Jumamosi, 13 Septemba 2014

MFUNGWA AKUTWA NA SIMU MWILINI


 Tatizo la kuingiza bidhaa kimagendo ndani ya magereza ya Kenya imekuwa kero kubwa kwa maafisa wa magereza.
Kwa baadhi ya watu simu ya mkononi ni kifaa tu cha mawasIliano ilihali kwa wengine ni kifa ambacho kinaweza kukuweka katika hali ya kufa kupona.
Mfungwa mmoja nchini Kenya amewaacha wengi vinywa wazi, baada ya simu tatu za mkononi kutolewa mwilini mwake. Inaarifia aliziingiza simu hizo mwilini mwake kupitia sehemu yake nyeti ya nyuma.
 
 Mfungwa ambaye alitolewa simu mwilini kwa kufanyiwa upasuaji.
Tatizo la kuingiza bidhaa kimagendo ndani ya magereza ni kero kubwa kwa maafisa wakuu wa magereza.
Wamekuwa kwa miaka mingi wakijaribu kulikomesha tatizo hilo bila mafanikio.Kwa njia yoyote ile wafungwa huingiza bidhaa kama simu katika magereza nchini Kenya kinyume na sheria za magereza.
Maafisa wa magereza wanakiri kwamba wafungwa hawa wakati mwingine hushirikiana na walinzi wa magereza kuingiza bidhaa katika magereza kimagendo.

Shearer asema Welbeck atang'ara Arsenal


 
Mshambuliaji wa Arsenal Danny Wellbeck kushoto 

Mshambuliaji mpya wa kilabu ya Arsenal Danny Welbeck anaweza kufunga mabao 25 kwa msimu mmoja ,hayo ni matamshi ya aliyekuwa mshambuliaji wa England Allan Shearer.
Wellbeck mwenye umri wa miaka 23 alijiunga na kikosi cha The Gunners kutoka kilabu ya Manchester United kwa kitita cha pauni millioni 16 katika siku ya mwisho ya dirisha la kuwasajili wachezaji wa soka barani ulaya na anaweza kuanzishwa kwa mara ya kwanza dhidi ya watetezi wa ligi hiyo Manchester City siku ya jumamosi.
Nimesikia watu wakisema kwamba Wellbeck hawezi kufunga mabao 20 ama 25 kwa msimu mmoja ,sikubaliani na hilo Shearer aliiambia Radio 5 live ya BBC'',.
''Sasa ana uwezo wa kuonyesha umahiri wake katika ligi hiyo.''.
Siku ya Alhamisi Meneja wa kilabu ya Manchester United Van Gaal alisema kuwa Wellbeck hakuweza kufunga mabao ya kutosha wakati alipkuwa katika kilabu hiyo ya Old Trafford.
Mshambuliaji huyo ambaye ni mzaliwa wa Manchester ambaye aliifunga mabao yote mawili timu ya Uingereza dhidi ya Switzerland siku ya jumatatu ,hajawahi kufunga zaidi ya mabao tisa katika ligi ya Uingereza tangu alipoanza kuchezea mwaka 2008.

WAATHIRIWA WA MABOMU MBAGALA WALALAMIKA


Nyumba iliyoharibiwa na bomu kama inavyoonekana.
Mkutano kati ya waandishi habari na Waathirika wa Mabomu Mbagala, ambao umefanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mbagala Kuu ,jijini Dar-Es-Salaam mapema leo .
Waathirika hao wapatao 1,361 kati yao 25 wameishapoteza maisha kutokana na athari za mabomu hayo.
Mlipuko huo wa mabomu ni tukio lililotokea tarehe 29 April mwaka 2009,majira ya saa sita kasa robo katika eneo la mbagala kuu,hii ni baada ya mabomu hayo kulipuka katika ghala la silaha ya kambi ya ulinzi ya jeshi ya jeshi la ulinzi la wananchi wa Tanzania(JWTZ) namba 671 kj.
Mabomu hayo yaliyokua yanalipuka kwa mfululizo yalisababisha vifo,kujeruhi,kuharibu makaazi na mali za watu kuharibiwa vibaya na kwa upande wa afya athari zilizojitokeza ni maradhi ya TB ama kifua kikuu,upofu wa macho,saratani,tezi yamkojo na kadhalika.
Leo hii wananchi wanadai kua serikali imewasahau na kuwatelekeza waathirika hao kiasi cha huduma za afya kukosekana,malazi kutorejea kama walivyoahidiwa na kila walipodai fidia wanapata majibu yasiyo faa ikiwemo, wanaoweza kusubiri wasubiri ama wasio kua na subira basi wajitoe.

Alichokiandika Steve Nyerere kuhusu kujiuzulu uongozi Bongo Movie.

mks 
Kupitia mtandao wa picha yaani Instagram aliyekuwa Rais wa Bongo Movie Unity,Steve Nyerere  leo ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo kwenye klabu hiyo ya Bongo Movie huku akishindwa kuweka sababu iliyomfanya kujiuzulu.
nyyerere 
Katika maelezo yake chini ya picha yake ameandika>>’Napenda kuwashukuru ndugu zangu wote wasanii wenzangu kaka zangu mama zangu rafiki zangu mimi pamoja na family yangu’
‘Nimeamua kujiuzulu uongozi wa Bongo Movie nabaki kuwa mwanachama wa kawaida nina imani tulifurahi pamoja tukahudhunika pamoja na daima tutakuwa pamoja’.

nyerere2

MAMA MZAZI WA NEY WA MITEGO AMTILIA SHAKA MWANAE

nay 5 
Mama mzazi wa mkali wa bongofleva Nay wa Mitego ameongea kwa mara ya kwanza na millardayo.com na kusema ana wasiwasi na mwanae ambae hivi karibuni ametoa video mpya aliyoifanya nchini Kenya.
Amekiri kweli kwamba siku kadhaa zilizopita ilibidi amwite na kumuweka chini Nay wa Mitego akitaka amueleze kama ni kweli amejiunga na ‘freemason’ ambayo wengi wanaitafsiri kwamba ni dini ya kumwabudu shetani kitu ambacho kiliwahi kukanushwa na aliyewahi kuwa mmoja wa viongozi wa freemasons Tanzania.
Mama anasema alimketisha Nay chini baada ya video ya ‘Mr. Nay’ kutoka ambapo baadhi ya picha sio za kawaida mfano damu pamoja na alama zilizotumika ndani yake. nay 4Amesema ‘Naitwa Matilda Mwaipopo ni mama mzazi wa Nay, kwakweli mwanangu namchukulia lakini sifa tu zinazokuja kama Nay kwenye magazeti, Nay freemason, watu wanakuja wananisimamisha…. mwanao Nay kweli? mbona tunasikia freemason? basi kichwa changu kinapagawa…. ‘
‘Nikiangalia miziki anayoifanya kama hii aliyoitoa juzi, jamani mwanangu anaambiwa freemason usikute kweli freemason, Nay wa Mitego nimemuita…. mwanangu vipi? ninayoambiwa ni ya kweli? Freemason wewe? mbona wimbo wako huu siuelewielewi?  ananiambia mama mimi sio freemason, namwambia hapana mwanangu hapana….. nasikia freemason watu wanatoaga hata wazazi sadaka’
nay 3‘Mimi ndio mama niliebakia baba yenu alifariki aliniacha ukiwa na miaka mitatu nimejitahidi kukulea mpaka leo…… unitoe sadaka mama yako kweli?????!!! Nay wa Mitego sana ni kucheka…… anaona tu mama kama anapagawa, lakini kwakweli mwanangu simuaminiamini miziki yake hii anayoifanya’
nay 2
Nay 1 
Unaweza kumsikiliza mama mzazi mwenyewe akiongea hapa chini…

EPL: Matokeo ya Man City vs Arsenal haya hapa

IMG_7139.JPG
Baada ya mapumziko ya takribani siku 14, hatimaye ligi kuu ya England imerejea tena leo kwa mchezo mkali kati ya Man City dhidi ya washika bunduki Arsenal.
Mchezo uliopigwa kwenye dimba la Emirates ulikuwa mkali na wa kusisimua kwa timu zote zikipoteza nafasi kadhaa za ushindi.
Matokeo ya mwisho ya mchezo yalikuwa sare ya 2-2.
Sergio Aguero alianza kuifungia City katika dakika ya 28, na mpaka mapumziko vijana wa Pellegrini walikuwa mbele kwa 1-0.
Kipindi cha pili kilianza vizuri kwa Arsenal na ndani ya dakika 15 tu Jack Wilshare aliisawazishia timu yake.
Dakika kadhaa baadae Alexis Sanchez akaongeza goli la pili, lakini furaha ya Arsenal ikadumu kwa muda mfupi baada ya Martin Demichelis kuisawazishia City kwa goli la kichwa kupitia kona ya David Silva.
Dakika chache kabla ya filimbi ya mwisho Man City walikosa makosa magoli kadhaa huku Samir Nasri akikataliwa goli baada ya kufunga akiwa offside.

EPL: Matokeo ya Chelsea vs Swansea City

IMG_7144.JPG
Mchaka mchaka wa ligi kuu ya England umeendelea tena jioni hii kwa mchezo uliowakutanisha vilabu viwili vilivyokuwa vikishika nafasi ya kwanza na ya pili katika msimamo wa ligi kuu ya England – Chelsea dhidi ya Swansea.
Mchezo huo uliopigwa kwenye dimba la nyumbani la Chelsea Stamford Bridge umeisha kwa ushindi wa 4-2 kwa vijana wa Jose Mourinho.
Swansea walikuwa wa kwanza kupata goli baada ya John Terry kujifunga katika dakika za mwanzo za mchezo kabla ya Diego Costa kusawazisha mwishoni mwa kipindi cha kwanza.
Kipindi cha pili Chelsea walirudi na kasi ya ajabu na kufanikiwa kupata mabao mawili haraka haraka kupitia Diego Costa tena ambaye leo alifunga hattrick.
Loic Remy akiingia kuchukua nafasi ya Diego Costa alifunga goli la nne kabla ya Jonjo Shelvey kuifungia Swansea goli la pili.
Mpaka refa wa mchezo Mark Claternburg anapuliza filimbi ya mwisho matokeo yalikuwa 4-2.

La Liga: Matokeo ya FC Barcelona dhidi ya Athletic Bilbao

IMG_7171.JPG
Ligi kuu ya Hispania maarufu kama La Liga imeendelea leo kwa michezo kadhaa kupigwa – FC Barcelona waliikaribisha Athletic Bilbao kwenye dimba la Nou Camp.
Mchezo huo uliomalizika muda mfupi uliopita umeisha kwa matokeo ya ushindi wa 2-0 kwa FC Barcelona.
Akiwa anahitaji magoli mawili tu kufikisha jumla ya magoli 400 katika maisha yake ya soka, Lionel Messi alishindwa kutimiza idadi hiyo lakini badala yake akatoa assists mbili za magoli ya ushindi ambayo yote yalifungwa na Neymar.
Timu zilipangwa kama ifuatavyo:
Barcelona: Bravo, Montoya, Mascherano (Pique 46), Mathieu, Alba, Busquets, Rakitic, Iniesta, Munir (Neymar 63), Messi, Pedro (Sandro 77).
Subs: Ter Stegen, Xavi, Sergi Roberto, Adriano.
Booked: Busquets.
Goal: Neymar 80, 84.
Athletic Bilbao: Iraizoz, De Marcos, Gurpegui, Laporte, Balenziaga, Susaeta (Ibai 64), Iturraspe, Benat (Unai Lopez 64), Mikel Rico (Viguera 83), Muniain, Aduriz.
Subs: Iago Herrerin, San Jose, Iraola, Etxeita.
Booked: Aduriz.
Referee: David Fernandez Borbalan.
Attendance: 80,081

EPL: Kilichoikuta Liverpool dhidi ya Aston Villa hiki hapa EPL: Kilichoikuta Liverpool dhidi ya Aston Villa hiki hapa

IMG_7180.JPG
Kwa mara ya nne mfululizo klabu ya Liverpool imekuwa ikikosa matokeo chanya kwenye uwanja wa nyumbani wa Anfield kila inapocheza na kikosi cha Paul Lambert – Aston Villa.
Leo hii wakiwa nyumbani Liverpool huku ikiwachezesha kwa mara ya kwanza Mario Balotelli na Adam Lallana ndani ya Anfield, kikosi cha Brendan Rogers kimepoteza mechi ya pili ya msimu baada ya kukubali kipigo cha 1-0 kutoka kwa Aston Villa.
Goli la mapema kipindi cha kwanA lilofungwa na Gabry Agbonlahor lilitosha kuiadhibu Liverpool mbele ya mashabiki wao.
Timu zilipangwa kama ifuatavyo:
Liverpool (4-2-3-1): Mignolet 6, Manquillo 6, Lovren 5.5, Sakho 6, Moreno 5.5, Gerrard 6, Henderson 6, Markovic 7 (Borini 71, 5), Coutinho 6, Lallana 5.5 (Sterling 61, 6), Balotelli 5.5 (Lambert 71, 5.5)
Subs (not used): Jones, Enrique, Toure, Lucas
Booked: Lallana, Moreno
Goals: NONE
Aston Villa (4-5-1): Guzan 7, Hutton 6, Senderos 7.5, Baker 8, Cissokho 7, Cleverley 7 (Sanchez 86), Westwood 7, Delph 7.5, Agbonlahor 7 (Bent 90), Weimann 7 (N’Zogbia 72, 6), Richardson 6.5
Subs (not used): Okore, Bacuna, Given, Grealish
Booked: Hutton
Goals: Agbonlahor (9)
Man of the match: Nathan Baker
Referee: Lee Mason
Attendance: 44, 689