BAADHI ya baa zilizopo katika viwanja vya Legho, Ubungo jijini Dar, leo 
zimevunjwa kufuatia agizo la mahakama kwa kile kilichodaiwa wamiliki 
walivamia eneo ambalo siyo lao.
Akizungumza na mwandishi wetu, dalali wa mahakama kutoka katika kampuni 
ya Mem Auctioneers and General Brokers Ltd, Elieza Mbwambo, alisema 
mmiliki halali  wa eneo hilo ni Dar Cool Makers Limited ambaye baada ya 
 kuvamiwa eneo lake alifungua kesi mahakamani mwaka 1993 ambapo 
iliendelea mpaka ilipofikia leo.
Wavamizi wa eneo hilo ambao ni John Ondoro Chacha, Jumuiya ya Wazazi CCM
 na mtu mwingine mmoja baada ya kuona mmiliki halali amepeleka kesi 
mahakamani nao wakaenda kuweka zuio ambapo Mahakama ya Hakimu Mkazi 
Kisutu iliamuru eneo hilo lirudi kwa mmliki halali ambapo wavamizi 
walitakiwa wabomoe vibanda walivyokuwa wamejenga walikokuwa wakifanya 
biashara ya baa.
“Januari 25 mwaka huu tulipewa oda na mahakama tuje kuwatoa hawa 
wavamizi, tuliweka tangazo kama wiki moja iliyopita lakini hawakujali 
hivyo leo ikawa ndiyo siku rasmi ya kuwaondoa na kama unavyoona ndiyo 
tunabomoa hivi.
“Mwenye kesi ya msingi ambaye ni John Ondoro Chacha alitakiwa kuwaambia 
wapangaji wake kwamba ameshindwa kesi lakini hakuwaambia ndiyo maana 
hata tangazo lilipowekwa hawakushtuka, kwa mujibu wa mahakama huyu 
Chacha ambaye kwa sasa ni marehemu na watoto wake ndiyo walikuwa 
wakipokea kodi ya kila mwezi kwa wafanyabiashara waliowapangia  wakati 
eneo hili siyo lao,” alisema Mbwambo.
Watu mbalimbali walionekana wakiwa wamesimama huku wakishangaa eneo hilo
 huku wengine wakilalamika kwamba watakuwa wanajiachia  wapi wakati 
walikuwa wamezoea viwanja hivyo.
Source-Global Publishers
Ijumaa, 5 Februari 2016
Home »
 » Bomoa Bomoa Zaikumba Sinza...Baa za Uwanjani Legho Zavunjwa 







 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Chapisha Maoni