Ijumaa, 20 Novemba 2015

Nina Wasiwasi na Naibu Spika Kama Atalihimili Bunge Hili

Sina wasiwasi ni elimu yake wala uwezo wake wa kujieleza, ila nina wasiwasi na hekima yake na busara zake kama zinaweza kustahimili mikiki mikiki ya bunge kama alivyoonyesha Anne Makinda.

Nafikiri wote tunaujua uwezo wa Prof. Muhongo kielimu lakini alifeli somo la hekima.

Najua bunge lina sheria zake kanuni zake miiko yake na desturi zake, lakini ni mara ngapi tumeona sheria zikikiukwa na wabunge wenyewe.

Kama tukisema yeye atakuwa "Iron Lady" kuwa kila mbunge akikosea anamhukumu kulingana na kanuni atafukuza wangapi, naje kama atafukuza karibu nusu ya wabunge ataonekana ni Naibu Spika mzuri au kiti kimemshinda.

Tuchukue mfano wa refa wa mpira wa mguu anayewatoa wachezaji kwa red kadi kila wanapofanya rafu, hivi timu ikibaki na nusu ya wachezaji huyo refa atakuwa bora?

Najaribu tu kumwangalia huyu Naibu Spika asije siku moja akatoa machozi kwa kuzomewa au kuulizwa maswali ya kuudhi akakiaibisha kiti.

Namuomba sana Spika Job Ndugai ajaribu kumsaidia msaidizi wake.

Tujadili kwa mstakabali wa nchi yetu.

By QuinineJamii Forums

Related Posts:

  • Al Shabaab waua 36 Mandera,Kenya                                   Wapiganaji wa Al Shabab&n… Read More
  • MKE WA KIONGOZI IS AKAMATWA                      Kiongozi wa IS Abu Bakr al-Baghdadi Vikosi vya usalama nchini Lebanon vimemkamata mkewe kiongo… Read More
  • Aliyewakosoa Sasha na Malia ajiuzuluSasha na Malia walikosolewa kwa kuvalia sketi fupi mbele ya umati katika White House Mfanyakazi katika chama cha Republican nchini Marekani amejiuzulu baada ya kukosolewa kwa kuwatuhumu wanawe Rais wa Marekani Barack Obam… Read More
  • BARNES:GERRAD BADO MZURI KWA LIVERPOOLSteven Gerrard bado ana kiwango cha juu kuendelea kuitumikia Liverpool Winga wa zamani wa Klabu ya Liverpool John Barnes anaamini kiungo na nahodha wa timu hiyo Steven Gerrard, bado ni mzuri vya kutosha kuendelea kuitumik… Read More
  • Man city wazidi kupanda                Wachezaji wa Klabu ya Man city  Kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini amesema ushindi wa timu yake dhidi ya Southampton unadhi… Read More

0 comments:

Chapisha Maoni