BAADHI ya baa zilizopo katika viwanja vya Legho, Ubungo jijini Dar, leo
zimevunjwa kufuatia agizo la mahakama kwa kile kilichodaiwa wamiliki
walivamia eneo ambalo siyo lao.
Akizungumza na mwandishi wetu, dalali wa mahakama kutoka katika kampuni
ya Mem Auctioneers and General Brokers Ltd, Elieza Mbwambo, alisema
mmiliki halali wa eneo hilo ni Dar Cool Makers Limited ambaye baada ya
kuvamiwa eneo lake alifungua kesi mahakamani mwaka 1993 ambapo
iliendelea mpaka ilipofikia leo.
Wavamizi wa eneo hilo ambao ni John Ondoro Chacha, Jumuiya ya Wazazi CCM
na mtu mwingine mmoja baada ya kuona mmiliki halali amepeleka kesi
mahakamani nao wakaenda kuweka zuio ambapo Mahakama ya Hakimu Mkazi
Kisutu iliamuru eneo hilo lirudi kwa mmliki halali ambapo wavamizi
walitakiwa wabomoe vibanda walivyokuwa wamejenga walikokuwa wakifanya
biashara ya baa.
“Januari 25 mwaka huu tulipewa oda na mahakama tuje kuwatoa hawa
wavamizi, tuliweka tangazo kama wiki moja iliyopita lakini hawakujali
hivyo leo ikawa ndiyo siku rasmi ya kuwaondoa na kama unavyoona ndiyo
tunabomoa hivi.
“Mwenye kesi ya msingi ambaye ni John Ondoro Chacha alitakiwa kuwaambia
wapangaji wake kwamba ameshindwa kesi lakini hakuwaambia ndiyo maana
hata tangazo lilipowekwa hawakushtuka, kwa mujibu wa mahakama huyu
Chacha ambaye kwa sasa ni marehemu na watoto wake ndiyo walikuwa
wakipokea kodi ya kila mwezi kwa wafanyabiashara waliowapangia wakati
eneo hili siyo lao,” alisema Mbwambo.
Watu mbalimbali walionekana wakiwa wamesimama huku wakishangaa eneo hilo
huku wengine wakilalamika kwamba watakuwa wanajiachia wapi wakati
walikuwa wamezoea viwanja hivyo.
Source-Global Publishers
Ijumaa, 5 Februari 2016
Home »
» Bomoa Bomoa Zaikumba Sinza...Baa za Uwanjani Legho Zavunjwa
Bomoa Bomoa Zaikumba Sinza...Baa za Uwanjani Legho Zavunjwa
Related Posts:
Dalili Muhimu za Mwanamke Aliefika Kileleni Mkiwa Faragha. Wanaume wengi sana hua tunadanganywa na wenza wetu kua tumewaridhisha vya kutosha lakini ukweli hua hakuna kitu Hua wanafanya kwa nia njema tu kwani wanaume hua tunajiskia amani sana kuambiwa umemfikisha mtoto w… Read More
Lady Jay Dee Afunga Ndoa Tena..Apost Picha Akiwa Honey Moon Msanii nguli na namba moja nchini kwa upande wa kina dada binti machozi, komamdo, anaconda, lady jay dee amefunga ndoa weekend hii kupitia mtandao wa I.G amepost baadhi ya picha akila honey moon uko Zanzibar … Read More
Model Calisah Afunguka Baada ya Kusambaa Kwa Video yake Akimla ‘Denda’ Wema Sepetu Weekend hii katika mitandao ya kijamii kumesambaa video inayomuonyesha malkia wa filamu nchini Wema Sepetu akiliwa denda na model Calisah. Wawili hao ambao walitumia nguvu nyingi kufanya siri mahusiano yao, wam… Read More
Michirizi Inayoonekana Kwenye Miili ya Akina Dada Inaashiria Nini? Hivi Ile michirizi inayoonekana kwa baadhi ya kinadada nyuma ya goti wakiwa wamevaa sketi fupi huwa ni ishara ya utamu wao kama Mwana FA alivyoimba "Michirizi ya utamu nyuma ya goti mimi hoi na moyo hai si… Read More
Taarifa Kuhusu Kinachoendelea Kwenye Kesi ya Scorpion Mtoa Macho Mahakamani Upelelezi wa kesi inayomkabili Salum Njwete maarufu kama Scorpion anayetuhumiwa kumsababishia upofu wa kudumu Saidi Mrisho umekamilika na hatimaye shauri hilo litasomwa Novemba 30 mwaka huu katika mahakama ya m… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni