Kabla mwaka 2014 haujaisha idadi ya watu maarufu wa Tanzania waliotangulia mbele za haki imezidi kuongezeka na hii ni baada ya taarifa kutoka Iringa zilizoanza kusambaa kuanzia saa tatu usiku November 11 2014.
Taarifa zilizothibitishwa ni kwamba rapper Geez Mabovu ambae ni maarufu kwenye muziki wa hiphop Tanzania, amefariki dunia kwenye hospitali aliyokua amelazwa nyumbani kwao Iringa alikokwenda wiki mbili zilizopita kutokea Dar es salaam.
Hii
ni picha ya July 2013 ambayo ni mara ya mwisho Geez Mabovu ameonekana
kwenye millardayo.com akiwa na Baba yake Dully Sykes maeneo ya Kinondoni
Dar es salaam nje ya Bar ya msanii Dudubaya aliyokua ameifungua wakati
huo.
Kwa mujibu wa Denis, Geez atazikwa kesho jioni November 13 2014. #RIP
0 comments:
Chapisha Maoni