BAADHI ya vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Bunda wamemtuhumu
mwenyekiti wa chama hicho wilayani hapa, Chacha Gimanwa, kwamba
alichangia jimbo la Bunda Mjini kuchukuliwa na mgombea wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika uchaguzi mkuu uliofanyika
Oktoba 25 mwaka huu.
Vijana hao walitoa tuhuma hizo, juzi wakati wakitembea matembezi ya
amani ya kushangilia ushindi wa mgombea urais wa CCM, Dk Jonh Magufuli
katika mitaa mbalimbali ya mji wa Bunda.
Katika uchaguzi mkuu uliopita CCM ilipoteza jimbo hilo, baada ya Stephen
Wasira aliyekuwa akitetea kiti hicho kushindwa na mgombea wa Chadema,
Ester Bulaya.
Hata hivyo Wasira ambaye pia ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
hivi karibuni akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza alidai
kuwa katika uchaguzi huo kulikuwa na hujuma.
Wanachama hao wa CCM wakiwa wamebeba mabango baadhi yao walisikika
wakimtaja moja kwa moja Gimanwa kwamba ndiye alisababisha CCM kushindwa
katika jimbo hilo na kuomba uongozi wa juu wa chama hicho umchukulie
hatua.
Hata hivyo, Gimanwa akizungumza na mtandao huu kwa njia ya simu jana
alisema kuwa tuhuma hizo hazina msingi wowote na kwamba kamwe hawezi
kukihujumu chama chake.
“Hicho ni kikundi cha watu wachache tu wanaotaka kuniharibia jina.Mimi
kura yangu ni moja na wapiga kura ni wengi, sasa iweje mimi nisababishe
mgombea wa jimbo la Bunda mjini ashindwe?” Alihoji.
Alisema yeye kama mwenyekiti wa CCM alikuwa akifanya kampeni pia katika
jimbo la Bunda vijijini, na siku tatu kabla ya uchaguzi mkuu alirudi
tena Bunda mjini na kuendelea na kampeni.
Jumapili, 1 Novemba 2015
Home »
» CCM Washikana 'Uchawi' Baada ya Kulipoteza Jimbo La Bunda
CCM Washikana 'Uchawi' Baada ya Kulipoteza Jimbo La Bunda
Related Posts:
CHADEMA na Katibu Mkuu mfu..Ukimya Wake ni Hatari kwa Mustakabari wa ChamaKiukweli huyu katibu mkuu hajui hata pa kuanzia Chama kinaonesha dalili za kuifuata TLP na UDP sioni harakati zake ki ukweli CHADEMA ilikosea sana Dr. Mashinji ni unpopular figure hata akitembea kwa miguu Karikoo hakuna wa ku… Read More
Nuh Mziwanda Afunguka Kuhusu Kurudiana na ShiloleMsanii Nuh Mziwanda ambaye kwa sasa anafanya poa na wimbo wake mpya ambao amemshirikisha Alikiba amefunguka na kusema kuwa hata kama ikitokea mpenzi wake huyo wa zamani akitaka kurudiana na yeye ni kitu kisichowezekana kwa sa… Read More
Jason Rweikiza Achaguliwa Kuwa Katibu wa Wabunge wa CCMWABUNGE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamemchagua Mbunge wa Bukoba Vijijini, Jason Rweikiza kuwa Katibu wao. Rweikiza anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Mbunge wa Peramiho, Jenista Mhagama, ambaye safari hii hakuwania nafasi … Read More
PICHA: Jionee kaburi atakalozikwa Papa WembaPicha hii inasemekana ndilo kaburi atakapozikwa mwanamziki Maarufu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo maarufu kwa jina la Papa Wemba. Huu ni zaidi ya ufahari, lakini mimi naona hauna maana.. … Read More
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Singida Asimamishwa Kazi Baada ya Kutoa Taarifa za Uongo Kuhusu Watumishi HEWAMkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Singida, Simion Mumbee amesimamishwa kazi baada ya kudaiwa kutoa taarifa za uongo kuhusu watumishi hewa. Katika taarifa hiyo, Mumbee anadai watumishi hewa 19 waliogundulika kwenye halmash… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni