Alhamisi, 12 Mei 2016

Mpinzani wa Museveni , Dr Kiiza Besigye Akamatwa Baada ya Kujiapisha Kuwa Rais

Mpinzani mkuu wa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, Dk. Kizza Besigye ambaye amekuwa akipinga ushindi wa Rais huyo, amekamatwa na polisi wa nchi hiyo baada ya jana kujiapisha kuwa Rais ikiwa ni siku moja tu (leo) kabla ya Museven kuapishwa.
Haijulikani ni vipi Dr Kiiza Besigye alikwepa vizuizi  vya polisi na kuibukia mjini Kampala ambapo alikutana na wandani wa chama chake na ''kula kiapo cha urais wa taifa hilo''.
Katika video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii Dr Besigye anaonekana ''akila kiapo'' mbele ya mtu aliyevalia mavazi sawa na ya ''jaji wa mahakama ya juu''.
Video hiyo ilisambazwa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii na kusababisha mamlaka inayosimamia mawasiliano nchini Uganda kuamrisha kampuni zinazotoa huduma za simu nchini humo kufunga huduma za mitandao ya kijamii
Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilimtangaza Yoweri Museveni kuwa mshindi katika uchaguzi mkuu uliopita akiwaacha kwa mbali wapinzani wake wakuu, Kizza Besigye na Amama Mbabazi.
Kadhalika, Mahakama Kuu nchini humo ilihalalisha ushindi wa Museveni baada ya kutupilia mbali shauri la pingamizi la ushindi huo lililowasilishwa na Amama Mbabazi.


Viongozi Wakuu Wote wa Taifa Wako nje ya Nchi ..Nani Anaongoza Nchi Kwa Sasa?

Viongozi wakuu wote wa Taifa wako nje ya nchi katika ziara za kiserikali kwenye mataifa tofauti.
Rais John Magufuli aliwasili Uganda jana asubuhi kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais mteule wa nchi hiyo, Yoweri Museveni zinazofanyika leo na Makamu wake, Samia Suluhu Hassan alikuwa Kigali, Rwanda kuhudhuria mkutano wa dunia wa uchumi.
Taarifa zilizopatikana na kuthibitishwa na Mwandishi wa Makamu wa Rais, Penzi Nyamngumi zimesema, Makamu wa Rais aliondoka nchini Jumanne akitokea Dodoma na angerejea kesho baada ya mkutano huo.
Kiongozi anayefuatia kwa wadhifa, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisafiri juzi kwenda London, Uingereza kumwakilisha Rais Magufuli katika mkutano wa wakuu wa nchi kujadili mapambano dhidi ya rushwa.
Majaliwa katika ziara hiyo ameongozana na Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju alipotakiwa kutoa ufafanuzi juu ya anayepaswa kukaimu urais, alisema Makamu wa Rais amekwisha rejea nchini na yuko Mwanza.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 37 (3), inaeleza kuwa endapo Rais atakuwa hayupo katika Jamhuri ya Muungano, kazi na shughuli za Rais zitatekelezwa na Makamu wa Rais, kama naye hayupo, yatatekelezwa na Waziri Mkuu.
Hata hivyo, Ibara ya 37 (6) (b) inasema Rais hatahesabiwa kwamba hayupo iwapo atakuwa nje ya Jamhuri ya Muungano kwa kipindi cha saa 24.


Jumamosi, 7 Mei 2016

Serikali yakamata Tani 4,900 za Sukari iliyofichwa Mbagala na Tabata jijini Dar

Baada ya muda mfupi wa rais kusema kuwa kuna wafanyabiashara wameficha Sukari, muda huu imeripotiwa kuwa huko Mbagala kuna Sukari ya zaidi ya tani 4,900 kwenye ghala la mfanyabiashara mmoja na imeelezwa zitachukuliwa hatua stahiki.
Chanzo: TBC, habari mpasuko

Shetta Akanusha Taarifa Kuwa Diamond Amewahi Kutoka Kimapenzi na Mkewe

Shetta amekanusha taarifa zilizozagaa mitandaoni kuwa Diamond amewahi kutoka kimapenzi na mama Qayllah.
Wiki kadhaa zilizopita Shetta alifuta picha zote kwenye akaunti yake ya instagram huku akiwaacha mashabiki wake wakijiuliza maswali mengi kutokana na kitendo hicho.
Akiongea kwenye kipindi cha Leo Tena, kinachoruka kupitia Clouds FM, Shetta amesema, “kuhusu suala la mama Qayllah kutoka na Diamond hakuna ukweli wowote.”
“Kuhusu suala la kufuta picha ni management yangu mpya ilinishauri hivyo ndiyo maana unaona nilifuta picha zote hizo. Team team tu wameanzisha na kuzisambaza mitandaoni lakini hakuna ukweli wowote namuamini sana mke wangu. Mimi na Diamond tuko vizuri ila hizo,” aliongeza.


Kajala Ahusishwa Undani wa Wimbo wa ‘Haya Yote ni Maisha’ ya P Funk

Msanii Madee amefunguka undani wa wimbo wa ‘Haya Yote Maisha’ wa Producer P Funk Majani ambao ameimba yeye, wimbo ambao ulishika chati na kugusa hisia za watu wengi.
Akiongea kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Madee amesema wimbo huo ni historia ya kweli ya P Funk na mwanamke ambaye ndiye mama wa mtoto wake wa kwanza, Kajala Masanja.
Madee aliendelea kusema baada ya mazungumzo P Funk alikubali kumpa beat na kwenda kuifanyia kazi, baada ya kukumbuka Madee mtindo alioutumia kwenye nyimbo zake.

“Haya yote maisha imetokea kipindi ambacho bado nipo na P Funk, alafu P Funk ana matatizo na mama mtoto wake Kajala, kwa hiyo wakati mi naenda pale kurekodi cheza kidogo, kabla sijamalizana na ile nakutana na beat ya yote maisha inaplay, alafu inaplay na chorus lakini hakuna verse, lakini the way ile beat inavyoplay majani anavyoiimba anaimba kwa feelings kinoma, nikamwambia bwana hii nyimbo mbona kali nigaie niimbe akasema hii na chana mwenyewe babu,” alisema Madee.
“Sema wewe ulivyochana kwenye kazi yake mola kuna ryhmes fulani naona unapita pita, unaongea kimajonzi hebu chukua hii beat kaandike, kwa hiyo nikapewa ile beat, aliniambia kwamba hii nyimbo ina feeling zangu, nataka uandike kitu hiki na hiki, kwa hiyo idea iliyotoka mule ni idea ya P Funk,” alisema Madee akimuongelea P Funk Majani.


Idadi ya Ajali zilizojitokeza wakati wa Majaribio Mabasi yaendayo Haraka

Wakala wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) umesema kutozingatia sheria za barabara za mradi wa mabasi hayo, kwa vyombo vingine vya moto vimesabisha ajali 14 wakati madereva wa mabasi hayo wakiendelea na mazoezi kwa ajili ya kuelekea kipindi cha mpito cha mradi kinachotarajia kuanza hivi karibuni.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala huo, Mhandisi Ronald Rwakatale amesema kuwa ajali hizo zimejitokeza wakati madereva wa mabasi ya mradi wakifanya mazoezi na kisha vyombo vingine vya moto viingilia barabara zake na kusabisha ajiali hizo.
Amesema ajali hizi ni matokea ya vyombo vingine vya usafiri kama magari madogo, daladala, bodaboda na waenda kwa miguu wamekuwa wakiingilia barabara za mabasi hayo na kusabisha ajali kutokana na kwamba barabara hizo haziruhusu mabasi hayo kupisha na vyombo vingine.
Mhandisi Rwakatale amesisitiza kuwa barabara za mabasi hayo ambazo ni za zege zimejengwa mahususi kwa ajili ya mabasi hayo hivyo madereva wa vyombo vingine wanahitajika kuheshimu sheria zinazoongoza mradi huo na kupita katika barabara walizotengewa na watakaokiuka sheria itachukua mkondo wake.
Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka unatarajiwa kuanza kipindi cha mpito mwezi huu wa Mei kutoa huduma ya usafiri kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam


IMEBAINIKA Rihanna na Drake Wamekuwa Kwenye Mahusiano ya Siri Kwa zaidi ya Mwezi sasa

Jarida la PEOPLE limefumua bonge moja la siri kuwa staa Rihanna na rapa Drake wamekuwa na mahusiano ya siri kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa.
Rihanna na Drake wamefanya collabo kama “Take Care” .“What’s My Name?” na “Work” ila pia wamekuwa wapenzi kwa muda sasa bila kutaka dunia ijue.
Rihanna ndio sababu ya Drake na Chris Brown kutoelewana ila kwa sasa inasemekana Kwa Rihanna pale Drake beki hazikabi

Young Dee Aporomoshewa Matusi Baada ya Kupost Picha Akivuta Bang

Usiku wa kuamkia May 6 2016 Paka Rapa Young Dee alipost picha akiwa anavuta kitu ambacho mashabiki wake kwenye mtandao wa instagram walitafsiri ni bangi na kuanza kumporomosshea comments kuwa anaelekea kuwa kama Chidi Benz,
Je Young hapa alikuwa anavuta bangi ? na kama ni bangi ni sawa kwa msanii kufanya hivi bongo kama tunavyoona nje kwa kina Wiz Khalifa.


Shilole Akanwa Laivu Mchana Kweupe...Nedy Adai Hawana Mahusiano ya Kimapenzi

Bongo fleva super staa Nedy Music ambaye hivi karibuni amejiunga na lebel ya Ommy Dimopz ya Pozi Kwa Poz amekanusha uvumi kuwa Shilole ni Mpenzi wake...Akihojiwa Clouds FM amesema hana uhisiano wa Kimapenzi na Shilole
Awali Nedy alitajwa akuwa mpenzi wa Shilole baada ya staa huyu kuachana na Nuh Mziwanda.


TAZAMA HAPA WIMBO MPYA WA SHETTA

Tazama Hapa Chini Video Mpya ya Mwanamuziki Shetta ya Wimbo Unaoitwa Namjua, Video Imefanywa South Africa...


Jason Rweikiza Achaguliwa Kuwa Katibu wa Wabunge wa CCM

WABUNGE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamemchagua Mbunge wa Bukoba Vijijini, Jason Rweikiza kuwa Katibu wao.
Rweikiza anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Mbunge wa Peramiho, Jenista Mhagama, ambaye safari hii hakuwania nafasi hiyo.
Katika uchaguzi huo uliofanyika juzi usiku katika ukumbi wa Msekwa uliopo ndani ya viwanja vya Bunge, Katibu huyo mpya wa Wabunge wa CCM alikuwa akipambana na Mary Chatanda, Mariam Kisangi na Abdalah Ulega.
Wabunge wote wa CCM pia walipiga kura kuwachagua wabunge 10 kati ya 21 walioomba ujumbe wa NEC.
Waliochaguliwa ni Livingstone Lusinde, Dk Hamis Kigwangalla, Stanslaus Nyongo, Steven Ngonyani, Peter Serukamba, Faida Bakari, Agness Marwa, Munde Tambwe, Angella Kairuki na Jamal Kassim Ali.
Wabunge ambao kura hazikutosha ni Mbaraka Dau, Alex Gashaza, Hawa Ghasia, Ibrahim Raza, Profesa Norman Sigalla ‘King’, Almas Maige, Angelina Malembeka, Yahya Massare, Mattar Ali Salum na Hafidh Ali Tahir


Snura Atoboa Siri Alipojifunzia Mauno

Msanii Snura ambaye jana video ya wimbo wake wa ‘Chura’ ulifungiwa na serikali kutokana na kutokuwa na maadili na kukiuka utamaduni wa kitanzania amefunguka na kusema kuwa yeye kukata viuno amejifunzia kwenye ngoma za asili.
Snura ameyasema hayo leo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari ambapo alikuwa akitoa ufafanuzi na kuomba radhi kwa watanzania kutokana na video yake hiyo kutokuwa na maadili na kuwadhalilisha wanawake.
“Mimi ni mwanamke na niliwachukua wanawake wenzangu kucheza lakini haina maana kuwa niliwachukua ili niwadhalilishe hapana, ila nakiri kuwa nilichokosea ni kuwaingiza kwenye maji ndiyo maana ilionekana kama ni udhalilishaji kwao. Lakini kucheza hakumdhalilishi mtu na ndiyo maana kuwa bendi wachezaji show wake wanakatika hata kwenye ngoma zetu za asili tunakatika, mimi nimejifunza kukatika kwenye ngoma za asili kwani ndiyo kipaji changu cha kwanza na huko ndiyo nimejifunzia kiuno” alisema Snura

Ijumaa, 6 Mei 2016

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Singida Asimamishwa Kazi Baada ya Kutoa Taarifa za Uongo Kuhusu Watumishi HEWA

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Singida, Simion Mumbee amesimamishwa kazi baada ya kudaiwa kutoa taarifa za uongo kuhusu watumishi hewa.
Katika taarifa hiyo, Mumbee anadai watumishi hewa 19 waliogundulika kwenye halmashauri hiyo hawajaisababishia hasara Serikali jambo linalodaiwa kuwa si kweli.
Akizungumza jana kwenye ufunguzi wa kikao cha maendeleo mkoani humo, Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mathew Mtigumwe alisema anamsimamisha kazi mkurugenzi huyo ili kupisha uchunguzi.
“Nilipotuma tume kufuatilia suala la watumishi hewa katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida, ilibaini wapo na wameisababishia Serikali hasara ya zaidi ya Sh125 milioni,” alisema Mtigumwe.
Alisema taarifa ya Mumbee ililenga kuidanganya Serikali. Mtigumwe alimuagiza Katibu Tawala wa Mkoa, Dk Angela Lutambi kumuandikia barua ya kumsimamisha kazi mara moja.
Mtigumwe alisema hana nafasi ya kufanya kazi na watumishi wa aina ya Mumbee.
Wakati huo huo; Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu amemsimamisha kazi Ofisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Philbert Mtweve kwa tuhuma za kuwalipa mishahara watumishi hewa wanane na kuisababishia Serikali hasara ya Sh27 milioni.


PICHA: Jionee kaburi atakalozikwa Papa Wemba

Picha hii inasemekana ndilo kaburi atakapozikwa mwanamziki Maarufu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo maarufu kwa jina la Papa Wemba.
Huu ni zaidi ya ufahari, lakini mimi naona hauna maana..


CHADEMA na Katibu Mkuu mfu..Ukimya Wake ni Hatari kwa Mustakabari wa Chama

Kiukweli huyu katibu mkuu hajui hata pa kuanzia Chama kinaonesha dalili za kuifuata TLP na UDP sioni harakati zake ki ukweli CHADEMA ilikosea sana Dr. Mashinji ni unpopular figure hata akitembea kwa miguu Karikoo hakuna wa kumshitukia kuwa ni kiongozi.
Ukimya wake ni hatari kwa mustakabari wa chama kwani watu wasiokuwa na vyeo kama akina Lowassa ndo wamekuwa msaada mkubwa kukisemea chama kwa sasa. Anaonekana kabisa ni uteuzi ambao ulikosewa na ni mtu asiyekua na ushawishi ndani ya chama.
Kutoka kwenye nchi ya viwanda mpaka nchi ya majipu alikuwa ana mengi ya kuongea lakini yupo kimyaa wakisubiri kuzungusha mikono mwaka 2020.
Huku serikali ya Magufuli ikijisafishia njia inaonekana haitapata upinzani mwaka 2020 kutokana na uchakavu wa CHADEMA.


Nuh Mziwanda Afunguka Kuhusu Kurudiana na Shilole

Msanii Nuh Mziwanda ambaye kwa sasa anafanya poa na wimbo wake mpya ambao amemshirikisha Alikiba amefunguka na kusema kuwa hata kama ikitokea mpenzi wake huyo wa zamani akitaka kurudiana na yeye ni kitu kisichowezekana kwa sasa.
Akizungumza kwenye kipindi cha 5SELEKT kinachorushwa na ting’a namba moja kwa vijana Nuh Mziwanda amesema kuwa kwa sasa yeye amefunga ukurasa wa mapenzi na Shilole hivyo hata ikitokea akataka kurudiana na yeye hawezi kufanya hivyo kwani ameshaanza maisha mapya ambayo anaona ni ya furaha zaidi.
Mbali na hilo Nuh Mziwanda ameeleza kuwa kwa sasa hataki tena maisha ya kiki na skendo alizoita kuwa ni za ajabu ajabu bali anataka kujenga jina lake kutokana na kazi zake kwenye muziki pamoja na kutengeneza muziki kama ‘Producer’


Mheshimiwa Rais Wanaodhani Wako Juu ya Sheria ni Wengi Sana...Soma Kisa Hichi

MIAKA michache iliyopita, wakati wa Serikali ya Awamu ya Nne ambayo imeshapita, kuna jambo moja lilinishangaza sana. Jambo hili lilimhusu Waziri wa Serikali hiyo na mlinzi wa benki.
Kilichotokea ni kwamba Mheshimiwa Waziri alikwenda kwenye mashine ya kutolea fedha, maarufu kama ATM, huenda kwa ajili ya kutoa fedha. Akiwa ndani ya kile chumba akaanza kuzungumza na simu. Akazungumza na simu kwa muda mrefu, hali iliyosababisha wateja waliokuwa wakiisubiri huduma hiyo kuanza kulalamika na kumlazimu mlinzi kumuomba Waziri awapishe wateja wengine waweze kupata huduma.
Hilo halikumfurahisha Waziri yule na badala yake akaanza kumwuliza mlinzi kama anajua yeye ni nani, kwa kuwa yeye kama Waziri ana mambo mengi ya maana na alikuwa akizungumza na simu muhimu. Kwa huyo Waziri, suala la kuzungumza kwenye chumba cha ATM na kuwanyima fursa wateja wengine kama yeye kuipata huduma waliyokuwa wakiihitaji kwa wakati, halikuwa tatizo kabisa.
Sakata la Mheshimiwa Waziri na mlinzi wa benki liliripotiwa kwenye vyombo vya habari na bahati mbaya mwisho wake ulikuwa wa kusikitisha, kwani mlinzi alifukuzwa kazi kutokana na kutimiza majukumu yake. Baadhi ya watu walipiga kelele, lakini hakuna kilichotokea. Sana sana, baba wa watu akabaki bila kazi, huku akiwaza ataitunzaje familia yake iliyokuwa ikimtegemea.
Sasa juzi hapa hali hiyo imejirudia tena.  Safari hii, hata hivyo, imemhusisha Mke wa Mheshimiwa Waziri mwingine, ambaye alibishana na askari wa usalama barabarani aliyekuwa akitimiza majukumu yake ya kazi kwa kumweleza makosa ya barabarani aliyoyatenda. Badala ya kusikiliza makosa yake na kuadhibiwa kwa kadiri ya matendo yake, mke huyu aliitumia karata yake ya kupitia mgongo wa mumewe na kutoa kauli za kuudhi zisizofaa kwa yule askari.
Kwa mara ya kwanza katika kipindi kirefu sana, mambo yanaelekea kubadilika na wale waliokuwa wakidhani wapo juu ya sheria, wanakumbushwa tena kwamba Tanzania sio ya kwao peke yao.
Taarifa zinasema kwamba Rais John Pombe Magufuli ameamuru askari wa usalama barabarani aliyekuwa akifanya kazi yake na kuishia kutolewa maneno yasiyofaa na Mke wa Waziri, apandishwe cheo.  Vilevile, ameshamuonya Waziri na Mke wake kuhusiana na tukio hilo, kwani hakuna mtu aliye juu ya sheria.
Binafsi, taarifa hiyo imenifurahisha sana. Tuseme tu ukweli kwamba Tanzania ilikuwa nchi ya ajabu sana. Ilikuwa na matabaka makubwa sana kiasi cha watu kuzungumzia kutaka hata kukimbilia kuishi nje ya nchi, kutokana na kujiona hawathaminiwi, huku wengine wakitamba mitaani na kufukuzisha watu kazi kana kwamba wao ndio wamiliki halali wa nchi hii.
Tanzania ilifika mahali ambapo huyu askari wa usalama barabarani ambaye Rais ameamua kumpandisha cheo, angekuwa katika hali ngumu sana. Kwanza angetafutiwa zengwe, kisha angehamishwa kituo cha kazi na kupelekwa kijijini huko kwenye kitengo cha kawaida kabisa. Wale aliowaudhi, wangehakikisha kwamba jamaa harudi tena mjini, na anasahaulika kabisa.
Lakini yote hii ni kutokana na ulimbukeni wa kada fulani kudhani wako juu ya sheria na hawatakiwi kuguswa, huku sie akina yakhe tukiendelea kulipa faini halali na wakati mwingine kuadhibiwa na askari mwenye hasira za kutendwa na watu wa aina ya Mke wa Waziri.
Lakini pamoja na taarifa njema hizi tulizozisikia mwishoni mwa wiki, bado tuna safari ndefu sana.  Bado wapo watu wanaodhani wako juu ya sheria, hawatakiwi kuguswa na wanaruhusiwa kufanya chochote wanachojisikia kukifanya kwa kuwa wao ni wao na hawawezi kulinganishwa na Watanzania wengine.
Katika hili, naomba nizungumze na Mheshimiwa Rais na kumweleza maajabu ya Tanzania, ambayo bado hayajaandikwa kwenye Kitabu cha Guinness Book of Records.
Mheshimiwa Rais, hivi unafahamu kwamba kwenye nchi hii mtu akiwa na gari lenye nembo za Serikali, kama vile STK, huwa anavunja tu sheria za barabarani na haulizwi chochote? Ataona watu wote tupo barabarani, tumesimama kwenye foleni, tunasubiri nafasi yetu ifike ili tuendelee na safari, lakini yupo radhi kupita hata njia za pembeni za watembea kwa miguu na hataguswa. Eti ile nembo tu ya STK inamfanya awe juu ya sheria.
Mheshimiwa Rais, wapo pia hawa wengine ambao wanadhani kwamba kutokana na vyeo walivyonavyo, vyeo ambavyo aidha wewe ama watangulizi wao mmewapa, basi hata wakifika maeneo ya huduma za umma, kama vile hospitali, hawahitaji kufuata utaratibu wa kusimama kwenye foleni kama sisi wengine tufanyavyo.  Watafika, watawaona mmesimama, watapitiliza bila kuwasemesha huku wakiwa wamekunja nyuso zao kwa hasira na ukijaribu kuhoji, watakuuliza “unajua mimi ni nani?” Hawa pia wanadhani wako juu ya sheria.
Mheshimiwa Rais, wapo pia wale ambao wanajiona wapo ‘grade’ ya juu zaidi. Hawa hufikia mahala pa kutumia magari ya umma, magari ambayo sisi tunayalipia kodi ili yanunuliwe, yakarabatiwe na yajazwe mafuta, lakini wao kuamua kuyatumia kwa mambo yao binafsi. Magari haya yatakwenda sokoni kununua mchicha na vitunguu, yatapaki saluni kumsubiri ‘mama’ ajiweke vizuri na yatapaki baa kusubiri bosi apate mapumziko ya kutosha, hata kama ni hadi usiku wa manane. Yaani sisi tunakatwa kodi ili wao watumbue maisha, kwani wanadhani kwamba wako juu ya sheria.
Mheshimiwa Rais, wapo na wale ambao hata tukiwa kwenye foleni za benki, basi wao wataingia na kupitiliza ili wahudumiwe kwanza, kana kwamba wengine tuliosimama pale ni milingoti ya TANESCO na hatuna mambo mengine ya kufanya. Ukihoji, utasikia: “kwani wewe hujui mimi ni nani?  Nina mambo muhimu ya kitaifa ya kufanya.” Unabaki unajiuliza, hivi kumbe kuna watu na WATU. Kwa kila kitu, wao wapo juu ya sheria.
Naomba tu niseme kwamba hali hii ilikera kiasi kwamba tukaizoea na ndio maana hata Mke wa Waziri alipotoa maneno yasiyofaa kwa askari wa usalama barabarani, hakuna aliyejua kwamba askari yule angepandishwa cheo na Waziri kuonywa. Sana sana, tulikuwa na uhakika kwamba hili litasambazwa sana kwenye mitandao ya jamii, huku wale wanaotukana askari kwamba wanachokitaka ni rushwa tu, wakiendeleza kauli hizo za kuudhi.
Watu walijiona kwamba wao ndio Watanzania halisi na wengine ni wa kusingiziwa.  Watu walijiona kwamba wao ndiyo pekee wenye haki miliki ya nchi.  Watu walijiona kwamba wao wako juu ya sheria. Mheshimiwa Rais, naomba nikuhakikishie kwamba watu hao bado wapo wengi…


Mfanyabiashara Dangote Atajwa Kutumbuliwa kwa Juliet Kairuki TIC

Wakati aliyekuwa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), ametajwa kutenguliwa uteuzi wake kwa kukataa kuchukua mshahara wa Serikali kwa miaka mitatu mfululizo, uchunguzi umebaini kuwa jipu la kusamehe kodi Kampuni ya Saruji ya Dangote ndilo lililomwondoa.
Uchunguzi uliofanywa umebaini kuwa mbali na Juliet Kairuki kutochukua mshahara wa Sh 5,000,000 kila mwezi aliopangiwa na Serikali kwa miaka mitatu, kwa maana kuwa ameacha kuchukua wastani wa Sh milioni 180 kwa muda huo, anatuhumiwa kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa wawakezaji bila kufuata utaratibu au sheria za nchi.
“Hili la mshahara ni cha mtoto. Amewadanganya wawekezaji wengi kuwa anaweza kuwapa msamaha wa kodi ya VAT, na sasa Serikali hii ilipoingia madarakani ikasema hana mamlaka hayo. Mwekezaji wa kwanza aliyedanganywa ni Dangote,” anasema mtoa taarifa wetu.
Uchunguzi uliofanywa umebaini kuwa Novemba, 2015 Kampuni ya Dangote iliingiza nchini makaa ya mawe tani 35,000 kutoka Afrika Kusini na kutaka makaa haya yasamehewe kodi zote.
“Kwa kweli tulishangaa sana. Kwanza, makaa ya mawe si bidhaa za mtaji (capital) bali ni za matumizi tu (consumables). Vifaa vinavyosamehewa kodi ni zile zinazotumika kuzalisha bidhaa nyingine leo, kesho, mwakani au miaka mitano ijayo na kuendelea, ila makaa ya mawe ukiyachoma yanaisha siku hiyo hiyo, hivyo hii si mtaji.
“Ukiacha hilo, hawa watu wa Dangote wameambiwa wanunue makaa ya mawe kutoka Kiwira au Ngaka, lakini hawataki,” kinasema chanzo chetu na kuongeza kuwa kwa mwaka uliopita, waliagiza tani 2,000 tu za makaa ya mawe kutoka Tancoal kinyume cha makubaliano ya kuongeza ajira nchini.
Afisa kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) amefichua katika uchunguzi huu kuwa kinachoendelea kwenye Kampuni ya Dangote ni balaa. “Hii kampuni tulidhani imekuja hapa kukomboa wananchi, lakini uhalisia siyo.
“Kampuni hii inafanya malipo bila kutoa kodi ya zuio, bidhaa inazoingiza nchini pamoja na nyingine kupata misamaha ya kodi bado inaongeza bei zinakuwa ghali mno kwa maana ya kuongeza gharama za uzalishaji na hivyo kupunguza kiasi cha kodi kinachostahili kulipwa… ni shida,” anasema afisa huyo kwa uchungu.
Kutokana na mkanganyiko huo, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata, ameunda timu ya kufanya ukaguzi maalumu kwa Kampuni ya Dangote ambayo imewakuta na hatia.
“Hiyo bilioni 20 ni uchunguzi wa awali, tunaweza kupata kiasi kikubwa zaidi. Tunawashukuru kwa kuandika habari za ukwepaji kodi, na nakuhakikishia sisi tunafuatilia kila mnachochapisha,” anasema mtoa habari wetu.
Afisa mwingine wa TRA anasema mbinu kubwa inayotumiwa na Dangote na kampuni nyingine ambazo tayari TRA imekwishaibaini mbinu wanazotumia kupunguza faida (Tax Base Erosion), kwa kuingia mikataba yenye gharama kubwa na kampuni walizo na uhusiano nazo kibiashara, kuonesha wametumia gharama kubwa wakati uhalisia wanafanya mbinu za kukwepa kodi.
Akizungumzia sakata hili, Mejena Mkuu Mwandamizi wa Kampuni ya Dangote, Vidya Dixit, amekiri kupokea ankara ya malipo kutoka TRA yenye thamani ya bilioni 20 na akasema: “Wakaguzi wa TRA wako hapa, wamefanya uchunguzi wao, wametuletea madai yao, na sisi tunawasiliana na mshauri wetu wa masuala ya kodi, ikithibitika kuwa tunadaiwa kiasi hicho Dangote ni kampuni kubwa, tutalipa.”
Dixit amesema TRA wamekagua mikataba mbalimbali wanayotumia akina Dangote kuagiza bidhaa na huduma, na wakaja na kiasi hicho, hivyo kwake halioni kama ni tatizo, washauri wao wa masuala ya kodi wakikuta ni kweli watalipa tu. Chanzo chetu kimetueleza kuwa mshauri wao ni Kampuni ya PriceWaterhouseCoopers (PWC) ya Afrika Kusini.
Meneja huyo alijibu pia swali kuwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TRA) inawadai dola 2,867,400 za Marekani (sawa na Sh bilioni 6.3), kwa kusema: “Mimi sisimamii idara ya uhasibu. Madeni hayo yanaweza kuwapo, ila Dangote ni kampuni kubwa, kama kuna madeni ya aina yoyote tutalipa tu baada ya kujiridhisha kuwa ni madeni halali.”
Kuhusu suala la tani 35,000 za makaa ya mawe kutoka Afrika Kusini, alisema wao kama Dangote hawapaswi kulaumiwa kwani walifuata taratibu zote: “TIC walitupa sisi msamaha wa kodi, sasa tumezungumza na Waziri wa Fedha akasema TIC hawana mamlaka ya kutoa msamaha wa kodi bila kutangaza kwenye Gazeti la Serikali (GN) na kweli hakukuwapo GN yoyote.
“Sasa hapa tunapata tabu kidogo, idara moja ya Serikali inasema hivi na idara nyingine inasema vile, tunapata shida kidogo,” anasema Dixit. Katika makaa hayo ya mawe pekee ambayo wanatakiwa kuyanunua kutoka nchini, Dangote wanadaiwa wastani wa Sh bilioni 1.1.
Kuhusu tuhuma zinazoelekezwa kwa kiwanda hicho kuwa kimewageuka wafanyabiashara wadogo na kupendelea wafanyabiashara wakubwa kwa njia ya kuwauzia saruji nyingi na kutowajali wadogo, Dixit anasema wao hawana ubaguzi na ucheleweshaji unaweza kutokea kunapotokea dharura.
Anasema kuna wakati wanaangalia nani ana ghala kubwa la kuhifadhia saruji kiasi gani, ila hiyo haiondoi ukweli kwamba hawabagui yeyote anayetaka kununua na kuuza saruji ya Dangote.
“Ukisema kuna walioshindwa kupata saruji kwa wiki moja au mbili, hilo naweza kukuelewa, lakini miezi miwili, wala asikudanganye mtu. Hilo haliwezekani. Ni kweli kule Lindi tunakotoa chokaa, machimbo yote kwa siku tatu zilizopita yalijaa maji, tukashindwa kupata chokaa, lakini zaidi ya hapo kila mtu anapewa fursa sawa ya kununua saruji bila ubaguzi,” anasema Dixit.
Awali, baadhi ya wafanyabiashara waliilalamikia Kampuni ya Dangote kuwa inauza saruji kwa upendeleo, hali inayowafanya wakose mapato kwani wamekopa mikopo benki na wanaishia kutopata saruji kwa wakati hivyo wanashindwa kulipa hiyo mikopo.
“Kuna mfanyabiashara ameweka kwenye akaunti ya Dangote Sh bilioni 2.5, huyu ndiye anayepewa saruji sisi wengine tunapuuzwa. Watanzania wengi wamekopa benki wastani wa Sh milioni 20, 30 au 50 wanaziweka kwenye kampuni ya Dangote na hawapati hiyo saruji. Hii inatutia hasara mno. Tunataka usawa katika biashara hii,” anasema mmoja wa wafanyabiashara anayedai ameweka Sh milioni 25 kwenye Kampuni ya Dangote, lakini hapatiwi saruji.
Pia, wanalalamikia bei kubwa ya saruji ya Dangote kwani wakati kiwanda kinaanza kujengwa Watanzania walitangaziwa kuwa mfuko mmoja wa saruji ungeuzwa kwa Sh 8,000, lakini sasa bei inafikia Sh 16,000 kwa mikoa kama Mwanza na kwa Dar es Salaam inauzwa kati ya Sh 10,800 na 12,500.
Kamishna Mkuu wa TRA, Kidata, hakuwa tayari kulizungumzia kwa undani suala la Dangote zaidi ya kusema: “Hili suala lipo, tunalifanyia kazi, ni mapema mno kulizungumzia kwa sasa.”
Hata hivyo, afisa mwingine mwandamizi alishangaa kusikia kuwa Dangote bado wanatafuta ushauri wa kisheria kama walipe kodi hiyo au la: “Hawa waliishakwenda hadi kwa Bwana Mkubwa wakakubali kulipa, sasa leo inakuwaje wanatafuta ushauri?” Alihoji afisa huyo.
Alichosema ni kuwa kila mfanyabiashara mkubwa kwa mdogo ajiandae kulipa kodi. “TRA haitaingilia mapato halali ya mfanyabiashara yeyote, ila kwa yeyote anayekwepa kodi hili halitavumiliki. Serikali ya sasa inasema hapa ni kazi tu, hakuna habari ya jina kubwa au dogo. Jipu ni jipu tu, bila kujali ni kubwa au dogo, yote yatakamuliwa tu.”


Wabunge wa UKAWA Wamzomea Profesa Tibaijuka huku Wakimwita Mwizi.......Ni Baada Ya Kupingana na Hoja za Tundu Lissu Aliyedai Zanzibar Ni Koloni La Tanganyika

Mbunge wa Muleba Kusini (CCM), Profesa Anna Tibaijuka jana alikuwa mkali bungeni akisema yeye si mwizi na kuwabeza wanaomuita hivyo kuwa wataisoma namba.
Profesa Tibaijuka alifikia hatua hiyo baada ya kuhamaki kutokana na baadhi ya wabunge wa upinzani kupaza sauti na kumuita mwizi wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria.
Profesa Tibaijuka alianza kwa kuwataka wabunge wamuunge mkono Rais John Magufuli kwa kuwa amechaguliwa na wananchi.
“Wenzetu ambao kazi yao ni kuja kutusimamia sisi (upinzani) wana haki ya kusema wanayoyasema, lakini hata sisi tuna haki ya kuyaweka vizuri ili yaeleweke kwa wananchi,” alisema.
Profesa Tibaijuka alisema upinzani ukifilisika utabaki kukemea kwa sababu ni lazima tu useme kitu, Bunge linageuka kijiwe na bungeni si mahali pa kupeleka hoja za vijiweni.
Kauli hiyo iliwakera wabunge wa upinzani ambao walianza kupaza sauti zao dhidi yake, hali iliyoonekana kumchanganya.
Akirejea hotuba ya msemaji wa kambi ya upinzani bungeni, Tundu Lissu kuwa Tanganyika inainyonya Zanzibar na kuifanya koloni lake, Profesa Tibaijuka alihoji: “Tanganyika inainyonya Zanzibar katika lipi? Hili ni jambo la kujiuliza. Nimejiuliza mimi kama mchumi. Kazi yangu ya kwanza nyinyi mnanijua nilikuwa kwenye shirika la makazi duniani, hamjui kwamba nilikuwa kwenye Shirika la Biashara la Dunia?” alihoji.
Kutokana na zomeazomea kuendelea, Spika wa Bunge, Job Ndugai aliingilia kati: “Waheshimiwa wabunge namlinda mzungumzaji, naomba muwe wavumilivu. Mheshimiwa Profesa endelea."
“Kwa wale wanaosema nimeiba mtaisoma namba, mimi si mtu wa kutishwa na vitu vya ovyoovyo.
"Mimi sitishwi na hoja za ovyoovyo, huyo (mtu) akaisome namba. Nasimama hapa kwa sababu nataka nitetee vitu. Mtu anapopotosha anaweza kuleta hatari. Tanganyika kwa mtizamo wa kiuchumi haiwezi kuinyonya Zanzibar.
“Katika Dunia ya ustaarabu unasikia hoja. Lissu hapa angeweza kuzomewa, lakini wastaarabu wakamsikiliza wamekomaa kisiasa,” alisema huku baadhi ya wabunge wakiendelea kumzomea.
Tibaijuka aliwahi kuwa waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakati wa utawala wa Rais Jakaya Kikwete na aliondolewa baada ya kutuhumiwa kupata mgawo wa fedha za Tegeta Escrow.


Mwita Waitara Azusha Tafrani Bungeni.......Ni Baada ya Kutaka Kumchapa Ngumi Mbunge wa Kasulu Aliyedai Tundu Lissu na Mnyika Ni Vichaa

Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema) ametolewa nje ya Bunge baada ya kutaka kumkwida Mbunge wa Kasulu Vijijini, Agustine Holle (CCM) aliyedai kuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mbunge wa Kibamba, John Mnyika wote wa Chadema kuwa wanaugua kichaa.
Waitara alionesha kukerwa na kauli hiyo hasa pale Holle alipokataa kufuta kauli yake, licha ya kutakiwa kufanya hivyo na Naibu Spika, Dk Tulia Akson.
Wakati Holle akichangia, Waitara alinyanyuka kwenye kiti chake na alipofika alipo mbunge huyo alimzungumzisha maneno ambayo hayakusikika na kuonesha kama kutaka kumpiga kabla ya kukaa kwenye kiti kilicho mbele yake ndipo, Holle alisikika akisema “wewe unataka nini” ndipo Naibu Spika alipogundua kuwa Waitara anataka kumpiga Holle na kumuamuru atoke nje lakini hakutii amri hiyo.
Kutokana na kutotii, Naibu Spika aliamuru askari wamtoe ndipo walipoingia zaidi ya askari watano na kutoka naye hadi nje ya geti kubwa la kuingilia bungeni.
Holle wakati anachangia bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa mwaka wa fedha 2016/2017, alimtaja Lissu ambaye ni Waziri Kivuli wa Wizara hiyo kuwa ana taarifa kuwa Lissu amewahi kuugua ugonjwa wa kichaa na hadi sasa ana faili kwenye Hospitali ya Vichaa ya Mirembe iliyopo mkoani Dodoma.
Hata hivyo, alipopewa nafasi na Naibu Spika kufuta kauli yake akasema “nafuta kauli yangu lakini kwa taarifa zilizozagaa nimeamini ni kweli na mbona kwao(Chadema) wapo wengi hata Mnyika sasa hivi yupo Muhimbili anatibiwa kichaa”.
Kutokana na kauli hiyo, Lissu alisema licha ya kuifahamu Hospitali ya Mirembe, hajawahi hata kuingia kwenye geti la hospitali hiyo wala kuugua ugonjwa huo na kutaka kiti cha Naibu Spika kimtake Holle athibitishe ; na akishindwa kanuni zielekeze hatua za kuchukua kama zilivyowekwa.


Alhamisi, 5 Mei 2016

Wabunge warushiana makonde Afrika Kusini


Wabunge nchini Afrika Kusini wamepigana bungeni baada ya spika kuamuru maafisa wa usalama kuwaondoa kwa lazima wabunge wa upinzani ambao walimbeza rais Jacob Zuma alipoingia bungeni tayari kulihutubia kikao.
Rais Zuma ambaye ameshindwa katika kesi mbili kuu zinazomhusisha na ubadhirifu wa mali ya umma na usimamizi mbaya alikuwa amefika bungeni kwa mara ya kwanza tangu kushindwa mahakamani.
Hata hivyo ujio wake uliwakera sana wabunge wa chama cha upinzani Economic Freedom Fighters (EFF).
Wabunge hao chini ya kiongozi wao Julius Malema walipiga mayowe na kumtupia matusi bw Zuma jambo lililomlazimu spika wa bunge kuamuru wabunge hao wa EFF kuondolewa nje.
Ijumaa iliyopita mahakama ya juu ya Afrika Kusini iliamua kuwa rais Zuma anapaswa kufikishwa kizimbani kufuatia kesi za ufisadi dhidi yake.
Kesi hiyo inahusiana na ufisadi uliotokea katika ununuzi wa silaha zenye thamani ya mabilioni ya dola mwaka wa 1999.
Zuma amekanusha madai yote dhidi yake, Anatarajiwa kukamilisha hatamu yake mwaka wa 2019.
Uamuzi huo wa mahakama ulikuwa msumari wa moto kwa kidonda cha Zuma ambaye mwezi uliopita alipatikana na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka yake alipokaidi amri yakulipa pesa za umma zilizotumiwa kukarabati nyumba yake ya Nkandla.

Kampuni yatozwa Sh118 Bilioni Poda yake Kusababisha Saratani

Poda ya Johnson, iliyodhaniwa kuwa ni kipodozi na tiba mujarabu kwa watoto na watu wazima duniani kote imebainika kusababisha saratani.
Jana, Mahakama ya St Louis ya Marekani, iliiamuru kampuni inayotengeneza poda hizo, Johnson & Johnson kumlipa Deane Berg wa Sioux Falls, South Dakota, Dola za Marekani 55 milioni (Sh118 bilioni ) baada ya kujiridhisha kuwa kipodozi hicho kilimsababishia saratani ya mayai ya uzazi (ovarian cancer).
Mpaka sasa, zaidi ya wanawake 1,000 wameshafungua kesi kuishtaki kampuni hiyo kwa madai ya kuwasababishia saratani hiyo baada ya kutumia poda ya Johnson kwa miaka mingi.
Ofisa Uhusiano wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania, (TFDA), Gaudensia Simwanza alisema wanazo taarifa juu ya madhara ya poda hizo ingawa bado hawajathibitisha kitaalamu kwa poda zilizopo nchini.
Alisema TFDA ilishafanya uchunguzi wa kimaabara kuhusu poda hizo lakini haikuona madhara yoyote.
Simwanza alisema FDA ilitakiwa pia kuwapa taarifa watumiaji wa bidhaa hizo duniani kuhusu madhara ya poda hizo.
Mwaka 2013, Berg alikuwa mwanamke wa kwanza kuishtaki kampuni hiyo baada ya kugundulika na saratani.
Baada ya kuridhishwa na malalamiko ya Berg, Mahakama iliamuru kampuni ya Johnson & Johnson kutoa onyo kuwa poda hizo, Johnson Baby Powder na sabuni ya Shower to Shower, zinasababisha saratani. Hata hivyo, kampuni hiyo haikufanya hivyo.
Baada ya mwaka mmoja, Berg alifungua tena kesi hiyo na Mahakama iliamuru alipwe kiasi hicho cha fedha.
Daktari wa Hospitali ya Wanawake, Brigham, Daniel Cramer alitoa ushahidi mbele ya Mahakama na kueleza kuwa zaidi ya wanawake 10,000 wamegundulika kuwa na saratani ya mayai ya uzazi kwenye hospitali hiyo.
Kadhalika, wanawake hao walibainika kuwa na chembechembe za ‘talcum’ kwenye kizazi.
Daktari wa Saratani wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Herry Tungaraza alisema kuna uwezekano wa kemikali ya ‘talcum’ kupenya kwenye ngozi, hadi kwenye damu na kuingia kwenye mayai ya uzazi na kisha kusababisha saratani.
Alisema si lazima poda hizi zimuathiri mtu kwa kuzitumia sehemu za siri tu, hata kama akizitumia kwa kupaka usoni, zinaweza kusafiri na kuathiri mayai ya uzazi. “Kama ingekuwa zinadhuru kwa kuzipaka sehemu za siri tu, basi zingeathiri zaidi shingo ya kizazi au nyumba ya uzazi, lakini mayai yapo mbali na ndiyo yaliyoathiriwa na saratani,” alisema.
Shahidi mwingine wa katika kesi ya Berg alithibitisha kuwa aliona chembechembe za ‘talcum kwenye uvimbe ulioko kwenye mayai ya Berg.
Mwathirika mwingine
Mei mwaka jana, Gloria Ristesund (62), alifungua kesi dhidi ya Johnson & Johnson kwa kushindwa kuwaonya wateja wake kuhusu poda hiyo kusababisha saratani.
Ristesund aligundulika na saratani, mwaka 2011 baada ya kutumia poda hiyo kwa kuipaka sehemu za siri kwa miaka kadhaa hasa. Mahakama iliamuru Ristesund pia kulipwa Dola 55 milioni.
Tovuti ya CNN inaeleza kuwa utafiti kuhusu kemikali za ‘talcum’ kusababisha saratani ulitolewa miaka mingi nyuma lakini Johnson & Johnson hawakutaka kuweka wazi ukweli huo kwa wateja wao.
“Ni kama kampuni zinazotengeneza sigara, wanajua kuwa imeshathibitishwa kuwa uvutaji wa sigara unasababisha saratani ya mapafu lakini wanauficha umma kuhusu hili,” ilisema taarifa ya CNN.


P Diddy Aongoza Orodha ya Forbes ya Wana Hip Hop Watano Wenye Mkwanja zaidi


Forbes wametoa orodha mpya ya wasanii wa hip hop wenye fedha zaidi, The Forbes Five.
Diddy ameongoza orodha hiyo mwaka huu kwa kuwa na utajiri ufikao dola milioni 750. Nafasi ya pili imekamatwa na Dr Dre mwenye dola milioni 710 huku Jay Z akifuatia kwa dola milioni 610.
Mwanzilishi wa Cash Money, Birdman amefuatia katika nafasi ya nne akiwa na dola milioni 110. Drake amechukua nafasi ya 50 Cent na kukamata nafasi ya tano kwa utajiri wa dola milioni 60.


Majibu ya Snura baada ya Chura wake Kupigwa Nyundo na Serikali

Baada ya wizara ya habari, utamaduni, sanaa na michezo kuufungia wimbo wa Snura, Chura jana, muimbaji huyo anaonesha kutoshtushwa na hatua hiyo hasa kutokana na support anaiyopata kutoka kwa mashabiki wake.
Kwa ufupi haoneshi stress, walau kwa kile alichokiandika kwenye Instagram. “Ingekua ndio hela leo ningekua bilionea lo!!! Nawapenda sana kwakweli na nawatakia usiku mwema,” aliandika Snura kwenye Instagram.
Aliongeza hashtag: #utaipenda2_ndimuimekolea_malimao_kama__210_habarizetuwanazo_ilazaohatuna.”
Pamoja na wimbo huo kufungiwa kuchezwa kwenye redio na TV, Snura aliagizwa kuhakikisha amefuta video zake zote mtandaoni.


Jumatano, 4 Mei 2016

IMF: Uchumi wa Tanzania waongoza Afrika Mashariki

Tanzania inatarajiwa kusajili kiwango cha juu zaidi cha ukuaji wa uchumi wake mwaka huu katika kanda ya Afrika Mashariki na kati.
Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la fedha la kimataifa - IMF.
Katika ripoti yake iliyotolewa hii leo Tanzania inatarajiwa kusajili kiwango cha juu cha ukuaji wa uchumi wake wa asilimia 6.9% mwaka wa 2016.
Kasi hiyo ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania ni ya pili tu nyuma ya Ivory Coast baina ya mataifa ya Kusini mwa jangwa la Sahara .
Tanzania inatarajiwa kusajili kiwango cha juu cha ukuaji wa uchumi wake wa asilimia 6.9% mwaka wa 2016.
Ivory Coast inatarajiwa kukuwa kwa kasi ya asilimia 8.5%.
Katika kanda ya Afrika Mashariki ,uchumi wa Kenya ndio wa pili kwa kasi ya ukuaji kwa asilimia 6%.
IMF hata hivyo inasema kuwa kasi ya ukuaji wa uchumi kusini mwa jangwa la Sahara unatarajiwa kupungua kwa mwaka wa pili mfululizo kutokana na kudorora kwa viwango vya uzalishaji na hivyo uwekezaji.
Kwa mujibu wa shirika la fedha la kimataifa - IMF, eneo hilo linakadiria kushuka kwa ukuwaji wa uchumi kwa asilimia 3 mwaka huu.
Kiwango hicho ni cha chini kabisa kuwahi kushuhudiwa katika miaka 15.
Mataifa yanayotegemea mapato yanayotokana na mafuta ndiyo yalioathirika zaidi kama vile Nigeria na Angola.
Mataifa yanayotegemea mapato yanayotokana na mafuta ndiyo yalioathirika zaidi kama vile Nigeria na Angola.
Aidha Zambia pia imeathirika vibaya kutokana na ukosefu wa soko la kimataifa la shaba yake.
Ripoti hiyo inaitaja Afrika Kusini kama moja ya mataifa ambayo kiwango chake cha ukuaji kimedorora kwa kiasi kikubwa mno.
Katika orodha ya mataifa yanayotarajiwa kuwa na kiwango cha juu cha ukuaji Kusini mwa jangwa la sahara Ivory Coast ndio inayoongoza.
Orodha ya mataifa ya kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara na viwango vya kasi ya ukuaji wa uchumi 2016.
Ivory Coast 8.5%
Tanzania 6.9%
Senegal 6.6%
Kenya 6%
Zambia 3.4%
Nigeria 2.3%
Afrika Kusini 0.6%

JISNI YA KUMTAMBUA ASIYE NA MAPENZI YA KWELI

Inawezekana upo katika uhusiano na tapeli wa mapenzi bila kujua, hiyo ni sumu na unachotakiwa kufanya sasa ni kuanza kumchunguza mpenzi wako mapema usije ukawa miongoni mwa walio katika foleni!
Hakuna kitu kibaya kama kuwa katika foleni ya wapenzi kwa mpenzi mmoja, tena mbaya zaidi awe ni yule ambaye moyo wako umempenda kwa dhati.
Kumbuka, kuwa katika uhusiano na mtu ambaye haeleweki ni sawa na kukaribisha matatizo katika maisha yako, huna sababu ya kuishi kwa wasiwasi ukiwa hujui mpenzi wako anakuchukulia vipi.
Anza kumuwekea mitego mapema. Lakini katika mitego yako achana na simu yake kabisa, huna sababu ya kuchunguza simu yake lakini kama ni msaliti utajua tu, unafikiri atajificha mpaka lini?
UTAMJUAJE MPENZI LAGHAI?
Hapa ndipo kwenye kazi, kwa bahati mbaya sana kama ikitokea ukampenda mtu sana hata kama akifanya mabaya kiasi gani unaweza usiyaone, kama wewe ni wa aina hii unapaswa kubadilika kifikra. Muone wa kawaida, fanya uchunguzi wako polepole na kama ukiona moja kati ya mambo yafuatayo, ujue kuna kitu.
(a) Hataki ujulikane na rafiki zake
Hii ni kati ya alama walizonazo matapeli wa mapenzi, ni mtu wa kufanya mambo kwa upekee sana. Kila dakika hakaukiwi na neno nakupenda sana, lakini moyoni mwake hakuna alama hata moja ya mapenzi kwako.
Ni vigumu kumtambua mtu wa aina hii lakini chunguza kuhusu hili, hapendi kabisa kukukutanisha na rafiki zake na hata mkikutana nao kwa bahati mbaya basi hatakutambulisha na kama akikutambulisha hatakutambulisha kama mpenzi wake rasmi. Ataishia kusema ninyi ni marafiki mlioshibana!
Tangu lini mpenzi akatambulishwa kama rafiki? Mtu anapomtambulisha mpenzi wake humtambulisha kwa kujisikia furaha moyoni kwamba anamtambulisha mpenzi wake lakini inakuwaje kwako akutambulishe kama rafiki?
(b) Msiri kupitiliza
Hii ni alama nyingine waliyonayo wanaume wa aina ninayoielezea katika mada hii. Siku zote mambo yake ni kwa siri kubwa, kama mna ahadi ya kukutana, hataki muongozane, atakuambia mkutane moja kwa moja sehemu husika. Hata muda wa kuondoka atafanya kila njia ili kila mmoja aondoke mwenyewe na kama mkiondoka pamoja basi ujue ni usiku na hakuna atakayewaona.
Ikitokea akakubali kuongozana na wewe, hatapenda muongozane pamoja. Atalazimisha utangulie mbele yeye afuate nyuma, kwa nini? kwa sababu anaogopa kujulikana kuwa yeye ni mpenzi wako na kama anaogopa anakupenda kweli? Mapenzi gani hayo yanafanywa kwa siri? anakupotezea muda huyo.
(c) Hapendi ndugu wafahamiane
Mpenzi wa aina hii ni mjanja sana, kwanza kabisa atajifanya mtu mwenye ‘ubize’ sana, yote hii ni kukwepa kuwajua ndugu zako au wewe kuwajua ndugu zake! Wakati mwingine anakuwa hapendi ndugu zako na wake wakutane wakijua wazi kuwa nyie mna uhusiano, hili ni tatizo.

SUMAYE:NASHANGAA KWA NINI RAIS MAGUFULI ANAPENDA SIFA

FREDERICK Sumaye, Waziri Mkuu Mstaafu ameeleza kushangazwa na Serikali ya Rais John Magufuli kupenda kusifiwa zaidi na kuchukia kukosolewa,
Sumaye bila kumtaja jina Rais Magufuli ameleza kushangazwa na hatua ya serikali kuminya uhuru wa habari na kwamba, kufanya hivyo kunalenga kuficha madudu yanayofanywa na watendaji wake.
“Wapowatawala ambao hawapendi kusemwa lakini wanapenda sana kusifiwa. Kiongozi mwenye tabia ya udikteta hataki kusikia kingine zaidi ya sifa zake tu.
“Huyo ni mtu hatari na katika nchi ya namna hiyo hakuna uhuru wa habari wala uhuru wa kutoa maoni kwa woga wa kupotezwa kusikojulikana,” amesema Sumaye.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyoratibiwa na Chama cha Waandishi wa Habri za Siasa (TAPOREA), Sumaye amesema, serikali inakiuka Katiba ya nchi.
Amesema, serikali yoyote inayopambana na vyombo vya habari na kuminya uhuru wa kufanya kazi zao huwa ina tatizo kwa upande wa wanaotawala.

POLISI MATATANI KWA KUOMBA RUSHWA YA MILIONI 7

POLISI mkoani Rukwa inawashikilia askari wake wawili wa Kituo Kikuu cha Polisi wilayani Nkasi, wakituhumiwa kuomba na kupokea rushwa ya zaidi ya Sh milioni 7.2 wamsaidie mtuhumiwa.
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Rukwa, Leonce Rwegasira alitaja askari hao kuwa ni Konstebo Filbert Ruhemeja na Konstebo Bahati Sengerema, ambao walikuwa wakifanya kazi katika Kituo cha Polisi mjini Namanyere wilayani Nkasi.
Alisema polisi inawafanyia uchunguzi wa kina askari wake wawili, wanaotuhumiwa kwa kashfa ya kuomba rushwa ya Sh milioni 7.2 na iwapo watabainika halitasita kuwatimua na kuwafikisha mahakamani.
.Alisema askari hao wawili wa polisi, wanatuhumiwa kuomba na kupokea rushwa ya fedha kutoka kwa mtu mmoja (jina linahifadhiwa) ili wamsaidie katika shitaka linalomkabili.

Pichaz: Mabusu ya Gigy Money kwa Idris Zawatoa Povu Mashabiki wa Wema Sepetu

Picha zinazomuonesha Gigy Money wakati akimpiga mabusu Idris Sultan wakiwa katika show ya Pool Party iliyofanyika Ijumaa iliyopita katika hotel ya Regency Park jijini Dar es salaam, zinawatoa povu mashabiki wa Wema Sepetu.
Picha hizo ziliibua hisia tofauti kwa mashabiki wa Wema Sepetu na kuanza kumshambulia Gigy. Haya ni maadhi ya maoni ya mashabiki hao.
Izack_da_real
Wee kilasiku wakudandia vya watu? Embu kua mbunifu tafuta wako @gigy_money
Jessy_jay_jacob
Mmmmmh unavyo ji sex sisha kwa @idrissultan kisa kashikilia icho kiuno  umeshia kupata manukato yake tu hapo
Aishafadhir
Jmn wa2 mnajua kukuza vtu khaaa….pic tu mnatoa maneno yote hayo jmn waachen binadamu wenzenu waish maisha yao jmn mnakera kwakwel…..idrs akpga pic na grl s bas wanamahusiano ?wema akpga pic n boys bas wanamahusiano ?2seme nyie hamna urafik na tofaut ya jnsia zenu? Huyu mdada akpost pic na mtu yeyote anatafuta kiki? Kwan yy n nan na idris n nan? Wote wanajuana na ndomana wakajselfiiiii …..Jmn hebu fanyen yenu mnachosha kila sku kuingilia mapenz yawa2 yenu huko yanawashnda
Katoto_lee
Muacheee umalayaa, we na dada yakoo Anaomba kupiga pichaa alafuuu anaanza kujiproud katokaa naeeeeyaaniii gig ni chefuuuuuuuuu
vivian
Shingo alivyolinyoosha ilimlad tu atafte kiki jaman kweli gigy money gigy elf20 shikamoo ney wa mitego
Pinkylioussalvado
Ahahaha,,shikamoo ney wa mitego(dem ana xura mbaya ila ana bonge LA tak

Jumanne, 3 Mei 2016

WASOMI WAKOSOA ASILIMIA 2% YA KODI ALIYOPUNGUZA RAIS MAGUFULI

Siku moja baada ya Rais Magufuli kushusha Kodi ya Mapato ya Mshahara ( Pay as you Earn – PAYE ) kutoka asilimia 11 iliyopo sasa hadi asilimia 9. Wataalamu wa uchumi nchini wamelipokea katika mtazamo tofauti
Mtaalamu wa Uchumi ambaye ni Msimamizi Fedha wa Kampuni ya Clouds Media Issa Masoud katika mahojiano yake na
mtembezi.com ameanza kwa kusema
“Sipingani na wengi waliosema kwamba punguzo la kodi ya mshahara kutoka 11% mpaka 9% (2%) ni kidogo sana ukilinganisha na gharama za maisha. Kwa misingi ya kwamba bado Watanzania wengi wanaofanyakazi wanawajibika kugharamia haya..
1. Afya
2. Makazi (kupanga na gharama za vifaa vya ujenzi)
3. Usafiri
4. Elimu- ingawa elimu inatolewa bure lakini bado ubora wake upo chini ukilinganisha na shule binafsi matokeo yake watu wengi watoto wao wanasoma shule binafsi tofauti na zamani.
4. Habari -mifumo yote ya kupata habari sasa hivi ni ya kulipia.
5. Huduma nyingine za jamii n.k
Kwa hiyo serikali ingejikita sana kwenye kurahisisha hayo mambo hapo juu ili kumsaidia huyu mwananchi wa chini.
Ingawa kwa upande mwengine, bado nchi nyingi duniani zinategemea kodi ya mishahara kama moja ya chanzo cha kueleweka cha mapato ya serikali, hata zile zenye mishahara mikubwa kama Ufaransa, Australia, Austria, German nk. wao kodi zao za mishahara zinafika mpaka 49.8%, kwa maana ya kwamba nusu nzima ya mshahara wako unarudi kama kodi.
Kwa hiyo kwa Tanzania punguzo la 2% kwenye idadi ya wafanyakazi zaidi ya milioni 15,000,000 kwa mujibu wa sensa ya 2012 (Serikalini na Binafsi) kwa kiasi cha Tsh. 3,800 ni jumla ya Tsh. 57 bilioni kwa mwezi serikali imejipunguzia kutoka kwenye mapato yake kwa mwezi, kwa hiyo kwa mwaka ni sawa na punguzo la pato la serikali kwa takribani zaidi ya shilingi bilioni 600 za Kitanzania.
Mapendekezo yangu ni kwamba serikali iangalie zaidi kwenye gharama za maisha sababu punguzo hilo ni kubwa sana serikalini ila ni dogo sana kwa mtu binafsi. Wananchi wasaidiwe kupunguza gharama ya vitu tajwa hapo juu. Ikiwemo ujenzi wa nyumba bora na nafuu kwa kuwapangisha au kuwauzia wafanyakazi.
Na serikali izidi kubuni vyanzo vingine vya mapato tofauti na kodi ya mshahara na kuhakikisha vilivyopo vinalipa kodi ipasavyo”
Kwa upande wake Mtaalamu na Mshauri wa Uchumi Malembo Lucas Elias kutoka Taasisi ya Umoja wa Maendeleo ya Afrika (ADA) licha ya kuunga mkono lakini amebainisha kuwa serikali inapashwa kuzingatia zaidi kasi ya maisha kwa kulinganisha kasi ya uzalishaji ili punguzo hilo liweze kuwa na tija kwa watumishi katika suala la chakula, malazi na mavazi.

PROF MUHONGO: TATIZO LA UMEME KUISHA MWAKA HUU MWEZI SEPTEMBA

SERIKALI inatarajia kuzindua mradi mkubwa wa kuboresha miundombinu ya kusafirisha umeme Septemba mwaka huu, utakaomaliza tatizo la umeme kukatika.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alisema kwa sasa miundombinu ya kusafirishia umeme ni midogo na katika kuboresha hilo, kuna mradi mkubwa utazinduliwa Septemba mwaka huu wa kusafirisha umeme.
Alisema mradi huo ni wa kusafirisha umeme kutoka kilovoti 220 hadi 400 kutoka Dar es Salaam-Tanga hadi Arusha na Iringa-Dodoma-Shinyanga, hivyo tatizo la kukatika umeme litatatuliwa.
Waziri huyo alitoa maelezo hayo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Korogwe Mjini, Mary Chatanda (CCM) aliyetaka kufahamu lini umeme utakoma kukatika wilayani Korogwe.
Akielezea hilo, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani alisema Serikali inafanya marekebisho ya transfoma na chanzo cha umeme cha Hale mkoani Tanga ili kumaliza tatizo la kukatika umeme mara kwa mara wilayani Korogwe na mkoani Tanga kiujumla.

ITALIA WAJA NA UTAALAMU WA KUPANDIKIZA KICHWA KWA MTU

Mtaalam wa upasuaji wa mfumo wa neva (neurosurgeon) Sergio Canavero kutoka nchini Italia, anakusudia kufanya jaribio la kwanza la kupandikiza kichwa cha binadamu kwenye mwili wa binadamu mwingine, ifikapo mwakani.
Wataalam wengi wa upasuaji wanafikiria wazo hilo ni la kiuwendawazimu, lakini sio kwa mtaalamu huyo, kwani anasema bado anapanga kujaribu pandikizo la kwanza la kichwa kwa binaadamu. (Head Transplant)
Dk. Canavero ambaye mpaka sasa ameshapata mtu wa kujitolea kufanya zoezi hilo, kijana mwenye asili ya Urusi ambaye ni mtaalam wa software Valery Spiridonov, ambaye ana tatizo la kupoteza nguvu kwa misuli yake ya mwili.
Dk. Canavero amesema mafanikio yake yameonesha kuwa mpango wake wa kupandikiza kichwa cha binadamu kwa mwili wa mtoaji (donor) bado upo, na ataanza mpango huo mwishoni mwa mwaka 2017 na unaweza kuwa njia ya kutibu waliopooza mwili.
“Ningesema tuna takwimu nyingi zinaendelea, ni muhimu kwa watu kuacha kufikiria jambo hili sio rahisi, hii inawezekana kabisa na tunaendelea kulifanyia kazi”, alisikika Dk, Canavero akimwambia mwanasayansi mchanga.
Timu iliyo nyuma ya kazi hiyo ilipost video ikimuonesha nyani ambaye alifanyiwa upandikizwaji huo, na kufanikiwa kutembea baada ya uti wa mgongo kutenganishwa na kuunganishwa tena’
Chanzo:mtembezi

VYAKULA VINAVYO ONGEZA HISIA KATIKA MAPENZI

Kama kawaida mara nyingi chakula ambacho kimeungwa pilipili hufanya hata mapigo ya moyo kuwa tofauti na wakati mwingine hata jasho kutoka au kamasi.
Kwenye pilipili kuna kitu kinaitwa Capsaicin ambacho hufanya pilipili iwe na hali ya ukali ambao huwezesha ubongo kutoa homoni ya Endorphins ambayo katika hali ya juu huleta mgusu wa hisia za raha.
MATUNDA NA MBOGA ZA MAJANI.
Mlo wenye matunda na mboga za majani una matokeo makubwa sana katika hamu ya tendo la ndoa kwa njia nyingi, kwani matunda na mboga za majani hupunguza kiwango cha mafuta na unene (Cholesterol), kuongezeka kwa mafuta mwilini huzuia mzunguko wa damu kwa kubana mishipa ya damu.
Pia wanandoa wanapozidi kunenepa ndipo na hali ya kufurahia au kutaka au hamu ya tendo la ndoa huzidi kupungua.
NAFAKA
Nafaka zina nyuzinyuzi (Fibre) na sukari ngumu (Complex Sugar) ambazo kusaidia kutunza uzito wa mwili, hivyo nafaka husaidia katika kuzalisha homoni za testosterone kwenye damu.
Na pia nafaka huwezesha mtu kuwa na nguvu hatimaye kwenda masafa marefu wakati wa tendo.
TANGAWIZI
Tangawizi ni kiungo ambacho husisimua sana mfumo wa mzunguko wa damu mwilini, na tangawizi zinajulikana sana kwa kusukuma damu kwenda sehemu za viungo vya uzazi yaani uke na uume, Inaweza kuliwa mbichi, au kupikwa na kuwa kama unga.
ASALI
Asali ina madini yanayoitwa Boron, ambayo husaidia mwili kutumia homoni ya Estrogen ambayo ni homoni inayohusika na viungo ya uzazi na mapenzi kwa mwanamke.
Pia kuna utafiti unaoonesha kwamba asali huongeza nguvu, kitendo ambacho kitapelekea mwanamke kuwa uwezo na hamu ya tendo la ndoa.
KARANGA
Karanga huhusika moja kwa moja na kutunza mfumo wa mzunguko wa damu kuwa na afya (Vascular System).
Pia mfumo wenye afya (mzunguko wa damu) katika uke na uume huwezesha mwanaume na mwanamke kupata msisimko wa mapenzi haraka hatimaye tendo la ndoa kuwa zuri, karanga zina madini muhimu kama vile Magnesium, asidi ya folic na zinc ambayo ni muhimu sana katika usalishaji wa mbegu za mwanaume.
CHOCOLATE
Chocolate ina phenylethylamine, kemikali ambayo husababisha hisia (feelings) za furaha wakati wa mwanamke au mwanaume kufika kileleni.

Siri Kuu Kuhusu Escrow zafichuka

SIRI kuu ya James Rugemalira, kumwaga mabilioni ya shilingi kwa baadhi ya majaji wa mahakama kuu, viongozi waandamizi serikalini na madhehebu ya kidini, wabunge na viogogo wa Ikulu, zimeanza kufumuka.
Nyaraka mikononi mwa gazeti hili zinaonesha zaidi ya asilimia 90 ya wale waliopewa fedha na Rugemalira, ni wale waliomsaidia “kufanikisha ukwapuaji wa zaidi ya Sh. 324 bilioni kutoka Benki Kuu (BoT) na kujinasua katika mikono ya sheria.”
“Rugemalira alishika kila mmoja. Kuanzia Ikulu ya Jakaya Kikwete, TAKUKURU, mahakama, BoT, hazina, ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali, viongozi wa madhehebu ya kidini na hata baadhi ya mawaziri wa zamani wenye ushawishi serikalini,” ameeleza kiongozi mmoja mwandamizi kutoka Ikulu.
Amesema, “…fedha katika akaunti ya Escrow zilihusisha mtandao mpana ulioratibiwa na Rugemalira na Harbinder Sigh Seth (Singasinga).”
Majaji wa mahakama kuu, Aloycious Mujulizi na Eudeus Ruhangisa, ni miongoni mwa waliokuwa na mawasiliano ya mara kwa mara na Rugemalira; na walikuwa washauri wake wakuu wa kisheria.
Mawasiliano kati ya Jaji Mujulizi na Jaji Ruhangisa yalifanyika kupitia kwa Rugemalira mwenywe na katika eneo jingine kupitia kwa mkewe, Benedicta.
Jaji Mujulizi na Jaji Ruhangisa walitajwa bungeni na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), kuwa miongoni mwa vigogo waliopewa mgawo wa fedha hizo na Rugemalira.
Bunge liliagiza majaji hao wachunguzwe na wachukuliwe hatua za kinidhamu na kisheria.
Hadi sasa, hakuna taarifa zozote kuwa majaji walichunguzwa na kuchukuliwa hatua.
Rugemalira alikuwa akimiliki asilimia 30 ya hisa katika kampuni ya kigeni ya IPTL kupitia kampuni yake ya VIP Engineering and Marketing Limited.
Jaji Mujulizi na Ruhangisa walilipwa na Rugemalira kila mmoja Sh. 404 milioni.
Mabilioni ya shilingi yaliyohifadhiwa katika akaunti ya Escrow yalikwapuliwa na Harbinder Sigh Seth, aliyejiita mmiliki wa IPTL kwa msaada mkubwa wa Rugemalira na kile kilichoitwa, “amri ya mahakama.”
Seth alidai kumiliki IPTL kupitia kampuni yake ya Pan African Power Tanzania Limited (PAP).
MwanaHALISI linaweza kuthibitisha kuwa kati ya tarehe 13 na 26 Novemba 2014, kilikuwa kipindi ambacho Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), ilimhoji Rugemalira juu ya ukwapuaji wa fedha katika akaunti ya Escrow.
Aidha, ni katika kipindi hichohicho, Rugemalira alikuwa na mawasiliano ya mara kwa mara na Jaji Mujulizi na Ruhangisa.
Wengine waliokuwa na mawasiliano na Rugemalira katika kipindi hicho, ni waziri wa nishati na madini, Prof. Sospeter Muhongo; aliyekuwa waziri wa mambo ya nje na uhusiano wa kimataifa, Bernard Membe na aliyekuwa katibu mkuu wa wizara hiyo, Eliakimu Maswi.
Aliyepata kuwa waziri wa utawala bora, Mathias Chakawe; aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU, Edward Hoseah; aliyekuwa mwanasheria mkuu wa serikali (AG), Frederick Werema na aliyekuwa waziri wa viwanda na biashara, Dk. Abdallah Kigoda, walikuwa pia na mawasiliano na Rugelalira.
Wengine ni naibu gavana wa BoT, Dk. Enos Bukuku; aliyekuwa Mnikulu Mkuu wa Ikulu, Shaban Gurumo; aliyekuwa Kamishna mkuu mamlaka ya mapato (TRA), Rished Bade na aliyekuwa mwanasheria mkuu wa serikali wakati wa ujio wa IPTL nchini (1994), Andrew Chenge.
Orodha ya waliokuwa katika mawasiliano na Rugemalira inahusisha pia mawaziri wa zamani, Paul Kimiti na Wilson Masilingi; aliyekuwa mhariri mtendaji wa magazeti ya serikali – Daily News na Habari Leo – Gabriel Nderumaki; aliyewahi kuwa waziri wa nishati na madini, Wiliam Ngeleja na mkurugenzi wa kampuni ya G and S Consultancy Limited, Dk. Gideon Shoo.
Wengine ni aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Kagera, Kanali mstaafu Constantine Massawe; Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Methodius Kilain; Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Eusebius Nzigilwa na aliyekuwa waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi, Prof. Anna Tibaijuka.
Prof. Tibaijuka alikiri kupokea kiasi cha Sh. 1.6 bilioni kutoka kwa Rugemalira. Hata hivyo, alisema kuwa fedha ambazo alipokea zilikuwa ni mchango wa shule yake ya Barbro Johanssen ya jijini Dar es Salaam na Kajumulo Girls High School iliyoko Bukoba.
Kwa mujibu wa taarifa, Dk. Hoseah alimruhusu Rugemalira kutafuta msaada popote pale, ikiwa ni pamoja na nje ya nchi na kwamba ofisi yake “ingetoa maofisa kumsaidia.”
“Kama una jambo la msingi kufanya nje ya nchi, una baraka zangu zote. Watakapohitajika maofisa wa TAKUKURU kwa ufafanuzi, wako tayari kukusaidia pale uliko,” anaeleza Dk. Hoseah na Rugemalira andishi lake la 16 Novemba 2014.
Dk. Hoseah anamaliza kwa kumueleza Rugemalira, “…nakutakia kila la kheri.”
Rugemalira alikuwa anaomba TAKUKURU kuingilia kati kile kinachoitwa, “mgogoro wa hisa kati ya IPTL na Benki ya Standard Chartered (SCB) ya Uingereza.”
Hata hivyo, Rugemalira anaonywa na Masilingi, ambaye wakati huo alikuwa balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, kuwa mwangalifu na mtulivu wakati suala hilo linaendelea.
Alisema, “mimi nikiwa mwanasheria, ninakushauri wewe na kampuni yako kushirikiana kwa ukamilifu na TAKUKURU. Suala la IPTL ni gumu. Limekuwa na mchanganyiko mkubwa. Akili nyingine haziwezi kulielewa.”
Masilingi anasema, “…nimebaini kwamba TAKUKURU ndio wanaolichukulia suala hilo kwa usiri mkubwa katika hatua za uchunguzi na wenyewe wanaweza kukusaidia kupata hukumu iliyo ya haki.”
Benki ya Standard Chartered ilikuwa inadai na mpaka sasa bado inadai kuwa mitambo ya kuzalisha umeme ya IPTL na fedha zilizopo kwenye akaunti ya Escrow, ni mali yake.
Inadai kuwa kampuni ya MECHMAR ya Malasia ilishindwa kurejesha mkopo iliochukua benki na kwamba hilo ni jambo linalosababisha mitambo ya IPTL iliyopo Tegeta Salasala, jijini Dar es Salaam, kuwa mali yake.
Akihutubia taifa kupitia wazee wa mkoa wa Dar es Salaam, wiki tatu baada ya Bunge kuagiza waliohusika katika wizi wa fedha za Escrow wachukuliwe hatua, aliyekuwa Rais wa Jamhuri, Jakaya Mrisho Kikwete alikiri kuwapo udanganyifu katika kufikia utoaji wa fedha hizo.
Alikiri baadhi ya nyaraka kughushiwa. Akakiri kuwa kampuni ya PAP imekwepa kodi ya serikali na kudai kuwa serikali yake bado inaendelea kuitafuta kampuni ya MECHMAR iliyodaiwa kuuza asimia 70 ya hisa zake ndani ya IPTL.
Rais alikiri kuwa aliyepewa fedha na serikali – PAP – hakuwa na sifa; serikali yake haikufanya uchunguzi yakinifu kuhusu historia, uhalali, sifa na uwezo wa kampuni ya PAP katika uwekezaji wa umeme, ununuzi wa mitambo na mtaji.
Naye mwanasheria wa Rugemalira, Camilo Schutte, katika barua aliyomwandikia Rugemalira, anasema “…baada ya kusoma ushauri wa Masilingi juu ya msaada wa TAKUKURU, itakuwa busara kuomba TAKUKURU kusubiri hukumu kati ya Standard Chartered na IPTL.”
Anasema kampuni ya Rugemalira (VIP) “…inapaswa kuomba TAKUKURU kufanya uchunguzi juu ya sera ya benki ya Standard Chartered kuhusu ununuzi wa madeni ambayo mchakato wake unaweza kuwa na rushwa.”
Camilo Schutte anamueleza Rugemalira katika barua yake hiyo na ambayo imenakiriwa kwa majaji, mawaziri, kiongozi wa TAKUKURU, maofisa wa Ikulu na watu wengine kuwa, “…tatizo la benki ya Standard Chartered, kama zilivyo taasisi nyingine, ni kufanya biashara ili kujipatia faida kubwa.”
Akiandika kwa Dk. Gideon Shoo, mwanasheria wa Rugemalira (Camilo Schutte) anaelekeza kufanyika mambo matatu kwa haraka.
Kwanza kutafuta, kwa “gharama yoyote ile,” watu wote wenye ushawishi mkubwa kwenye jamii ambao wanapigia kelele ukwapuaji wa fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow.
Miongoni mwa waliotajwa, ni Zitto Kabwe, mbunge wa sasa wa Kigoma Mjini; David Kafulila, ambaye alikuwa mbunge wa Kigoma Kusini; Balozi wa Uingereza nchini, Dianna Melrose; Wilson Masilingi na balozi wa Finland nchini.
Pili, Camilo Schutte anasema, ni sharti mtandao wao ujiridhishe ikiwa watu wanaolizungumzia jambo hilo wanalifahamu kwa undani au wanalijua nusunusu au hawalijui kabisa.
Kwa maoni ya mwanasheria wa Rugemalira, wabunge waliokuwa wameshupalia jambo hilo walikuwa hawana taarifa zozote muhimu kuhusu suala hilo.
Tatu, mwanasheria alimtaka Dk. Shoo kuangalia athari za taarifa zilizosambazwa juu ya ukwapuaji wa fedha hizo, kwa kampuni ya IPTL na Rugemalira binafsi.
“Baada ya kukamilisha haya, naomba unijulishe haraka ili tuweze kupanga mikakati ya kukabiliana na kila tatizo nililolitaja hapo juu,” anaeleza Camilo Schutte.
Kupatikana kwa mawasiliano haya kumekuja mwaka mmoja na nusu baada ya mabilioni ya shilingi kukwapuliwa BoT; na Bunge kuelekeza serikali kufanya uchunguzi.
Aidha, kupatikana kwa taarifa kuwa Rugemalira alikuwa na mawasiliano ya karibu na “kindungu” na mkuu wa TAKUKURU, kumekuja wakati ambapo taasisi hiyo imeshindwa kuanika orodha ya watu walionufaika na mgawo wa fedha hizo kutoka benki ya Stanbic.
Bunge liliagiza serikali kufikisha mahakamani watuhumiwa wote wa Escrow, ikiwa ni pamoja na kufilisi mtambo wa IPTL na kuitangaza benki ya Stanbic kuwa taasisi ya kutakatisha fedha.
Bunge liliagiza pia kuchunguza na kuwajibisha majaji waliotajwa kunufaika na mgawo wa fedha kupitia benki ya Mkombozi na kumfukuza nchini, anayejiita mmiliki wa IPTL, Harbinder Sigh Seth.
Akizungumzia kutajwa kwa Dk. Hoseah na baadhi ya majaji katika mawasiliano na Rugemalira, mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu amesema jambo hilo linaongeza shaka juu ya uadilifu wa viongozi wa CCM na serikali yake.
Ameliambia gazeti hili katika mahojiano kwa njia ya simu, “…hili liserikali lote limeoza. Kuanzia Ikulu, mfumo wa mahakama hadi viongozi wa madhehebu ya kidini; kote kumejaa rushwa.”
Lissua ameongeza, “Tulisema ndani ya Bunge, kwamba majaji wamehongwa na hivyo tukataka wachunguzwe, lakini serikali ya CCM imegoma kwa kuwa walioiba waliwajua na walishirikiana nao.”
Mwanasiasa huyo wa upinzani anasema, “utapeli huu ulifanywa na serikali ya Rais Kikwete, BoT, Benki ya Stanbic na PAP.”
Amesema, “…sasa kama kweli wanataka kusafisha nchi, basi waanzie hapo. Siyo kukimbizana na vidagaa. Waanze na maofisa wao wa Ikulu waliokuwa wameigeuza ofisi ya umma kuwa ofisi binafsi.”
Chanzo: Mwanahalisi

Punguzo Kodi ya Mishahara Kwa Wafanya Kazi Laibua Mapya

Uamuzi wa Rais John Magufuli kupunguza asilimia mbili ya Kodi ya Mshahara (PAYE) umeibua mjadala baada ya kubainika kuwa utampa nafuu ndogo mfanyakazi, huku wachambuzi wakihamia kwenye kodi nyingine ya mapato kwa kuzingatia viwango vya mishahara.
Baadhi ya wadau wanapendekeza kodi hiyo, inayoitwa excess charge, ipunguzwe kumpa unafuu mfanyakazi, huku wengine wakishauri kuweka nguvu kwenye uchumi wa viwanda na kilimo na baadhi wakishauri juhudi zifanyike kudhibiti mfumuko wa bei ili mshahara utosheleze mahitaji ya mfanyakazi.
Baadhi ya wadau wanapendekeza kodi hiyo, inayoitwa excess charge, ipunguzwe kumpa unafuu mfanyakazi, huku wengine wakishauri kuweka nguvu kwenye uchumi wa viwanda na kilimo na baadhi wakishauri juhudi zifanyike kudhibiti mfumuko wa bei, ili mshahara utosheleze mahitaji ya mfanyakazi.
Juzi katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, Rais alitangaza kupunguza kodi ya PAYE kutoka asilimia 11 hadi tisa, lakini kwa mujibu wa wahasibu uamuzi huo ni punguzo la Sh1,100 kwa wafanyakazi wa mshahara wa kima cha chini na Sh3,800 kwa mshahara unaoanzia Sh360,000 na kwenda juu.
Akifafanua kuhusu PAYE, mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Richard Kayombo alisema kiwango cha mapato kisichozidi Sh170,000 hakina kodi, lakini mapato ya kati ya Sh170,000 hadi 360,000 yalikuwa yanakatwa asilimia 11 na hivyo sasa yatakatwa asilimia tisa.
Alisema mapato yanayoanzia Sh360,000 hadi 540,000 hukatwa PAYE pamoja na asilimia 20 ya excess charges, wakati mshahara unaozidi Sh540,000 hukatwa PAYE pamoja na asilimia 25 ya makato ya excess charges.
Suala hilo pia lilizungumzwa na mchambuzi wa masuala ya kijamii na kisiasa, Godlisen Malisa katika waraka alioutuma kwenye mtandao kuchambua punguzo hilo la Rais Magufuli.
Malisa alionyesha kushangazwa na kitendo cha baadhi ya watu kusifu punguzo hilo, wakiwamo wabunge wa upinzani.
“Kama Rais angepunguza excess charges, angalau zikafika 10% kutoka 30% ziliko sasa, ingekua na maana kubwa sana kuliko kupunguza PAYE,” anasema Malisa katika waraka huo.
“Kwa kifupi ni kuwa punguzo hilo litawanufaisha zaidi wenye mishahara chini ya 720,000/= lakini kwa wanaolipwa zaidi ya hapo hakuna benefit (manufaa) yoyote. Hata hao wanaolipwa chini 720,000/= bado watanufaika kidogo sana.”
Alidai kwamba kama kuna mbunge yeyote anayeshangilia punguzo ni wazi kuwa hajui hesabu, hivyo anatakiwa kukumbushwa ili aelewe kuwa kupunguza PAYE wakati makato yanayozingatia viwango vya mishahara yako palepale, ni kiini macho.
“Yaani Rais JPM alichofanya ni kutulazimisha tukatae ongezeko la mshahara,” anasema.
Alisema ni kweli wapinzani waliomba PAYE ipunguzwe tangu mwaka 2011 kwamba isomeke kwa tarakimu moja na ndivyo alivyoahidi JPM, lakini pia walishauri kuwa gharama za makato hayo ya zaidi yalingane.
“Nimeamua kusema hivi maana naona wabunge wengi wa (vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi) Ukawa wanacheza ngoma ya Magufuli. Wanaanza kujitapa (kwamba) upinzani tulishauri jambo hili tangu mwaka 2011,” anasema.
“Wengine wanapiga picha hadi hotuba ya kambi ya upinzani iliyozungumzia jambo hilo. Waambieni wakae kimya na wasiendelee kuongea vitu wasivyovijua.”
Mtaalamu wa masuala ya kodi, Dk Mariam Nchimbi alisema kiwango cha mshahara kingepandishwa ni wazi kingesaidia wengi kujipanga vyema, ikiwa ni pamoja na kuendelea kulipa kodi zinazostahili.
“Ni wazi kwamba kwa hatua hiyo ya Rais imewasaidia kwa kiasi fulani wale wanaolipwa mishahara ya kiwango cha kati, lakini wale wa kiwango cha juu pia walipaswa kupunguziwa japo kwa asilimia 28 badala ya 35 inayokatwa sasa,” alisema.
Lakini wachambuzi wengine waligeukia suala la kukuza uchumi wakisema ndilo litakalosaidia mfanyakazi kunufaika na mshahara wake.
Profesa Humphrey Moshi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) alisema mshahara wenye nafuu kwa maisha ya wafanyakazi wengi utapatikana kutokana na uwepo wa viwanda vya kutosha pamoja na kilimo kuimarishwa.
“Kuna mambo mengi ya kuangalia ili mfanyakazi awe na mshahara ambao unampa unafuu wa maisha,” alisema Profesa Moshi.
“Pato la Taifa linahusika kwa kiasi kikubwa, hivyo kama litajengewa mazingira ya kukua, itakuwa vyema. Inatakiwa viwanda vichangie pato hilo kwa asilimia 25 na si asilimia nane kama ilivyo sasa.”
Alisema anaamini baadhi ya viwanda hivyo vitakuwa vya kusindika mazao, kutakuwa na kilimo cha biashara ambacho kitaongeza tija.
“Ninaamini kuwa mbali na maeneo hayo, viwanda vingine vingi vinaweza kuendelezwa kama vya usindikaji mazao ya kilimo na uzalishaji ,” alisema.
Alisema kwa upande wa Serikali mshahara wenye nafuu ya maisha kwa watumishi wake unapaswa kujengewa mazingira labda kwa kuweka idara maalumu ambayo inaangalia viwango vya mishahara.
“Kwa ilivyo sasa ni wazi kuna watumishi ambao wananufaika kama alivyowahi kueleza Rais. Yaani watu wanalipwa mishahara kama wapo Ulaya. Sasa mfano unaweza kukuta mtu kaajiriwa hapa UDSM ni msomi kwa viwango, lakini analipwa Sh3 milioni wakati mwenye digrii aliye Benki Kuu analipwa Sh6 milioni,” alisema.
Profesa Moshi alihoji kwa viwango hivyo viwili tofauti, nini kimetumika kuamua mwenye elimu kubwa alipwe kidogo na mwenye elimu ndogo alipwe zaidi.
Alisisitiza kuwa Serikali inapaswa kuzibana bodi za taasisi zake ambazo zimejijengea mazingira ya kulipa mishahara ya mamilioni ya fedha bila kujali hali ya nchi kwa ujumla.
Msomi mwingine, Dk Ulingeta Mbamba kutoka Shule ya Biashara ya UDSM, alisema Serikali inabidi idhibiti mfumuko wa bei.
“Ni wazi kwamba hata kama Serikali itaongeza mshahara, bidhaa zikawa zinapandishwa kiholela, hakuna siku kiwango cha mshahara kinaweza kutosheleza maisha ya watumishi,” alisema.

Wasafi Wadaiwa Kumpora Producer Frag Ngoma ya 'Bado' iliyoibwa na Harmonize Feat. Diamond

Producer Frag kutoka Uptown Music ametumbua jipu baada ya kuibuka na kusema kuwa yeye ndiye aliyetengeneza wimbo wa Bado wa Harmonize na Diamond.
Frag aliiambia Enewz kuwa pamoja na kazi kubwa aliyoifanya kuhakikisha ngoma hiyo inakuwa poa lakini bado WCB wakamzima na hawakumlipa hata senti tano na kuambulia elfu thelathini pekee ya nauli.
“Kawaida nikifanya kazi uptown music lazima saini zangu ziwepo lakini kwa kule wasafi saini zangu hazikuwekwa, na sijajua kwasababu gani hazikuwekwa wangeweka tu ata ile saini ya jina langu ili kunitengezea heshima kwa watu wengine ”, alisema Frag.

Aliyejifungua Watoto 3 Anaomba Asaidiwe kwani naye ni Mgonjwa wa Pumu

MKAZI wa Kijiji cha Mapinduzi Kata ya Kigwe Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma Julietha Sokoine (24) amejifungua watoto wa watatu na ameiomba serikali, taasisi,mashirika na watu binafsi kumpatia msaada wa kifedha utakaomsaidia kuwatunza watoto hao.
Pia alisema msaada huo pia utamuwezesha kupata tiba ya ugonjwa wa pumu ambao umemsababisha kuvimba mwili wote.
Akizungumza mwishoni mwa wiki, Sokoine ameiomba jamii kumsaidia kutokana na kukabiliwa na tatizo la ugonjwa wa pumu ambao pia umesababisha kuwa na hali ngumu ya kimaisha ambayo inamfanya kushindwa kuwatunza vizuri watoto wake.
Alisema watoto hao, Daniel Sokoine,David Sokoine na Davis Sokoine walizaliwa kwa pamoja Machi 22, mwaka huu katika hospitali ya mkoa wa Dodoma huku kati ya wawili wa wakiwa na uzito kilo mbili na nusu na wa mwisho kilo mbili.
“Hali yangu siyo mzuri kutokana na mimi mwenyewe kukabiliwa na tatizo la ugonjwa wa pumu,ambapo wakati mwingine nalazimika kuwanywesha maziwa ya ngombe watoto hao pindi ninapozidiwa na ugonjwa huo”alisema .
Kwa upande wake baba wa watoto hao Sokoine Chipanta alisema pamoja na juhudi za kilimo hata hivyo mazao yake yalinyauka na jua.
Alisema kutokana na hali hiyo analazimika kutafuta vibarua ili kuweza kupata fedha kwa ajili ya kununua chakula pamoja na matunzo ya watoto hao.
Alisema kwa wale wote watakaoguswa na kuamua kumpa msaada wawasiliane naye kwa namba ya simu +255 652 744 510.

PENZI la Mwanamuziki Shaa na Master Jay...Shaa Afunguka Kinachoendelea Kwa Sasa....

Master J na Shaa wamekuwa kwenye uhusiano kwa miaka mingi sasa na wameendelea kuwa imara.
akini pamoja na kuwa hivyo, bado uhusiano wao wa kikazi una nafasi kubwa zaidi. Hali hiyo ndiyo imemfanya Shaa kujitahidi kutofautisha uhusiano wao na kazi kwakuwa kwake Master J ni bosi wake.
Master J na Shaa walikutana kwa mara ya kwanza kwenye mradi wa Cocacola Popstars takriban miaka 10 iliyopita.
Bonyeza HAPA kudownload application ya UDAKU SPECIAL kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Labels: Master J , Shaa
WEKA MAONI YAKO HAPA CHINI
“Bosi wangu meaning ni CEO wa MJ Records, label iliyonisaini na ananisupport sana namshukuru mwenyezi Mungu, ni CEO lakini ni one of my best friends, nimemfamu sasa for ten years,” Shaa alikiambia kipindi cha Chill na Sky.
“He is one of my close advisors, ananishauri sana na nasikiliza sana ushauri wake, akikataa kitu nazingatia, akiniambia fanya hivi nasikiliza. Kwahiyo kama Shaa, Master ni my CEO, my boss and my very close friend, kama Sarah hayo ni ya Sarah.”


Wabunge Watwangana Ngumi Bungeni..

Wanachama wa chama tawala cha Uturuki cha AK na chama kinachoungwa mkono na Wakurdi wamepigana ngumi bunge kuhusiana na mpango kuwaondolea kinga wabunge ya kutoshitakiwa.
Wabunge wakionyeshana umwamba Bungeni nchini Uturuki
Ngumi hizo ziliibuka bungeni wakati kamati ya bunge ilipokutana kujadili mabadiliko hayo yanayoungwa mkono na serikali ili kubadili Katiba kuwaondolea kinga hiyo wabunge.
Baadhi ya wabunge walikunjana mashati kwenye meza, wengine wakirusha chupa za maji na kurushiana ngumi bungeni.

Ole Wao Wanaowapa Ujauzito Wanafunzi-Ummy

Serikali imewaagiza Maafisa maendeleo ya Jamii na maafisa ustawi wa Jamii wa wilaya,kata na mikoa nchini kuwafatilia wanaume wanaowapa ujauzio wanaume wanaowapa ujauzito watoto wa shule na kuwafikisha Mahakamani.
Akizungumza leo bungeni katika kipindi cha maswali na majibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu, amesema serikali haitamvumilia mwanaume yoyote anaempa mwanafunzi ujauzito.
Mhe. Ummy amesema kuwa serikali ya awamu ya tano itawachukulia hatua wanaume wote na hakutakuwa na huruma juu ya hilo huku akisisitiza wanawake ambao si wanafunzi ni wengi mitaani.
Hapo awali Akijibu Swali la Mbunge wa Ileje, Mhe. Janeth Mbene, Naibu Waziri wa TAMISEMI, Mhe. Seleman Jaffo amesema kuwa tatizo la watoto kupewa ujauzito nchini linatokana na vishawishi wanavyokutana wakiwa njiani wakati wanakwenda mashuleni.

Jumatatu, 2 Mei 2016

Baada ya Kutoka Marekani Mtoto Getrude Clement Akaribishwa Bungeni Leo

Getrude Clement mwenye umri wa miaka 16 ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu anayesoma shule ya Sekondari Mnarani iliyopo jijini Mwanza, leo amepata nafasi ya kufika bungeni Dodoma baada ya kupewa mwaliko wa Serikali
Hivi karibuni Getrude alihutubia viongozi mbalimbali wa dunia kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa uliohusu mabadiliko ya tabia nchi uliofanyika New York Marekani ambapo leo Bungeni amewahimiza Watanzania kutunza mazingira na kufuata maelekezo yanayotolewa na Serikali na wataalamu wa mazingira ili kuyatunza mazingira wanamoishi.
Getrude amesema kuwa amefarijika kwa kuwawakilisha vijana wa Tanzania na dunia kwenye mkutano wa mabadiliko ya tabia nchi ambapo mataifa 175 yalikutana kusaini makubaliano ya Paris.
Katika kuwahimiza vijana kujenga tabia ya kutunza mazingira, Getrude amewaasa vijana hasa wanafunzi kusimamia suala la utunzaji wa mazingira wakiwa shuleni kwa kwa kujiunga na klabu mbalimbali ambapo yeye amejiunga na klabu ya “Mali Hai” iliyopo shuleni anaposoma.
Kwa upande wa Watanzania kwa ujumla kwenye utunzaji wa mazingira, Getrude amesema kuwa ni vema wajifunze kutoka mataifa mengine yanavyosimamia utunzaji wa mazingira hasa matumizi ya mifuko ya plastiki.
Mwanafunzi huyo amekaribishwa na kutambulishwa kwa wabunge leo mjini Dodoma kwa heshima ya kuliwakilisha vema taifa wakati wa utiaji saini makubaliano ya namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki moon alimkaribisha Getrude kwa viongozi hao na kusema “Ni furaha yangu kumualika Getrude Clement ambaye pia ni mwakilishi wa vijana anayeishi Tanzania na anaziwakilisha sauti za vijana”.