SHIRIKA la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), limeeleza kuridhishwa kwake na utendaji wa Rais John Magufuli katika mapambano ya rushwa, kuongeza uwajibikaji na ukusanyaji wa mapato.
Mwakilishi Mkazi wa UNDP nchini, Alvaro Rodriguez, alisema hayo jana katika semina ya wabunge kuhusu Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu ya Dunia.
Alisema Serikali ya Awamu ya Tano, imekuwa ikipambana na rushwa na kusimamia kwa karibu ukusanyaji mapato, hali aliyosema itasaidia maendeleo kwa kuwa hakuna nchi iliyoendelea bila kuchapakazi.
Rodriguez alisema mbali na kuona maendeleo katika baadhi ya mikoa na mitaa, ameona jitihada hizo za Serikali na amefurahishwa na kuridhika nazo.
Mwakilishi huyo pia alisema Serikali ya Tanzania na Ofisi ya Umoja wa Mataifa (UN), zimekuwa zikifanya kazi pamoja katika harakati za usambazaji wa malengo ya dunia kwa Watanzania.
Alisisitiza umuhimu wa malengo hayo kueleweka kwa wabunge, ili katika jukumu lao la kuisimamia Serikali, wawe mabalozi wa utekelezaji wa malengo hayo katika ufuatiliaji kwenye ngazi zote za utawala.
Jumapili, 5 Juni 2016
Home »
» UN WAKUNWA NA KASI YA JPM
UN WAKUNWA NA KASI YA JPM
Related Posts:
Mwanaume aliyebakwa baada ya kupanda lifti ya mtu asiyemjua. Mwanaume mmoja amebakwa katika barabara ya daraja lenye shughuli nyingi mjini Newcastle baada ya kukubali kupanda lifti ya mtu asiyemjua.Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 24 aliingia kwenye gari hilo dogo mapema alfajiri a… Read More
Angalia magoli 10 bora ya kombe la dunia – Messi vs Van Persie nani katisha? Michuano ya kombe la dunia ipo kwenye hatua ya robo fainali ambayo itaanza rasmi Ijumaa hii. Michuano hii ya mwaka huu imekuwa na magoli mengi na bora katika historia ya michuano hii mikubwa kabisa katika soka.youngluvega.c… Read More
Taarifa ya Kaimu Balozi wa Libya, Tanzania aliyejiua kwa kujipiga risasi. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Tanzania leo imepokea taarifa kutoka ubalozi wa Libya nchini ikieleza kuwa aliyekuwa Kaimu Balozi wa Libya Bw. Ismail Nwairat, amefariki dunia jana kwa kujipiga risa… Read More
Jinsi Beyonce alivyobadilisha mistari ya wimbo wake jukwaani kufuatia matatizo ya ndoa yake. Wanandoa Beyonce na Jay Z wamekuwa wakipambana na uvumi kuwa sasa ndoa yao iko juu ya mawe kutokana na matatizo makubwa yanayoendelea tangu kusambaa kwa video ikimuonyesha dada wa Beyonce Solange akimshambulia Jay Z. Na s… Read More
Dar es salaam Julai 02, 2014, Gari hili la Magereza lapigwa risasi likiwa na wafungwa ndani. Taarifa za awali zinadai kuwa Basi lililokuwa limebeba wafungwa limeshambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana eneo la Mayfair Mikocheni jijini Dar es salaam.Basi hili lilikuwa likitokea mahakama ya Mwanzo Kawe ambapo kwa… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni