Saa chache baada ya rais Magufuli
kutangaza baraza lake la Mawaziri ambalo limekuwa baraza dogo kama
alivyoahidi, aliyekuwa mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) na mbunge
wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu wamekosoa uteuzi wa Profesa
Sospeter Muhongo na Dk. Harison Mwakyembe.
Dk. Mwakyembe alikuwa waziri wa Uchukuzi
katika serikali ya awamu ya nne na hivi sasa ameteuliwa kuwa waziri wa
Katiba na Sheria. Profesa Muhongo ambaye alijiuzulu kwa kashfa ya Escrow
katika serikali ya awamu ya nne, amerudishwa katika wizara ya Nishati
na Madini.
Profesa Lipumba amekosoa uteuzi wa profesa Muhongo kwa madai kuwa uteuzi wake umelitia doa baraza hilo.
“Kwa kitendo kama hiki, Rais Magufuli
amejiwekea dosari kutokana na uteuzi huu. Maana yake ni kuwa katika
kashfa ile Profesa Muhongo hakuwa na hatia,” Profesa Lipumba aliliambia
gazeti la Mwananchi.
Profesa Lipumba aliongeza kuwa wananchi
watapata ugumu kumuelewa Rais kutokana na ahadi zake kuwa atapambana na
rushwa na ufisadi.
Naye Tundu Lissu aliliambia gazeti hilo
kuwa uteuzi wa Dk. Harison Mwakyembe hakuwa sahihi kwa kuwa ndiye
aliyekuwa waziri wa Uchukuzi na punde baada ya rais Magufuli kuingia
ikulu, Mamlaka ya Bandari ikabainika kukumbwa na kashfa ya upotevu wa
makontena.
“Juzi Rais Magufuli aliufumua uongozi wa
Bandari ya Dar es Salaam kutokana na kashfa, miongoni mwa waziri
waliokuwa wakisimamia sekta hiyo ni Dk. Harrison Mwakyembe, eti leo
amemrudhisha kundini?” Lissu ananukuliwa.
Lissu aliongeza kuwa Muhongo pia hakufaa kuwa miongoni mwa mawaziri kwa kuwa alifukuzwa na Bunge kutokana na sakata la Escrow.
Hata hivyo, Profesa Lipumba alimpongeza rais kwa kutekeleza ahadi yake ya kuunda baraza dogo kwa lengo la kubana matumizi.
Ijumaa, 11 Desemba 2015
Home »
» Profesa Lipumba, Lissu wapinga uteuzi wa Muhongo na Mwakyembe
Profesa Lipumba, Lissu wapinga uteuzi wa Muhongo na Mwakyembe
Related Posts:
Rais Magufuli Afunguka na Kusema Yeye si Kichaa wala Dikteta ila Inafika Wakati Lazima Afanye Hivyo!! RAIS Dk. John Magufuli amesema anapochukua hatua yeye si kichaa, si dikteta, si shetani wala si mnyama, ila ni mpole, lakini amefika mahali lazima afanye hivyo kwani ndani ya Serikali yanafanyika mambo ya ajabu. Kauli h… Read More
Siri Imefichuka..Kumbe Rwanda ilitoa Mafunzo ya Kijeshi kwa Wakimbizi wa Burundi Wamwondoe Nkurunziza Madarakani Ripoti ya siri ya Umoja wa Mataifa(UN): Rwanda ilitoa mafunzo ya kijeshi kwa wakimbizi wa Burundi wamwondoe Nkurunziza madarakani. Burundi imekabiliwa na machafuko tangu mwezi Aprili 2015, wakati Rais Pierre Nkurunziza a… Read More
Njia Kumi na Moja za Kumfanya Mpenzi Wako Asitoke nje na Michepuko 1. TAMBUA THAMANI YAKE Unapokuwa Umeapa Kuwa Utampenda Mwenzako Hadi Kifo Kitakapowatenganisha, Uwe Umefanya Hivyo Kwenye Nyumba Ya Ibada Au Kwingine, Lazima Ufahamu Jinsi Ya Kutambua Juhudi Za Mpenzi Au Mwenzi Wako,… Read More
Mke wa Dr Slaa Josephine Mushumbusi Ajibu Kuhusu Tuhuma za Kuomba Mkopo Bank Kwa Kutumia Nyumba ya Slaa Mke wa Dr Slaa Amejibishana na Wadau Katika page yake ya Facebook na kujikuta akijibu tuhuma zilizozagaa jana kwenye magazeti kuwa aliomba mkopo wa sh mil 300 kwa kutumia nyumba ya Dr Slaa... Soma Majibisha yao hapa; B… Read More
Imebainika Mashine ya CT Scan Iliyofungwa Muhimbili Hospital ni ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto imekiri kwamba mashine ya CT Scan iliyofungwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ilikuwa ni ya kituo cha kisasa cha kutolea huduma za afya cha Benjamin Mkapa… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni