Diamond Platnumz amesema akiachana na muziki anataka kuwa Waziri wa
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ili kuweka vitu sawa na kutoa fursa
zaidi kwa vijana.
Akizungumza katika kipindi cha Papaso cha TBC FM, Diamond alisema kama
akiingia kwenye siasa basi nia yake ni kuwa Waziri wa Michezo.
“Kwa sasa hivi siasa bado ila nikiingia kwenye siasa baadaye akimaliza
mheshimiwa Nape nachukua mimi kile cheo cha Waziri wa Michezo,” alisema
na kuongeza;
“Kile nakiweza kabisa kwa sababu mimi ukinimbia sijui kuhusu mpira,
movie mimi naweza kabisa nikiwa Waziri, nikavifanya na vikawa na
maendeleo.
"Ni kitu ambacho naweza siyo nasema nataka kuwa mbunge ila mimi nataka
ile siku nimeacha kufanya muziki naingia kwenye siasa basi nakuwa Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na kuboresha vitu”
Diamond ambaye hakuweka wazi kwamba ataingia kwenye siasa kupitia chama
gani, mwaka jana katika kampeni za uchaguzi mkuu uliomuingiza rais
Magufuli madarakani, alishiriki kikamilifu kwenye kampeni za CCM na
kutengeneza wimbo pamoja na video.
Jumanne, 26 Januari 2016
Home »
» Diamond Platnumz: Baada Ya Nape Nnauye Mimi Ndo Waziri wa Habari Na Michezo Mtarajiwa
Diamond Platnumz: Baada Ya Nape Nnauye Mimi Ndo Waziri wa Habari Na Michezo Mtarajiwa
Related Posts:
LOWASSA AKAGUA SHULE ILIYOUNGUA HUKO MONDULI Kiasi cha wanafunzi 100 wa shule ya sekondari ya Erikisongo wilayani Monduli wamenusurika kifo baada ya vyumba vitano vya mabweni yao kuteketea na moto leo (Jumatano) asubuhi. Moto huo ambao inaelezwa chanzo chake… Read More
MADEREVA WA VYOMBO VYA MOTO MUWE MAKINI Gari aina ya Toyota Hilux limetumbukia kwenye mtaro uliopo Sinza-Makaburini jijini Dar es Salaam baada ya dereva aliyekuwa akiliendesha gari hiyo kushin… Read More
Ajali ya Ndege:Miili imewasili Uholanzi Miili ya abiria wa ndege ya Malaysia MH17 imewasili Eindhoven Ndege mbili za kijeshi zinazobeba miili 40 kati ya 282 ya abiria wale waliofariki kutokana na mkasa wa ndege ya Malaysia iliyodunguliwa huko mash… Read More
AJALI YA NDEGE YAUA 51 TAIWAN Taswira kutoka eneo la ajali. Vikosi vya uokoaji vikiwa eneo la tukio. TAKRIBANI watu 51 wamepoteza maisha huku saba wakijeruhiwa baada ya ndege waliyokuwemo kuanguka iliposhindwa kutua kwa dharura huko Taiwan, nchini… Read More
TOFAUTI ZA DINI ZISIWAGAWE WATANZANIA ,MWINYI Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Saidi Meck Sadiki akiongea na watoto wanaotoka katika vituo mbalimbali vya kulelea watoto yatima vya jijini Dar es salaam , wakazi wa jiji la Dar es salaam na viongozi mbalimba… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni