Viongozi wakuu wote wa Taifa wako nje ya nchi katika ziara za kiserikali kwenye mataifa tofauti.
Rais John Magufuli aliwasili Uganda jana asubuhi kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais mteule wa nchi hiyo, Yoweri Museveni zinazofanyika leo na Makamu wake, Samia Suluhu Hassan alikuwa Kigali, Rwanda kuhudhuria mkutano wa dunia wa uchumi.
Taarifa zilizopatikana na kuthibitishwa na Mwandishi wa Makamu wa Rais, Penzi Nyamngumi zimesema, Makamu wa Rais aliondoka nchini Jumanne akitokea Dodoma na angerejea kesho baada ya mkutano huo.
Kiongozi anayefuatia kwa wadhifa, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisafiri juzi kwenda London, Uingereza kumwakilisha Rais Magufuli katika mkutano wa wakuu wa nchi kujadili mapambano dhidi ya rushwa.
Majaliwa katika ziara hiyo ameongozana na Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju alipotakiwa kutoa ufafanuzi juu ya anayepaswa kukaimu urais, alisema Makamu wa Rais amekwisha rejea nchini na yuko Mwanza.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 37 (3), inaeleza kuwa endapo Rais atakuwa hayupo katika Jamhuri ya Muungano, kazi na shughuli za Rais zitatekelezwa na Makamu wa Rais, kama naye hayupo, yatatekelezwa na Waziri Mkuu.
Hata hivyo, Ibara ya 37 (6) (b) inasema Rais hatahesabiwa kwamba hayupo iwapo atakuwa nje ya Jamhuri ya Muungano kwa kipindi cha saa 24.
Alhamisi, 12 Mei 2016
Home »
» Viongozi Wakuu Wote wa Taifa Wako nje ya Nchi ..Nani Anaongoza Nchi Kwa Sasa?
Viongozi Wakuu Wote wa Taifa Wako nje ya Nchi ..Nani Anaongoza Nchi Kwa Sasa?
Related Posts:
Vita Ya Malipo Kiduchu Haijawahi Kumuacha Modo Salama! AMANDA Swartbooi moja kati ya wauza nyago katika video Afrika akitokea Afrika Kusini. Amanda ametokea kujizolea umaarufu kwa kipindi kifupi cha mwaka jana ambapo ametokea katika video kadhaa Afrika ikiwemo Coolest Kid ya D… Read More
WCB Wabadilike Uimbaji Nashangaa kuona wasanii wote wanaimba key moja mwisho wa siku haitambuliki huyu ni nani sababu wanaigana kama wataendelea hivi watachokwa hakuna anayetaka kubadika. Baada yakuja huyo Lava Lava nikazani anakuja na key tof… Read More
Madiwani wa Moshi Wasusa Semina Kisa Malipo ya Posho Kuwa Madogo..Wataka Walipwe Laki Moja Kwa Kikao..!! HALI ya taharuki imeibuka katika Halmashauri ya Moshi baada ya madiwani kugomea mafunzo ya utaratibu ulioboreshwa wa uendeshaji ruzuku ya maendeleo kwenye mamlaka za Serikali za mitaa (LGDG), wakishinikiza kulip… Read More
Kajala Aibuka na Haya Kuhusu Wema Sepetu..Adai Hata Mwanae ni Shahidi..!!! TASNIA ya filamu nchini imepambwa na wasanii wa kike wenye urembo unaovutia macho na hakika kwenye orodha ya waingizaji wenye kipaji, uwezo na mvuto huwezi kumuacha, Kajala Masanja. Huyu ndiyo bosi wa kampuni ya Kaja… Read More
Friji Lateketeza Jengo la Ghorofa 27 kwa Muda wa Dakika 15..!!! MOTO uliozuka kwenye jengo la ghorofa 27 lililoko London Magharibi kwa dakika 15 baada ya friji kulipuka, itakuwa ni moja ya ajali mbaya kupata kutokea katika historia ya nchi hii huku kukiwa na hofu ya kutokuw… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni