Jumatatu, 14 Desemba 2015

Kazi ya kwanza kuifanya Naibu Waziri Kigwangwala baada ya kuapishwa Dec 12 (+video).

Kwenye zama hizi za Hapa kazi tu za Mheshimiwa Rais John Magufuli,tunashuhudia mambo mengi ambayo mengine tulikua hatuyafikirii kama yanawezekana kufanyika kutoka kwa viongozi wetu,Dec 12 Mawaziri na Manaibu wao walioteuliwa na Rais Magufuli waliapishwa na baada ya kuapishwa...

Giroud na Ramsey waipeleka Arsenal kileleni, huku wakiiombea ushindi Chelsea

December 13 mechi za Ligi Kuu Uingereza ziliendelea kama kawaida, baada ya December 12 kupigwa michezo kadhaa ya muendelezo wa Ligi. Mchezo wa kwanza kupigwa Jumapili ya December 13 wa Ligi Kuu Uingereza ni mchezo kati ya Aston Villa dhidi ya Arsenal. Arsenal wanaoufundishwa na kocha waliyedumu nae kwa...

Real Madrid wakubali kuacha point tatu katika dimba la El Madrigal dhidi ya Villarreal

Baada ya December 12 watani zao wa jadi klabu ya FC Barcelona ya Hispania kucheza mchezo wake wa 15  wa Ligi Kuu Hispania dhidi ya klabu ya Deportivo La Coruna katika uwanja wao wa nyumbani Nou Camp na kuambulia sare ya kufungana goli 2-2, December 13 ilikuwa zamu ya Real Madrid kucheza dhidi ya Villarreal. Wakati...

Wakati Wapinzani Wakipinga Uteuzi wa Waziri Sospeter Muhongo, Mwenyewe Aibuka na Kusema Haya Makubwa

WAKATI wapinzani wakipinga uteuzi wa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, waziri huyo amewasihi wananchi kumvumilia kidogo, ili baada ya muda mfupi atoe mpango wa maendeleo ya wizara hiyo, ambao pamoja na mambo mengine, utaelezea bei ya nishati hiyo itakavyoshuka.  Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kuapishwa...

Wafanyabiashara 15 Waliokaidi Agizo la Rais Kukiona Cha Moto

MAKAMPUNI 15 yaliyokwepa kodi baada ya kutorosha makontena yao, yamejisalimisha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), lakini yameshindwa kulipa kodi ndani ya siku saba za msamaha wa Rais John Magufuli. Kodi inayodaiwa kwa kampuni hizo ni Sh bilioni 3.75, hivyo watachukuliwa hatua za kisheria kwa kukwepa kulipa kodi, ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani. Kaimu...

Mdahalo Wa Tahliso Kujadili Hotuba ya Magufuli Waingia Dosari Baada Ya Wanafunzi wa UDSM Kuupinga

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye  jana alinusuru kuvunjika kwa mdahalo ulioandaliwa na Jumuiya ya Taasisi za Elimu ya Juu (TAHLISO), baada ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuupinga. Mdahalo huo ulilenga kujadili hotuba ya Rais Dk. John Magufuli aliyosoma bungeni Novemba 20, mwaka huu wakati akizindua Bunge la 11. Dosari ...

Chadema Bado Hawajakubali Yaishe...Waapa Kumshughulikia Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo Bungeni

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeahidi kumshughulikia Bungeni, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kikidai kuwa bado hajasafishwa kwenye kashfa ya akaunti ya  Escrow. Ahadi hiyo ilitolewa juzi na Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema Taifa, John Mnyika katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Handeni, akimnadi...

Asipofunga Zipu…Nay wa Mitego Atakufa Kwa Ngoma

Staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Eribaliki ‘Nay wa Mitego’  akijiachia na mrembo mpya mwenye umbo dogo kwenye bwawa la kuogelea katika Hoteli ya White Sands iliyopo Mbezi Beach jijini Dar. KIWEMBE! Ndivyo unavyoweza kusema kufuatia staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Eribaliki ‘Nay wa Mitego’ kunaswa akiwa na mrembo mpya mwenye umbo dogo yaani (mbichii) huku...

Nape: Nitaanza Kushughulikia Sheria na Nidhamu Michezoni

Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo, Nape Nnauye ameahidi kushughulikia sheria mbalimbali zinazosimamia sekta hiyo ili kuongeza nidhamu michezoni. Nape aliyeapishwa juzi kuanza kibarua hicho, ataiongoza wizara hiyo iliyokuwa ikiongozwa na Dk Fenella Mukangara, huku ndoto za Watanzania zikiwa ni kuona kiwango cha michezo kilichoporomoka, kinakua. Akizungumza ...

Diamond Platnumz na Zari Washinda Tuzo Nchini Uganda

STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platinumz’ pamoja na mchumba wake Zarinah Hassan ‘Zari The Bossy Lady’ wamepata Tuzo za Abryanz Style and Fashion (ASFA 2015) zilizofanyika Kampala, Uganda usiku wa kuamkia leo.Wawili hao wameibuka kidedea katika kipengele cha East Africa Most Stylish Couple. Mbunifu wa mavazi, Martin Kadinda naye ameibuka kidedea...