Alikiba ametolea ufafanuzi post yake ya Instagram iliyozua mjadala kwa
mashabiki mbalimbali wa muziki ambao waliipokea kwa hisia tofauti.
Siku ya Jumatatu Nov.16 Muimbaji huyo wa single mpya ‘Nagharamia’ aliandika, “Asanteni
sana najua mmepiga kura sana lakini nilikuja kugundua baada ya
kufuatilia kuwa kuna mambo yanaendelea ya watu wanadiriki hata kupoteza
pesa zao kwaajili yangu ila nawaomba fans msinielewe vibaya I will
always be there for you #hapakazitu #kingkiba,” post ambayo baadae aliifuta.
Kupitia kipindi cha Ala Za Roho cha Clouds Fm na Diva The Bawse, king
Kiba amesema kuwa watu walimuelewa vibaya kwenye post hiyo na ndio
sababu kubwa ya kuamua kuifuta,
“watu walinielewa vibaya mimi nilikua
nawaambia mafans wangu, sababu wao ndo wananipigia Kura mimi
sikumaanisha kuhusu tuzo walinielewa vibaya” alisema Kiba.
Hata hivyo licha ya kwamba yeye hakushinda kipengele hata kimoja kati ya
vinne alivyotajwa kuwania kwenye tuzo za AFRIMA 2015, lakini
hakumpongeza hata msanii mmoja wa Tanzania aliyeshinda ambao ni Diamond
na Vanessa Mdee. Kusuhu hilo Alikiba alisema,
“Siwezi ku-post kitu kuhusu Kushinda Kwao,
unajua hakuna uzalendo. watu wangapi wanafanya Vitu vizuri hawapongezwi?
Mimi nafanya vingapi? Sisi sio wazalendo…Unajua watu mimi hawanijui
Wanahisi kama mimi nina ringa hivi au nina wivu, ila mimi nawapenda
wasanii wote pia mziki mzuri” alisema Alikiba.
Alipoulizwa kuhusu uhusiano wake na Diamond ukoje kwa sasa, ndipo alimpongeza Platnumz kwa ushindi wa tuzo 3.
“Mimi sina tatizo na Diamond, nasikia kashida
tuzo 3, nampongeza Sana sababu tumepata mtu ambaye anatutambulisha
kimataifa ni Kitu poa Sana…Mimi na Diamond we are good” alimaliza Alikiba.
Ijumaa, 20 Novemba 2015
Home »
» Alikiba Atolea Ufafanuzi Post ya ‘Utata’ Aliyoandika Instagram, na Ampongeza Diamond Kwa Ushindi wa AFRIMA
Alikiba Atolea Ufafanuzi Post ya ‘Utata’ Aliyoandika Instagram, na Ampongeza Diamond Kwa Ushindi wa AFRIMA
Related Posts:
UKAWA Watishia Kutoshiriki Uchaguzi Mkuu wa Jumapili CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinachoungwa mkono na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kimetishia kutoshiriki katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 25, mwaka huu. Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chadema, R… Read More
Magufuli Asimamisha Jiji La Dar.......Asema Tanzania Inahitaji Rais Mkali. CHADEMA Wampokea Kwa Ishara Ya Vidole Viwili Juu Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, amesema nchi inahitaji rais mkali ili mambo yaende huku akishangazwa na mmoja wa vigogo kufungua kesi kupinga mradi wa maji. Amesema watu wa aina hiyo wataki… Read More
Hatimaye Mama Maria Nyerere Ampigia Kampeni Magufuli CCM tayari wameshatengeneza video ya mama Maria Nyerere akiwaomba akina mama wotewampigie kura Magufuli. Video hii iko inasambaa Whatsup. Kaongea mengi kuwa ni mchapa kazi na Mwadilifu. Swali langu kwa bibi angu mama Ma… Read More
Muonekano wa Gari ya Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye, Toyota Land Cruiser Baada ya Kupata Ajali Mbaya Jana Usiku Muonekano wa gari ya Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye, Toyota Land Cruiser baada ya kupata ajali mbaya jana usiku akiwa njiani kuelekea Lindi akitokea jijini Dar es Salaam. … Read More
Katibu Mwenezi wa CCM Nape Nnauye Apata Ajali Mbaya ya Gari KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye amepata ajali mbaya jana usiku akiwa njiani kuelekea Lindi akitokea jijini Dar es Salaam. Nape ambaye pia ni mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtama, Lindi &… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni