
Shilingi billion 473 zimetengwa kwa ajili ya kutoa mikopo 
kwa wanafunzi wa elimu ya juu nchini kwa mwaka huu ikilinganishwa na 
Shilingi bilioni 341 zilizotolewa  mwaka jana ikiwa ni ongezeko la Tsh. 
bilioni 132 katika bajeti ya mwaka huu.
Hayo yalisemwa  jana jijini Dar es salaam na Mwenyekiti wa 
shirikisho la wanafunzi wa vyuo vikuu Tanzania(Tahliso)  bwn. 
Nzilanyingi  John  alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu 
kuaandaa mdahalo kujadili hotuba ya Rais Dkt. John Magufuli aliyoisoma 
Dodoma wakati wa ufunguzi wa bunge la kumi na moja .
Alisema kuwa kwa kipindi kifupi kumekuwa na  mabadiliko ya 
haraka yaliyotokea katika sekta ya elimu nchini kwa mwaka huu  kwani 
kuna ongezeko la zaidi ya wanafunzi 1800 waliopata mkopo ikilinganishwa 
na mwaka uliopita ambapo ni wanafuzi 34128 pekee ndio waliofanikiwa 
kupata mkopo.
“Mpaka sasa jumla ya wanafunzi 51,675 wa mwaka wa kwanza
 wamepata mkopo na lengo ni kufikia 53,032, pia jumla ya wanafunzi 91 wa
 shahada ya uzamili  na wanafunzi 113 wanaosoma vyuo vya nje tayari 
wamepata mkopo” alisema John.
Aliongeza kuwa katika kipindi kifupi kijacho bodi ya mikopo
 imehakikisha kutoa mikopo kwa wanafunzi zaidi ya elfu moja wanaochukua 
Diploma maalumu ya ualimu Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na hivyo 
kukamilisha adhma yao ya kutoa mikopo kwa wanafunzi 53,032.
Aidha shirikisho hilo ambalo ni umoja wa viongozi wa 
serikali za wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu nchini umeandaa mdahalo 
wenye lengo la kutoa fursa kwa watanzania wengi kujadili hotuba hiyo  na
 namna rais alivyoanza kutekeleza majukumu yake katika nafasi hiyo.
Mdahalo huo utafanyika jijini Dar es Salaam tarehe 13 mwezi
 huu katika ukumbi wa Nkurumah na wazungumzaji wakuu katika mdahalo ni 
Mtaalamu mbobevu wa uchumi kutoka chuo kikuu cha Mzumbe Prof.Honest 
Ngowi, Dkt. John Lingu kutoka Idara ya Sayansi ya Siasa ya Chuo Kikuu 
cha Dar es Salaam na Mwanadiplomasia Christopher Liundi.






 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Chapisha Maoni