WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto imekiri
kwamba mashine ya CT Scan iliyofungwa katika Hospitali ya Taifa ya
Muhimbili ilikuwa ni ya kituo cha kisasa cha kutolea huduma za afya cha
Benjamin Mkapa kilichopo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Akijibu swali la nyongeza bungeni mjini Dodoma, Naibu Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Khamis Kigwangalla
alisema mashine hiyo iliingia nchini kwa lengo la kupelekwa katika kituo
hicho lakini ikapelekwa Muhimbili kutokana na kutokamilika kwa majengo
ya kufungwa mashine hiyo katika kituo hicho.
Alisema, uamuzi huo waliuchukua pia kwa sababu hela ya kununua mashine
nyingine ambayo itapelekwa kufungwa katika kituo hicho ilikuwepo na kwa
sasa mchakato wa ununuzi unaendelea.
Dk Kigwangalla alikuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Chemba,
Juma Nkamia (CCM) aliyetaka jibu la Serikali kama ni kweli ilichukua
mashine ya kituo hicho na kufunga katika Hospitali ya Taifa Muhimbili
ama ilinunua.
Awali katika swali la msingi msingi, Nkamia alitaka kujua mpango wa
Serikali wa kununua mashine mpya ya CT -Scan kwa ajili ya Hospitali ya
Taifa Muhimbili.
Kuhusu hilo, Dk Kigwangalla alisema, Desemba mwaka jana Serikali
ilipeleka mashine ya CT-Scan katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili
ambayo inatumia teknolojia ya kisasa yenye X-ray tube mbili na uwezo wa
kupiga picha ya 128 slice mara mbili.
Ijumaa, 5 Februari 2016
Home »
» Imebainika Mashine ya CT Scan Iliyofungwa Muhimbili Hospital ni ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
Imebainika Mashine ya CT Scan Iliyofungwa Muhimbili Hospital ni ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
Related Posts:
HII NI KUHUSU WANAJESHI KUPIGANA NA POLISI TARIME JUZI, WANGAPI WAMEUMIA? KISA? Hii ni taarifa kutoka Tarime mkoani Mara ambako watu 12 wamejeruhiwa wakati wa mashambulizi ya kurushiana risasi kati ya askari wa JWTZ kituo cha Nyandoto na polisi wa kituo cha stendi. Kwa mujibu wa magazeti ya Ni… Read More
Kinshasa:Chimbuko la virusi vya HIV Kinshasa mwaka 1955, janga la HIV lilikuwa linatesa mjini humu na kote nchini DRC hasa mkoa wa Katanga Ugonjwa wa ukimwi uligunduliwa miaka ya 1920 mjini Kinshasa, nchini Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo. Wanasayansi … Read More
Picha za palikofanyika birthday party ya Diamond… kabla watu hawajaingia Party ilifanyika Golden Jubilee Towers Dar es salaam ambapo kama hujaona pichaz za kilivyohappen unaweza kuchek post iliyotangulia kabla ya hii kwenye hii siku kubwa ya Diamond aliyotimiza miaka 25 ya kuzaliwa. … Read More
Mambo 10 aliyoyasema Madee kuhusu ishu yake ya kuwekwa Polisi. Madee alikamatwa na Polisi saa kadhaa zilizopita baada ya tukio la yeye kuibiwa simu akiwa kwenye gari tena likitembea ambapo waliohusika ni watu wawili wakiwa kwenye pikipiki saa tisa usiku akitoka Kigamboni Dar e… Read More
USAJILI WA KUDUMU FALCAO MANCHESTER UNITED HABARI KAMILI HII HAPA Wakati mkataba wake wa mkopo ukiwa umebakisha miezi nane kuisha, usajili Radamel Falcao kwenda Manchester United umechukua nafasi kwenye vyombo vya habari. Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Uingereza ni kwamba Man Uni… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni