WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto imekiri
kwamba mashine ya CT Scan iliyofungwa katika Hospitali ya Taifa ya
Muhimbili ilikuwa ni ya kituo cha kisasa cha kutolea huduma za afya cha
Benjamin Mkapa kilichopo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Akijibu swali la nyongeza bungeni mjini Dodoma, Naibu Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Khamis Kigwangalla
alisema mashine hiyo iliingia nchini kwa lengo la kupelekwa katika kituo
hicho lakini ikapelekwa Muhimbili kutokana na kutokamilika kwa majengo
ya kufungwa mashine hiyo katika kituo hicho.
Alisema, uamuzi huo waliuchukua pia kwa sababu hela ya kununua mashine
nyingine ambayo itapelekwa kufungwa katika kituo hicho ilikuwepo na kwa
sasa mchakato wa ununuzi unaendelea.
Dk Kigwangalla alikuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Chemba,
Juma Nkamia (CCM) aliyetaka jibu la Serikali kama ni kweli ilichukua
mashine ya kituo hicho na kufunga katika Hospitali ya Taifa Muhimbili
ama ilinunua.
Awali katika swali la msingi msingi, Nkamia alitaka kujua mpango wa
Serikali wa kununua mashine mpya ya CT -Scan kwa ajili ya Hospitali ya
Taifa Muhimbili.
Kuhusu hilo, Dk Kigwangalla alisema, Desemba mwaka jana Serikali
ilipeleka mashine ya CT-Scan katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili
ambayo inatumia teknolojia ya kisasa yenye X-ray tube mbili na uwezo wa
kupiga picha ya 128 slice mara mbili.
Ijumaa, 5 Februari 2016
Home »
» Imebainika Mashine ya CT Scan Iliyofungwa Muhimbili Hospital ni ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
Imebainika Mashine ya CT Scan Iliyofungwa Muhimbili Hospital ni ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
Related Posts:
WASOMI WAKOSOA ASILIMIA 2% YA KODI ALIYOPUNGUZA RAIS MAGUFULI Siku moja baada ya Rais Magufuli kushusha Kodi ya Mapato ya Mshahara ( Pay as you Earn – PAYE ) kutoka asilimia 11 iliyopo sasa hadi asilimia 9. Wataalamu wa uchumi nchini wamelipokea katika mtazamo tofauti Mtaalamu wa Uchum… Read More
Siri Kuu Kuhusu Escrow zafichuka SIRI kuu ya James Rugemalira, kumwaga mabilioni ya shilingi kwa baadhi ya majaji wa mahakama kuu, viongozi waandamizi serikalini na madhehebu ya kidini, wabunge na viogogo wa Ikulu, zimeanza kufumuka. Nyaraka mikononi mwa ga… Read More
PROF MUHONGO: TATIZO LA UMEME KUISHA MWAKA HUU MWEZI SEPTEMBA SERIKALI inatarajia kuzindua mradi mkubwa wa kuboresha miundombinu ya kusafirisha umeme Septemba mwaka huu, utakaomaliza tatizo la umeme kukatika. Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alisema kwa sasa miun… Read More
VYAKULA VINAVYO ONGEZA HISIA KATIKA MAPENZI Kama kawaida mara nyingi chakula ambacho kimeungwa pilipili hufanya hata mapigo ya moyo kuwa tofauti na wakati mwingine hata jasho kutoka au kamasi. Kwenye pilipili kuna kitu kinaitwa Capsaicin ambacho hufanya pilipili i… Read More
ITALIA WAJA NA UTAALAMU WA KUPANDIKIZA KICHWA KWA MTU Mtaalam wa upasuaji wa mfumo wa neva (neurosurgeon) Sergio Canavero kutoka nchini Italia, anakusudia kufanya jaribio la kwanza la kupandikiza kichwa cha binadamu kwenye mwili wa binadamu mwingine, ifikapo mwakani. Wataalam… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni