tano.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA, Dk. Philip Mpango alisema Mamlaka hiyo iliagizwa na Waziri Mkuu Majaliwa kuchukua hatua mara moja kwa kufuatilia na kubaini wamiliki wa Bandari Kavu (ICD) zilizohusika katika kashfa hiyo.
Alisema mbali na hilo walitakiwa kuwatambua wamiliki wa makontena hayo, bidhaa zilizokuwemo, kuwalipisha wahusika kodi iliyokwepwa pamoja na kuwachukulia hatua watumishi waliohusika na upotevu huo.
Dk. Mpango aliyataja makampuni hayo kuwa ni Lotai Steel Tanzania Ltd iliyokuwa na makontena 100, Tuff Tryes Centre Company 58, Binslum Tyres Company Ltd 33, Tifo Global Mart Company Limited 30, Ips Roofing Company Limited 20, Rushywheel Tyre Centre Co Ltd 12 na Kiungani Trading Co Ltd 10.

Makampuni mengine yaliyotajwa ni Homing International Limited (9), Red East Building Materials Company Ltd (7), Tybat Trading Co Limited (5), Zing Ent Ltd (4), Juma Kassem Abdul (3), Salum Link Tyres (3), Ally Masoud Dama (2), Cla Tokyo Limited (2), Farid Abdullah Salem (2), Salum Continental Co (2), Zuleha Abbas Ali (2) na Snow Leopard Building (2).
Wamiliki wengine wa makampuni ambayo yalikuwa na kontena moja moja ni Abdulaziz Mohamed Ally, Ahmed Saleh Tawred, Ali Amer, Ally Awes Alhamdany, Awadhi Salim Saleh, Fahed Abdallah Said, Hani Said, Hassan Husrin Suleyman, Humud Suleiman Humud, Kamil Hussein Ali na Libas Fashion.
Wengine ni Nassir Salehe Mazrui, Ngiloi Ulomi Enterprises Co Ltd, Omar Hussein Badawy, Said Ahmad Hamdan, Said Ahmed Said, Salumu Peculier Tyres, Sapato N. Kyando, Simbo Yonah Kimaro, Strauss International Co. Ltd na Swaleh Mohamed Swaleh.
Alisema kwa ujumla, makampuni hayo yalipitisha makontena 329 ambayo yaliondolewa kinyume cha taratibu kutoka ICD ya Azam inayomilikiwa na Said Salim Bakhresa And Company Limited.

Dk. Mpango alisema bidhaa zilizokuwemo ndani ya makontena hayo ni pamoja na matairi ya magari, samani mbalimbali, betri za magari, vifaa vya ujenzi, nguo na bidhaa zingine mchanganyiko.

27 WALIOKAMATWA
Aidha, Dk. Mpango alisema watumishi 35 wa Mamlaka hiyo wanaofanya kazi katika vitengo mbalimbali wamesimamishwa kazi, wakiwemo 27 waliokamatwa wiki hii katika geti namba tano.
Alisema watumishi hao wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano huku akisisitiza kuwa mtumishi yoyote wa TRA atakayebainika kuhusika katika hujuma hiyo atachukuliwa hatua kali za kinidhamu kwa mujibu wa sheria na kanuni za kazi kulingana na makosa atakayokutwa nayo.
Alisema TRA inaendelea kupanga safu ya watumishi wake ili kuthibiti upotevu wa malipo ya kodi na kwamba wanapitia upya taratibu za utoaji leseni kwa Bandari Kavu ili kuondoa mianya na kuweka udhibiti katika uondoshaji wa mizigo katika bandari zote na bohari za forodha.

“Pamoja na hatua hizi, TRA inafuatilia kwa kina ili kubaini mawakala wote wa forodha walioshiriki katika upotevu wa makontena hayo na kuwachukulia hatua ikiwemo kuwafungia leseni pamoja na adhabu zingine kwa mujibu wa sheria,” alisema Dk. Mpango
Mwishoni mwa wiki iliyopita serikali ya awamu tano chini ya Rais John Magufuli ilibaini ukwepaji wa kodi kwa kutorosha makontena 329 ambayo yamenyima serikali kodi ya Sh. bilioni 80.
Rais Magufuli alimsimamisha kazi Kamishna Mkuu wa TRA, Rished Bade huku Jeshi la Polisi likiwashikilia maofisa kadhaa waandamizi wa Mamlaka hiyo akiwemo Kamishina wa Forodha, Tiagi Masamaki.
Masamaki na wengine saba walifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu jana.


NIPASHE

Kigogo wa Bandari Afariki Kwa Presha...Undani wa Kifo chake Waelezwa Hapa

WAKATI Rais John Magufuli akiwa kwenye zoezi la kutumbua majipu kwenye Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), mshtuko mkubwa umetokea kufuatia kigogo mwenye wadhifa wa Artsan One (TPA) jijini Dar, Elia Eliampenda Kimaro (51) kufariki dunia ghafla kwa shinikizo la damu (presha) akiwa nyumbani kwake, Mikwambe, Kigamboni, Dar.

Kimaro alifariki dunia Novemba 30, mwaka huu kwa uthibitisho wa daktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambako marehemu alikimbizwa kwa ajili ya matibabu.

Kifo cha Kimaro kimetokea wakati kukiwa na sintofahamu kubwa miongoni mwa wafanyakazi wa mamlaka hiyo kuhusiana na utolewaji wa makontena 349 kinyemela na kuisababishia serikali kukosa mapato ya kiasi cha shilingi bilioni 80.

Taarifa kutoka ndani ya familia, marehemu alisumbuliwa na maradhi hayo kwa muda mrefu. Lakini ghafla alfajiri ya Novemba 30, hali yake ilibadilika na hivyo kukimbizwa Muhimbili ambako daktari alisema alishafariki dunia.

Mwandishi aliweza kufika msibani ambapo aliwashuhudia wafanyakazi wengi wa bandarini na TRA bandarini wakiwa hapo kwa ajili ya maandalizi ya mazishi.

Baadhi ya wafanyakazi hao, walisikika wakidai, marehemu alikuwa miongoni mwa vigogo waliokuwa wakichunguzwa kwa utolewaji wa makontena 349 siku chache zilizopita.

“Pia nasikia baada ya waziri mkuu (Kassim Majaliwa) kutoa mwongozo siku zile bandarini, watu wa usalama wa taifa walishamfuata hapa kwake mara kadhaa na kumhoji.

"Lakini pia, kuna madai kwamba, miamala yake ya kibenki nayo ilifuatiliwa na jamaa hao ambapo walikuta pesa nyingi,” alisikika akisema mmoja wa wafanyakazi hao ambaye alipogundua kuna waandishi wa habar alifunga kinywa.

Nao baadhi ya waendesha bodaboda wa eneo hilo, walionekana kushangazwa sana kufuatia taarifa za kifo cha kigogo huyo, wakidai siku moja kabla, walionana naye akiwa mzima wa afya.

Hata hivyo, walisema mara baada ya taarifa za kifo, walishangaa kuona magari yake ya kifahari yakiondolewa kutoka nyumbani kwake hapo:

“Labda waliyapeleka mahali ili kupata nafasi ya kuweka maturubai ya msiba. Si unajua majumba haya ya ghorofa, yana nafasi zaidi ya kwenda juu kuliko upana,” alisema mmoja wa bodaboda hao.

Mwendesha bodaboda mmoja alisema: “Mzee wa bandari alikuwa mtu poa sana. Hata madereva wa daladala zake wameumia. Unajua jamaa alikuwa na mkwanja wa maana. Hii nyumba ya hapa ‘cha mtoto’, ana nyumba nyingine Yombo (Dar), magari ndiyo usiseme. Yaani tumempoteza mtu muhimu sana.”

Marehemu Kimaro alizikwa Desemba 2, mwaka huu kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar. Ameacha mke na watoto wanne.

Credit: GPL

Taarifa Sahihi Kuhusu Hotel ya Serena Kufungwa Kwa Amri ya Serikali Kwa Kosa la Kukwepa Kulipa Kodi

Serena Hotel
HOTELI ya kimataifa ya Serena jana ilikumbwa na msukosuko wa kuandamwa na waandishi wa habari baada ya kusambaa kwa tetesi kuwa imefungwa kwa amri ya serikali kwa kosa la kukwepa kulipa kodi.


Tetesi hizo zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii jana asubuhi, zikieleza kuwa maofisa wa Mamlaka ya Mapato (TRA) wameifunga hoteli kufunga kwa kukwepa kuliko kodi serikalini.



Mbali ya kusambazwa kwa uvumi huo, zilitumwa pia picha zilizokuwa zikionyesha sehemu ya hoteli hiyo ikiwa imezungushwa uzio uliokuwa na rangi nyeupe na nyekundu ambao ni alama inayotumika kuonyesha kusitisha kwa huduma katika eneo hilo.



Tetesi hizo zilikwenda mbali zaidi kwa kueleza kuwa uongozi wa hoteli hiyo ulikuwa mbioni kubadilisha jina kwa lengo la kukwepa kulipa kodi.



Hata hivyo, mwandishi wetu baada ya kufika hotelini hapo kwa lengo la kufuatilia ukweli wa tetesi hizo alikuta shughuli za ukarabati wa sehemu ya kupokea wageni zikiendelea, huku wageni wakielekezwa kutumia mlango wa dharura ambako kumetengezwa sehemu ya muda ya kupokelea wageni.



Uongozi wa Hoteli ya Serena kupitia Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko, Seraphine Lusala, ulilazimika kutoa taarifa kwa vyombo vya habari ukikanusha kufungwa kwa hoteli hiyo na kusisitiza kuwa kinachoendelea hotelini hapo ni matengenezo.



“Si kweli kama hoteli imefungwa, tunafanya matengenezo na yalikuwa yafanyike tangu miaka mitatu iliyopita, kilichofanyika sasa ni kubadilisha eneo la mapokezi yaliyohamishiwa milango mingine na tumeanza na eneo hilo pamoja na sehemu ya mazoezi,” alisema Lusala.



Alisema matengenezo hayo yanalenga kuifanya hoteli hiyo kuwa ya kiwango cha juu zaidi na yatachukua miezi  10.



Lusala alisema awamu ya kwanza ya matengenezo itachukua miezi minne na miezi minne ijayo itahusu matengenezo sehemu ya vinywaji, chakula, eneo la uwanja na baadaye maeneo mengine ya wazi.

Death Has Forgotten Me, Now I Have Lost All Hope to Die....179-Year-Old Man Cries Out (Pictured)

An Indian man who claims to be born in 1835 is not only the oldest man in the world, but also the man who has lived the longest since the history of mankind (according to the Guinness World Records).

According to the information transmitted, Mahashta Mûrasi was born in Bangalore on January 6, 1835.

In 1903, he lived in Varanasi, where he worked until 1957, until his retirement at the already venerable age of 122.

According to WorldNewsDailyReport, all official documents to identify this man support his version.

"I have been alive for so long, that my great grand-children have been dead for years," says Mr Mûrasi. "In a way, death has forgotten me. And now I have lost all hope to die!"

Mkuu wa Mkoa Wa Dar es Salaam Awaagiza Wakurugenzi Kuwaondoa Ombaomba Waliko Barabara za Jiji

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri za jiji la Dar es Salaam, kuwaondoa ombaomba wote walioko katika barabara za jiji, kwani wanachangia uchafu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini jana, Sadiki alisema utekelezaji wa kauli ya Rais John Magufuli ya kutumia siku ya Desemba 9 mwaka huu kufanya usafi, utakwenda sambamba na kuwaondoa ombaomba hao, ambao wanachangia kuongeza uchafu.

“Siwezi kusema wao ni uchafu lakini mazingira yanayowazunguka katika maeneo wanayofanyia shughuli zao wanayachafua, wanajisaidia kwenye mifuko na kutupa ovyo,” alisema.

Alisema viongozi ambao wako katika maeneo ambayo ombaomba hao wanarudi, wahakikishe hawarudi mjini kwa sababu imekuwa ni tabia ya omba omba hao wanaporudishwa baada ya muda kurudi tena jijini.

Aidha, aliiagiza Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kushirikiana na Jeshi la Polisi kuwaondoa wapigadebe katika vituo vya daladala kwani wamekuwa kero kwa abiria.

Rais Magufuli Amkalia Kooni Kigogo Aliyetaka Kuchukua Ufukwe wa Coco Beach na Kuwekeza...Amsema Kimafumbo

Akitumia lugha ya mafumbo na moja kwa moja alisema hata ukiwa na fedha hata ukiwa na uwezo wa kufoji documents jua serikali ipo tena ya Magufuli. 

Akauliza hivi wakazi milioni nne wa DSM wakiamua kuvamia na kutwaa eneo lao utaenda wapi? Kwanini msitafute maeneo sehemu nyingine na si hili la wanyonge wanapopumzikia? 

Siku 30 za Kuwa Madarakani Kama Rais , Magufuli Aokoa Sh1trilioni

 Rais John Magufuli leo ametimiza mwezi mmoja tangu alipoapishwa kushika wadhifa huo huku akiweka rekodi ya kuokoa kiasi cha Sh997.4 bilioni (karibu Sh 1trilioni) ambazo zilikuwa zitumike kwa matumuzi yasiyo ya lazima, na ukwepaji kodi.

Sh997.4 bilioni zilizookolewa zitaweza kutumika kununua magari ya wagonjwa, kujenga zahanati, kujenga barabara za lami, kununua madawati, kujenga vyumba vya madarasa, kuchimba visima, kununua mashine za uchunguzi wa magonjwa, magari ya wanafunzi, pikipiki kwa maofisa kilimo, mikopo ya elimu ya juu au kujenga viwanja vya michezo kadri Serikali itakavyoelekeza.

Dk Magufuli aliapishwa Novemba 5 katika hafla iliyofana na alianza kazi ya kutafuta na kuziba mianya ya upotevu wa fedha Novemba 6 alipotembelea Hazina. Katika mazungumzo ya watendaji wa wizara hiyo Rais Magufuli alipiga marufuku safari zote za nje na kwamba zitakuwa zinaruhusiwa kwa kibali maalumu.

Novemba 7 alitembelea Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambako aliagiza mashine za MRI na CT-Scan zitengenezwe na aliagiza Sh3 bilioni zitolewe kugharimia matengenezo kati ya Sh7 bilioni zilizokuwa zinahitajika.

Novemba 19, Dk Magufuli aliwasilisha bungeni jina la Kassim Majaliwa, mbunge wa Ruangwa kwamba ndiye alimpendekeza kuwa Waziri Mkuu. Baada ya jina kupitishwa na Bunge, Novemba 20 Kassim Majaliwa aliapishwa.

Jioni alilihutubia Bunge akionyesha mwelekeo wa Serikali yake ya awamu ya tano. Katika hotuba hiyo iliyowasisimua wabunge na hata wananchi waliosikiliza kupitia televisheni na redio, Dk Magufuli aliahidi kupambana na mafisadi, kubana matumizi, kuhimiza utendaji kazi, kuinua uchumi na kulinda amani na utulivu.

Baada ya hapo Magufuli na Waziri Mkuu, Majaliwa wamekuwa wakitembelea maeneo muhimu kwa uchumi wa nchi kama Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bandari na Kampuni ya Reli Tanzania (TRL)

Utendaji huo wa Serikali wa Magufuli ndani ya mwezi moja na kipindi kabla hajaunda baraza la mawaziri, umetazamwa na jamii kuwa ni mbinu ya kusafisha nchi na kutengeneza mazira safi ili mawaziri watakaoteuliwa wafuate kasi hiyo.

Fedha zilizookolewa

Kwa kuzingatia ripoti ya matumizi ya fedha za safari zilizolipwa kama nauli na posho kwa kipindi cha kati ya mwaka 2013 na 2015 kiasi hicho ni pamoja na Sh356.3 ambazo zingeweza kutumika kwa safari hizo. Dk Magufuli aliagiza kwamba baadhi ya shughuli zitafanywa na mabalozi wa Tanzania walioko nje.

Novemba 19 alipozindua Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano mjini Dodoma, Dk Magufuli aliagiza Sh225 milioni zilizokuwa zimekusanywa kwa ajili ya hafla ya wabunge, zipelekwe kununua vitanda katika Hospitali ya Taifa Muhimbili. Fedha hizo zilinunua vitanda 300, magodoro 300, mablanketi 1675, na viti vya magurudumu 30.

Pia, katika hotuba yake bungeni, Dk Magufuli alirejea uamuzi wake wa kufuta safari za nje kwa watendaji wa Serikali na kueleza safari hizo zimeigharimu Serikali Sh356.3bilioni ambazo zingeweza kujenga barabara ya lami yenye urefu wa kilomita 400.

Novemba 23, Dk Magufuli alitangaza kufutwa kwa maadhimisho ya Siku ya Uhuru Desemba 9 na akaagiza Sh4 bilioni ambazo zingetumika zitumike kufanya upanuzi wa barabara ya Morocco kwenda Mwenge. Kazi hiyo imeanza.

Novemba 25, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alitangaza kufutwa maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani na akaelekeza kwamba fedha zilizopangwa kwa ajili ya sherehe hizo zitumike kununua dawa za kufubaza makali ya ukimwi (ARVs).

Novemba 27, Waziri Mkuu Majaliwa alitembelea bandarini na kubaini makontena 349 ambayo yalitolewa bandarini bila kulipiwa ushuru na kuifanya Serikali kukosa mapato ya Sh80 bilioni.

Tayari wenye makontena hayo wameanza kulipia na jana  TRA ilitangaza kukusanya Sh6.3 bilioni kati ya hizo Sh80 bilioni. Katika ziara yake nyingine ya kushtukiza Desemba 3 Majaliwa alibaini makontena 2,431 yalitolewa bila kulipiwa kodi. Ikiwa makontena hayo yangelipiwa kodi viwango sawa na yale 349 Serikali ingepata Sh557.2 bilioni.

Desemba 3, Dk Magufuli alifanya mazungumzo na jumuiya ya wafanyabiashara nchini na akawataka wote ambao waliondoa mizigo yao bandarini bila kulipa kodi, wajitahidi kulipa katika kipindi cha siku saba kuanzia juzi vinginevyo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Makontena ni shida

Desemba 1, makontena mengine tisa yalikamatwa na TRA eneo la Mbezi, Tangibovu yakiwa yametoroshwa bila kulipuiwa ushuru wa Sh58 milioni. Jumla ya Sh637.2 zimeokolewa kutokana na mkakati wa kukusanya fedha kutoka kwenye makontena 2,431 pamoja na 349 na hayo tisa.

Matumizi ya Sh 997.4 bilioni

Kwa muda mrefu, Serikali imekuwa ikikwama kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kutokana na kukosa fedha. Dk Magufuli alikiri juzi kuwa hakuna fedha za maendeleo zilizokuwa zimetolewa kwa wizara zote katika mwaka huu wa fedha wa 2015/16, lakini baada ya miezi sita juzi ndiyo zimetolewa Sh120 bilioni.

Dk Magufuli hakusema Serikali imepata wapi fedha hizo, lakini huenda ni sehemu ya fedha ambazo ameokoa katika kipindi cha mwezi mmoja.

Kama fedha hizo zingeelekewa katika ujenzi wa barabara, na kwa kuzingatia kilomita moja inajengwa kwa Sh1 bilioni, fedha hizo zitaweza kujenga karibu au zaidi ya kilomita 1,000, ambao ni umbali kutoka Dar es Salaam hadi Kigoma au Dar es Salaam mpaka Tunduma.

Aidha, Sh997.4 bilioni zingeweza kununua magari 3,325 ya kubebea wagonjwa kwa gharama ya Sh300 milioni kwa kila moja na kuwezesha kila mkoa kupata magari 133 ya aina hiyo.

Pia, zahanati moja yenye vifaa vyote muhimu ujenzi wake unagharimu kati ya Sh600 milioni na Sh700 milioni. Hivyo, fedha hizo zingeweza kujenga zahanati 1,425 yaani kila mkoa ungepata zahanati 57.

Vilevile, wakati maelfu ya wanafunzi wa shule ya msingi na sekondari wanasoma kwa kukaa chini kutokana na kukosa madawati, Sh997.4 bilioni zitaweza kutengeneza madawati yenye miguu ya chuma 33,249,142 kwa gharama ya Sh30,000 kwa kila moja na kuwezesha kila mkoa kupata madawati 1,329,966.

Pengine, fedha hizo zinaweza kujenga vyumba vya madarasa 132,996 kwa bei ya Sh7.5 milioni kwa darasa moja, hatua ambayo itawezesha kujengwa kwa vyumba vya madarasa 5,319 kila mkoa nchini.

Kipimo maarufu cha CT-Scan ambacho ufanyaji wake wa kazi unasuasa Muhimbili kwa muda mrefu, kinauzwa kwa wastani wa Sh900 milioni, hivyo, Sh997.4 bilioni zitaweza kununua mashine 1,108 ambazo zingesambazwa na kila mkoa ukapata mashine 44.

Gharama za kuchimba kisima kifupi ni kati Sh1 milioni na Sh3 milioni kulingana na jiografia ya eneo husika, hivyo Sh997.4 bilioni zitaweza kuchimba visima 332,491; kila mkoa ukapata visima 13,299.

Pia, kwa kuwa Serikali inahimiza uboreshaji wa sekta ya kilimo, Sh997.4 bilioni zitaweza kununua pikipiki 332,491 na kugawiwa kwa maofisa kilimo kwa ajili ya kufuatilia utekelezaji wa kilimo vijijini na kila mkoa ungepata pikipiki 13,299.

Kama fedha hizo zitaelekezwa kwenye mikopo ya elimu ya juu, zitaweza kugharamia wanafunzi 249,368 wa mwaka wa kwanza kwa asilimia 100 kwa wastani wa Sh4 milioni kwa kila moja kwa ajili ya chakula, malazi na ada.

Wabunge: Magufuli Futa Wakuu wa Wilaya na Mikoa

BAADHI ya wabunge kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM)  kutoka mkoa wa Dodoma wamemshauri Rais John Magufuli kuondoa nafasi za Ukuu wa Mikoa na Wilaya na badala yake kazi hizo zifanywe na Makatibu tawala wa mikoa na Wakurugenzi wa halmashauri husika. 

Wakizungumza  kwa masharti ya kutokutaka kutajwa majina wabunge hao walisema hakuna sababu yoyote ya kuwepo kwa Mkuu wa Mkoa wala Mkuu wa wilaya kwani hawana kazi na badala yake ni kuiogezea mzigo serikali.
Mmoja wa wabunge kutoka kati ya majimbo ya Nyanda za juu kusini,alisema ili kudhiilisha kuwa wakuu wa mikoa na wilaya hawana kazi ni hivi tu ambavyo wanaonekana kukurupika kwa kuwawajibisha watumishi waliopo chini yao.

“Inasikitisha kuona wakuu wa Wilaya na Mikoa wanavyokurupuka kwa sasa kuwawajibisha watendaji ambao wapo chini yao kwa kuwanasa vibao ama kuwasweka rumande.
“Hapo utajiuliza muda wao walikuwa wapi hata hivyo ukiangalia vizuri utagundua wazi kuwa wakuu wa
Mikoa na Wilaya hawana kazi yoyote ya kufanya na badala yake watendaji wakuu ni Makatibu tawala wa Mikoa au wakurugenzi wa Halmashauri husika” amesema Mbunge huyo.
Wabunge wakipendekeza hayo baadhi ya watumishi katika halmasauri ya Dodoma,nao kwa masharti ya kutokutaka kutajwa majina wamesema kwamba kutokana na kasi ya utendaji wa Rais Magufuli sasa wanasiasa wanalazimisha kuingilia masuala ambayo ni ya kitaalam.
“Tunashangaa zaidi kuona wanasiasa kama vile wakuu wa wilaya na wakuu wa Mikoa wakiwakaripia watumishi ambao ni wanataaluma.

“Na pale wanasiasa wanaposhauriwa juu ya utendaji wao wanakuwa wakali wakali zaidi kwa sasa kilichobaki ni watumishi kukaa kimya ili wawasikilize wanasiasa lakini matokeo yake kazi zitalala” alisema Mtumishi huyo.

Yapo mambo mengine kwa sasa ambayo uwezi kuyafanya kutokana na kuhitajika kwa vitendea kazi,wakati mwingine unatakiwa kutoa tiba wakati huo hakina vifaa.
Watumishi hao wanalazimika kutoa yao ya moyoni kutokana na taarifa mbalimbali zinaziripotiwa kuwa wapo baadhi ya wakuu wa Wilaya na wakuu wa Mikoa ambao wanawazaba watumishi vibao na kuwashweka ndani watumishi.

Wakati huohuo baadhi ya wanasheria mkoani Dodoma wamewataka baadhi viongozi wa serikali kuacha kutumia madaraka yao vibaya kwa kuwadhibu baadhi ya watumishi wanaochelewa kazini kwani kufanya hivyo ni kosa.

Siku za hivi karibuni vyombo vya habari kumezagaa taarifa za baadhi ya viongozi ndani ya serikali wamedaiwa kutumia nyadhifa zao vibaya kwa kuwapiga au kuwasweka lumande watumishi wa ngazi ya chini pindi wanapobainika kuchelewa kufika kazini.
Wanasheria hao kwa kuweka weka sawa suala la wakuu wa mikoa na wilaya au kiongozi yotote kumpiga mtumishi walisema kwa kufanya hivyo ni kosa la jinai.

Wakizungumza na MwanaHalisi online mjini hapa juzi, bila kumlenga kiongozi yeyote, Wanasheria hao  walisema ni kosa kwa mtumishi wakiwemo viongozi kupigana katika sehemu za kazi.
Mmoja  wa mawakili  wa Kituo cha Sheria cha Goldmac Attorneys Advocates, Modester Mganga, alisema watumishi wote wa Idara za serikali wanapaswa kuzingatia sheria sehemu za kazi pamoja na utawala bora na si vinginevyo.

Alisema kuwa endapo kama ni kweli kuna mfanyakazi ambaye amefanyiwa vitendo hivyo vya kupigwa au kuwekwa rumande anayo haki ya kwenda kushitaki kwenye vyombo vya sheria kwa vile sheria za kazi ziko wazi kwamba zina kataza watumishi kupigana sehemu za kazi.