Jumatano, 14 Oktoba 2015

DR MTIKILA ALIUAWA KABLA YA AJALI DP

MAPYAA! Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrati (DP), Abdul Juma Mluya ameibuka na kusema mazingira ya kifo cha aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho, Mchungaji Christopher Mtikila yamejaa utata huku akiweka wazi kwamba, inavyoonekana aliuawa kabla ya ajali yenyewe.
Mtikila alifariki dunia katika ajali ya gari aina ya Toyota Corolla namba T189 ARG, Oktoba 4, 2015 iliyotokea kwenye Kijiji cha Msolwa, Bagamoyo, Pwani. Wengine watatu walijeruhiwa.
mtikila2
Mti ambao gari liliugonga kwa juu kabla ya kupinduka.
Akizungumza na Uwazi mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye ofisi ndogo ya chama hicho nyumbani kwa marehemu, Mikocheni B jijini Dar, Mluya alisema hata watu waongee vipi, lakini uchunguzi wao umeonesha kwamba, kiongozi wao aliuawa tofauti na eneo la ajali na mwili kwenda kutupwa pale.
ROHO YAKE ILIWINDWA KWA SIKU 40
Mluya alisema: “Ndugu mwandishi, Mchungaji Mtikila kama kufa alikuwa afe muda mrefu sana pengine siku arobaini zilizopita (mpaka siku ya kifo cha kweli), kwa sababu amewindwa na watu ambao hatujajua lengo lao kubwa lilikuwa nini!
“Kila alikokwenda kwa shughuli za kichama kulikuwa na timu ya watu inayomfuatilia.”
mtikila4
...Baada ya Kupinduka
MARA YA KWANZA
“Tarehe siikumbuki, lakini ni Septemba mwanzoni. Tulikuwa Bunda, Mara kwenye shughuli za chama, kuna watu ambao walikuwa hawaeleweki walitufuata mpaka hotelini.
“Baada ya kubaini hilo, nilimuuliza mwenyekiti kuhusu ratiba aliyokuwa nayo ya kuzungumza kwenye runinga ya Staa TV.
“Alinipa ratiba. Baada ya kumaliza kuzungumza, nilimwambia Bunda si mahali pa kulala hivyo nilimshauri aondoke, aende Mwanza. Na nilimwambia dereva wake aondoke bila kuaga.”
mtikila4 (2)
WAKIWA NJIANI
“Lakini cha ajabu, wakiwa njiani wakielekea Mwanza kuna gari liliwafuata kwa nyuma kwa mwendo ambao waliutulia shaka. Dereva wa mwenyekiti alipokuwa akiongeza mwendo, naye anaongeza, akipunguza naye anapunguza.
“Ilibidi dereva amwambie mwenyekiti naye akamtaka dereva aongeze kasi hadi Mwanza.”
“Katika ratiba yetu tulitaka kufanya ziara za kichama kuanzia  Oktoba 18,  mwaka huu kwa kuanzia mkoa wa Kigoma na kwingineko. Pamoja na kufuatiliwa kote kule mwenyekiti hakuwa na roho ya uoga hata kidogo. Alimtanguliza sana Mungu.
“Kwa hiyo wasiwasi mkubwa wa kufuatiliwa na watu hao ulianza Mara na Mwanza kwa nyakati tofauti.
“Septemba 11, mwaka huu ndiyo tarehe ambayo sasa nilianza kukariri matukio hayo hatua kwa hatua. Siku hiyo tulikwenda kwenye Kijiji cha Usangu mkoani Pwani kwa ajili ya kufanya kampeni ya mgombea udiwani. Baada ya kumaliza tuliamua kurudi Dar lakini njiani dereva akasema kuna watu hawajui wanakuja nyuma yetu.”
WAPOTEA NJIA KWA KUFUATILIWA
“Tulijikuta tukipotea njia na kutokea mjini Kisarawe (Pwani). Pale tulifika kituo cha mafuta ambapo tulikuta gari aina Toyota Land Cruiser VX limepaki kama vile ni watu pia walikuwa wakitufuatilia.
“Lengo la kusimama pale lilikuwa kupata chakula lakini hatukufanya hivyo kulingana na mazingira. Tukaanza safari ya kurudi Dar. Tulipofika Pugu Sekondari, gari lile lilitupita kwa kasi na kupotea.
“Tulipofika Tazara gari lile lilionekana na wakati huo yalikuwa mawili. Kilichotushangaza ni upya wa magari lakini eti namba zinaanzia na A. Mimi nilifikiria kwamba, pengine ni za idara  ya  usalama  wa  taifa  zilikuwa doria  mbalimbali hasa kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi.
“Ndugu mwandishi, mimi ninafanya kazi ya siasa, niko makini sana. Niliwaambia wenzangu kuwa tunafuatiliwa.
“Ndani ya gari sisi tulikuwa na viongozi wa kuwapeleka Temeke. Lakini baada ya kufika huko lile VX tulikutana nalo. Tulipomuacha yule tuliyempeleka kule, tukawa tunampeleka mchungaji nyumbani kwake (Mikocheni) lakini bado lile gari lilikuwa likitufuatilia.”
WAPIGA CHENGA
“Tulipofika maeneo ya Msasani kwa Mwalimu (Julius Nyerere) dereva alikunja kona kuelekea kwa mchungaji na lile gari likakunja kona na kurudi lilikotoka.”
SIKU NYINGINE
“Siku iliyofuata tulipanga mipango yote ambapo sasa tulisema Oktoba 18, mwezi huu tuanze ziara ya mkoa wa Kigoma  na maeneo  mengine ya Kanda ya Ziwa.
“Mimi niliondoka kuelekea Shinyanga, yeye (Mchungaji) aliandaa safari ya kwenda Njombe kwenye kampeni ya mgombea Ubunge Jimbo la Njombe.”
OKTOBA 2, 3, 2015
“Mwenyekiti aliondoka Dar Oktoba 2, kuelekea Njombe. Oktoba 3, alinipigia simu asubuhi na kunijulisha kuwa  jana yake walipata ajali maeneo ya Makambako wakati wanakwenda.
“Nilimuuliza alipata matibabu, akajibu kuna viongozi wa Njombe walifika na kumchukua hivyo yuko sawasawa.”
TAARIFA YA AJALI
“Siku hiyo hiyo walifanya kampeni na jioni yake walianza safari ya kurejea Dar. Walipofika Mkoa wa Pwani, saa kumi na moja alfajiri, Mchungaji Mgaya alinipigia simu na kuniambia walikuwa njiani wanarudi Dar, wamepata ajali mbaya sana. Lakini hakuniambia kama mchungaji amefariki dunia.
“Nilianza kufuatilia tukio hilo na kuuliza kama kuna msaada wowote wameupata, akasema mpaka muda huo polisi walikuwa hawajafika. Mimi napenda sana kufungua mitandao ya kijamii, nilipofungua nikakuta picha zilishasambaa kwenye mitandao kitu ambacho nilijiuliza usiku huo huyo mpigapicha alikuwa wapi?”
SHAKA KUBWA YA DP
“Sisi DP, mashaka yetu makubwa ni mazingira mazima ya namna kiongozi huyo alivyofariki dunia. Hata mtoto hawezi kudanganywa kwa namna hiyo. DP ina taasisi ya kufanya uchunguzi iitwayo Liberty International Foundation iliyokuwa ikisimamiwa na marehemu. Ipo kazini kwa sasa ili kubaini ukweli wa kifo cha mwenyekiti na tutaweka wazi kila kitu.”
“Laini pia tunaitaka serikali kufanya uchunguzi na kutoa taarifa hadharani.”
MWENYEKITI KIJIJI AIBUKA NA YAKE
Uwazi pia lilifika aneo la ajali na kujionea kwa macho mazingira yake na kupata maelezo kutoka kwa baadhi ya mashuhuda.
Joshua Mohamed Msigala ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Msolwa, Chalinze, Pwani palipotokea ajali. Yeye anasimulia mambo aliyoelezwa na mmoja wa majeruhi, Mchungaji Patrick Mgaya siku ya tukio.
“Kwanza kabisa waandishi wa habari mmefanya vizuri kufika eneo la tukio na kujionea hali halisi. Nawaeleza hali halisi ilivyokuwa mpaka mimi kufika eneo la ajali.
“Siku hiyo asubuhi ya saa kumi na moja na nusu kama sikosei, nikiwa nyumbani nilipigiwa simu na dereva mmoja wa lori anayenijua. Akasema ameona ajali maeneo yangu lakini hajui kama kuna waliokufa au la!”
MWENYEKITI AWAHI NA BODABODA
“Kusikia hivyo, nilichukua bodaboda ili niwahi. Nilifika ndani ya dakika kama kumi tangu kutokea kwa ajali. Nilikuta mwili wa Mtikila umelala pembeni ya gari huku wengine watatu waliodai walikuwa ndani ya gari wakiwa wamesimama tu.
“Ila kati ya hao watatu, mmoja alijitambulisha kuwa ni Mchungaji Mgaya, yeye wakati nafika alikuwa akiongea kwa simu.”
ALICHOAMBIWA NA MCHUNGAJI
“Nilimuuliza mchungaji ilikuwaje? Akasema wakati wanapata ajali hiyo, marehemu Mtikila na wengine wawili walichomoka ndani ya gari hali iliyosababisha kifo cha Mtikila. Hata hivyo, kwa upande wangu sikuamini kama wote walichomoka kutoka kwenye gari bali mazingira yalionesha walitoka wenyewe.
“Mchungaji alizidi kuniambia kuwa, gari lilipaa juu zaidi ya futi kumi na kugonga mti kisha likapinduka na kulalia paa (kwenye Uwazi siku ya tukio, mchungaji alisema gari lilibiringika).
“Lakini pia siamini, kwani pamoja na kuona alama katika mti sikubali kama zilisababishwa na ajali kwani kama ni hivyo gari lingekuwa limepondeka zaidi juu lilikoangukia tofauti na lilivyokuwa likionekana.”
KILICHOMSHANGAZA ZAIDI MWENYEKITI
Mwenyekiti huyo alizidi kusimulia kushangaa kwake: “Kitu kingine kinachonishangaza ni kwamba, kwa maelezo yao gari liliacha barabara likawa linaendeshwa pembeni kwa umbali wa meta mia moja (urefu wa uwanja wa mpira). Kwa nini dereva asipunguze mwendo ambapo angefanya hivyo gari lisingefika kwenye mti.”
“Kinachoshangaza kingine ni kwamba, hakuna majeraha yaliyoonekana kwa macho kwa walionusurika hata kuonesha kwamba walikatwa na vioo wakati wakirushwa nje kutoka ndani ya gari. Hata viti vya mbele vilikuwa vilevile, havikuharibika na kama majeruhi walirushwa nje walipitia wapi?”
WALIOFIKA AWALI
Mwenyekiti huyo alisema anawashukuru askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wa Kambi ya Kizuka na Sangasanga waliokuwa wakipita ambapo walifika kutoa msaada.
“Baadaye mimi nilifanya mawasiliano na Polisi wa Kituo cha Chalinze (Bagamoyo) ambapo walifika eneo la tukio. Pia polisi wa mkoa nao walifika na saa 12:30 asubuhi majeruhi na mwili wa marehemu walipelekwa Hospitali Teule ya Rufaa Tumbi.”
Naye Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Msolwa, Joseph Hamad kwa upande wake alisema alipokea taarifa saa 3 asubuhi na alipowasiliana na mwenyekiti alimwambia yupo katika eneo la tukio.
Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho waliohojiwa na Uwazi walisema wameshangazwa na ajali hiyo iliyosababisha kifo cha Mchungaji Mtikila na kuitaka serikali kufanya uchunguzi wa kina.
SIMU YA MTIKILA YAZUA UTATA
Mpaka tunakwenda mitamboni, familia ya Mtikila ilisema, jana ilitarajia kufuatilia simu ya marehemu kwani haijulikani ilipo na pia kujua walipo dereva (George Ponella) na msaidizi wake (Ally Mohamed) ambapo awali, dereva alishikiliwa na jeshi la polisi.
Habari imekusanywa na Makongoro Going, Haruni Sanchawa na Issa Mnali.

Source:GPL

MWANASIASA MKONGWE MZINDAKAYA AFUNGUKA MAKUBWA KUHUSU CCM NA WALIOHAMA

MWANASIASA mkongwe nchini, Chrisant Mzindakaya amewataka viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wagombea wao wa nafasi mbalimbali, wasigombane na waliohama chama hicho kwa kusisitiza kwamba wakifanya hivyo, watakuwa wanakosea.

Mzindakaya alisema, CCM ni chama chenye heshima kubwa duniani na chenye Ilani ya Uchaguzi bora, yenye heshima. Alisisitiza kuwa rais bora wa awamu ya tano atatoka katika chama hicho.
Alisema hayo juzi akiwawakilisha wazee wa mkoa wa Rukwa kwenye mkutano wa kampeni ya kuwanadi wagombea urais, ubunge na udiwani kwa tiketi ya CCM uliofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Ndua, Manispaa ya Sumbawanga.

Mkutano huo wa kampeni ulihudhuriwa na Mjumbe wa Kamati Kuu CCM Taifa na Halmashauri Kuu, Mizengo Pinda ambaye pia ni Waziri Mkuu. Wengine ni pamoja na viongozi waandamizi wa CCM mkoa na wilaya.

“Sisi wazee wa mkoa huu tunasema chama cha siasa chenye heshima kubwa duniani ni CCM ambapo bila wasiwasi ndiko atakakotoka rais wa awamu ya tano ambaye ni Dk John Magufuli …

FROLA MBASHA AKIRI MWANAE SI WA EMMANUEL MBASHA

OHOOO! Kimenuka tena. Mwimbaji wa nyimbo za Injili, Flora Mbasha amesema mwanaye mdogo (jina linahifadhiwa) hahusiani hata kidogo na aliyekuwa mumewe, Emmanuel Mbasha huku akidai kuwa anamtambua mwanaume huyo kama mzazi mwenzake kwa mtoto mmoja tu (Liz), Risasi Jumatano linakupa zaidi.
Akizungumza na waandishi wetu kwa njia ya simu mwishoni mwa wiki, Flora alisema amechoshwa na manenomaneno yanayosemwa juu yake na Emmanuel na kwamba kama mumewe huyo ameamua kumwaga ugali, yeye yupo tayari kumwaga mboga.

Mwimbaji huyo alisema kwamba kauli aliyoitoa hivi karibuni kuwa anampenda mumewe na kwamba yupo tayari kuishi naye haikutoka moyoni, isipokuwa alifanya hivyo kwa huruma tu, kwa sababu mwanaume huyo ni mtu katili, mwenye roho mbaya na asiyemuogopa Mungu.
“Mtu mwenyewe alimtelekeza mtoto (Liz) kwa zaidi ya mwaka mmoja, ni mtu mbaya sana, sina mapenzi na Mbasha hata kidogo, ni afadhali niolewe na chizi anayeokota makopo kuliko kurudiana na mtu katili na mnyama kama huyo, namheshimu kama mzazi mwenzangu kwa Liz,” alisema.
Mtoto anayedaiwa kuibua mazito.

“Huyo mwanaume hafai kabisa, ni katili, namfananisha na shetani, anajifanya mwema kwa watu wakati hajawahi kuiomba msamaha familia, sikubaliani kabisa na hukumu ya mahakama, ukweli anaujua kwamba alibaka na hata mkimtaka huyo binti mumhoji nitamleta, isitoshe sasa hivi hata mtoto wake hamjali, hajui anasoma vipi, hajawahi kulipa hata shilingi ya ada, mimi mwenyewe ndo nahangaika kumlea mwanangu Liz ambaye anasoma kidato cha kwanza.


“Hastahili kabisa kuitwa baba sababu mzazi mwenye akili hawezi kutelekeza familia hata kama tumegombana, nimemwachia nyumba niliyojenga kwa pesa yangu na pesa zote aliweka kwenye akaunti yake na zote nilimwachia lakini kashindwa kuihudumia familia.”


Flora anajulikana kuwa na watoto wawili, mdogo akiwa ni yule aliyezaliwa wakati wanandoa hao wakiwa katika mzozo uliosababisha watengane hadi hivi sasa. Alipoulizwa kwa nini anadai aliyekuwa mumewe kumtelekeza mtoto mmoja tu, badala ya wawili, alifunguka.
“Huyu mwanangu mdogo hausiki naye kabisa, tena asiwe anamtaja kabisa kwa sababu hamhusu, hajui hata matumizi yake yakoje, mengine kaka achana nayo tu,” alisema Flora.
Mwimbaji huyo mwenye kipaji alipoulizwa sababu za kufuta kesi ya kudai talaka, aliyoifungua hivi karibuni katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakati anadai hamtaki na hawezi kurudiana naye, alisema alifanya hivyo baada ya kushinikizwa na mtu ambaye hata hivyo, alikataa kumtaja.
Mwimba Injili Bongo, Flora Mbasha.\

Flora alisema familia yake haijaridhishwa kabisa na suala la kesi ya ubakaji iliyokuwa ikimkabili mumewe kumalizika kwa kuachiwa huru na kwamba wanajipanga kwa ajili ya kukata rufaa.“Hiyo kesi imeisha kisiasa, Mbasha aliwahi kukiri kuwa ni kweli alifanya kitendo hicho, iweje leo aonekane hana hatia? Tutakwenda kukata rufaa ili haki itendeke.”

Baada ya kuzungumza na Flora, mwandishi wetu alimtafuta Mbasha kwa lengo la kumuuliza kuhusu madai ya mtoto yule mdogo kutohusika naye kama alivyosema mkewe, naye bila ‘kutafuna maneno’, alisema hata yeye hamtambui huyo mtoto mdogo, ila anaomba arudishiwe mtoto wake mkubwa, Liz na maisha mengine yaendelee.
“Hata mimi simtambui huyo mwingine, ninachoomba anirudishie tu mtoto wangu mkubwa Liz, huyo mwingine sihusiki naye kabisa kama alivyosema, yeye (Flora) ndiye anajua mhusika wa huyo mtoto, lakini si mimi na wala hajakosea kusema hivyo, nililitambua hilo tangu zamani, anipe tu mwanangu wa kwanza,” alisema Mbasha.

Source:GPL-meandikwa na Brighton Masalu, Mayasa Mariwata na Gladness Mallya