Wabunge wawili Bashe na Musukuma wamekamatwa leo asubuhi kabla ya kikao
cha Kamati Kuu kuanza kutokana na kudaiwa kubeba ajenda ya "kwenda
kumpinga Mwenyekiti".
Kundi hili la wabunge lililokuwa na mjumbe mwingine, Adam Malima
lilipanga Peter Serukamba ndiye awe kinara wa kuanzisha hoja ya kumpinga
mwenyekiti.
Hata hivyo, kabla ya kutimiza azma yao walijikuta mikononi mwa Polisi
huku Serukamba akidhibitiwa na kukosa kuwasilisha hoja ya kumpinga
mwenyekiti, Magufuli.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa amethibisha na
kuwataja waliokamatwa kuwa ni Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe na
Mbunge wa Geita vijijini ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita,
Joseph Kasheku maarufu kama Musukuma na Malima.
“Hao ndio waliokamatwa na bado tunaendelea na mahojiano na wengine bado tunaendelea kuwatafuta,”amesema Mambosasa.
Chanzo chetu kimedokeza kwamba huenda wakaendelea kushikiliwa hadi pale mkutano mkuu utakapomalizika!
Chanzo:Jamii Forums
Jumamosi, 11 Machi 2017
Home »
» DODOMA: Bashe, Malima na Musukuma Mbaroni Wakidaiwa Kupanga Kuhujumu Vikao Vinavyoendelea
DODOMA: Bashe, Malima na Musukuma Mbaroni Wakidaiwa Kupanga Kuhujumu Vikao Vinavyoendelea
Related Posts:
NI ZAIDI YA VIPODOZI,NI ASILI VISIVYO NA KEMIKALI;ORIFLAME.
Ni aina mbali mbali za vipodozi kwa wanaume na wanawake,vimetengenezwa kwa ubora wa hali ya juu visivyo na kemikali.Ni vipodozi asili kabisa kulingana na ngozi yako jaribu aina hizi uone maajabu ya vitu asilia.
Bidhaa hi… Read More
MAN CITY YAANZA VIBAYA UEFA
Man City ilipata kichapo cha goli moja bila jibu
Mechi zilizochezwa usiku wa kuamkia leo za Klabu
Bingwa barani ulaya ambapo Manchester City walianza vibaya michuano
hiyo baada ya kupata kichapo cha goli moja bila m… Read More
OMBI LA WAFUNGWA HUKO KENYA
Mkuu wa magereza anasema hakuna nafasi za kuweka vyumba vya faragha kwa wafungwa kushiriki tendo la ndoa.
Kamishna-Generali wa Magereza nchini Kenya
Isaiah Osugo amekataa ombi la wafungwa kuruhusiwa kufanya tendo la… Read More
Polisi wadaiwa kutesa raia Nigeria
Polisi nchini Nigeria wamedaiwa kuwatesa wanaume
na wanawake pamoja na watoto. Taarifa hii ni kwa mujibu wa shirika la
kutetea haki za binadamu la Amnesty International.
Shirika hilo
limechapisha ripoti yake ambayo inada… Read More
Vyombo vya habari,usalama vyakutana TZ
Uhasama wa kiutendaji kati ya vyombo vya habari
na vya ulinzi na usalama nchini Tanzania huenda ukapungua kwa kiasi
kubwa baada ya pande hizo kuanza kukaa pamoja na kujadili mambo
yanayokwamisha utekelezaji wa majukumu … Read More







0 comments:
Chapisha Maoni