Poda ya Johnson, iliyodhaniwa kuwa ni kipodozi na tiba mujarabu kwa watoto na watu wazima duniani kote imebainika kusababisha saratani.
Jana, Mahakama ya St Louis ya Marekani, iliiamuru kampuni inayotengeneza poda hizo, Johnson & Johnson kumlipa Deane Berg wa Sioux Falls, South Dakota, Dola za Marekani 55 milioni (Sh118 bilioni ) baada ya kujiridhisha kuwa kipodozi hicho kilimsababishia saratani ya mayai ya uzazi (ovarian cancer).
Mpaka sasa, zaidi ya wanawake 1,000 wameshafungua kesi kuishtaki kampuni hiyo kwa madai ya kuwasababishia saratani hiyo baada ya kutumia poda ya Johnson kwa miaka mingi.
Ofisa Uhusiano wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania, (TFDA), Gaudensia Simwanza alisema wanazo taarifa juu ya madhara ya poda hizo ingawa bado hawajathibitisha kitaalamu kwa poda zilizopo nchini.
Alisema TFDA ilishafanya uchunguzi wa kimaabara kuhusu poda hizo lakini haikuona madhara yoyote.
Simwanza alisema FDA ilitakiwa pia kuwapa taarifa watumiaji wa bidhaa hizo duniani kuhusu madhara ya poda hizo.
Mwaka 2013, Berg alikuwa mwanamke wa kwanza kuishtaki kampuni hiyo baada ya kugundulika na saratani.
Baada ya kuridhishwa na malalamiko ya Berg, Mahakama iliamuru kampuni ya Johnson & Johnson kutoa onyo kuwa poda hizo, Johnson Baby Powder na sabuni ya Shower to Shower, zinasababisha saratani. Hata hivyo, kampuni hiyo haikufanya hivyo.
Baada ya mwaka mmoja, Berg alifungua tena kesi hiyo na Mahakama iliamuru alipwe kiasi hicho cha fedha.
Daktari wa Hospitali ya Wanawake, Brigham, Daniel Cramer alitoa ushahidi mbele ya Mahakama na kueleza kuwa zaidi ya wanawake 10,000 wamegundulika kuwa na saratani ya mayai ya uzazi kwenye hospitali hiyo.
Kadhalika, wanawake hao walibainika kuwa na chembechembe za ‘talcum’ kwenye kizazi.
Daktari wa Saratani wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Herry Tungaraza alisema kuna uwezekano wa kemikali ya ‘talcum’ kupenya kwenye ngozi, hadi kwenye damu na kuingia kwenye mayai ya uzazi na kisha kusababisha saratani.
Alisema si lazima poda hizi zimuathiri mtu kwa kuzitumia sehemu za siri tu, hata kama akizitumia kwa kupaka usoni, zinaweza kusafiri na kuathiri mayai ya uzazi. “Kama ingekuwa zinadhuru kwa kuzipaka sehemu za siri tu, basi zingeathiri zaidi shingo ya kizazi au nyumba ya uzazi, lakini mayai yapo mbali na ndiyo yaliyoathiriwa na saratani,” alisema.
Shahidi mwingine wa katika kesi ya Berg alithibitisha kuwa aliona chembechembe za ‘talcum kwenye uvimbe ulioko kwenye mayai ya Berg.
Mwathirika mwingine
Mei mwaka jana, Gloria Ristesund (62), alifungua kesi dhidi ya Johnson & Johnson kwa kushindwa kuwaonya wateja wake kuhusu poda hiyo kusababisha saratani.
Ristesund aligundulika na saratani, mwaka 2011 baada ya kutumia poda hiyo kwa kuipaka sehemu za siri kwa miaka kadhaa hasa. Mahakama iliamuru Ristesund pia kulipwa Dola 55 milioni.
Tovuti ya CNN inaeleza kuwa utafiti kuhusu kemikali za ‘talcum’ kusababisha saratani ulitolewa miaka mingi nyuma lakini Johnson & Johnson hawakutaka kuweka wazi ukweli huo kwa wateja wao.
“Ni kama kampuni zinazotengeneza sigara, wanajua kuwa imeshathibitishwa kuwa uvutaji wa sigara unasababisha saratani ya mapafu lakini wanauficha umma kuhusu hili,” ilisema taarifa ya CNN.
Alhamisi, 5 Mei 2016
Home »
» Kampuni yatozwa Sh118 Bilioni Poda yake Kusababisha Saratani
Kampuni yatozwa Sh118 Bilioni Poda yake Kusababisha Saratani
Related Posts:
MKUU WA USALAMA WA CHAMA CHA KIKOMUNISTI CHINA AKAMATWA Aliyekuwa mkuu wa usalama nchini China Zhou Yongkang amefukuzwa kutoka Chama cha Kikomunisti na atafunguliwa mashtaka huku kukifanyika uchunguzi wa ufisadi. Zhou alikuwa kiongozi wa kitengo cha usalama cha China kab… Read More
Mahakama ya ICC imetoa hukumu ya kesi iliyokuwa inamkabili Rais Kenyatta Mahakama ya Kimataifa ya ICC imetupilia mbali kesi ya jinai iliyokua inamkabili Rais wa Kenya,Uhuru Kenyatta kutokana na kutokamilika kwa ushahidi. Mwendesha mkuu wa mashitaka Fatou Bensouda ameondoa kesi dhidi ya Ken… Read More
EPL: Mambo yazidi kuwa magumu kwa Wenger: Matokeo ya Stoke vs Arsenal Wakati akiwa kwenye shinikizo la kutakiwa kutimuliwa, mambo yamezidi kuwa magumu kwa kocha mkongwe zaidi kwenye ligi kuu ya England Arsene Wenger. Akiiongoza timu kwenda mpaka kwenye dimba la Brittania kucheza dhidi ya … Read More
EPL: Kilichoikuta Chelsea leo katika mechi vs Newcastle < Ligi kuu ya Uingereza imeendelea leo hii na viongozi wa ligi klabu ya Chelsea leo walisafiri hadi katika dimba la St James Park kucheza Newcastle United. Wakiwa hawajapoteza mchezo wowote katika ligi kuu msimu huu C… Read More
Rapper mwingine wa TZ aliyetunukiwa shahada ya kwanza chuo kikuu . Rapper kutokea Unity Entertainment Stereo ambaye ameachia wimbo wake uitwao ‘Wako’ aliomshirikisha muimbaji wa Kenya,Victoria Kimani leo Des 6 ameongezewa CV yake ya Elimu baada ya kutunukiwa shahada ya ‘B… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni