WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto imekiri
kwamba mashine ya CT Scan iliyofungwa katika Hospitali ya Taifa ya
Muhimbili ilikuwa ni ya kituo cha kisasa cha kutolea huduma za afya cha
Benjamin Mkapa kilichopo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Akijibu swali la nyongeza bungeni mjini Dodoma, Naibu Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Khamis Kigwangalla
alisema mashine hiyo iliingia nchini kwa lengo la kupelekwa katika kituo
hicho lakini ikapelekwa Muhimbili kutokana na kutokamilika kwa majengo
ya kufungwa mashine hiyo katika kituo hicho.
Alisema, uamuzi huo waliuchukua pia kwa sababu hela ya kununua mashine
nyingine ambayo itapelekwa kufungwa katika kituo hicho ilikuwepo na kwa
sasa mchakato wa ununuzi unaendelea.
Dk Kigwangalla alikuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Chemba,
Juma Nkamia (CCM) aliyetaka jibu la Serikali kama ni kweli ilichukua
mashine ya kituo hicho na kufunga katika Hospitali ya Taifa Muhimbili
ama ilinunua.
Awali katika swali la msingi msingi, Nkamia alitaka kujua mpango wa
Serikali wa kununua mashine mpya ya CT -Scan kwa ajili ya Hospitali ya
Taifa Muhimbili.
Kuhusu hilo, Dk Kigwangalla alisema, Desemba mwaka jana Serikali
ilipeleka mashine ya CT-Scan katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili
ambayo inatumia teknolojia ya kisasa yenye X-ray tube mbili na uwezo wa
kupiga picha ya 128 slice mara mbili.
Ijumaa, 5 Februari 2016
Home »
» Imebainika Mashine ya CT Scan Iliyofungwa Muhimbili Hospital ni ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
Imebainika Mashine ya CT Scan Iliyofungwa Muhimbili Hospital ni ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
Related Posts:
RANIERI KUIKOSA MECHI YA CHELSEA NA TOTTENHAM Boss wa Leicester City Claudio Ranieri anauwezekano mkubwa asiangalie mechi ya Chelsea na Tottenham hii leo kwa sababu atakuwa ndani ya ndege kutoka Italia. Mbweha hao weupe kutoka Kings Power watachukua ubingwa Premier Leag… Read More
Lulu Michael:Mastaa Bongo Mtaishia Kuchambana Instagram tuuZA uso laivu! Staa mwenye mvuto Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefunguka kuwa mastaa wengi Bongo wataishia kuchambana kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram badala ya kutafuta elimu ili siku moja wapate nyadhifa serikalini.… Read More
Meya wa Kinondoni Agawa Bure Maeneo ya Biashara Leo na Kufuta Umiliki wa Vibanda na Vizimba 100Meya wa Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam Mstahiki Boniface Jacob amezua taharuki kwa wamachinga wa ubungo na kukimbia biashara zao wakiambatana naye mithili ya Maandamano mara baada ya kutangaza kufuta umiliki wa vi… Read More
DAYNA NYANGE AITAMANI NDOA Biblia Takatifu kitabu cha Mathayo 19:3 unasema “Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake, ataungana na mke wake, kwa hiyo wao si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asikite… Read More
RAIS KABILA AMFUKUZA KAZI WAZIRI ALIYEPIGA PUNYETO OFISINI Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Joseph Kabila amemfukuza kazi Naibu Waziri wa Posta na Mawasiliano, Enock Sebineza kutokana na utovu wa nidhamu baada ya kuvuja kwa video mitandaoni ikimuonesha akijichua nyeti zake a… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni