Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad,
amerejea kauli yake ya kutotambua kufutwa kwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar
uliofanyika tarehe 25 mwezi uliopita.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mara baada ya
kikao cha mashauriano na viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA,
Maalim Seif amesema Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Bw Jecha
Salim Jecha hana mamlaka ya kufuta uchaguzi huo, na kinachohitajika na
kuendelea na mchakato wa kuhakiki kura zilizobakia na mshindi
kutangazwa.
Kuhusu tamko lililotolewa na serikali juu ya kufutwa rasmi kwa uchaguzi
huo kupitia tangazo lililochapishwa kwenye gazeti rasmi la serikali
tarehe sita mwezi huu, Maalim Seif amesema tamko hilo limekosa uhalali
tangu lilipotolewa na Mwenyekiti wa ZEC.
Maalim Seif ambaye pia ni Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CUF amesema
Chama chake hakijalizingatia tamko hilo na wala hakijadili uwezekano wa
kurejewa kwa uchaguzi huo, kwa madai kuwa uchaguzi ulikamilika bila ya
kuwepo malalamiko kutoka chama chochote cha siasa na wala Tume ya
Uchaguzi.
Mapema akizungumza baada ya kikao hicho cha mashauriano, aliyekuwa
mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chadema Mhe.
Edward Lowassa amesema kikao hicho kilichojadili Mkwamo wa kisiasa
Zanzibar kimekwenda vizuri.
Hata hivyo amesema ufafanuzi zaidi utatolewa Jumapili ijayo ambapo
viongozi hao wanakusudia kuzungumza na waandishi wa habari jijini Dar es
Salaam.
Kabla ya kikao hicho Maalim Seif alifanya mazungumzo na Balozi wa Umoja
wa Ulaya (EU) Bw. Filberto Seregondi katika hoteli ya Serena jijini Dar
es Salaam na kuelezea hatua zinazochukuliwa kukwamua mkwamo wa kisiasa
Zanzibar.
Balozi Seregondi ambaye anamaliza muda wake wa utumishi hapa
nchini,aliambatana na ujumbe wa waangalizi wa uchaguzi mkuu wa Tanzania
kutoka Umoja huo.
Ijumaa, 13 Novemba 2015
Home »
» Maalim Seif azugumza na Balozi wa EU na viongozi wa UKAWA....Atoa Msimamo Mzito
Maalim Seif azugumza na Balozi wa EU na viongozi wa UKAWA....Atoa Msimamo Mzito
Related Posts:
Rungu la TRA Yalishukia BAKWATA...Magari 82 Yaingizwa Kwa Jina lao Bila Kulipiwa Kodi..Watwangwa Barua Nzito Rungu la TRA Yalishukia BAKWATA...Magari 82 Yaingizwa Kwa Jina lao Bila Kulipiwa Kodi..Watwaga Barua Nzito, Isome HApa chini: … Read More
Tibaigana Afunguka...Huyu Ndiye Rais Niliyemtaka Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna mstaafu Alfred Tibaigana amesema Rais John Magufuli amepatikana wakati sahihi, kwa kuwa nchi inamhitaji kiongozi ambaye akitoa amri inatek… Read More
Katibu Mkuu Tamisemi Akagua Miundombinu ya Mfumo wa Mabasi Yaendayo Haraka WATOA huduma katika kipindi cha mpito cha mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam, kampuni ya UDA-RT wameihakikishia serikali na wananchi kuwa matayarisho yanaendelea vizuri tayari kwa huduma hi… Read More
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Desemba 7, Ikiwemo ya Kukosekana Kwa Mawaziri Kwaokoa Mamilioni … Read More
Jakaya Kikwete Aibukia 'Sauzi' Magufuli Akitumbua Majipu Magogoni Aliyomwachia.... Wakati Rais John Magufuli akitimiza siku 31 akiwa amejifungia Ikulu kutatua kero za nchi bila kusafiri nje ya nchi, Rais mstaafu Jakaya Kikwete (pichani) ameendelea kujumuika katika hafla za kimataifa baada… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni