Saa chache baada ya rais Magufuli
kutangaza baraza lake la Mawaziri ambalo limekuwa baraza dogo kama
alivyoahidi, aliyekuwa mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) na mbunge
wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu wamekosoa uteuzi wa Profesa
Sospeter Muhongo na Dk. Harison Mwakyembe.
Dk. Mwakyembe alikuwa waziri wa Uchukuzi
katika serikali ya awamu ya nne na hivi sasa ameteuliwa kuwa waziri wa
Katiba na Sheria. Profesa Muhongo ambaye alijiuzulu kwa kashfa ya Escrow
katika serikali ya awamu ya nne, amerudishwa katika wizara ya Nishati
na Madini.
Profesa Lipumba amekosoa uteuzi wa profesa Muhongo kwa madai kuwa uteuzi wake umelitia doa baraza hilo.
“Kwa kitendo kama hiki, Rais Magufuli
amejiwekea dosari kutokana na uteuzi huu. Maana yake ni kuwa katika
kashfa ile Profesa Muhongo hakuwa na hatia,” Profesa Lipumba aliliambia
gazeti la Mwananchi.
Profesa Lipumba aliongeza kuwa wananchi
watapata ugumu kumuelewa Rais kutokana na ahadi zake kuwa atapambana na
rushwa na ufisadi.
Naye Tundu Lissu aliliambia gazeti hilo
kuwa uteuzi wa Dk. Harison Mwakyembe hakuwa sahihi kwa kuwa ndiye
aliyekuwa waziri wa Uchukuzi na punde baada ya rais Magufuli kuingia
ikulu, Mamlaka ya Bandari ikabainika kukumbwa na kashfa ya upotevu wa
makontena.
“Juzi Rais Magufuli aliufumua uongozi wa
Bandari ya Dar es Salaam kutokana na kashfa, miongoni mwa waziri
waliokuwa wakisimamia sekta hiyo ni Dk. Harrison Mwakyembe, eti leo
amemrudhisha kundini?” Lissu ananukuliwa.
Lissu aliongeza kuwa Muhongo pia hakufaa kuwa miongoni mwa mawaziri kwa kuwa alifukuzwa na Bunge kutokana na sakata la Escrow.
Hata hivyo, Profesa Lipumba alimpongeza rais kwa kutekeleza ahadi yake ya kuunda baraza dogo kwa lengo la kubana matumizi.
Ijumaa, 11 Desemba 2015
Home »
» Profesa Lipumba, Lissu wapinga uteuzi wa Muhongo na Mwakyembe
Profesa Lipumba, Lissu wapinga uteuzi wa Muhongo na Mwakyembe
Related Posts:
MONACO YAINGIA VITANI NA REAL MADRID KUISAKA SAINI YA TORRES Monaco na Atletico Madrid wanaitaka saini ya Fernando Torres. KLABU ya Monaco imeingia katika vita na Atletico Madrid kuiwinda saini ya mshambuliaji wa Chelsea, Fernando Torres. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Hispania mw… Read More
Hii ndio idadi ya waliokufa baada ya mji wa Lamu Kenya kukumbwa na mashambulizi ya risasi. Wizara ya mambo ya ndani Kenya imesema kuwa zaidi ya watu 29 wameuawa katika mashambulizi mawili tofauti katika makazi ya Pwani ya nchi hiyo karibu na mpaka wa Somalia. Watu 20 waliuawa katika eneo la Gamba kaunti ya Ta… Read More
TOFAUTI ZA DINI ZISIWAGAWE WATANZANIA ,MWINYI Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Saidi Meck Sadiki akiongea na watoto wanaotoka katika vituo mbalimbali vya kulelea watoto yatima vya jijini Dar es salaam , wakazi wa jiji la Dar es salaam na viongozi mbalimba… Read More
Hiki ndicho kitu kikubwa atakachofanya Diamond siku ya birthday ya mama yake. Mama yake Diamond amezaliwa tarehe 7/7 na siku hiyo Diamond amepanga kufanya kitu kikubwa akiwa anasherekea. Mwaka huu anafanya kitu ambacho hadi mashabiki zake watafurahia siku hiyo na hii ni nafasi yako kukijua. … Read More
WAZIRI MKUU AFUNGUA MKUTANO WA TATHMINI YA UTEKELEZAJI BRN Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Benno Ndulu akichangia hoja wakati wa mkutano wa kupitia taarifa ya mwaka mmoja ya utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa sasa (BRN) uliofanyika leo Jumatano Julai 23, 2014 kati… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni