BAADHI ya vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Bunda wamemtuhumu
mwenyekiti wa chama hicho wilayani hapa, Chacha Gimanwa, kwamba
alichangia jimbo la Bunda Mjini kuchukuliwa na mgombea wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika uchaguzi mkuu uliofanyika
Oktoba 25 mwaka huu.
Vijana hao walitoa tuhuma hizo, juzi wakati wakitembea matembezi ya
amani ya kushangilia ushindi wa mgombea urais wa CCM, Dk Jonh Magufuli
katika mitaa mbalimbali ya mji wa Bunda.
Katika uchaguzi mkuu uliopita CCM ilipoteza jimbo hilo, baada ya Stephen
Wasira aliyekuwa akitetea kiti hicho kushindwa na mgombea wa Chadema,
Ester Bulaya.
Hata hivyo Wasira ambaye pia ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
hivi karibuni akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza alidai
kuwa katika uchaguzi huo kulikuwa na hujuma.
Wanachama hao wa CCM wakiwa wamebeba mabango baadhi yao walisikika
wakimtaja moja kwa moja Gimanwa kwamba ndiye alisababisha CCM kushindwa
katika jimbo hilo na kuomba uongozi wa juu wa chama hicho umchukulie
hatua.
Hata hivyo, Gimanwa akizungumza na mtandao huu kwa njia ya simu jana
alisema kuwa tuhuma hizo hazina msingi wowote na kwamba kamwe hawezi
kukihujumu chama chake.
“Hicho ni kikundi cha watu wachache tu wanaotaka kuniharibia jina.Mimi
kura yangu ni moja na wapiga kura ni wengi, sasa iweje mimi nisababishe
mgombea wa jimbo la Bunda mjini ashindwe?” Alihoji.
Alisema yeye kama mwenyekiti wa CCM alikuwa akifanya kampeni pia katika
jimbo la Bunda vijijini, na siku tatu kabla ya uchaguzi mkuu alirudi
tena Bunda mjini na kuendelea na kampeni.
Jumapili, 1 Novemba 2015
Home »
» CCM Washikana 'Uchawi' Baada ya Kulipoteza Jimbo La Bunda
CCM Washikana 'Uchawi' Baada ya Kulipoteza Jimbo La Bunda
Related Posts:
PICHA HIZI ZINAONESHA SHANGWE YA SERENGETI FIESTA 2014 MKOANI MOROGORO NI SHEEEEEDAH . Show ya Serengeti Fiesta 2014 iliyofanyika Jumapili,Sept 21 kwenye uwanja wa Jamhuri Stadium imefana baada ya wakazi wa (88.5) Morogoro kupokea kwa shangwe burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali Tazama picha z… Read More
UJIO WAKE STEVE RNB,NI NOUMA Ni baada ya kimya kirefu kutoka kwa msanii Steve rnb sasa amerudi na ngoma kali.Unaweza kuiskiliza online au kudownload kuihifadhi katika kifaa chako. … Read More
Kesi ya Emmanuel Mbasha imesogezwa tena mpaka October. Kesi ya mwimbaji wa nyimbo za Injili Emmanuel Mbasha imepigwa kalenda kwa mara nyingine tena kwa sababu Hakimu anayeendesha kesi hiyo kupata shughuli nyingine nje ya ofisi. Mbasha alipanda kizimbani katika mahakama… Read More
MASHABIKI WAMTUKANA BALOTELLIUjumbe wa Balotelli ulioibua hisia za ubaguzi wa rangi kwenye mtandao wa twitter Polisi nchini Uingereza wameanzisha uchunguzi kuhusu tukio ambalo mshambulizi wa Liverpool kutoka Italia Mario Balotelli alitukanwa kut… Read More
EPL: Matokeo ya Man City vs Chelsea haya hapa Home » General News » EPL: Matokeo ya Man City vs Chelsea haya hapa EPL: Matokeo ya Man City vs Chelsea haya hapa Posted by: TZA Sports September 21, 2014 General News Baada ya Man United kupokea… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni