Diamond Platnumz amesema akiachana na muziki anataka kuwa Waziri wa
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ili kuweka vitu sawa na kutoa fursa
zaidi kwa vijana.
Akizungumza katika kipindi cha Papaso cha TBC FM, Diamond alisema kama
akiingia kwenye siasa basi nia yake ni kuwa Waziri wa Michezo.
“Kwa sasa hivi siasa bado ila nikiingia kwenye siasa baadaye akimaliza
mheshimiwa Nape nachukua mimi kile cheo cha Waziri wa Michezo,” alisema
na kuongeza;
“Kile nakiweza kabisa kwa sababu mimi ukinimbia sijui kuhusu mpira,
movie mimi naweza kabisa nikiwa Waziri, nikavifanya na vikawa na
maendeleo.
"Ni kitu ambacho naweza siyo nasema nataka kuwa mbunge ila mimi nataka
ile siku nimeacha kufanya muziki naingia kwenye siasa basi nakuwa Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na kuboresha vitu”
Diamond ambaye hakuweka wazi kwamba ataingia kwenye siasa kupitia chama
gani, mwaka jana katika kampeni za uchaguzi mkuu uliomuingiza rais
Magufuli madarakani, alishiriki kikamilifu kwenye kampeni za CCM na
kutengeneza wimbo pamoja na video.
Jumanne, 26 Januari 2016
Home »
» Diamond Platnumz: Baada Ya Nape Nnauye Mimi Ndo Waziri wa Habari Na Michezo Mtarajiwa
Diamond Platnumz: Baada Ya Nape Nnauye Mimi Ndo Waziri wa Habari Na Michezo Mtarajiwa
Related Posts:
DAYNA NYANGE AITAMANI NDOA Biblia Takatifu kitabu cha Mathayo 19:3 unasema “Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake, ataungana na mke wake, kwa hiyo wao si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asikite… Read More
Baada ya Kutoka Marekani Mtoto Getrude Clement Akaribishwa Bungeni LeoGetrude Clement mwenye umri wa miaka 16 ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu anayesoma shule ya Sekondari Mnarani iliyopo jijini Mwanza, leo amepata nafasi ya kufika bungeni Dodoma baada ya kupewa mwaliko wa Serikali Hivi … Read More
Donald Trump Asema Uchina “inaibaka” MarekaniMgombea mkuu wa chama cha Republican Donald Trump ameshutumu Uchina na kusema imekuwa “ikiibaka” Marekani kupitia sera zake za kibiashara. Ameambia watu waliohudhuria mkutano wa kisiasa Indiana kwamba Uchina imekuwa ikitekele… Read More
Waziri Makamba Awasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.Serikali inaendelea kusimamia mazingira na kuhakikisha mifuko ya plastiki inayotumika nchini iwe ni ile inayokidhi viwango vianavyokubalika ili kuondokana na changamoto ya kuzagaa kwa mifuko hiyo katika maeneo mbalimbali. Kau… Read More
Aliyejifungua Watoto 3 Anaomba Asaidiwe kwani naye ni Mgonjwa wa Pumu MKAZI wa Kijiji cha Mapinduzi Kata ya Kigwe Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma Julietha Sokoine (24) amejifungua watoto wa watatu na ameiomba serikali, taasisi,mashirika na watu binafsi kumpatia msaada wa kifedha utakaomsaidia k… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni