Jumamosi, 5 Desemba 2015

Taarifa Sahihi Kuhusu Hotel ya Serena Kufungwa Kwa Amri ya Serikali Kwa Kosa la Kukwepa Kulipa Kodi

Serena Hotel
HOTELI ya kimataifa ya Serena jana ilikumbwa na msukosuko wa kuandamwa na waandishi wa habari baada ya kusambaa kwa tetesi kuwa imefungwa kwa amri ya serikali kwa kosa la kukwepa kulipa kodi.


Tetesi hizo zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii jana asubuhi, zikieleza kuwa maofisa wa Mamlaka ya Mapato (TRA) wameifunga hoteli kufunga kwa kukwepa kuliko kodi serikalini.



Mbali ya kusambazwa kwa uvumi huo, zilitumwa pia picha zilizokuwa zikionyesha sehemu ya hoteli hiyo ikiwa imezungushwa uzio uliokuwa na rangi nyeupe na nyekundu ambao ni alama inayotumika kuonyesha kusitisha kwa huduma katika eneo hilo.



Tetesi hizo zilikwenda mbali zaidi kwa kueleza kuwa uongozi wa hoteli hiyo ulikuwa mbioni kubadilisha jina kwa lengo la kukwepa kulipa kodi.



Hata hivyo, mwandishi wetu baada ya kufika hotelini hapo kwa lengo la kufuatilia ukweli wa tetesi hizo alikuta shughuli za ukarabati wa sehemu ya kupokea wageni zikiendelea, huku wageni wakielekezwa kutumia mlango wa dharura ambako kumetengezwa sehemu ya muda ya kupokelea wageni.



Uongozi wa Hoteli ya Serena kupitia Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko, Seraphine Lusala, ulilazimika kutoa taarifa kwa vyombo vya habari ukikanusha kufungwa kwa hoteli hiyo na kusisitiza kuwa kinachoendelea hotelini hapo ni matengenezo.



“Si kweli kama hoteli imefungwa, tunafanya matengenezo na yalikuwa yafanyike tangu miaka mitatu iliyopita, kilichofanyika sasa ni kubadilisha eneo la mapokezi yaliyohamishiwa milango mingine na tumeanza na eneo hilo pamoja na sehemu ya mazoezi,” alisema Lusala.



Alisema matengenezo hayo yanalenga kuifanya hoteli hiyo kuwa ya kiwango cha juu zaidi na yatachukua miezi  10.



Lusala alisema awamu ya kwanza ya matengenezo itachukua miezi minne na miezi minne ijayo itahusu matengenezo sehemu ya vinywaji, chakula, eneo la uwanja na baadaye maeneo mengine ya wazi.

Related Posts:

  • TOFAUTI ZA DINI ZISIWAGAWE WATANZANIA ,MWINYI Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Saidi Meck Sadiki akiongea na watoto wanaotoka katika vituo mbalimbali  vya kulelea watoto yatima vya  jijini Dar es salaam , wakazi wa jiji la Dar es salaam na viongozi mbalimba… Read More
  • WAZIRI MKUU AFUNGUA MKUTANO WA TATHMINI YA UTEKELEZAJI BRN Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Benno Ndulu akichangia hoja wakati wa mkutano wa kupitia taarifa ya mwaka mmoja ya utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa sasa (BRN) uliofanyika leo Jumatano Julai 23, 2014 kati… Read More
  • LOWASSA AKAGUA SHULE ILIYOUNGUA HUKO MONDULI Kiasi cha wanafunzi 100 wa shule ya sekondari ya Erikisongo wilayani Monduli wamenusurika kifo baada ya vyumba vitano vya mabweni yao kuteketea na moto leo (Jumatano) asubuhi. Moto huo ambao inaelezwa chanzo chake… Read More
  • Ajali ya Ndege:Miili imewasili Uholanzi Miili ya abiria wa ndege ya Malaysia MH17 imewasili Eindhoven Ndege mbili za kijeshi zinazobeba miili 40 kati ya 282 ya abiria wale waliofariki kutokana na mkasa wa ndege ya Malaysia iliyodunguliwa huko mash… Read More
  • AJALI YA NDEGE YAUA 51 TAIWAN Taswira kutoka eneo la ajali. Vikosi vya uokoaji vikiwa eneo la tukio. TAKRIBANI watu 51 wamepoteza maisha huku saba wakijeruhiwa baada ya ndege waliyokuwemo kuanguka iliposhindwa kutua kwa dharura huko Taiwan, nchini… Read More

0 comments:

Chapisha Maoni