Alhamisi, 15 Septemba 2016

CONGO DRC: WAASI WA MAI MAI WAMEWATEKA MADEREVA 5 WA TANZANIA, WANATAKA $ 4,000 KWA KILA DEREVA



KUNA TAARIFA KUWA waasi wa Mai Mai wamewateka madereva wa Tanzania watano na kuchoma baadhi ya magari. Wanadai usd 4000 kwa kila Dereva amasivyo watawapiga risasi. Wametoa deadline ya majeshi kuondoka pia.

Chama cha Wamiliki wa Magari ya Mizigo nchini Tanzania (TATOA) kinaripoti kwamba, waasi wa Mai Mai nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), wamewateka nyara madereva wa Tanzania na kuchoma baadhi ya magari ya mizigo. Waasi hao wanadai dola za Kimarekani elfu nne (karibu shilingi za Kitanzania milioni tisa) kwa kila dereva ama sivyo watawapiga risasi madereva wote. Pia waasi hao wametoa siku ya mwisho (deadline) ya majeshi yanayolinda amani nchini humo kuondoka.

TATOA inasema imezungumza na mmiliki wa kampuni ya Simba Logistics, Mzee Azim Dewji ambaye amethibitisha taarifa hizi na pia balozi wa Tanzania DRC pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje tayari serikali inashughulikia suala hili. Jumla ya magariyaliyotekwa ni 12 kati ya hayo magari 8 ya Tanzania na 4 ya Kenya. Magari 4 ya Tanzania yamechomwa moto na madereva wote walichukuliwa na waasi lakini bahati nzuri madereva wawili wa Tanzania walifanikiwa kuwatoroka. Tukio hilo limetokea sehemu inaitwa Kasebebena na Matete, wastani wa kilomita 30 kutoka mji wa Namoya.

TATOA inawashauri wanachama waliopakia mzigo kuelekea huko kuwasiliana na madereva wao ili wasitishe safari, kusubiri taarifa ya hali ya usalama kutolewa.

Mai Mai Kata ni kundi la waasi nchini DRC ambalo linadai kupigania uhuru wa jimbo la Katanga, na linaongozwa na Gédéon Kyungu Mutanga, ambaye aliunda kundi hilo mara tu alipotoroka kutoka gerezani mwaka 2011.


Tumezungumza na mmiliki wa kampuni ya Simba Logistics Mzee Azim Dewji amethibitisha taarifa hizi na tayari tumezungumza na balozi wa Tanzania DRC pamoja na wizara ya mambo ya nje tayari serikali inashughulikia swala hili. Jumla ya gari zilizotekwa ni 12 kati ya hizo gari 8 za Tanzania na 4 za Kenya.

Gari 4 za Tanzania zimechomwa moto na madereva wote walichukuliwa na waasi lakini bahati nzuri madereva wawili wa Tanzania walifanikiwa kuwatoroka. Tukio limetokea sehemu inaitwa Kasebebena na Matete kilometer 30 kutoka mji wa Namoya.

Tunawashauri wanachama waliopakia mzigo kuelekea huko kuwasiliana na madereva wao wasitishe safari ili kusubiri taarifa ya hali ya usalama kutolewa.

Tutazidi kuwapatia update information.

NAMANGA: EDWARD LOWASSA ASIMAMISHWA NA WANANCHI WAMWELEZE UGUMU WA MAISHA


Mh Edward Lowassa Mjumbe wa kamati kuu wa chama Cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA ) na Chama kikuu cha Upinzani TANZANIA na Waziri Mkuu mstaafu amesimamishwa na Wananchi wa Namanga Mpakani mwa Tanzania na Kenya . 

Wananchi wamemueleza Ugumu na ukali wa Maisha walionayo ikiwa ni pamoja na kudorora kwa mzunguko wa fedha mpakani hapo leo hii akiwa safarini Toka Nairobi Kenya alipokwenda kuhudhuria mazishi ya Marehemu Ole Ntimama.

GAVANA BOT AFICHUA SIRI YA KILIO CHA FEDHA KUPOTEA MTAANI


Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Profesa Benno Ndulu jana alitolea ufafanuzi hali ya kiuchumi nchini huku akieleza siri ya kilio kinachovuma cha fedha kupotea mtaani na nyingine zikidaiwa kufichwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Profesa Ndulu alisema kuwa kwakuwa taasisi hiyo ndiyo inayofahamu fedha zote zilizopo benki na zilizopo mtaani, inafahamu kuwa hakuna fedha iliyopotea bali fedha zimepotea kwa watu waliokuwa wanazipata kwa njia ya udanganyifu kwakuwa sasa Serikali imebana mianya hiyo.

“Hakuna fedha iliyopotea, Serikali imebana shughuli za watu na ‘mission town’ sasa shughuli zote zinafanywa na Serikali. Hivyo, kwao fedha zimepotea, lakini kwetu hazijapotea,” alisema Profesa Ndulu.

Hata hivyo, Profesa Ndulu alikiri kupungua kwa fedha katika mabenki nchini hali iliyopelekea kupunguza kasi ya utoaji mikopo kwa wananchi. Alisema hali hiyo ilitokana na kuhamishwa fedha za mashirika ya umma na taasisi kutoka benki za biashara kwenda BoT.

“Fedha hizo zitarudi katika benki hizo wakati zitakapopelekwa kwenye Halmashauri kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali,” Profesa Ndulu aliahidi.

Katika hatua nyingine, Gavana huyo wa Benki Kuu alisema kuwa uchumi unatarajiwa kukuwa kwa asilimia 7.2 mwaka huu, huku akibainisha kuwa moja kati ya sababu zinazopelekea ukuaji huo ni  ongezeko la uzalishaji wa umeme na saraju.

Akizungumzia hali ya deni la taifa, alisema kuwa deni la taifa la ndani limeongezeka kutoka shilingi  trilioni 8.6 Mwezi Desemba mwaka jana hadi shilingi trilioni 10 mwezi Juni mwaka huu.

Profesa Ndulu alibainisha kuwa wakati deni linalotokana na kukopa ndani likipaa, deni linatokana na ukopaji wa limepungua baada ya Serikali kupunguza ukopaji nje ya nchi.

EDWARD LOWASSA AMPONGEZA RAISI JOHN POMBE MAGUFULI


Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa amempongeza Rais Magufuli kwa kuondoa urasimu katika taasisi za serikali na kusema hiyo itasaidia kurejesha utendaji kazi kwa ufanisi.

Lowassa ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na mtangazaji wa BBC, John Nene nchi Kenya ambapo alisema urasimu umepungua na hili amejitahiidi lakini kuna mambo baadhi hayako vizuri.

Lowassa hakuwa tayari kusema ni mambo gani haswa hayakua yakienda sawa lakini alimkosoa Rais Magufuli kwa kile alichodaiwa kuwa analeta dalili za udikteta.

Lowassa alikuwa ni mpinzani mkuu wa Rais Magufuli katika uchaguzi mkuu mwaka 2015 akigombea kupitia CHADEMA na kuungwa mkono na vyama vinavyounda UKAWA.

Amekosoa pia uamuzi wa serikali ya awamu ya tano kupiga marufuku maandamano, mikutano na vikao vya ndani vya vyama siasa huku vyombo vya habari vikifungiwa na wale wote wanamkosoa wakifikishwa mahakamani.

Akielezea Opersheni UKUTA, Lowassa alisema kuwa walipanga kuandamana ili kupinga dalili za udikteta alizoanza kuzionyesha Rais Magufuli.

DADA WA DAIMOND ESMA PLATNUMZ AKIRI KUMPENDA SANA PETIT MAN AWAOMBA NYAKU NYAKU WASIMNYAKUE



Dada wa Diamond ameamua kufunguka ya moyoni na kudai anampenda sana mume wake Petit Man ambae walitengana kwa muda kutokana na kutokuelewa hapa na pale lakini kwa sasa inaonekana wameweka mambo sawa...Ameandika haya kwenye ukurasa wake

_esmaplatnumz
Baby dady mkimuona mwambieni mi Nampenda tuu ukiniuliza hata sijui... kuna wakati unaweza kufichaficha au kujionesha hupendi au ukajikaza usiseme unachojisikia kusema but mi naona bora uwe muwazi ili roho yako Iwe na Amani... Jamani mi Nampenda huyu kaka plz nyakunyaku kuweni makini huyu mi nahisi km kafika kigoma mwisho wa reli...na natania msije nikomoa...hamchelewi...

FAIZA ALLY AFUNGUKA KUMPENDA SUGU KUTOKA MOYONI..ADAI HAOGOPI KUCHEKWA KWA KIGEUGEU CHAKE


Faiza Ally Amefunguka haya Katika ukurasa wake wa Instagram:



Leo nimeamka akili yangu inawaza mapenzi tu... Mkatae mkubali mapenzi yana nafasi kubwa sana ktk maisha... Na mapenzi hayana baunsa...😅 Mimi nampenda sana baba mtoto wangu - Nina mpenzi yes lkn nampenda yeye zaidi - ana mpenzi Sawa lkn hainizui kuongea hisia zangu... Nachekwa Sawa lkn wanao nicheka hawako ktk maisha yangu Kwa hiyo sio muhimu sana na sioni aibu kusema hisia zangu Kwa mtu ninae mpenda... Nampenda Kila siku Kila mwaka Na sijui nta Acha lini kumpenda.... Ila naamini Kama Mungu alivyo mleta-alivyo muondoa Ndio atakavyo nisahaulisha Na kuniletea mwingine au pengine kum rudisha .... Mapenzi kwangu yana sound hivi➡️➡️➡️➡️ muonyesha unampenda - ajue unampenda- kuwa mkweli- usimuogope- simama Kwenye ukweli- kuwa halisi Na uache maisha yaendelee - usilazimishe- usijikaze -usijifiche- usijifanye ..... Mimi ni Karatasi jeupe nisome lkn ni hiari yako kunielewa sio lzm unielewe lkn mwisho wa siku silazimishi yote heri ..... Nakupenda sana baba mtoto - pengine una niona uchafu au sina dhamani lkn moyo wangu ndio ume kuchagua - usinihukumu -usinichukie iko siku Mungu ataleta heri zake ntakusahau utapata Amani Na mpenzi wako Na mm Na wangu au labda ntakufa hutanisikia Tena ila Kwa sasa Naomba uniache vile najisikia .....Nakupenda Joseph Tanzania inajua.... Mama yangu anajua... Mtoto wetu anajua na nitaka dunia ijueeeeeeeeeee😭 Nakupenda sanaaaaa baba Sasha - usiniulize Kwa nini.... mm mwenyewe sijui Nakupenda tu hivyo yani ........ Tag him mwambie mama Sasha anakupenda zaidi Kila siku Na hakunaga Na sizani Na Kama unapendwa zaidi ya ninavyo kupenda ! Na Kama unapendwa Basi una bahati sana mshukuru Mungu Maana Natamani kupendwa Kama ninavyo kupendwa.....💔💔💔 Acha nichoreke haina kwere kuchoreka Kwa ninae mpenda sio kesi ...😭

WASANII NA VIONGOZI WA WCB WAALIKWA NYUMBANI KWA RAISI MSTAAFU JAKAYA KIKWETE


Rais mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete Jumatano hii aliwaalika wasanii wa label ya WCB pamoja na viongozi nyumbani kwake na kula nao chakula cha mchana. JK ambaye ni mmoja kati ya marais ambaye amesupport sana wasanii wa muziki nchini, aliwaalika wasanii hao nyumbani kwake na kuzungumza nao mambo mbalimbali kuhusu muziki wao. Mmoja kati ya viongozi wa juu wa label hiyo, Sallam alimshukuru rais huyo kwa kuwaalika nyumbani kwake na kuzungumza nao mawili matatu kuhusu muziki. 
 “Former President JM Kikwete and Former First Lady Mama Salma Kikwete. Asanteni kwa mwaliko wenu!! Allah awape afya njema,” Sallam aliandika instagram.