Wabunge wawili Bashe na Musukuma wamekamatwa leo asubuhi kabla ya kikao
cha Kamati Kuu kuanza kutokana na kudaiwa kubeba ajenda ya "kwenda
kumpinga Mwenyekiti".
Kundi hili la wabunge lililokuwa na mjumbe mwingine, Adam Malima
lilipanga Peter Serukamba ndiye awe kinara wa kuanzisha hoja ya kumpinga
mwenyekiti.
Hata hivyo, kabla ya kutimiza azma yao walijikuta mikononi mwa Polisi
huku Serukamba akidhibitiwa na kukosa kuwasilisha hoja ya kumpinga
mwenyekiti, Magufuli.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa amethibisha na
kuwataja waliokamatwa kuwa ni Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe na
Mbunge wa Geita vijijini ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita,
Joseph Kasheku maarufu kama Musukuma na Malima.
“Hao ndio waliokamatwa na bado tunaendelea na mahojiano na wengine bado tunaendelea kuwatafuta,”amesema Mambosasa.
Chanzo chetu kimedokeza kwamba huenda wakaendelea kushikiliwa hadi pale mkutano mkuu utakapomalizika!
Chanzo:Jamii Forums
Jumamosi, 11 Machi 2017
Home »
» DODOMA: Bashe, Malima na Musukuma Mbaroni Wakidaiwa Kupanga Kuhujumu Vikao Vinavyoendelea
DODOMA: Bashe, Malima na Musukuma Mbaroni Wakidaiwa Kupanga Kuhujumu Vikao Vinavyoendelea
Related Posts:
Jinsi Ya Kumfanya Mwanamke Apagawe KwakoKuna vitu vingi ambavyo unaweza kutumia kwa manufaa yako ili kufanya wanawake wakuone unavutia. Amini usiamini, hivi vitu si lazima uwe tajiri wala uwe na urembo wowote. Mwanzo kati ya vitu hivyo vingi ni rahisi kuvitumia … Read More
Mke Wangu Ana Mimba, Katokea Kunichukia na Kampenda Mume wa Mtu Jirani na Chumba Tulichopanga Husika na kichwa cha habari hapo juu Mimi kijana mwenzenu nasikitika sana na hii tabia ya mke wangu, kwakweli ana nichan… Read More
Majibu ya Kamanda Mambosasa Kuhusu Kutofautiana Kauli na RPC IringaMtandao kumekuwa na Gumzo kuhusu kauli ya Kamanda Mambosasa na RPC wa Iringa kutofautina kuhusu kupatiikana kwa Abdul Nondo Mwanafunzi aliyedaiwa Kutekwa, Kamanda Mambosasa alisema Abdul Nondo alikutwa akiendelea na Shughu… Read More
Huu Hapa Ukweli Mchungu Kwa Wadada Wanaolalamika Hawana Bahati za Kuolewa....Wanaume wengi hawajafikia ndoto zao, wanatamani kupata wanawake watakaowatia moyo kuwafikisha kwenye ndoto zao! Ukweli mchungu ni kwamba wanawake hawawataki wanaume ambao bado wako safarini kuelekea ndoto zao! Wanataka wal… Read More
Nabii Aliyemuamuru Muumini ‘Piga Kelele’ Aeleza Tukio lilivyokuwa Nabii Olivia kutoka kanisa la Repohim Ministry Sinza jijini Dar es salaam amefunguka kwa mara ya kwanza kuzungumzia clip ya video ambayo ilisambaa mtandaoni wiki hii ikimuonesha akimuamuru muumini kupiga kelele kwa nguvu… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni