Jumamosi, 23 Mei 2015

IRELAND YAFANYA MAAMUZI KUHUSIANA NA NDOA ZA JINSIA MOJA

wapiga kura wajitokeza kwa wingi nchini Ireland ili kuamua kuhusu kuhalalishwa kwa ndoa za watu wa jinsia moja.

Wapiga kura wengi wameripotiwa kujitokeza kwenye kura ya maoni nchini Ireland ya kuamua iwapo ndoa za watu wa jinsia moja zinaweza kuhalalishwa .
Katika sehemu nyingine ukiwemo mji mkuu Dublin na miji mingine, idadi ya wapiga ilitarajiwa kufikia takriban asilimia 60.

Ndoa za jinsia moja   

Wataalamu wengi wa Ireland walio katika mataifa ya kigeni walirudi nyumbani kupiga kura.
Wale wanaounga mkono ndoa za jinsia moja walitarajia watu wengi kujitokeza.

Wapenzi wa jinsia moja wakitoka katika kituo cha kupiga kura

Ikiwa kura hiyo itafanikiwa Ireland itakuwa nchi ya kwanza kuhalalisha ndoa za jinsia moja kupitia upigaji kura.
Matokeo yanatarajiwa kutangazwa baadaye leo.

 

ZAIDI YA WATU 40 WAUAWA MEXICO

Polisi nchini Mexico

Takriban watu 43 wameuawa wakati wa ufyatulianaji wa risasi katika jimbo la Michoacan nchini mexico kati ya vikosi vya usalama na genge moja lenye silaha.
Mapigano hayo yalianza wakati magari ya polisi yalipofyatuliwa risasi kwenye barabara moja kuu katika kijiji kilicho karibu na mpaka na jimbo la Jalisco.
Moja ya megenge hatari zaidi ya madawa ya kulevya, liko eneo hilo na limekuwa likipigana vita vigumu katika jimbo la Michoacan kwa miaka mingi.
Maafisa kutoka kwa idara za usalama wanaelekelea eneo hilo kufanya uchunguzi.

REAL MADRID YAWASILIANA NA BENITEZ

Rafael Benitez

Mkufunzi wa kilabu ya Napoli Rafael Benitez ameorodheshwa miongoni mwa makocha wataokumrithi Carlo Ancelotti katika kilabu ya Real Madrid.
Ancelotti anatarajiwa na wengi kuachana na kilabu hiyo baada ya mechi ya mwisho na Getafe wikiendi hii.
Mazungumzo kati ya Real Madrid na Benitez yanaendelea huku kandarasi ya Benitez katika kilabu ya Napoli ikitarajiwa kukamilika mwezi ujao,ijapokuwa hakuna makubaliano yalioafikiwa.
Klabu ya West Ham pia iliwasiliana na kocha huyo ambaye aliwahi kuifunza Chelsea na Liverpool.

Carlo Ancelotti

Mkufunzi wa West Ham ambaye anaiandaa West Ham dhidi ya Newcastle anatarajiwa kuanzisha mazungumzo na klabu hiyo kuhusu hatma yake wiki ijayo.
Benitez alianza kazi ya ukufunzi katika kilabu ya Real Madrid B na pia amewahi kuifunza Valladolid,Osasuna,Etramadura,TenerifeValencia na Inter Milan.

DAVID LUIZ:'NIMEWAHI KUSHIRIKI NGONO'

David Luiz kushoto 


Mlinzi wa klabu ya Paris St-Germain David Luiz amevishtumu vyombo vya habari kwa kukosa heshima baada ya kukanusha madai kwamba yeye hajawahi kushiriki katika tendo la ngono.
Ripoti hizo zilianza kusambaa baada ya mchezaji huyo wa zamani wa Chelsea mwenye umri wa miaka 28 kusema katika instagram kwamba yeye na mpenziwe ''wako tayari kungojea''.
Aliiambia BBC focus kwamba.''Dini yangu,ubaatizaji wangu,nafurahia.
Watu wanasema maneno kila mahala kuhusu iwepo mimi sijawahi fanya tendo la ngono.''Ukweli ni kwamba mimi nishawahi kushiriki katika tendo hilo''.
 
    Luiz 
Aliongezea:Watu wengine katika vyombo vya habari hawaheshimu maisha ya watu.
Mimi ninawaheshimu wenzangu kwa hivyo sina bughudha ya aina yoyote.

 

Hivi ndivyo ilivyokuwa kwenye #TuzozaWatu2015.. Pichaz na list yote ya washindi iko hapa



 Kilichosubiriwa kwa hamu na watu wengi ni tukio zima la Tuzo za Watu ambapo fainali yake ilikuwa jana MAY 22 2015.. Kutokana na utaratibu uliowekwa washiriki wote waliteuliwa na watu na baadae mchakato ukakamilika kwa kuwapigia kura washiriki hao.

Yes.. jana usiku shughuli yote ilikuwa pale Hyatt Regency, hapa nina baadhi ya PICHAZ ambazo nimekuwekea pamoja na list ya washindi wote.
Mtangazaaji Zamaradi Mketema wa Clouds TV na Clouds radio

Mtangazaji wa runinga anayependwaSalim Kikeke (BBC Swahili)
                  Muigizaji wa kike wa filamu anayependwa- Wema Sepetu
                                                  Ommy Dimpoz


List ya washindi hii hapa
Mtangazaji wa redio anayependwa- D’Jaro Arungu – TBC FM.
Kipindi cha redio kinachopendwa- Papaso – TBC FM.
Mtangazaji wa runinga anayependwaSalim Kikeke (BBC Swahili)
Kipindi cha runinga kinachopendwa- Mkasi (EATV)
Blog/Website inayopendwa- millardayo.com
Muongozaji wa video anayependwa- Hanscana
Muongozaji wa filamu anayependwa- Vincent ‘Ray’ Kigosi
Muigizaji wa kike wa filamu anayependwa- Wema Sepetu
Muigizaji wa kiume wa filamu anayependwa- Hemedy PHD
Mwanamuziki wa kike anayependwa- Lady Jaydee
Mwanamuziki wa kiume anayependwa- Ali Kiba
Filamu inayopendwa- Kigodoro
Video ya muziki inayopendwa
Nani kama Mama – Christian Bella f/ Ommy Dimpoz.