Ijumaa, 20 Novemba 2015

Alikiba Atolea Ufafanuzi Post ya ‘Utata’ Aliyoandika Instagram, na Ampongeza Diamond Kwa Ushindi wa AFRIMA

Alikiba ametolea ufafanuzi post yake ya Instagram iliyozua mjadala kwa mashabiki mbalimbali wa muziki ambao waliipokea kwa hisia tofauti.

Siku ya Jumatatu Nov.16 Muimbaji huyo wa single mpya ‘Nagharamia’ aliandika, “Asanteni sana najua mmepiga kura sana lakini nilikuja kugundua baada ya kufuatilia kuwa kuna mambo yanaendelea ya watu wanadiriki hata kupoteza pesa zao kwaajili yangu ila nawaomba fans msinielewe vibaya I will always be there for you #hapakazitu #kingkiba,post ambayo baadae aliifuta.

Kupitia kipindi cha Ala Za Roho cha Clouds Fm na Diva The Bawse, king Kiba amesema kuwa watu walimuelewa vibaya kwenye post hiyo na ndio sababu kubwa ya kuamua kuifuta,

watu walinielewa vibaya mimi nilikua nawaambia mafans wangu, sababu wao ndo wananipigia Kura mimi sikumaanisha kuhusu tuzo walinielewa vibaya” alisema Kiba.

Hata hivyo licha ya kwamba yeye hakushinda kipengele hata kimoja kati ya vinne alivyotajwa kuwania kwenye tuzo za AFRIMA 2015, lakini hakumpongeza hata msanii mmoja wa Tanzania aliyeshinda ambao ni Diamond na Vanessa Mdee. Kusuhu hilo Alikiba alisema,

Siwezi ku-post kitu kuhusu Kushinda Kwao, unajua hakuna uzalendo. watu wangapi wanafanya Vitu vizuri hawapongezwi? Mimi nafanya vingapi? Sisi sio wazalendo…Unajua watu mimi hawanijui Wanahisi kama mimi nina ringa hivi au nina wivu, ila mimi nawapenda wasanii wote pia mziki mzurialisema Alikiba.

Alipoulizwa kuhusu uhusiano wake na Diamond ukoje kwa sasa, ndipo alimpongeza Platnumz kwa ushindi wa tuzo 3.

Mimi sina tatizo na Diamond, nasikia kashida tuzo 3, nampongeza Sana sababu tumepata mtu ambaye anatutambulisha kimataifa ni Kitu poa Sana…Mimi na Diamond we are goodalimaliza Alikiba.

Wazanzibari Wanaoishi Uingereza Waandamana Wakitaka Maalim Seif Sharif Hamad Atangwe mshindi wa Kiti cha Urais

Wazanzibari wanaoishi nchini Uingereza jana walifanya maandamano wakidai haki ya kutangazwa ushindi wa Chama Cha Wananchi (CUF) katika uchaguzi mkuu wa Zanzibar uliofanyika Octoba 25 mwaka huu
Maandamano hayo yaliandaliwa na Jumuiya ya Zanzibar Welfare Association (ZAWA) ambapo wazanzibari hao walitoka maeneo mbali mbali katika miji yao na kukusanyika katika eneon la  Downing Street kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron na uongozi huo kukabidhi barua yao yenye malalamiko kutaka suala la Zanzibar lishughulikiwe.
Maandamano hayo yalifanyika kwa lengo la kuongeza shindikizo kwa mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuchukua hatua za haraka ya kuhakikisha Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) inakamilisha kazi ya kutangaza matokeo ya uchaguzi huo.

Zanzibar  iliingia katika mkwamo wa kisiasa baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar, Jecha Salum Jecha Octoba 28 kutangaza kuufuta uchaguzi wote kwa madai kwamba ulikumbwa na matatizo mbali mbali.

Wakati jecha akitoa tangazo la kufuta matokeo bila ya kushauriana na tume yake alikuwa tayari ameshatangaza matokeo ya kura za urais za majimbo 31 kati ya 54 ya Zanzibar pia washindi wa nafasi za uwakilishi na udiwani katika majimbo hayo walishatangazwa na walishakabidhiwa vyeti vyao.

Rashid Ali ambaye ni kiongozi wa ZAWA  alisema jana kuwa wamewasilishwa barua hiyo wakiamini kwamba suala la Zanzibar litashughulikiwa ili wananchi wa Zanzibar waweze kuendelea na maisha yao ya kawaida.

Mwakilishi wa ZAWA, Hassan Khamis alisema wameamua kupeleka barua kwenye ofisi za waziri Mkuu wakiamini suala hilo litashughulikiwa ikiwa ni pamoja na serikali ya Tanzania kuchukua hatua madhubuti na za haraka kaika kushughulikia suala hilo ambalo limewaweka wazanzibari roho juu.





Nina Wasiwasi na Naibu Spika Kama Atalihimili Bunge Hili

Sina wasiwasi ni elimu yake wala uwezo wake wa kujieleza, ila nina wasiwasi na hekima yake na busara zake kama zinaweza kustahimili mikiki mikiki ya bunge kama alivyoonyesha Anne Makinda.

Nafikiri wote tunaujua uwezo wa Prof. Muhongo kielimu lakini alifeli somo la hekima.

Najua bunge lina sheria zake kanuni zake miiko yake na desturi zake, lakini ni mara ngapi tumeona sheria zikikiukwa na wabunge wenyewe.

Kama tukisema yeye atakuwa "Iron Lady" kuwa kila mbunge akikosea anamhukumu kulingana na kanuni atafukuza wangapi, naje kama atafukuza karibu nusu ya wabunge ataonekana ni Naibu Spika mzuri au kiti kimemshinda.

Tuchukue mfano wa refa wa mpira wa mguu anayewatoa wachezaji kwa red kadi kila wanapofanya rafu, hivi timu ikibaki na nusu ya wachezaji huyo refa atakuwa bora?

Najaribu tu kumwangalia huyu Naibu Spika asije siku moja akatoa machozi kwa kuzomewa au kuulizwa maswali ya kuudhi akakiaibisha kiti.

Namuomba sana Spika Job Ndugai ajaribu kumsaidia msaidizi wake.

Tujadili kwa mstakabali wa nchi yetu.

By QuinineJamii Forums

Yanayojiri Bungeni Dodoma Muda Huu..Wabunge wa Ukawa Walianzisha na Kutolewa Nje ya Bunge na Spika

Wabunge  wanaounga  umoja  wa  Katiba  Ya  Wananchi, UKAWA  wametolewa  nje  ya  ukumbi  wa bunge  muda  huu  baada  ya  kugoma  kutambua  ujio  wa  Dr Shein bungeni  na  kuanza  kuzomea  huku  wakisema  Maalim Seif....Maalim Seif

Spika  wa  bunge,Job Ndugai  aliwataka  wabunge  hao waache kuzomea  na  badala  yake  wakae chini  lakini  wakakaida, hali  iliyomfanya  awaamuru  watoke  nje kwa  hiari  yao  kabla  nguvu  ya  dola  haijatumika  kuwatoa.

Model Maarufu Bongo Aibua Shutuma Nzito Kwenye Tasnia ya Mitindo..Adai Tasnia Imejaa Machoko ili Usonge Mbele ni Lazima Uwakaze

Model wa Kiume Anayejulikana kama @calisah Huku Instagram Ameibuka na Tuhuma nzito iliyopo kwenye Tasnia hiyo ya Mitindo na Urembo ...

Ameandika Haya Kwenye Ukurasa Wake wa Instagram:

|Sikutaka kuandika chochote kuhusiana na tuzo za swahilifashionweek. Ila naamini waliopo kwenye category zote ndio waliostahili kuwepo...

Na naamjni waliangalia vigezo vyao na kuhisi pengine wao ndio waliostahili. Mtazamo wangu kwa upcoming models wote wanaotamani kesho na kesho kutwa kuja kua model km mimi au mwingine yeyote. Tambueni hii tasnia imeandamwa na machoko (gays) sasa basi...... hawa watu wanahisi wanauwezo wa kukontro models wake kwa kukidhi haja zao. Na ikiwa utaenda nao sawa bc watakutumia vizuri na watamtumia mtu mwingine yeyote mwenye muonekano mzuri kwakua wao wanajua kua ili usongee mbele ni lazima uwakaze. 

Na usipo wakaza utaanza kuona safari yako inaanza kua ngumu na watatafuta njia yeyote ili wakuzime na ikiwemo kutaka kupandisha watu juu ambao walikua hawapo kwenye hiyo level ili tu wakuoneshe kua wao wanapower. Kuna ma_disigner wengi sana ktk hii tasnia yetu. Msibabaike kwa vitisho na msikubali kuuza utu wenu ili mpate show au kuwepo kwenye award yoyote, mkifanye hivyo mtatumiwa na kuachwa na kisha wao kwenda kutafuta wengine, they always looking for what new. Sijakasirika kutokuwepo kwenye tuzo za swahilifashionweek or nah kwani nilijua muda mrefu kua siwezi kua huko na ndio maana hua sijishulishagi kwenda hata kwenye cast, na sijawahi kwenda kwenye cast yoyote ya swahilifashionweek tangu inaanza.

Cz I naw evrythng. ..... Models kama hamtakua makini mtaendea kutumiwa kwa kuafurahisha watu kila cku, sitaki na wala sitataka kua kua kwenye award yoyote na wala hakuna quma yeyote ninarmuogopa cz hakuna anaenipa hela ya kula kati yenu nyote, taftani hao models wenye njaa.... wawakaze halafu ndio muwape tuzo zenu, "Ushauri wangu kwa models wengine ambao wamekua_dissaponted. Tulieniii..... tengenezeni portfolio zenu nzuri na mtafute kazi nje ya nchi.... tuige mfano kwa @daxx_cruz @flavianamatata na wengine waliotangulia... mkibaki hivyo hamtafkia kokote kwa kutegemea wakina @martinkadindaofficial na kina @mustafahasanali they got nothing to help u... Hakuna yeyote kati yao mwenye uwezo wakukuangusha ikiwa utajiweka vizuri na kufokas soko la mbele. Msikubali kubaika na kuuza utu wako ili mpate jina bila ya hela|  Calisah

LIVE TOKA BUNGENI: Rais Magufuli Ampa Hongera Zitto Kabwe Kwa Kutokuleta Fujo Bungeni na Kubakia Ndani ya Bunge Wakati Ukawa Wametoka

LIVE TOKA BUNGENI:Muda huu Rais Magufuli Anatoa Hotuba yake ndani ya Bunge na Amempa Hongera Zitto Kabwe Kwa Kutokuleta Fujo Bungeni na Kubakia Ndani ya Bunge Wakati Ukawa Wametoka Baada ya Kutolewa na Spika kutokana na Utovu wa nizamu walioonyesha kwa Kupiga Makelele

JE Unakichukuliaje Kitendo cha ZITTO KABWE Kubaki Bungeni Wakati Wabunge wa Upinzani Wote Wametoka Nje ?

JE Unakichukuliaje Kitendo cha ZITTO KABWE Kubaki Bungeni Wakati Wabunge wa Upinzani Wote Wametoka Nje Kushinikiza Maalim Seif Atangazwe Mshindi wa Urais Zanzibar?

TOA MAONI YAKO

Ijumaa, 13 Novemba 2015

Soma Story ya Kusikitisha ya Huyu Dada, Mume Wake Anamlazimisha Kufanya Mapenzi ya Watu Watatu na Amegundua Kuwa ni Shoga Pia


Kutoka Instagram:

MMH DUNIA HII INA MAMBO KWAKWEL.COZZ LEO NIKO KI EMOTION ZAID EMBU NGOJA NI SHARE NA NYIE BAADHI YA STORY NAZO POKEA INBOX...kuna dada nilikuwa naongeaga nae ila kutokana na sababu zangu nisingependa mtaja jina...naomba nikuletee Story yake ya kusikitisha Hapa Chini:
.
Masta hata ukinipost kweny wall yako mungu nishaidi ila tangu nimekujua umekuwa mkarimu sana kwangu ndio maana leo hii nimeamua kukufungukia ili unisaodie tu kimawazo maana kadri siku zinavyo zidi kwenda ndivyo nazid changanyikiwa...

Kama nilivyo kwambia nimeolewa huu mwaka wa 3 mimi na mume wang tumejuana huu unaenda mwaka wa 5,masta ilianza kama utan baada nilipo jifungua mtoto wang wa kwanza alipo fikisha miez 8 skumoja mume wng alinitamkia habar ya ku invite 3 person in our bedroom nilijua utani so tukajibizana na alipoona sikupenda idea akaanza jichekesha na kusema he was joking yakaisha...ila baada ya miez kadhaa aliirudia hii mada tena ila this time alijipanga na kuni Converse sana yan alinipa darasa la uwakika nikajikuta nakubali,masta kesho yake kwel akaja na mdada mashallah mpaka nyumban chumban kwangu kikatokea cha kutokea ila baada ya hapo nilijiona mjinga sana nililia siku nzima but nilikuwa dhaifu cz usiku wake baby akanileta pochi jipya la prada nikaridhika...

Mchezo ulikuwa ni huo kwa takriban kama miez 6 nahis nilijikuta nazoea mpa nilipo jikuta nina mimba, for his respect mwenyewe alinitamkia kuwa we need to stop..ila skumoja rafiki yake alikuja home amelewa na walikuwa wamegombana baada ya kutapeliana na alianza kumcharukia huku akimwita GAY sikutilia maanan cz nilijua ni mikwaruzano tu na pombe masta baada ya kujifungua mtoto wangu wa 2 in 6 month ananitamkia tena huo mchezo this time nilikuwa mkali coz tayari mtoto wang wa 1 alishaanza kuongea na sikutaka kaone huo ujinga pili habari zilikuwa zinasambaa kuwa mimi na mume wang tunahuo mchezo..basi Masta nyumba ikaanza waka moto kila siku kelele iskumoja alinitamkia kuwa either i like it or not ataendelea kufanya coz hiyo ndio furaha yake...

Wakat nimerudi Tanzania kwaajiri ya holiday siku ya kurudi marekan tulichelewa ndege Transit na coz hatukuwa na simu ya mawasiliano mimi na wanangu tulirudi home kwa kumshtukia baada ya kuingia ndani nilimkuta mume wangu akifanya mapenzi na watu wawili mmoja alikuwa mwanamke yule wa mwanzo ambae alimleta first time mwengine mwanaume, that was the most painful thing nimewahi shuudia Masta nilihisi moyo umestop nilianguka chini huku nikiwa nimembabe mtoto wangu mdogo kifuani...nimekuja stuka niko hospital.

Kinacho niuma zaidi dada yangu baada ya kutoka hospital nilikuwa tayari kumsamehe mume wangu kama angeliniomba msamah lakini haikuwa hivyo baada ya Two Montn ananiambia nichague moja NIENDELEE KUWA NA YEYE NA NIKUBALI MATAKWA YAKE YA KUINGIZA WATU NDANI AU TUACHANE...Masta nilikosa jibU na kujikuta natoa machozi aliniambia kuwa ananipa muda nijifikilie lakini sasa masta maneno ya watu kusema kuwa ni gay yalikuwa ya kizidi ila sababu sikuwa na uelewa mzuri wa haya mambo nilikuwa nikibisha coz mume wang alikuwa na uwezo wa kunibebesha mimba...mpaka siku nyingine tena nilimfumania kweny gari lake akiwa na mwanaume mwenzie wakifanya uchafu wao...

Dadangu roho inaniuma na siku nyingi sana nilikuwa natafuta njia ya kutoa hili dukuduku moyon coz sijawah muelezea mtu masta naogopa walimwengu watanicheka coz always huwa wananisema naringa na kujifanya kuwa nina pesa kisa navaa vitu vya gharama...baada ya hilo tukia mume wangu kwa mdomo wake alinitamkia kuwa yeye anai enjoy kufanya mapenz na wanaume pamoja na wanawake at the same time so kama mke anataka nimsapoti...hivi navyo kwambia atanaka divorce kisa nimekataa kukubaliana na yeye na kuhusu watoto he doesnt seems to care masta wanangu bado wadogo na wakiume wameshazoea kila siku daddy daddy daddy coz ana waspoil mume ananambia nikiachana nae hataki kujua anything about me na watoto atakuwa anatuma tu pesa...shida sio pesa masta NISAIDIE NIFANYE NINI NAHISI NAKUWA KICHAA SOON...naogopa kuwaadisia ndugu na rafiki zangu Masta
.
.
MWISHO...DUH EMBU TUMSAIDIE HUYU DADA KIMAWAZO

Maalim Seif azugumza na Balozi wa EU na viongozi wa UKAWA....Atoa Msimamo Mzito

Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, amerejea kauli yake ya kutotambua kufutwa kwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar uliofanyika tarehe 25 mwezi uliopita.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mara baada ya kikao cha mashauriano na viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA, Maalim Seif amesema Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Bw Jecha Salim Jecha hana mamlaka ya kufuta uchaguzi huo, na kinachohitajika na kuendelea na mchakato wa kuhakiki kura zilizobakia na mshindi kutangazwa.

Kuhusu tamko lililotolewa na serikali juu ya kufutwa rasmi kwa uchaguzi huo kupitia tangazo lililochapishwa kwenye gazeti rasmi la serikali tarehe sita mwezi huu, Maalim Seif amesema tamko hilo limekosa uhalali tangu lilipotolewa na Mwenyekiti wa ZEC.

Maalim Seif ambaye pia ni Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CUF amesema Chama chake hakijalizingatia tamko hilo na wala hakijadili uwezekano wa kurejewa kwa uchaguzi huo, kwa madai kuwa uchaguzi ulikamilika bila ya kuwepo malalamiko kutoka chama chochote cha siasa na wala Tume ya Uchaguzi.

Mapema akizungumza baada ya kikao hicho cha mashauriano, aliyekuwa mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chadema Mhe. Edward Lowassa amesema kikao hicho kilichojadili Mkwamo wa kisiasa Zanzibar kimekwenda vizuri.

Hata hivyo amesema ufafanuzi zaidi utatolewa Jumapili ijayo ambapo viongozi hao wanakusudia kuzungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Kabla ya kikao hicho Maalim Seif alifanya mazungumzo na Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) Bw. Filberto Seregondi katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam na kuelezea hatua zinazochukuliwa kukwamua mkwamo wa kisiasa Zanzibar.

Balozi Seregondi ambaye anamaliza muda wake wa utumishi hapa nchini,aliambatana na ujumbe wa waangalizi wa uchaguzi mkuu wa Tanzania kutoka Umoja huo.

Maskini..Lowassa Asalimu Amri Kwa Polisi...Atoa Ujumbe Huu Hapa Kwa Wafuasi Wote wa Ukawa Kuhusu Mkutano Wake

Maskini..Lowassa Asalimu Amri Kwa Polisi Kuhusu Mkutano aliokuwa aufanye kuongea na Wananchi...Atoa Ujumbe Huu Hapa Kwa Wafuasi Wote wa Ukawa Kuhusu Mkutano Wake

Watanzania Wasiwekeze Kila Kitu Kwa Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu

Mbwana Samatta (kushoto) pamoja na Thomas Ulimwengu (kulia)

Stars inatoka katika kambi ya wiki moja na siku kadhaa nchini Afrika Kusini itawakabili ‘Mbweha wa Jangwani’ baada ya kufuzu hatua ya kwanza kwa ushindi wa jumla wa magoli 2-1 dhidi ya Malawi mwezi uliopita.

Kwa mara ya kwanza Stars itaingia uwanjani kucheza na timu bora zaidi Afrika ikiwa na mfungaji bora wa ligi ya mabingwa Afrika, namzungumzia kijana wa miaka 22, Mbwana Samatta.

Sina shaka kuhusu uwezo wa Samatta ambaye nilimshuhudia Jumapili iliyopita akiipa ubingwa wa Afrika upande wa vilabu timu ya TP Mazembe ya DR Congo.

Sitazungumzia sana mechi yenyewe lakini ningependa kuwaambia Watanzania wenzangu kuwa hatupaswi kuamini moja kwa moja katika uwezo wa mchezaji mmoja au wawili katika timu na ili kuishinda Algeria wachezaji wote kuanzia kwa golikipa hadi mchezaji wa mwisho katika safu ya ushambuliaji wanapaswa kucheza katika kiwango cha kufanana.

Samatta anazungukwa na nahodha wa timu ya taifa ya Zambia ambayo Jumatano hii iliifunga Sudan 1-0 jijini, Khartoom. Namzungumzia kiungo mshambuliaji Rainford Kalaba, pembeni ya Samatta pale TP Mazembe anacheza na mchezaji pekee wa timu ya Taifa ya Ivory Coast anayecheza barani Afrika, Roger Assale, Mghana, Solomon Asante, n.k

Kiujumla, Samatta anazungukwa na ‘rundo’ la wachezaji wenye vipaji ambao wanajituma sana ndani ya uwanja kwa muda wote wa mchezo. Huduma ambayo ‘Samagoal’ amekuwa akiitoa klabuni kwake ni tofauti kidogo na ile ambayo Watanzania wamekuwa wakitaraji kutoka kwa mchezaji huyo ambaye ni miongoni mwa wachezaji 10 bora wanaocheza ndani ya Afrika kwa mwaka huu wa 2015.

Kwa nini Samatta wa TP Mazembe ni tofauti na huyu anayeichezea Stars? Ubora wake ni uleule, tofauti ni kwamba, akiwa TP anakutana na wachezaji wenye vipaji kama yeye ambao pia hucheza kwa nidhamu, kujituma na kufuata maelekezo ya benchi la ufundi.

Mafanikio ya Samatta na ‘patna’ wake Thomas Ulimwengu ndani ya klabu yao wiki iliyopita ni ya ‘mfanowe’. Ni wachezaji wa kwanza wa Kitanzania kucheza mchezo wa fainali wa ligi ya mabingwa Afrika. Katika michezo miwili ya fainali kati ya TP Mazembe na USM Algers ya Algeria, Samatta amefanikiwa kufunga magoli mawili kati ya manne ya TP na kutengeneza goli lingine moja.

Ushindi wao wa taji la mabingwa Afrika umewafanya Watanzania wengi kujenga imani kwamba, Stars inaweza kuishinda na kuitoa Algeria! Kila kitu kinawezekana katika mchezo wa soka, lakini ukitazama aina ya wapinzani ambao tunakwenda kucheza nao ni sawa na ‘mlima mrefu’ ambo tunapaswa kuupandaa.

Ulimwengu anacheza kwa kupambana sana akiwa klabuni kwake TP Mazembe na amekuwa akicheza hivyo hivyo hadi timu ya Taifa Stars. Lakini Samatta anahitaji ‘muunganiko’, anahitaji wachezaji wenzake wacheze kwa asilimia ya juu. Anahitaji wachezaji ambao wana uwezo wa kuusoma mchezo. Kila Mtanzania ukimuuliza hivi sasa kwanini anaamini Stars itashinda dhidi ya Algeria anakwambia “Mbwana Samatta”.

Lakini mchezo wa mpira wa miguu si kama mchezo wa ngumi au tenis, mtu anapambana mwenyewe. Akiwa mzuri anapata matokeo. Lakini mchezo wa mpira wa miguu unahitaji sana uwezo wa kiuchezaji wa mchezaji mwingine. Ukitaka kuuona uwezo halisi wa Samatta katika timu ya Taifa ni lazima, Shomari Kapombe, Nadir Haroub, Kelvin Yondan, Ally Mustapha wote wacheze inavyotakiwa katika idara zao.

Timu ambayo Samatta aliifunga magoli mawili katika fainali ya CAF Champions league haina hata mchezaji mmoja katika timu ya Taifa ya Algeria! Inamaanisha kuwa wanategemea zaidi mkusanyiko wa wachezaji wao wanaofanya vizuri barani Ulaya. Algeria ina wachezaji wanaofanya vizuri katika ligi kuu England, Hispania, Ureno na kwingineko.

Algeria wamekuja na ‘timu kabambe’, Rais M’Bolhi (Antalyaspor/Uturuki), Azzedine Doukha (JS Kabylie), Malik Asselah (CR Belouizdad). Viungo: Mehdi Zeffane (Rennes/Ufaransa), Mohamed Khoutir Ziti (JS Kabylie), Faouzi Ghoulam (Napoli/Italia), Djamel Mesbah (Sampdoria/Italia), Carl Medjani (Trabzonspor/Uturuki),Aïssa Mandi (Reims/Ufaransa), ukweli itakuwa mechi ngumu kwa Stars kuliko Algeria.

Ijumaa, 6 Novemba 2015

Mchumba Wangu Ameanza Kuvaa ''SHANGA" Miguuni...Nahisi Ameanza Kamchezo....

Nimekuwa kwenye mahusiano ya takribani miaka mitatu(3) sasa na msichana ambaye awali alikuwa yupo chuoni ila kwa sasa ni mfanyakazi taasisi fulani hivi (jina kapuni). Amepangiwa nje ya MKOA wa DAR nilipo.

Tulipoanza mahusiano haya hakuwahi kunionyesha anayonionesha hivi sasa.

Amekuwa akipost pictures mbalimbali akiwa amevaa ''vimini'' na ''vishanga (vikuku)'' miguu yote Miwili....

Nimejaribu kumuuliza nini MANTIKI ya hizo picha, kanijibu eti "...mbona kawaida tu,..

NIPO SO FRUSTRATED; ISIJE IKAWA KAANZA KALE KATABIA... MAANA NILISHA MTAMBULISHA KWA BAADHI YA NDUGU.

Mke wa Deo Filikunjombe Ampigia Kampeni Mdogo wa Filikunjombe Achukue Ubunge Jimbo Aliloliacha Mmewe..Adai Wengine Msiwasikilize Hawana Hata Mahali pa Kufikia Ludewa

Tanzania bado iko kwenye majonzi baada ya msiba wa aliyekuwa mbunge wa Ludewa,Deo
Najua kuna watu walikuwa na maswali juu ya atakayewaongoza wakazi wa Ludewa, sasa leo Novemba 5, 2015 mke wa marehemu Deo Filikunjombe ‘ Saraha’ ameyaandika maneno haya kupitia akaunti yake ya instagram kuhusiana aliyeteuliwa kugombea jimbo la Ludewa.

Nawaombeni wana ludewa wote kwa heshima nawaomba niwaambie ukweli kuwa huyu ndie anayeweza kuvaa viatu vya mume wangu mpendwa kwani mara nyingi amewahi kumchangia kaka yake ada za watoto tuliokuwa tunawasomesha huko ludewa naombeni msidanyike na maneno ya hao wagombea wengine mbona leo ndo wamekuja ludewa walikuwa wapi kujakuleta maendeleo mpaka iwe baada ya deo kufariki kati ya wagombea wote hakuna rafiki wa mume wangu’ – Saraha
‘hata mmoja tena kwa macho yangu nimewaona wakipewa misaada walete Ludewa na hawakufikisha na mara nyingi amelalamika na kuwaomba jamani tupeleke maendeleo nyumbani hakuna aliesikia hata mmoja ndo maana hawana nyumba ya kufikia matokeo yake wanawaomba kura ilingali hata hawana pakufikia wamefikia nyumba ya kulala wageni mkitaka kumwona mbunge mta mkuta wapi tuwemakini Deo amefanya mengi mpeni mdogo wake amalizie aliyoahidi asanteni sana wanaludewa niwaganili sana mdalikhe sana ccm hoyeeeeeeechagua ccm chagua Philipo filikunjombe hapa kazi tu’ – Saraha

Rais Kikwete Aachia Madara Kistaili...Awasamehe Wafungwa 4,160 Watoke Gerezani

RAIS mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete ametoa msamaha kwa wafungwa 4,160 katika kuaga na kukabidhi madaraka ya Serikali kwa Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli.

Dk Magufuli aliapishwa jana kuwa Rais wa Tano wa Tanzania katika sherehe zilizofana kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam huku Kikwete akimaliza miaka yake 10 ya kuongoza nchi kama ilivyoelekezwa na Katiba.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe kwa vyombo vya habari jana Dar es Salaam, kati ya wafungwa hao, wafungwa 867 wataachiwa huru na wafungwa 3,293 watapunguziwa vifungo vyao na kubaki gerezani wakitumikia sehemu ya vifungo vyao vilivyobaki.

“Ni mategemeo ya Serikali kwamba wafungwa watakaoachiwa huru watarejea katika jamii kushirikiana na wananchi wenzao katika ujenzi wa Taifa na watajiepusha na utendaji makosa ili wasirejee tena gerezani,” alisema Chikawe katika taarifa hiyo.

Chikawe aliwataja walionufaika na msamaha huo kuwa ni wafungwa wote wapunguziwe moja ya sita ya vifungo vyao zaidi ya punguzo la kawaida linalotolewa chini ya Kifungu cha 49(1) cha Sheria ya Magereza Sura ya 58 isipokuwa wafungwa walioorodheshwa katika ibara ya 1 (i-xix).

Aliwataja wengine kuwa ni wafungwa wagonjwa wenye magonjwa kama Ukimwi, kifua kikuu, saratani ambao wako kwenye hatua ya mwisho ambao watathibitishwa na waganga chini ya Mganga mkuu wa mkoa au wilaya.

Pia wazee wenye umri zaidi ya miaka 70, wafungwa wa kike walioingia na mimba gerezani na walioingia na watoto wanaonyonya na wasionyonya na walemavu wa mwili na akili na ulemavu huo uthibitishwe na jopo la waganga.

Kwa mujibu wa Chikawe, msamaha hautawahusu wafungwa wenye adhabu za kunyongwa, waliohukumiwa kunyongwa na adhabu hiyo baadaye kubadilishwa kuwa kifungo cha maishaau kifungo gerezani.

Wengine ni wafungwa waliotumikia kifungo kwa makosa ya usafirishaji na utumiaji wa dawa za kulevya, makosa yanayohusu uombaji, upokeaji na utoaji rushwa, unyang’anyi na kujaribu kutenda makosa hayo, kubaka, kulawiti au kujaribu kutenda makosa hayo.

Aidha, makosa mengine ambayo vifungo vyake haviko kwenye msamaha huo ni makosa ya kuwapa mimba wanafunzi, wizi wa magari, pikipiki au kujaribu kutenda makosa hayo, matumizi mabaya ya madaraka, waliowahi kupunguziwa vifungo na Rais.

“Wengine ni waliopatikana na hatia kwa kuwazuia watoto kupata masomo, utekaji watoto, usafirishaji binadamu, ukatili dhidi ya albino, usafirishaji nyara za Serikali na ujangili,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

Mengine ni wanaotumikia vifungo kwa makosa ya wizi na ubadhirifu wa fedha za Serikali, kutoroka au kujaribu kutoroka wakiwa chini ya ulinzi halali na wafungwa wanaotumikia vifungo chini ya Sheria ya Bodi ya Parole Sheria Namba 25 ya Mwaka 1994 ya Sheria ya Huduma kwa Jamii Namba 6 ya Mwaka 2002.

Nchi Ina Wanafiki Sana wa Kisiasa...Ukawa Wamsusia Magufuli Uwanja wa Taifa ila Bungeni Wamejiandikisha Kwenda Kumsikiliza Kwasababu Kuna Posho-Habibu Mchange


Mwanasiasa Habibu Mchange Ameandika yafutayo katika ukurasa wake wa Facebook kuhusu Ukawa:

'Nchi ina WANAFIKI SANA WA KISIASA HII..
Ukawa wamesusia kuapishwa Rais lakini UKAWA HAO HAO wameenda Bungeni kujiandikisha kama watahudhuria hotuba ya Rais BUNGENI na wamelipwa posho inayoendana na shughuli hiyo. sasa hii ndio kusema Baniani Mbaya kiatu chake Dawa ama? Au kwa kuwa Uwanja wa Taifa hakukuwa na POSHO?.. kungekuwa na POSHO kama kawa asingesusa mtu?...ukiamua kususa unasusa jumla sio nusu nusu. Utapeli wa kisiasa wa namna hii haufai..wangesusia vyote! 
By Habibu Mchange

Maalim Seif Aweka Ngumu Adai Hawawezi Kurudia Uchaguzi Zanzibar

Mgombea urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amesema CUF inaendelea kutafuta haki ya Wazanzibar ya kutaka Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec) kuendelea kutangaza matokeo ya uchaguzi ili mshindi ajulikane na hatimaye kuapishwa.

Aliyasema hayo wakati akizungumza na wafuasi wa chama hicho katika makao makuu ya CUF Mtendeni juzi, baada ya kurudi safari yake ya kuonana na rais wa awamu ya nne, Dk. Jakaya Kikwete, Ikulu, jijini Dar es Salaam.
Aliwaambia wanachama hao kuwa hakuna kurudi nyuma katika kudai haki yao kwa njia ya amani na utulivu ili matokeo yatangazwe na mshindi wa urais ajulikane.

“Niwahakikishieni vijana na wanachama wa CUF kuwa hakuna kurudi nyuma, tunaendelea kudai haki yetu na tunashukuru dunia nzima inatuunga mkono kwa hili,”alisema Maalim Seif, ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar (SUK).

Alisema kuwa wapinzani wao, Chama Cha Mapinduzi (CCM) mpango wao ni kutaka kuendelea kuwa katika madaraka wakijua kuwa muda wa Dk. Ali Mohammed Shein wa kukaa madarakani umekwisha, lakini wanang’ang’ania aendelee kinyume cha Katiba.

Aidha, alisema kuwa hakuna dawa yoyote ya kumaliza mgogoro ulipo Zanzibar isipokuwa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec) kuendelea kutoa matokeo ya uchaguzi wa Oktoba 25, mwaka huu ili mshindi ajulikane na kuapishwa.

“Wanaosema kuwa uchaguzi urejewe waachieni wenyewe, sisi katika CUF hakuna msamiati huo kwa sasa kurejea uchaguzi, huo ndio msimamo wetu,” alisisitiza Maalim Seif.

Alisema kuwa kwa uwezo wa Mungu haki yao wataipata na kuwataka vijana kuendelea kuwa watulivu na kuendelea kutunza amani ya nchi kwa kutokubali kuchokozeka. Alisema CUF na viongozi wake hawatakubali kuwa chanzo cha kuvuruga amani ya nchi na wataendelea kuhubiri amani wakati wote.

Mvutano wa kisiasa unaoendelea Zanzibar ulisababishwa na Mwenyekiti wa Zec, Jecha Salim Jecha, kutangaza kufuta uchaguzi wa Zanzibar wa rais na wawakilishi Oktoba 28, kwa madai kuwa ilibaini kuwapo kwa kasoro kadhaa kisiwani Pemba.

Hata hivyo, waangalizi wa nje na ndani wameeleza kushangazwa ha hatua ya Jecha, kwa kuwa hawakushuhudia kasoro zozote hadi walipotoa ripoti ya awali.

Aidha, asasi za nchini na mataifa kadhaa yakiwamo Uingereza, Ireland na Marekani yameshatoa taarifa ya kushangazwa na uamuzi wa Jecha na kushauri mchakato wa kutangaza matokeo uendelee.

MTOTO WA KARUME AIBUA MAPYA
Mjadala kuhusiana na hatma ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar uliofutwa na Jecha, umechukua sura mpya, baada ya mmoja wa watoto wa Rais wa zamani, Dk. Amani Abeid Karume, kuibuka na kufichua kile anachoamini kuwa ni sababu ya utata uliojitokeza sasa.

Mtoto huyo ni Mwanasheria, Fatma Karume, ambaye akiwa pamoja na Rais wa Chama cha Wanasheria wa Zanzibar (ZLS), Awadh Ali Said, waliuambia umma kupitia mahojiano ya moja kwa moja kwenye kituo kimoja cha televisheni jijini Dar es Salaam juzi kuwa sababu mojawapo ya kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar ni muundo wa uongozi unaomruhusu rais wa visiwa hivyo kuwa mmoja wa wajumbe katika Baraza la Mawaziri la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akifafanua, Fatma alisema kuwapo kwa nafasi ya moja kwa moja ya Rais wa Zanzibar kwenye Baraza la Mawaziri kunaibua mgongano inapotokea mshindi wa upande mmoja akiwa ni wa kutoka chama kingine na hiyo ni sababu mojawapo wanayoamini kuwa imechangia kufutwa kwa uchaguzi na pia kukwaza ukuaji wa demokrasia visiwani humo.

Alisema ni dhahiri hali huwa ngumu kwa baraza la mawaziri linaloundwa na watu wa itikadi ya chama kimoja kuchanganyika na mwingine mwenye itikadi tofauti, hasa katika mazingira ya kuwa na usiri katika baadhi ya mambo na kwamba, hilo huchangia kusuasua kwa maendeleo ya kidemokrasia visiwani Zanzibar.

Hata hivyo, ili kuondokana na mgogoro kama uliopo sasa, Fatma alisema ni muhimu kwa viongozi wa kisiasa nchini na kwingineko barani Afrika kuzingatia sheria na katiba zilizopo.

Awali, ilisisitizwa na wanasheria hao kuwa uamuzi wa kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar uliochukuliwa na Mwenyekiti wa Zec peke yake, haukuzingatia sheria na katiba na ndiyo maana sasa kumeibuka mgogoro wa kikatiba kwani kifungu kinachotumika kuhalalisha hoja ya kuendelea kubaki madarakani kwa Dk. Shein kimekuwa kikitafsiriwa vibaya kwa maslahi ya kisiasa.

Akielezea zaidi, Awadh alisema hakuna kifungu chochote kinachomruhusu Jecha kufuta uchaguzi na ndiyo maana hadi sasa hakuna mtu aliyethubutu kutaja kwa uwazi ni sheria ipi imempa nguvu mwenyekiti huyo wa Zec kufuta uchaguzi wa Zanzibar.

Source: Nipashe

Luis Munana Afichua Siri ya Jinsi Alivyojikuta Akipendana na Wema Sepetu

Wiki iliyopita picha za mtandaoni zilionesha kuwa Wema Sepetu na mshiriki wa Big Brother Hotshots kutoka Namibia, Luis Munana wamefunga ndoa.

Hakuna taarifa rasmi kutoka kwa wawili hao baada ya ‘ndoa’ hiyo kufungwa lakini Luis ameimbia Clouds E ya Clouds FM kuwa picha zilizosambaa n halisi na zilipigwa kwenye tukio hilo lililoshuhudiwa na familia zao zote mbili.

“Kwa sasa siwezi kuzungumzia chochote kuhusu picha hizo na ndio maana niliamua kuzifuta kwenye akaunti yangu kwakuwa lilikuwa tukio la faragha,” alisema Luis.

Luis alisema alikutana na Wema kwenye Instagram Party na kubaini kuwa wote walikuwa wakipendana bila kujua. “Alikuwa crush wangu, nami nilikuwa crush wake,” alisema.

Edward Lowassa/Zitto Kabwe Wapeleka Kilio CCM

Hawa jamaa wawili kwa kweli kwa pamoja tunaweza kusema wamepeleka kilio mtaa wa Lumumba, waswahili husema kwa mjinga huenda kicheko lakini kwa mwelevu huenda kilio.

Ujio wa Lowassa UKAWA umepeleka kilio kikubwa sana CCM japo kuwa wanajikazakinyasa wanakufa na Tai shingoni. Majuzi Mh. January Makamba aliita waandishi wa habari na kujinasibu eti CCMimepata wabunge 176 mpaka sasa na kufanikiwa kugomboa majimbo 11 yaliyokuwa yawapinzani.

Sasa habu ona hapo chini kilio Lowassa alichokipeleka CCM ambacho Makamba hakupenda kutaja.

1. Viti maalumu vya CCM vimepungua kwa 40% toka 79bunge lilopita la10 mpaka 62 bunge la11. Wakati CHADEMA na CUF viti hivyo vimeongezeka haya ni maumivu makubwa

2. CCM imenyang`anywauongozi wa majiji 4 kati ya majiji 5imebakiwa na uongozi katika jiji moja tu la Mwanza,. Majiji yafuatayo CCM nichama cha upinzani , Jiji la Mbeya, Jiji kuu la Dar-es-Salaam, Jiji la kitaliila Arusha na jiji la Tanga ambalo ilikuwa ni ngome yao, ngome imevunjwa.

3. Ruzuku ya CCM imepungua kwa 40% kutokana na kuraza rais alizopata , mgao wa ruzuku utakuwa 60 kwa 40 kwa maana 58% alizopataRais Magufuri kwa desilimali ya karibu itakuwa 60, na 39.8% ya kura za Lowassaalizopata kwa desilimali ya karibu itakuwa 40. Kwa hiyo CHADEMA imeinya`anyaCCM 20% ya ruzuku, je! Siyo maumivu hayo?

4. Uongozi wa halmashauri ndiyo usiseme. Kabla yaLowassa halmashauri zilizokuwa zinaongozwa na wapinzani zilikuwa 5 sasahalmashauli hizo zimeongezeika na kufika 30, katika halmashauri hizo CCMwatakuwa bachbancher.

5. Kilio kikubwa zaidi ni cha Zitto Kabwe alichowapaCCM katika halmashauri ya Kigoma/ujiji. Katika halmashauri hii hakuna mkuu wawilaya au mkuu wa mkoa kutia pua, halmashauri hii ni mali ya Zitto Kbakwe kwamaana ya Meya hadi madiwani. Halmashauri hii mwenyekiti wa CCM au mkuu wawilaya au mkuu wa mkoa wataenda kufanya nini? Wakati wakuu hao wameng`ang`anakumnyang`anya Kafulila ubunge wake huku nyuma Zitto anachukua halmashauri ya mjini,shame on them

6. Kuna kilio manispaa ya Mtwara/Mkindani na Mtwaravijijini kwa Hawa Ghasia, huenda Umeya wa Shilingi na wa Ndazigula umeotambawa.

Haya ndo ilitakiwa Mh. January Makamba ayaseme katika kile kikao chawaandishi wa habari alichokiitisha.

Source: ebaeban/Jamii Forums

TB Joshua ni Mgeni wa Nani Nchini Tanzania? Maswali Yazidi Baada ya Kutoonekana Uwanja wa Taifa Katika Sherehe za Kuapishwa

Kinyume na ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari Hajaonekana kwenye sherehe za kupishwa kwa Mh. Rais na wala jina Lake halikuwemo kwenye orodha ya wageni.

Hivi majuzi muhubiri maarufu kutoka nchini Nigeria TB Joshua aliwasili nchini kwa kile kilichoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari ikiwemo gazeti la Mwananchi kwamba muhubiri huyo amekuja nchini kushuhudia kupishwa kwa Rais Dr. John Pombe Magufuli.

Alipowasili uwanja wa ndege hapa Tanzania alipokelewa na baadhi ya viongozi walioongozwa na Dr. John Pombe Magufuli na akaenda moja kwa moja kumsalimia Rais Kikwete Ikulu magogoni Dar es Salaam.

Baada ya kutoka Ikulu muhubiri huyo alielekea nyumbani kwa aliyekuwa mgombea urais wa UKAWA na waziri mkuu mstaafu Mh. Edward Lowassa eneo ambalo ameonekana kuwepo kwa Muda mrefu akizungumza na Lowassa na viongozi wengine wa UKAWA.

MASWALI

1. Je, ujio wa Muhubiri huyo ilikuwa ni msafara binafsi Kinyume na ilivyoripotiwa na vyombo vya habari?

2. Vyombo vyetu vya habari havikupewa taarifa sahihi kuhusu sababu za ujio wa kiongozi huyo?

3. Kama ni msafara binafsi kwanini apokelewe na rais mteule na kutembelea Ikulu?

4. Je ni viongozi wa UKAWA wamemzuwia kuhudhuria sherehe hizo za kupishwa Rais kutokana na wao kugomea kusaini matokeo?

5. Je, bado yupo nchini? Maana kama tulijulishwa kuhusu ujio wake si vibaya tukajuzwa kuhusu kuondoka kwake.

Nawasilisha:

Forget About Zari ! .....Lulu And Diamond In Love !.....His Family Wants Him To Marry Lulu ?

Hot gossip is that, Lulu Elizabeth Michael and Diamond Platnumz are in love secretly and Diamond's family has no problem about it. This comes after reports broke Diamond and his baby mama Zari The Boss Lady are in bad terms. Reports further say that Zari frequently saw Lulu's messages to Diamond ones of them being so romantic, and when Zari questioned Diamonds sisters kept telling Lulu and Diamond's are close friends for a long time.

Recently gossip and entertainment newspapers and blogs have been reporting Lulu and Diamond's so sudden closeness, even during Romy Jonesi birhday(Diamond's cousin) Lulu spent most of her time with Diamond and weeks later which was Diamond's birthday the two were together most of the time too.

When Diamond's sister Esma Platnumz approached by GPL paparazzi to give a comment on Lulu and Diamond's friendship she had this to say "yeah, you guys we have told you our brother(Diamond) has no problem with anyone, to Lulu he has no problem their relationship is open, first of all Lulu is beautiful, she is cool and she has what it takes to be someone's wife, we have no problem with her, if she and Diamond agree to one another we will welcome her warmly" said Esma

When Diamond asked he replied "please these are family issues, sometimes it is better to let somethings pass as they are, I have been close to Lulu for a long time, let it be that and end there"

After Diamond, paparazzi started looking for Lulu and finally the talented actress was spotted at Wema Sepetu's birthday over the weekend. When Lulu asked about being in love with Diamond she denied it claiming she can't do it because Diamond used to date Wema Sepetu "to date Diamond ! where can I start ?, and how could I have come here at Wema's birthday while Diamond is Wema's ex ?, nothing like that, he is my close friend"

 Leave that alone, Recently it was reported Lulu and Wema were in cold war because Wema was unhappy the way Lulu supports Diamond in every move let alone their closeness which frightened Wema who used to date Diamond and rumors suggest Wema still loves Diamond despite their separation. However Lulu attended Wema's Royal birthday over the weekend and they were snapped together.

Do you believe Lulu and Diamond are new couple in town ?

Jumapili, 1 Novemba 2015

BUTIKU: WAZANZIBAR MSIKUBALI KURUDIA UCHAGUZI

Taasisi ya mwalimu Nyerere imeitaka tume ya uchaguzi ya Zanzibar ZEC kufanya kazi kwa kuzingatia katiba ya nchi na sheria na sio kutanguliza mbele maslahi binafsi ya kisiasa hatua ambayo inaweza kusababisha machafuko na umwagaji wa damu.

Akizungumza na vyombo vya habari mjini Musoma, mkurugenzi mtendaji wa taasisi hiyo mzee Joseph Butiku, amesema amekerwa na tabia ya ZEC kusitisha uchaguzi na kushindwa kuwatangazia wananchi kiongozi wao waliomchagua, huku ikishindwa kuheshimu matakwa ya wananchi waliopiga kura katika visiwa vya Zanzibar.

Aidha mzee Butiku amewataka wananchi wa Zanzibar kutokubali tena kurudia upigaji wa kura hadi hapo yatakapotolewa maelezo ya kuridhisha na wahusika waliosababisha uchaguzi huo kufutwa pia waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria

Kwa sababu hiyo amewataka viongozi kuheshimu sheria na katiba ya nchi na kwamba chama ambacho kinadhani kimeshindwa katika uchaguzi huo kikubali matokeo badala ya kuifanya zanzibar ni mali ya chama fulani pekeee.

CCM Washikana 'Uchawi' Baada ya Kulipoteza Jimbo La Bunda

BAADHI ya vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Bunda wamemtuhumu mwenyekiti wa chama hicho wilayani hapa, Chacha Gimanwa, kwamba alichangia jimbo la Bunda Mjini kuchukuliwa na mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu.

Vijana hao walitoa tuhuma hizo, juzi wakati wakitembea matembezi ya amani ya kushangilia ushindi wa mgombea urais wa CCM, Dk Jonh Magufuli katika mitaa mbalimbali ya mji wa Bunda.

Katika uchaguzi mkuu uliopita CCM ilipoteza jimbo hilo, baada ya Stephen Wasira aliyekuwa akitetea kiti hicho kushindwa na mgombea wa Chadema, Ester Bulaya.

Hata hivyo Wasira ambaye pia ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika hivi karibuni akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza alidai kuwa katika uchaguzi huo kulikuwa na hujuma.

Wanachama hao wa CCM wakiwa wamebeba mabango baadhi yao walisikika wakimtaja moja kwa moja Gimanwa kwamba ndiye alisababisha CCM kushindwa katika jimbo hilo na kuomba uongozi wa juu wa chama hicho umchukulie hatua.

Hata hivyo, Gimanwa akizungumza na mtandao huu kwa njia ya simu jana alisema kuwa tuhuma hizo hazina msingi wowote na kwamba kamwe hawezi kukihujumu chama chake.

“Hicho ni kikundi cha watu wachache tu wanaotaka kuniharibia jina.Mimi kura yangu ni moja na wapiga kura ni wengi, sasa iweje mimi nisababishe mgombea wa jimbo la Bunda mjini ashindwe?” Alihoji.

 Alisema yeye kama mwenyekiti wa CCM alikuwa akifanya kampeni pia katika jimbo la Bunda vijijini, na siku tatu kabla ya uchaguzi mkuu alirudi tena Bunda mjini na kuendelea na kampeni.

Watu Sita Wapoteza Maisha Katika Ajali ya Gari Morogoro

Watu sita wamefariki dunia baada ya gari ndogo waliokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na basi la abiria mali ya kampuni ya Princess Muro, lililokuwa likitokea Dar es salaam kuelekea Tunduma, katika eneo la hifadhi ya taifa ya Mikumi, barabara kuu ya Morogoro-Iringa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Leonard Paulo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo katika eneo la hifadhi ya taifa ya Mikumi, ikihusisha gari ndogo la abiria aina ya Toyota Noah lenye namba za usajili T 359 BBA iliyokuwa imebeba abiria sita wakiwemo wanawake wawili na wanaume wanne ambayo ilipasuka tairi ya Mbele ya kuyumba ovyo barabarani na kugongana na basi hilo la Princess Muro lenye namba T 160 BBC na kusababisha vifo kwa abiria wote wa Noah.

Amesema basi hilo la abiria aina ya Zangton lililoharibika zaidi mbele huku Noah ikiharibika kabisa, likuwa likiendeshwa na Silos Wilfred (55) mkazi wa Mbeya ambaye anahojiwa na polisi kuhusiana na tukio hilo, na kwamba basi alilokuwa akiendesha lilikuwa na abiria 59 ambao hawakupata madhara makubwa, isipokuwa michubuko kidogo kwa baadhi yao na walitafutiwa usafiri kuendelea na safari.

Katika upekuzi wa miili ya abiria waliokuwa kwenye Noah inayodaiwa kuhusika na ubebaji wa magazeti, viligundulika vitambulisho vimne vya Ali Nduti Mohamed (27), mkazi wa Mbeya,Sani Elion Mkwabe (24) mkazi wa Kunduchi, Patrick Mkelegene (43) mkazi wa Buguruni Malapa na Selemani Omary (30) ambaye makazi yake hàyajaweza kujulikana Mara moja.

Miili ya watu hao waliopoteza maisha imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.

Nimeikumbuka Kauli ya DK SLAA "Chama Changu Chadema Hakiwezi Kushinda Urais Mwaka huu 2015 Kutokana na Kula Matapishi Yetu..."

DK Slaa
"Chadema hakikuwa chama cha kukumbatia ufisadi na mafisadi..hakikuwa chama cha kusomba watu na magari mikutanoni...hakikuwa chama cha kuiba na kununua kura...sasa Chadema hii si ile tulioijenga....
nimeamua kustaafu siasa maana najua chama changu hakiwezi kushinda urais mwaka huu 2015 kutokana na kula matapishi yetu..." Dk Slaa:

Je Slaa ni mkweli??

Mengi Azomewa Diamond Jubilee, Aokolewa na Membe

Mzee yamemkuta leo pale kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee leo.Ameokolewa na Mh Membe ambaye amemtoa kwa gari lake(pichani).Lakini pia Mwandishi Sam Maela wa ITV leo mchana kapata mshike mshike wa kushiba pale Lumumba,ilibidi aokolewa na polisi.Jamani haste haste.Kuna maisha baada ya Uchaguzi.Lile lilikuwa gemu tu.Mwacheni huyo Mzee,
 SOURCE - JAMII FORUMS

Bella Amfumania Kalama na Mchepuko Ambae ni Mdogo wake...Avua Pete ya Uchumba

Isabelah na Wagoni wake
Tukio hilo lilijiri nyumbani kwa Bella, Makumbusho jijini Dar es Salaam baada ya kurejea ghafla kutoka safari ya kimuziki kwenye kampeni za udiwani katika Mikoa ya Iringa na Morogoro.

Siku ya tukio, paparazi wetu alikuwa akipita na hamsini zake katika eneo hilo ndipo alipokutana na songombingo hilo ambapo kelele za Bella zilifika nje huku milio ya vyombo kuvunjwa ikitawala.Paparazi wetu alitia nanga kwenye nyumba hiyo ambapo majirani nao walianza kufika na kumkuta Bella akimshushia kipondo mdogo wake huyo huku akianika uhusiano wao.



Isabelah Akivua pete ya Uchumba



“Huyu ni mdogo wangu kabisa. Tunachangia mama. Nilimleta hapa kwa ajili ya muziki. Sasa mimi nikiwa safarini, kuna mtu alinipigia simu na kuniambia Winnie anaingia na kulala na Kalama chumbani kwangu.

“Sikutaka kumwambia Kalama kuhusu nilichoambiwa, nikaamua kuja ghafla ili nithibitishe. Kumbe kweli. Yaani mdogo wangu kabisa ananifanyia hivi jamani?” alihoji Bella huku akivua pete ya uchumba aliyovalishwa na Kalama na kumtupia.
Mazingira ya eneo la tukio, sakafuni kulikuwa na vipande vya chupa ambavyo vilitokana na Bella kuvunja glasi kwa lengo la kutaka kumpasua kichwani mdogo wake.

Juzi, paparazi wetu alifika tena nyumbani hapo na kuambiwa na msichana mmoja kwamba, Kalama aliondoka baada ya tukio huku Winnie akipokea msamaha wa ‘damu nzito kuliko maji’.Bella alipopigiwa simu na kuulizwa hatima yake na Kalama, alisema: “Mimi na Kalama basi japo ananipigiapigia simu kuniomba msamaha.”
Kalama hakupatikana kuzungumzia hilo.
GPL