Wabunge nchini Afrika Kusini wamepigana bungeni baada ya spika kuamuru maafisa wa usalama kuwaondoa kwa lazima wabunge wa upinzani ambao walimbeza rais Jacob Zuma alipoingia bungeni tayari kulihutubia kikao.
Rais Zuma ambaye ameshindwa katika kesi mbili kuu zinazomhusisha na ubadhirifu wa mali ya umma na usimamizi mbaya alikuwa amefika bungeni kwa mara ya kwanza tangu kushindwa mahakamani.
Hata hivyo ujio wake uliwakera sana wabunge wa chama cha upinzani Economic Freedom Fighters (EFF).
Wabunge hao chini ya kiongozi wao Julius Malema walipiga mayowe na kumtupia matusi bw Zuma jambo lililomlazimu spika wa bunge kuamuru wabunge hao wa EFF kuondolewa nje.
Ijumaa iliyopita mahakama ya juu ya Afrika Kusini iliamua kuwa rais Zuma anapaswa kufikishwa kizimbani kufuatia kesi za ufisadi dhidi yake.
Kesi hiyo inahusiana na ufisadi uliotokea katika ununuzi wa silaha zenye thamani ya mabilioni ya dola mwaka wa 1999.
Zuma amekanusha madai yote dhidi yake, Anatarajiwa kukamilisha hatamu yake mwaka wa 2019.
Uamuzi huo wa mahakama ulikuwa msumari wa moto kwa kidonda cha Zuma ambaye mwezi uliopita alipatikana na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka yake alipokaidi amri yakulipa pesa za umma zilizotumiwa kukarabati nyumba yake ya Nkandla.
Alhamisi, 5 Mei 2016
Home »
» Wabunge warushiana makonde Afrika Kusini
Wabunge warushiana makonde Afrika Kusini
Related Posts:
Picha za actors 10 waliotajwa na Forbes kwa kulipwa pesa nyingi 2014 Forbes.com kwa wakati huu wametoa list ya mastaa 10 wa kiume ambao wamelipwa pesa nyingi zaidi kwenye kazi zao za filamu. Muigizaji mweusi ni Will Smith peke yake kwenye top 10 wengine wote ni wazungu. 1 Robert Downey J… Read More
Baada ya Davido kuambiwa anajionyesha na mali zake kwenye instagram..amejibu kama ifuatavyo..Msanii staa wa Nigeria Davido ni mtu ambae huwa anaonyesha kwenye mitandao vitu vingi anavyonunua mfano saa za Rolex za dhahabu, magari ya kifahari, nyumba na vitu vingine ambapo baada ya kuulizwa kuhusu ishu hii ya kupen… Read More
Listi ya mastaa wa Real Madrid watakao tembelea bongoVODACOMA Tanzania ni miongoni mwa makampuni yaliyojitokeza kudhamini ziara ya magwiji waliocheza kwa mafanikio makubwa katika klabu ya Real Madrid. Kikosi cha magwiji hao maarufu kama `Real Madrid Legends` kitafanya ziar… Read More
MADEREVA WA VYOMBO VYA MOTO MUWE MAKINI Gari aina ya Toyota Hilux limetumbukia kwenye mtaro uliopo Sinza-Makaburini jijini Dar es Salaam baada ya dereva aliyekuwa akiliendesha gari hiyo kushin… Read More
TBL YATOA MSAADA WA SH. MIL. 45 ZA KISIMA KIJIJI CHA KAMBI YA SIMBA KARATU Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Doris Malulu akipeana mkono na Mwenyekiti wa Kijiji cha Kambi ya Simba, Damian John wakati wa makabidhiano ya mfano wa hundi ya Sh. Milioni 45 zilizotolewa kwa ajili ya … Read More
0 comments:
Chapisha Maoni