Jumanne, 26 Januari 2016

Diamond Platnumz: Baada Ya Nape Nnauye Mimi Ndo Waziri wa Habari Na Michezo Mtarajiwa

Diamond Platnumz amesema akiachana na muziki anataka kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ili kuweka vitu sawa na kutoa fursa zaidi kwa vijana.

Akizungumza katika kipindi cha Papaso cha TBC FM, Diamond alisema kama akiingia kwenye siasa basi nia yake ni kuwa Waziri wa Michezo.

“Kwa sasa hivi siasa bado ila nikiingia kwenye siasa baadaye akimaliza mheshimiwa Nape nachukua mimi kile cheo cha Waziri wa Michezo,” alisema na kuongeza;

“Kile nakiweza kabisa kwa sababu mimi ukinimbia sijui kuhusu mpira, movie mimi naweza kabisa nikiwa Waziri, nikavifanya na vikawa na maendeleo.

"Ni kitu ambacho naweza siyo nasema nataka kuwa mbunge ila mimi nataka ile siku nimeacha kufanya muziki naingia kwenye siasa basi nakuwa Waziri  wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na kuboresha vitu”

Diamond ambaye hakuweka wazi kwamba ataingia kwenye siasa kupitia chama gani, mwaka jana katika kampeni za uchaguzi mkuu uliomuingiza rais Magufuli madarakani, alishiriki kikamilifu kwenye kampeni za CCM na kutengeneza wimbo pamoja na video.

Related Posts:

  • LOWASSA AKAGUA SHULE ILIYOUNGUA HUKO MONDULI Kiasi cha wanafunzi 100 wa shule ya sekondari ya Erikisongo wilayani Monduli wamenusurika kifo baada ya vyumba vitano vya mabweni yao kuteketea na moto leo (Jumatano) asubuhi. Moto huo ambao inaelezwa chanzo chake… Read More
  • MADEREVA WA VYOMBO VYA MOTO MUWE MAKINI Gari aina ya Toyota Hilux limetumbukia kwenye mtaro uliopo Sinza-Makaburini jijini Dar es Salaam baada ya dereva aliyekuwa akiliendesha gari hiyo kushin… Read More
  • Ajali ya Ndege:Miili imewasili Uholanzi Miili ya abiria wa ndege ya Malaysia MH17 imewasili Eindhoven Ndege mbili za kijeshi zinazobeba miili 40 kati ya 282 ya abiria wale waliofariki kutokana na mkasa wa ndege ya Malaysia iliyodunguliwa huko mash… Read More
  • AJALI YA NDEGE YAUA 51 TAIWAN Taswira kutoka eneo la ajali. Vikosi vya uokoaji vikiwa eneo la tukio. TAKRIBANI watu 51 wamepoteza maisha huku saba wakijeruhiwa baada ya ndege waliyokuwemo kuanguka iliposhindwa kutua kwa dharura huko Taiwan, nchini… Read More
  • TOFAUTI ZA DINI ZISIWAGAWE WATANZANIA ,MWINYI Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Saidi Meck Sadiki akiongea na watoto wanaotoka katika vituo mbalimbali  vya kulelea watoto yatima vya  jijini Dar es salaam , wakazi wa jiji la Dar es salaam na viongozi mbalimba… Read More

0 comments:

Chapisha Maoni