Jumanne, 2 Desemba 2014

MKE WA KIONGOZI IS AKAMATWA

                      Kiongozi wa IS Abu Bakr al-Baghdadi


Vikosi vya usalama nchini Lebanon vimemkamata mkewe kiongozi wa kundi la wapiganaji wa kiislamu la IS Abu Bakr al-Baghdadi karibu na mpaka na Syria na mwanawe mvulana.
Jeshi linasema kuwa Mkewe Baghdadi alikamatwa pamoja na mwanawe ingawa majina yao hayajatolewa. Walikamatwa na wakuu wa ujasusi baada ya kuingia Lebabon siku kumi zilizopita.
Jarida la al-Safir liliripoti kuwa mkewe Baghdadi anahojiwa katika ofisi za waizara ya usalama nchini Lebanon.
Mnamo mwezi Juni, Baghdadi alitajwa kama kiongozi wa kundi hilo katika maeneo ya Syria na Iraq ambayo yanadhibitiwa na IS.
Mwezi jana kundi hilo lilikannusha madai kuwa kiongozi huyo aliuawa au kujeruhiwa, katika shambulizi la angani lililofanywa na majeshi ya Marekani, mjini Mosul.
Kundi lenyewe lilitoa kanda ambapo lilisema utawala wao unapanuka na kutoa wito kwa wapiganaji wa jihad kujitolea mhanga.
Jarida lililoripoti kukamatwa kwa mkewe Baghdadi, limesema kuwa maafisa wa usalama walikuwa wameiweka operesheni yao kama siri kubwa kiasi kwamba hakuna aliyekuwa na taarifa kuhusu operesheni yenyewe.
Mwandishi wa BBC Jim Muir, ambaye yuko, anasema kuwa kukamatwa kwa mkewe Baghdadi na mwanawe kutawaweka katika hali tatanishi ambayo inaendelea kuibuka Lebanon.
Kundi la IS pamoja na kundi lengine la jihad al-Nusra linawazuilia wanajeshi 20 wa Lebabon kama mateka.

Related Posts:

  • WATU 115 WAFARIKI KANISANI NIGERIA  Muhubiri T.B Joshua amewashangaza wengi kwa kusema aliona ndege ikizunguka jengo hilo kabla ya kuporomoka Serikali ya Afrika Kusini inasema kuwa watu miamoja na kumi na tano wengi wao wakiwa raia wa Afrika Kusini, … Read More
  • MANUEL"CHELSEA NI TIMU NDOGO"Pellegrini ameikejeli Chelsea kwa kucheza kama timu ndogo  Kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini ameikejeli Chelsea kwa kucheza kama timu ndogo timu hizo zilipoambulia sare ya Moja kwa moja uwanjani Etihad. An… Read More
  • Huyu ndio msanii staa wa kimataifa anaekuja Fiesta Dar 2014.   Wakati Tour ya Fiesta ikiwa inazunguka kwenye mikoa mbalimbali Tanzania ambapo weekend hii ni Mbeya na Songea, ametangazwa msanii wa kimataifa ambae ni rasmi atapanda kwenye stage ya Fiesta Dar es salaam Oct… Read More
  • MASHABIKI WAMTUKANA BALOTELLIUjumbe wa Balotelli ulioibua hisia za ubaguzi wa rangi kwenye mtandao wa twitter  Polisi nchini Uingereza wameanzisha uchunguzi kuhusu tukio ambalo mshambulizi wa Liverpool kutoka Italia Mario Balotelli alitukanwa kut… Read More
  • Safari za Treni Tanzania kuongezeka.   Dr. Harryson Mwakyembe ni miongoni mwa Mawaziri ambao wanazungumziwa sana na vijana pamoja na Watanzania wengine kwenye marika mbalimbali kutokana na jinsi anavyochapa mzigo ndio maana sio ajabu hata kumsikia akit… Read More

0 comments:

Chapisha Maoni