Jumanne, 3 Mei 2016

PROF MUHONGO: TATIZO LA UMEME KUISHA MWAKA HUU MWEZI SEPTEMBA

SERIKALI inatarajia kuzindua mradi mkubwa wa kuboresha miundombinu ya kusafirisha umeme Septemba mwaka huu, utakaomaliza tatizo la umeme kukatika.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alisema kwa sasa miundombinu ya kusafirishia umeme ni midogo na katika kuboresha hilo, kuna mradi mkubwa utazinduliwa Septemba mwaka huu wa kusafirisha umeme.
Alisema mradi huo ni wa kusafirisha umeme kutoka kilovoti 220 hadi 400 kutoka Dar es Salaam-Tanga hadi Arusha na Iringa-Dodoma-Shinyanga, hivyo tatizo la kukatika umeme litatatuliwa.
Waziri huyo alitoa maelezo hayo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Korogwe Mjini, Mary Chatanda (CCM) aliyetaka kufahamu lini umeme utakoma kukatika wilayani Korogwe.
Akielezea hilo, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani alisema Serikali inafanya marekebisho ya transfoma na chanzo cha umeme cha Hale mkoani Tanga ili kumaliza tatizo la kukatika umeme mara kwa mara wilayani Korogwe na mkoani Tanga kiujumla.

Related Posts:

  • TOFAUTI ZA DINI ZISIWAGAWE WATANZANIA ,MWINYI Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Saidi Meck Sadiki akiongea na watoto wanaotoka katika vituo mbalimbali  vya kulelea watoto yatima vya  jijini Dar es salaam , wakazi wa jiji la Dar es salaam na viongozi mbalimba… Read More
  • AJALI YA NDEGE YAUA 51 TAIWAN Taswira kutoka eneo la ajali. Vikosi vya uokoaji vikiwa eneo la tukio. TAKRIBANI watu 51 wamepoteza maisha huku saba wakijeruhiwa baada ya ndege waliyokuwemo kuanguka iliposhindwa kutua kwa dharura huko Taiwan, nchini… Read More
  • LOWASSA AKAGUA SHULE ILIYOUNGUA HUKO MONDULI Kiasi cha wanafunzi 100 wa shule ya sekondari ya Erikisongo wilayani Monduli wamenusurika kifo baada ya vyumba vitano vya mabweni yao kuteketea na moto leo (Jumatano) asubuhi. Moto huo ambao inaelezwa chanzo chake… Read More
  • Ajali ya Ndege:Miili imewasili Uholanzi Miili ya abiria wa ndege ya Malaysia MH17 imewasili Eindhoven Ndege mbili za kijeshi zinazobeba miili 40 kati ya 282 ya abiria wale waliofariki kutokana na mkasa wa ndege ya Malaysia iliyodunguliwa huko mash… Read More
  • MADEREVA WA VYOMBO VYA MOTO MUWE MAKINI Gari aina ya Toyota Hilux limetumbukia kwenye mtaro uliopo Sinza-Makaburini jijini Dar es Salaam baada ya dereva aliyekuwa akiliendesha gari hiyo kushin… Read More

0 comments:

Chapisha Maoni