Ijumaa, 9 Juni 2017
Home »
» Vita Ya Malipo Kiduchu Haijawahi Kumuacha Modo Salama!
Vita Ya Malipo Kiduchu Haijawahi Kumuacha Modo Salama!
AMANDA Swartbooi moja kati ya wauza nyago katika video Afrika akitokea Afrika Kusini. Amanda ametokea kujizolea umaarufu kwa kipindi kifupi cha mwaka jana ambapo ametokea katika video kadhaa Afrika ikiwemo Coolest Kid ya Davido akimshirikisha Nasty C wa Afrika Kusini, Four4 ya JR pamoja na Show Me ya Rich Mavoko akiwa na Harmonize.
Licha ya kufanya poa huko, ameshawahi kukiri kuwa kuuza nyago katika video hizo kunamlipa kwani kumempa mafanikio ya kujisomesha katika Chuo Kikuu cha Afrika Kusini (UNISA) akiwa mwaka wa pili katika masomo ya biashara. Ukija Bongo wapo wauza nyago katika Video za Kibongo ambao ni ‘visu’ lakini wanaangushwa na malipo kiduchu kutoka kwa wasanii husika kiasi cha kufikia kuangalia kazi nyingine za kufanya huku baadhi wakijiingiza katika muziki.
Katika makala haya nimekuchambulia baadhi tu ya wauza nyago (modo)ambao vita hii ya malipo kiduchu haijawahi kuwaacha salama kwani wengine wameamua kuachana na kuuza sura na wengine kujiingiza katika kuimba.
Alikuja kwa kasi, akavuma katika Video ya Kwetu ya Rayvanny na baada ya hapo akatokomea. Kutokana na kuitendea haki video hiyo, wengi walimtabiri kama miongoni mwa wauza nyago watakaokuja kuliteka soko. Hajashiriki tena katika kuuza sura kwenye video nyingine hadi sasa huku ikisemekana kukwepa malipo kiduchu kwa kila anayemfuata kufanyanaye kazi.
Alianza kuuza sura katika Video ya Naogopa ya Mirror kisha katika Remix ya Burger Movie Selfie ya Belle9 na baada ya hapo aliamua kuachana na suala la kuuza nyago na kujiingiza rasmi kwenye Muziki wa Bongo Fleva. Lulu anasema malipo kiduchu na mastaa wengine wakitaka kumtumia bure katika video zao ndivyo vilivyomkimbiza kwenye kuuza sura na kuamua kuimba ambapo kwa sasa anabamba na Ngoma ya Usimuache.
Ni modo ambaye pia muuza nyago katika video za Kibongo. Kutokana na malipo kiduchu katika video hizo kumemfanya kupotea kimyakimya katika orodha wauza sura Bongo. Ameshawahi kukiri kulipwa kiasi kikubwa katika video moja tu (Salome ya Diamond) tangu aingie katika kuuza nyago huku akiwa na kumbukumbu ya kulipwa kiduchu katika Video ya Magubegube ya Barnaba.
Naye ni miongoni mwa wauza nyago walioanza kupotea kwenye ramani ya muziki Bongo kisa hazilipi. Alianza kutokea katika Video ya Masogange ya Belle9 na baada ya hapo akaonekana kwenye Video ya Magubegube ya Barnaba iliyotoka 2012. Mara ya mwisho kuonekana katika ulimwengu wa wauza nyago ilikuwa katika Video ya Msambinungwa ya Tunda Man akishirikiana na Ali Kiba iliyotoka mwanzoni mwa mwaka 2014.
Related Posts:
HUYU NDO MKE WA MAREHEMU MBUNGE DEO FILIKUNJOMBE ALIYE FARIKI KWENYE AJALI YA HELIKOPTA YA CCM Huyu Ndo Mke wa Marehemu Mbunge Deo Filikunjombe Aliyefariki Kwenye Ajali ya Helkopta ya CCM … Read More
BAADA YA KUJITOA CCM BAKOZI JUMA MWAPACHU ATOA MPYA..ADAI HATA NYERERE ANGEKUWEPO ANGEJITOA CCM Siku moja baada ya kutangaza kujitoa CCM, kada mkongwe wa chama hicho, Balozi Juma Mwapachu amesema uamuzi alioufanya ni sahihi ambao hata Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere angekuwa hai angeufanya kwa sasa. Balozi M… Read More
P-square na Fally Ipupa Walitamani Kuwachukua Dancers wa Diamond Dancers wa P-Square pamoja na msanii mkubwa wa nchini Congo, Fally Ipupa walijaribu kumshawishi Diamond ili wafanye kazi ya pamoja na dancers wake. Akizungumza na Bongo5 jana mmoja wa dancers hao, Imma Platnumz, alisema … Read More
MWANAMUZIKI ALI KIBA ATOA WIMBO MPYA...USIKILIZE HAPA JINA LA WIMBO MAUMIVU Huu ni wimbo mpya wa msanii Ali Kiba ambao umevuja unaitwa “Maumivu” Producer: Manecky … Read More
PICHA ZA MABAKI YA HELIKOPTA ILIYOPOTEZA UHAI WA MBUNGE DEO FILIKUNJOMBE Mwili wa Deo Filikunjombe ukitolewa Eneo la tukio baada ya kuteketea kwa Moto kufuatia ajali ya helkopta. Waliofariki mbali ya Filikunjombe wengine ni Mwenyekiti wa TLP Mkoa wa Iringa Blanka Francis Haul… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni