BAADHI ya baa zilizopo katika viwanja vya Legho, Ubungo jijini Dar, leo
zimevunjwa kufuatia agizo la mahakama kwa kile kilichodaiwa wamiliki
walivamia eneo ambalo siyo lao.
Akizungumza na mwandishi wetu, dalali wa mahakama kutoka katika kampuni
ya Mem Auctioneers and General Brokers Ltd, Elieza Mbwambo, alisema
mmiliki halali wa eneo hilo ni Dar Cool Makers Limited ambaye baada ya
kuvamiwa eneo lake alifungua kesi mahakamani mwaka 1993 ambapo
iliendelea mpaka ilipofikia leo.
Wavamizi wa eneo hilo ambao ni John Ondoro Chacha, Jumuiya ya Wazazi CCM
na mtu mwingine mmoja baada ya kuona mmiliki halali amepeleka kesi
mahakamani nao wakaenda kuweka zuio ambapo Mahakama ya Hakimu Mkazi
Kisutu iliamuru eneo hilo lirudi kwa mmliki halali ambapo wavamizi
walitakiwa wabomoe vibanda walivyokuwa wamejenga walikokuwa wakifanya
biashara ya baa.
“Januari 25 mwaka huu tulipewa oda na mahakama tuje kuwatoa hawa
wavamizi, tuliweka tangazo kama wiki moja iliyopita lakini hawakujali
hivyo leo ikawa ndiyo siku rasmi ya kuwaondoa na kama unavyoona ndiyo
tunabomoa hivi.
“Mwenye kesi ya msingi ambaye ni John Ondoro Chacha alitakiwa kuwaambia
wapangaji wake kwamba ameshindwa kesi lakini hakuwaambia ndiyo maana
hata tangazo lilipowekwa hawakushtuka, kwa mujibu wa mahakama huyu
Chacha ambaye kwa sasa ni marehemu na watoto wake ndiyo walikuwa
wakipokea kodi ya kila mwezi kwa wafanyabiashara waliowapangia wakati
eneo hili siyo lao,” alisema Mbwambo.
Watu mbalimbali walionekana wakiwa wamesimama huku wakishangaa eneo hilo
huku wengine wakilalamika kwamba watakuwa wanajiachia wapi wakati
walikuwa wamezoea viwanja hivyo.
Source-Global Publishers
Ijumaa, 5 Februari 2016
Home »
» Bomoa Bomoa Zaikumba Sinza...Baa za Uwanjani Legho Zavunjwa
Bomoa Bomoa Zaikumba Sinza...Baa za Uwanjani Legho Zavunjwa
Related Posts:
Rais Kikwete Aachia Madara Kistaili...Awasamehe Wafungwa 4,160 Watoke Gerezani RAIS mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete ametoa msamaha kwa wafungwa 4,160 katika kuaga na kukabidhi madaraka ya Serikali kwa Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli. Dk Magufuli aliapishwa jana kuwa Rai… Read More
Maalim Seif Aweka Ngumu Adai Hawawezi Kurudia Uchaguzi Zanzibar Mgombea urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amesema CUF inaendelea kutafuta haki ya Wazanzibar ya kutaka Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec) kuendelea kutangaza matokeo ya uchaguzi … Read More
Nchi Ina Wanafiki Sana wa Kisiasa...Ukawa Wamsusia Magufuli Uwanja wa Taifa ila Bungeni Wamejiandikisha Kwenda Kumsikiliza Kwasababu Kuna Posho-Habibu Mchange Mwanasiasa Habibu Mchange Ameandika yafutayo katika ukurasa wake wa Facebook kuhusu Ukawa: 'Nchi ina WANAFIKI SANA WA KISIASA HII.. Ukawa wamesusia kuapishwa Rais lakini UKAWA HAO HAO wameenda Bungeni kujian… Read More
Mke wa Deo Filikunjombe Ampigia Kampeni Mdogo wa Filikunjombe Achukue Ubunge Jimbo Aliloliacha Mmewe..Adai Wengine Msiwasikilize Hawana Hata Mahali pa Kufikia Ludewa Tanzania bado iko kwenye majonzi baada ya msiba wa aliyekuwa mbunge wa Ludewa,Deo Najua kuna watu walikuwa na maswali juu ya atakayewaongoza wakazi wa Ludewa, sasa leo Novemba 5, 2015 mke wa marehemu Deo Filikunjombe ‘ S… Read More
Luis Munana Afichua Siri ya Jinsi Alivyojikuta Akipendana na Wema Sepetu Wiki iliyopita picha za mtandaoni zilionesha kuwa Wema Sepetu na mshiriki wa Big Brother Hotshots kutoka Namibia, Luis Munana wamefunga ndoa. Hakuna taarifa rasmi kutoka kwa wawili hao baada ya ‘ndoa’ hiyo kufungwa … Read More
0 comments:
Chapisha Maoni