Watu sita wamefariki dunia baada ya gari ndogo waliokuwa wakisafiria
kugongana uso kwa uso na basi la abiria mali ya kampuni ya Princess
Muro, lililokuwa likitokea Dar es salaam kuelekea Tunduma, katika eneo
la hifadhi ya taifa ya Mikumi, barabara kuu ya Morogoro-Iringa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Leonard Paulo amethibitisha kutokea
kwa ajali hiyo katika eneo la hifadhi ya taifa ya Mikumi, ikihusisha
gari ndogo la abiria aina ya Toyota Noah lenye namba za usajili T 359
BBA iliyokuwa imebeba abiria sita wakiwemo wanawake wawili na wanaume
wanne ambayo ilipasuka tairi ya Mbele ya kuyumba ovyo barabarani na
kugongana na basi hilo la Princess Muro lenye namba T 160 BBC na
kusababisha vifo kwa abiria wote wa Noah.
Amesema basi hilo la abiria aina ya Zangton lililoharibika zaidi mbele
huku Noah ikiharibika kabisa, likuwa likiendeshwa na Silos Wilfred (55)
mkazi wa Mbeya ambaye anahojiwa na polisi kuhusiana na tukio hilo, na
kwamba basi alilokuwa akiendesha lilikuwa na abiria 59 ambao hawakupata
madhara makubwa, isipokuwa michubuko kidogo kwa baadhi yao na
walitafutiwa usafiri kuendelea na safari.
Katika upekuzi wa miili ya abiria waliokuwa kwenye Noah inayodaiwa
kuhusika na ubebaji wa magazeti, viligundulika vitambulisho vimne vya
Ali Nduti Mohamed (27), mkazi wa Mbeya,Sani Elion Mkwabe (24) mkazi wa
Kunduchi, Patrick Mkelegene (43) mkazi wa Buguruni Malapa na Selemani
Omary (30) ambaye makazi yake hàyajaweza kujulikana Mara moja.
Miili ya watu hao waliopoteza maisha imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.
Jumapili, 1 Novemba 2015
Home »
» Watu Sita Wapoteza Maisha Katika Ajali ya Gari Morogoro
Watu Sita Wapoteza Maisha Katika Ajali ya Gari Morogoro
Related Posts:
Taarifa ya Jeshi la Polisi kuhusu ajali iliyotokea Tabora Aug 19. Taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora ambayo ameitoa leo kwa Waandishi wa habari ni kuhusu ajali ambayo ilitokea jana Aug 19 majira ya saa 9 alasiri ambayo ilihusisha mabasi mawili. Mabasi hayo ni AM Coach na S… Read More
Waandamanaji wataka Nawaz Sharif ajiuzulu Waandamanaji wanopinga serikali nje ya bunge la Pakistan, hawaonyeshi ishara yoyote ya kuondoka,hadi pale waziri mkuu Nawaz Sharif atakapojiuzulu, dai ambalo serikali imekataa kwa misingi ya kuwai kinyume n… Read More
WATU 32 WAMEFARIKI KWENYE MAPOROMOKO YA ARDHI Watu 32 wamefariki katika maporomoko ya ardhi(landslide) katika mkoa wa Hiroshima nchini Japan.Maporomoko hayo yamesababishwa na mvua kubwa zilizonyesha kwa saa 24 kuamkia Jumatano asubuhi zikiwa sawa na kipimo cha … Read More
Uliipata hii ya Wanafunzi Kenya kupelekwa Mahakamani baada ya kukutwa wamelewa? Sio kitu kigeni kuona watu wenye umri zaidi ya miaka 18 wanakunywa Pombe wanalewa na hata pombe hiyo kugharimu maisha yao ila sio kawaida kukutana ama kuona mtoto wa miaka kati ya 14-17 ni mlevi wa kupindukia na … Read More
Mfanyakazi wa benki afikishwa mahakamani kwa kuiba pesa za abiria walipotea na Malaysia airline Mwanamke mmoja mwenye cheo cha juu katika bank kubwa iliyopo Kuala Lumpur Malaysia pamoja na mumewe wameshtakiwa kwa kuiba pesa kutoka katika account za abiria na wafanyakazi wa ndege ya Malaysia iliyopotea kwenye bahar… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni