KIMENUKA! Baada ya Miss Tanzania 2006
aliye pia nyota wa sinema za Bongo, Wema Sepetu ‘Madam’ kunaswa na
Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) akidaiwa kutumia umeme wa shirika
hilo kinyemela, kuna madai atapandishwa kortini.
Taarifa kutoka chanzo makini zinasema
kuwa, mrembo huyo alifanya ‘manuva’ hayo katika nyumba anayoishi,
Kijitonyama, Dar hivyo kuweza kuliingizia hasara shirika hilo hali
ambayo shirika hilo haliwezi kumvumilia.
“Amefanya ile michezo ya kuchezea mita.
Mita inakuwa inasoma umeme mdogo lakini mzigo unaotumika ndani mkubwa,
haufanani na malipo halisi ambayo alistahili kulipia,” kilisema chanzo
chetu na kuongeza:
“Maofisa wa Tanesco juzikati ndiyo
wakampitia. Inasemekana Wema alikuwa ndani na Idris (yule mshindi wa Big
Brother Africa). Idris ndiye alitoka lakini Madam hakuinua miguu yake
kwenda nje, wakamng’olea mita na kuondoka nayo.”
Baada ya chanzo hicho kuvujisha ubuyu
huo sambamba na picha zilizosemekana ni za siku ya tukio wakati maofisa
hao walipofika nyumbani hapo na kufanya ‘ambushi’, paparazi wetu
alimpigia simu Wema kwa muda mrefu lakini hakupatikana, akampigia mtu wa
karibu na Madam, Ahmed Hasheem ‘Petit Man’ ambapo alipatikana na
kusema:
“Unajua kaka mimi si msemaji wa Wema.
Mimi ni msemaji wa wasanii walio kwenye lebo ya Wema ya Endless Fame.
Kama unataka msemaji wake, cheki na Martin Kadinda.”
Alipotafutwa Martin, alijibu kwa kifupi:
“Kaka hata mimi nazisikia hizo habari lakini sipo Dar, nikirudi
nitakwenda kucheki halafu nitakupa taarifa kamili.”
Juzi Jumanne, paparazi wetu alifika
nyumbani kwa Wema ili kujionea sakata hilo lakini hakufanikiwa kuingia
getini baada ya kugonga geti kwa muda mrefu bila majibu.
Mmoja wa majirani wa mrembo huyo aliyeomba hifadhi ya jina, alipoulizwa kuhusu kufahamu sakata hilo, alisema:
“Kiukweli sisi wenyewe tulishangaa.
Tunaamini Madam si mtu kuchezea mita. Ni mtu anayejiweza, anayejitambua
sasa tumeshtuka kuona mita inatolewa.”
Paparazi wetu alifika Ofisi za Tanesco
Mkoa wa Kinondoni Kaskazini (Mikocheni) ili kuzungumza na wahusika
lakini akakosa ushirikiano.
Hata hivyo, mfanyakazi mmoja wa Kitengo
cha Emergency (Dharura) aliyeomba kufichwa jina lake, alisema ni kweli
zoezi hilo lilifanyika nyumbani kwa Wema, Jumatatu iliyopita na kukutana
na kadhia hiyo ambapo alisema madam huyo atapandishwa mahakamani kujibu
mashitaka ya kuiibia Tanesco.
GPL
Ijumaa, 11 Desemba 2015
Home »
» Wema Sepetu Kortini Kwa Uwizi wa Umeme..Tanesco Waeleza Makubwa
Wema Sepetu Kortini Kwa Uwizi wa Umeme..Tanesco Waeleza Makubwa
Related Posts:
Madiwani wa Moshi Wasusa Semina Kisa Malipo ya Posho Kuwa Madogo..Wataka Walipwe Laki Moja Kwa Kikao..!! HALI ya taharuki imeibuka katika Halmashauri ya Moshi baada ya madiwani kugomea mafunzo ya utaratibu ulioboreshwa wa uendeshaji ruzuku ya maendeleo kwenye mamlaka za Serikali za mitaa (LGDG), wakishinikiza kulip… Read More
Friji Lateketeza Jengo la Ghorofa 27 kwa Muda wa Dakika 15..!!! MOTO uliozuka kwenye jengo la ghorofa 27 lililoko London Magharibi kwa dakika 15 baada ya friji kulipuka, itakuwa ni moja ya ajali mbaya kupata kutokea katika historia ya nchi hii huku kukiwa na hofu ya kutokuw… Read More
UVCCM Wampa za Uso Lowassa Kuhusu Sakata la Makinikia..!!! Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UVCCM) umemtaka Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya Rchmond Edward Lowassa kuacha uongo kwani hana historia ya kupigania maslahi ya umma. Aidha, imesema madai ya low… Read More
Alichokisema Kafulila Baada ya Serikali Mkoani Kilimanjaro Kuharibu Shamba la Mbowe..!!! ALIYEKUWA Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila amelaani hatua ya Mkuu wa Wilaya ya Hai, Gelasius Byakanwa kutumia mamlaka yake kuvamia na kuharibu shamba la Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe. Juzi, Kamati ya U… Read More
Maajabu Marekani Imesaini Mkataba wa Kuizia Qatar Ndege za Kivita Aina ya F-15 kwa $12billions..!! Wengi Mnakumbuka Sekeseke la Juzi ambapo Marekani waliishutumu Qatar kusaidia kifedha Mitandao ya Ugaidi. Balozi mbalimbali zilifungwa na Sasa Marekani na Qatar wamesaini deal ya Kuuziana ndege za Kivita aina… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni