BAADHI ya vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Bunda wamemtuhumu
mwenyekiti wa chama hicho wilayani hapa, Chacha Gimanwa, kwamba
alichangia jimbo la Bunda Mjini kuchukuliwa na mgombea wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika uchaguzi mkuu uliofanyika
Oktoba 25 mwaka huu.
Vijana hao walitoa tuhuma hizo, juzi wakati wakitembea matembezi ya
amani ya kushangilia ushindi wa mgombea urais wa CCM, Dk Jonh Magufuli
katika mitaa mbalimbali ya mji wa Bunda.
Katika uchaguzi mkuu uliopita CCM ilipoteza jimbo hilo, baada ya Stephen
Wasira aliyekuwa akitetea kiti hicho kushindwa na mgombea wa Chadema,
Ester Bulaya.
Hata hivyo Wasira ambaye pia ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
hivi karibuni akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza alidai
kuwa katika uchaguzi huo kulikuwa na hujuma.
Wanachama hao wa CCM wakiwa wamebeba mabango baadhi yao walisikika
wakimtaja moja kwa moja Gimanwa kwamba ndiye alisababisha CCM kushindwa
katika jimbo hilo na kuomba uongozi wa juu wa chama hicho umchukulie
hatua.
Hata hivyo, Gimanwa akizungumza na mtandao huu kwa njia ya simu jana
alisema kuwa tuhuma hizo hazina msingi wowote na kwamba kamwe hawezi
kukihujumu chama chake.
“Hicho ni kikundi cha watu wachache tu wanaotaka kuniharibia jina.Mimi
kura yangu ni moja na wapiga kura ni wengi, sasa iweje mimi nisababishe
mgombea wa jimbo la Bunda mjini ashindwe?” Alihoji.
Alisema yeye kama mwenyekiti wa CCM alikuwa akifanya kampeni pia katika
jimbo la Bunda vijijini, na siku tatu kabla ya uchaguzi mkuu alirudi
tena Bunda mjini na kuendelea na kampeni.
Jumapili, 1 Novemba 2015
Home »
» CCM Washikana 'Uchawi' Baada ya Kulipoteza Jimbo La Bunda
CCM Washikana 'Uchawi' Baada ya Kulipoteza Jimbo La Bunda
Related Posts:
MADUKA YA UCHUMI SUPERMARKET YAFUNGWA TANZANIA NA UGANDA Uongozi wa Uchumi Supermarket umetangaza kufunga shughuli zake katika maduka yake yaliyopo Tanzania na Uganda ili kutoa nafasi ya kuzuia mtikisiko wa kifedha unaoikumba kampuni hiyo. Ofisa Mtendaji Mkuu wa Uchumi, Dk Jul… Read More
KILA KITU AANIKA:HATIMAYE AGNESS MASOGANGE AFUNGUKIA PENZI LA DAVIDO VIDEO Queen mwenye umbo tata Bongo, Agness Jerald ‘Masogange’ alifungukia penzi lake na staa wa muziki kutoka Nigeria, Davido. Akizungumza na Amani Masogange alisema kuwa kuna uvumi unaovumishwa na baadhi ya watu kwamba a… Read More
MGOMBEA WA URAISI CCM DR. JOHN POMBE MAGUFULI AMFAGILIA DAIMOND PLATNUMZ MGOMBEA urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Magufuli amemmwagia sifa lukuki, mkali wao ndani ya muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kutokana na ushindi wa tuzo tatu za Afrimma zilizofanyika wikiendi iliyop… Read More
Rihanna:NINA HAMU YA KUFANYA MAPENZI LAKINI.......(PICHA) Rihanna anasema yeye ni kama wanawake wengine kiasi cha kuwa na hamu ya kufanya mapenzi na kwamba hajavunja amri ya sita kwa muda mrefu sasa. rihanna-cover Akiongea kwenye jarida la Vanity Fair, Rihanna alisema hawezi tu… Read More
DR MTIKILA ALIUAWA KABLA YA AJALI DP MAPYAA! Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrati (DP), Abdul Juma Mluya ameibuka na kusema mazingira ya kifo cha aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho, Mchungaji Christopher Mtikila yamejaa utata huku akiweka wazi kwamb… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni