SHIRIKA la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), limeeleza kuridhishwa kwake na utendaji wa Rais John Magufuli katika mapambano ya rushwa, kuongeza uwajibikaji na ukusanyaji wa mapato.
Mwakilishi Mkazi wa UNDP nchini, Alvaro Rodriguez, alisema hayo jana katika semina ya wabunge kuhusu Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu ya Dunia.
Alisema Serikali ya Awamu ya Tano, imekuwa ikipambana na rushwa na kusimamia kwa karibu ukusanyaji mapato, hali aliyosema itasaidia maendeleo kwa kuwa hakuna nchi iliyoendelea bila kuchapakazi.
Rodriguez alisema mbali na kuona maendeleo katika baadhi ya mikoa na mitaa, ameona jitihada hizo za Serikali na amefurahishwa na kuridhika nazo.
Mwakilishi huyo pia alisema Serikali ya Tanzania na Ofisi ya Umoja wa Mataifa (UN), zimekuwa zikifanya kazi pamoja katika harakati za usambazaji wa malengo ya dunia kwa Watanzania.
Alisisitiza umuhimu wa malengo hayo kueleweka kwa wabunge, ili katika jukumu lao la kuisimamia Serikali, wawe mabalozi wa utekelezaji wa malengo hayo katika ufuatiliaji kwenye ngazi zote za utawala.
Jumapili, 5 Juni 2016
Home »
» UN WAKUNWA NA KASI YA JPM
UN WAKUNWA NA KASI YA JPM
Related Posts:
Sentensi 4 kwanini maandamano ya CHADEMA Dodoma kesho yamezuiliwa. Polisi Dodoma wametangaza kuyazuia maandamano ya chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA yaliyokua yamepangwa kufanyika Alhamisi ya tarehe 18/09/2014 ambapo wametaka Wananchi wayapuuze. Kaimu Kamanda wa Polisi Mk… Read More
UGANDA YAHARIBU SHAMBULIZI LA KIGAIDI Vikosi vya usalama nchini Uganda Maafisa wa polisi nchini Uganda wameimarisha usalama katika maeneo mengi ya uma katika mji mkuu wa Kampala kufuatia kukamatwa kwa washukiwa kadhaa wa makundi ya kigaidi na vil… Read More
MAYWEATHER AMCHAPA TENA MAIDANA Floyd Mayweather (kushoto) akimtupia konde mpinzani wake Marcos Maidana. Maidana akijibu mashambulizi wakati wa pambano hilo. Mayweather akimshambulia mpinzani wake.… Read More
OMBI LA WAFUNGWA HUKO KENYA Mkuu wa magereza anasema hakuna nafasi za kuweka vyumba vya faragha kwa wafungwa kushiriki tendo la ndoa. Kamishna-Generali wa Magereza nchini Kenya Isaiah Osugo amekataa ombi la wafungwa kuruhusiwa kufanya tendo la… Read More
Habari njema! Fastjet tena kwenye headlines!! wameanza kwenda Uganda. Shirika la ndege la Fastjet limepata sifa kubwa nchini Tanzania kutokana na kusafirisha kwake abiria na kuanza kuiunganisha Afrika kwa kasi ambapo baada ya kuanzisha safari za nyumbani kati ya Mwanza – Dar, Kilimanjaro – D… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni