SHIRIKA la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), limeeleza kuridhishwa kwake na utendaji wa Rais John Magufuli katika mapambano ya rushwa, kuongeza uwajibikaji na ukusanyaji wa mapato.
Mwakilishi Mkazi wa UNDP nchini, Alvaro Rodriguez, alisema hayo jana katika semina ya wabunge kuhusu Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu ya Dunia.
Alisema Serikali ya Awamu ya Tano, imekuwa ikipambana na rushwa na kusimamia kwa karibu ukusanyaji mapato, hali aliyosema itasaidia maendeleo kwa kuwa hakuna nchi iliyoendelea bila kuchapakazi.
Rodriguez alisema mbali na kuona maendeleo katika baadhi ya mikoa na mitaa, ameona jitihada hizo za Serikali na amefurahishwa na kuridhika nazo.
Mwakilishi huyo pia alisema Serikali ya Tanzania na Ofisi ya Umoja wa Mataifa (UN), zimekuwa zikifanya kazi pamoja katika harakati za usambazaji wa malengo ya dunia kwa Watanzania.
Alisisitiza umuhimu wa malengo hayo kueleweka kwa wabunge, ili katika jukumu lao la kuisimamia Serikali, wawe mabalozi wa utekelezaji wa malengo hayo katika ufuatiliaji kwenye ngazi zote za utawala.
Jumapili, 5 Juni 2016
Home »
» UN WAKUNWA NA KASI YA JPM
UN WAKUNWA NA KASI YA JPM
Related Posts:
Al Shabaab waua 36 Mandera,Kenya Wapiganaji wa Al Shabab&n… Read More
Obama na vurugu za Marekani &nb… Read More
FIFA:Madai mapya ya ufisadi yazuka Rais wa FIFA Sepp Blatter akimkabidhi rais wa Urusi Vladmir Putin Haki za kuandaa dimba la dunia la mwaka 2018 Madai zaidi yameibuka kuhusu ufisadi uliofanyika wakati wa shughuli ya kuwatafuta waandalizi wa … Read More
Man city wazidi kupanda Wachezaji wa Klabu ya Man city Kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini amesema ushindi wa timu yake dhidi ya Southampton unadhi… Read More
Man U na Arsenal zawika,Chelsea yazuiwa Mchezaji wa chelsea Wiilian akikabiliana na mwenzake wa Sunderland Mkufunzi Gus Poyet aliihangaisha timu ya Chelsea na kuwajaribu viongozi hao wa Ligi kupi… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni